Mgogoro wa kibiashara baina ya Reginald Mengi na Rostam Aziz kuibuka upya

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau,

Mdau wangu ambaye yupo karibu sana na Mfanyabiashara Reginald Mengi amenidokeza kuwa jana amefanya mazungumzo na mfanyabiashara huyo. Mazungumzo yao yalijikita kutathmini hatma ya wawekezaji wa ndani katika kipindi cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015. Katika mazungomzo hayo, Reginald Memgi ameonesha wasiwasi wake na hali ya mambo inavyoenda ndani ya chama tawala, CCM.

Kwamba, ndani ya chama hicho kumeibuka kundi la watu ambao wanautafuta urais kwa udi na uvumba kwa maslahi yao binafsi. Anasema kuwa lipo shinikizo kutoka kwa wafanyabiashara ambao wanageuza siasa kuwa mtaji katika biashara zao.


Mengi anaenda mbali kwa kutukumbusha Watanzania kuwa wapo wafanyabiashara ambao wamegeuka kuwa matajiri kupitia siasa. Kwamba, watu hao hawakuwa lolote kabla ya kuingia kwenye siasa ila baadaye wamegeuka kuwa wafanyabiashara wakubwa tena wakimiliki makampuni ambayo yanashinda zabuni mbalimbali kirahisi.

Reginald Mengi anatoa mfano wa Rostam Aziz. Kwamba, Rostam hakuwa maarufu kabla hajaingia kwenye siasa na kwamba ukiangalia makampuni yake karibu yote yameshiriki kuliibia taifa kwa namna moja ama nyingine hasa kupitia ukwepaji kodi na kushinda zabuni kijanja ujanja.


Reginald Mengi anakumbusha mgogoro wake na Rostam ulioibuka kama miaka minne iliyopita na kusema kwamba mgogoro huo haujamalizika isipokuwa uliahirishwa tu baada ya Rostam kuwa nje ya nchi kwa muda mrefu. Anasema kuwa hakukosea kumuita Rostam kama ni fisadi papa na kwamba amekuwa kikwazo kikubwa katika maendeleo ya nchi. Kwamba, Mengi ataendeleza mapambano yake dhidi ya Rostam.

Mengi anasema kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu, watanzania na hasa chama tawala kinapaswa kuwa macho sana na aina ya watu ambao watateuliwa kuwania nafasi mbalimbali. Anasema kuwa Edward Lowasa ni mtu ambaye wana mahusiano mazuri ila kwa mtazamo wake anasema kuwa hafai kuwa Rais wa Tanzania kutokana na tabia zake binafsi na aina ya watu waliomzunguka.

Anatolea mfano kuwa huwezi kuwa mtu safi ilhali umezungukwa na watu waliojaa madudu na uchafu wa kila aina. Kitendo cha Lowasa kumkumbatia Rostam kunaendelea kumuweka pabaya kwenye harakati zake za kwenda Ikulu.


Wadau, hakika watu wenye akili wameanza kuzinduka.
 
Mnaelekea kushindwa vita sasa mnataka kumwingiza Mzee Mengi! Ninakubaliana na wewe kuhusu Lowassa watu wanaomzunguka( wawekezaji).
 
mama umechemka, tafuta pa kutokea!
Mengi anasema kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu, watanzania na hasa chama tawala kinapaswa kuwa macho sana na aina ya watu ambao watateuliwa kuwania nafasi mbalimbali. Anasema kuwa Edward Lowasa ni mtu ambaye wana mahusiano mazuri ila kwa mtazamo wake anasema kuwa hafai kuwa Rais wa Tanzania kutokana na tabia zake binafsi na aina ya watu waliomzunguka. Anatolea mfano kuwa huwezi kuwa mtu safi ilhali umezungukwa na watu waliojaa madudu na uchafu wa kila aina. Kitendo cha Lowasa kumkumbatia Rostam kunaendelea kumuweka pabaya kwenye harakati zake za kwenda Ikulu.
kwa Mengi huyu anayefaamika kwa kutumia vyombo vyake kuwashughulikia watu asingeshadadia habari za Lowassa.
DSC02956.jpg
 
Membe ana maadui kumi na moja (11).wanasubiri kuhama nchi je unawafahamu mkuu Lizaboni
 
Last edited by a moderator:
idoyo
Edward Lowasa katoa fedha nyingi sana kwenye media. Kila chombo kitakachotangaza habari yake kilitengewa shilingi milioni kumi. Kwa mtu mwenye kutafuta fedha kwa udi na uvumba hawezi kuacha fedha hizo. Hapo deal la biashara limefanyika. Utaona kama habari hiyo itaendelezwa.
 
Last edited by a moderator:
kweli Lowasa kachoka sana sijui anataka kupima afya gani wakati mwili wake wote unaumwa.
 
Edward Lowasa katoa fedha nyingi sana kwenye media. Kila chombo kitakachotangaza habari yake kilitengewa shilingi milioni kumi. Kwa mtu mwenye kutafuta fedha kwa udi na uvumba hawezi kuacha fedha hizo. Hapo deal la biashara limefanyika. Utaona kama habari hiyo itaendelezwa.

Mkuu hizo mbona kidogo sana kamwaga pesa nyingi sana.
 
Simchafui Lowasa. Ila napost kila kinachojitokeza dhidi ya huyu fisadi

Najua wewe ni mwanaCCM, hivi akipitishwa huyu 'fisadi' Lowassa kuwania urais kupitia chama chenu, utampigia kura Lowassa, utachagua mgombea mmojawapo wa upinzani au utaamua ku-abstain? Maana yaonekana unamchukia kweli kweli!
 
All TRUTH
kama Mengi angekuwa hamkubali Lowassa, wala asingeruhusu kuripotiwa kwa habari hii! Yupo radhi asiuze gazeti, anajulikana alivyo! Pamoja na kuandikwa na magazeti mengi, karatasi la CCM, Uhuru, halijaandika!
 
Last edited by a moderator:
Mie lowasa kanifurahisha sana kasema hatoki ng'o CCM wasiompenda watoke wao, na Rostam alienda kuzichanga aje amsapoti Lowasa rafiki yake, mnahangaika kuchongonisha watu humu kisa si Mengi na Rostam bali lowasa. Sasa umefika muda wa wana CCJ kusajili chama chenu. Lowasa kawashika pabaya CCM.
 
mwasu
Hamna CCJ wala JCC wanaona ngoma inovyonoga. BMK limewamaliza wengi. Hakuna ugomvi wowote wa Mengi na Rostam na EL. Spin doctors too late, shame on you
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom