Mgogoro wafukuta NCCR - Mageuzi

Mgogoro wafukuta NCCR - Mageuzi

aisee yaani NCCR naionea huruma sana, mbatia kukiua chama chake kisa ukawa, wamepoteza viti vingi vya NCCR bungeni, mtu kama kafulili tutammisi sana aisee,, inabidi NCCR wajitoe ukawa ili kujenga chama chao upya, naona joka la chadema limeimeza nccr vibaya sana,, ombi langu kwa mbatia: Jenga chama chako ili 2020 mpate wabunge wengi mjengoni, acha kutumika kuwa msemaji wa chadema na ukawa, mfikilie mtu kama davis kafulila ameanguka.

Mbatia anahusikaje kwa wale wabunge wa Kigoma kukosa ubunge? Infact kama siyo Ukawa hata Mbatia asingekuwa mbunge.
 
Mbatia angejiunga tu na Chadema yaishe.

atafunikwa kule

amekosea mahesabu, hakuna tatizo kupata kiti kimoja, maana amejitoa sadaka kwa UKAWA. Tatizo ni kuwa chama chake hakijaimarika pale kimesambaratika
 
Hatari hiyo kutoka wabunge wanne mpk mmoja dah kuna haja ya mh kujipima na kuchukua maamuzi
 
Kafulila hata bila Mbatia ameshinda ni zengwe kachewzewa kafanya meng jimbon mwake m/kit awepo asiwpo his pipo love him!!!!plus hvi mwenyekti na yy c alikua anagombea na azunguke mara ngap?? JK na Zitto ni wenyevti pia walizunguka nchi nzima??? Heri baba riz alikua rais ila zitto hata mama Anna alikua anamsupport????? Chama ni kipya vip ubunge na madiwan zitto aliwaombea kura!!!! Don't blame Mbatia mambo ni mengi huwez please kila mtu plus ni hyuhyu Kafulila rumour had t alikua anataka mpindua mwenzie so may be walikua na tofauti zao

Ebu jitathmini mwenyewe ulichoandika yaonesha hujui siasa ila unajua kuongea. Ni darasa la ngap?
 
Chama kiasisi ni chama kikongwe nchini na chenye heshima na historia ndefu si nchini pekee bali hata katika bara zima la Afrika ambapo kwa nyakati tofauti nchi mbalimbali zimekua zikija Tanzania kujifunza siasa zake.
Licha ya ukongwe wake lakini mikakati mahiri ndani ya chama hiki imekifanya badala yakwenda uzeeni,chenyewe kinarudi ujanani ilihali miaka inazidi kusonga mbele.
Leo nimeona niandike andiko hili na wana CDM wekeni hili kwenye kumbukumbu siku moja historia italihukumu andiko hili.
-Mkakati wa kwanza,
Ni mkakati wa muda mrefu si kwa uchawi wala kwa hujuma au kutumia nguvu ya dola hapana,ni kwa sayansi ya siasa kuhakikisha NCCR mageuzi inapata ushindani madhubuti kuhakikisha inafifia na hatimae inafikia hatamu ambapo kwa sasa upo hatua za mwisho kabisa.
UKAWA wanajidanganya wanaposema ili washike dola wanahitaji viongozi kutoka chama asisi na hapa ndipo mwisho wa siku wanakataa matokeo halali ambayo wameshindwa kihalali na kidemokrasia tena kwa sababu ambazo chanzo chake ni wao wenyewe.
Japo nazungumzia NCCR,lakini nimeitaja UKAWA ili tujifunze kwa mifano kwani na wao wanakanyaga nyayo zilezile walizokanyaga NCCR mageuzi.
Hakuna asiemfaham Mzee mrema ambaye kwa misingi ile ile alijiunga NCCR na akapokelewa kwa vigezo hivihivi ambavyo leo Lowasa kapokelewa CDM kwamba ukitaka kuangusha chama dola utahitaji viongozi wenye nguvu kutoka chama dola.Lakini swali ni je ninini hatma ya NCCR leo?
NCCR walimchukua mrema kutoka chama asisi lakini je chama asisi kilianguka?
Komeo na kitasa cha mwisho kabisa ni mh Mbatia,yeye amepata kua mbunge wakipekee,huyu ni mbunge mteule ambaye aliteuliwa na mh Raisi ambaye kimsingi ameonesha umahiri mkubwa akiwa bungeni kwa kutetea na kumpigania mama tanzania,
lakini swali ni je,ni kweli kwamba mbatia ni mahiri kiasi cha kua kipaumbele kupata nafasi alionayo kuliko wapambanaji wiliopo ndani ya chama asisi?
Hivi kuna anaejiuliza hili swali?
Lakini nini hatma ya NCCR leo hii chini ya mikono ya mbatia?
2-Mkakati wa pili
Hapa star wa mchezo ni Lowasa stay tuned.
Hiki ndicho chama mama na chama asisi nchini.
 
Yeye kama mwenyekiti hajawai kukanyaga jimboni kwa kafulila kumpigia kampeni? Mkuu, unaelewa implication yake?

Slaa aliwaambia mkimteua Lowassa itatuchukua muda mwingi kumsafisha. Sasa huyu bwana mzee alikuwa ubavuni mwa Lowassa kumsaidia kusema maana Lowassa mwenyewe hajiwezi
 
Back
Top Bottom