GE2025 Mgombea aahidi wajumbe akiwa mbunge, wajumbe watafanyia mikutano hoteli yenye kiyoyozi, na atawapeleka Afrika kusini kujifunza kuhusu bima

GE2025 Mgombea aahidi wajumbe akiwa mbunge, wajumbe watafanyia mikutano hoteli yenye kiyoyozi, na atawapeleka Afrika kusini kujifunza kuhusu bima

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,777
Wakati watiania wanane wa ubunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Kibamba wakiendelea kunadi sera zao, ameibuka mtiania Alphonce Temba aliyeahidi kuwapeleka wajumbe Afrika Kusini kwa ajili ya kujifunza masuala ya bima ya kifo.

Amesema wataenda kupata elimu ya bima ya kifo itakayosaidia watu kuondokana na changamoto ya kuzuia maiti kwa kukosa fedha.

"Ninao mkakati wa kuja na bima ya kifo nitaondoka na wajumbe mmoja mmoja kila kata twende Afrika Kusini wakajifunze waione kama inafaa tuje tuitambulishe hapa ili iiwasaidie wanaopata vifo vya ghafla na hawana uwezo wa kumudu gharama" amesema Temba.

"Nikipatiwa nafasi nikawa Mbunge mwaka 2027 na 2030 hatukaa hapa tukaa kwenye hoteli nzuri yenye kuyoyozi," amesema Temba.

Watia nia wengine wanaoendelea kuzunguka katika kata za Goba, Mbezi na Saranga, ni Angellah Kairuki, Issa Mtemvu, Nestory Yamungu, Angelo Nyonyi, Joseph Chikongoye, Consolatha Rwiza na Mwamini Mbwambo.

Watiania hao wameahidi kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa Kibamba ikiwemo, ardhi, eneo la maziko, shule, maji, mazingira, soko na huduma za afya. Imeandikwa na Mintanga Hunda. Video na Sute Kamwelwe.

 
Wakati watiania wanane wa ubunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Kibamba wakiendelea kunadi sera zao, ameibuka mtiania Alphonce Temba aliyeahidi kuwapeleka wajumbe Afrika Kusini kwa ajili ya kujifunza masuala ya bima ya kifo.

Amesema wataenda kupata elimu ya bima ya kifo itakayosaidia watu kuondokana na changamoto ya kuzuia maiti kwa kukosa fedha.

"Ninao mkakati wa kuja na bima ya kifo nitaondoka na wajumbe mmoja mmoja kila kata twende Afrika Kusini wakajifunze waione kama inafaa tuje tuitambulishe hapa ili iiwasaidie wanaopata vifo vya ghafla na hawana uwezo wa kumudu gharama" amesema Temba.

"Nikipatiwa nafasi nikawa Mbunge mwaka 2027 na 2030 hatukaa hapa tukaa kwenye hoteli nzuri yenye kuyoyozi," amesema Temba.

Watia nia wengine wanaoendelea kuzunguka katika kata za Goba, Mbezi na Saranga, ni Angellah Kairuki, Issa Mtemvu, Nestory Yamungu, Angelo Nyonyi, Joseph Chikongoye, Consolatha Rwiza na Mwamini Mbwambo.

Watiania hao wameahidi kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa Kibamba ikiwemo, ardhi, eneo la maziko, shule, maji, mazingira, soko na huduma za afya. Imeandikwa na Mintanga Hunda. Video na Sute Kamwelwe.

View attachment 3428675
Huyo mtiania mwenye PhD mbona anajikanyaga kanyaga kuliko hata watiania wenye elimu ya la saba B?
 
Wameamua wenyewe kugeuza chama chao kuwa chama cha walugaluga.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom