- Thread starter
- #21
Kwani John alizungumza na mitungi siku ile? Mgeja kawapiga nyundo ya kila 20, hamsimami tena daima mtaendelea kulala huku mkiwa mahututi
Mkurupukaji utamjua tu! Naivety!!
Kwani John alizungumza na mitungi siku ile? Mgeja kawapiga nyundo ya kila 20, hamsimami tena daima mtaendelea kulala huku mkiwa mahututi
Bila hata kuzungumzia hoja yake, lakini Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Hamisi Mgeja ni mtovu wa adabu kwa kuwa alikuwa akizungumza na waandishi wa habari na akijua kuwa kwa kupitia wao atakuwa akizungumza na Watanzania, alikuwa akitafuna bazoka!! Achilia mbali waandishi na wananchi, lakini mtu mwenye adabu na heshima zake hawezi kuzungumza na mwingine huku akiwa anatafuna Big-G
Source: ITV News hivi punde tu.
Nimecheka sana.Eti huyo
ni mwenyekiti mwenye historia iliyotukuka ndani ya chama na mpambe wa
heshima wa mgombea urais
Waganga wa jadi wabaya sana. ndivyo walivyomuelekeza!!!!
Cha kufurahisha EL yeye anaendelea na anachofanya bila kuwajibu..mnabaki mkibwatukiana
Lowasa bana! Anadhihirisha yeye ni mtendaji sio mzee wa porojo,anaona akiwajibu atapoteza muda subirini na leo Jumapili afanye harambee nyingine ili mpate cha kuitisha press next week
Ndio maana Tanzania haiendelei maana ni akili ndogo inatawala akili kubwa halafu utasikia maendeleo kwa kila mtanzania, kweli maendeleo kwa viongozi kama hawa?
Are you serious? Fergie yupo kwenye michezo na pia ni commercial
Je yeye,tamko lake ni mashindano ya ligi gani ?
Mzee tofautisha michezo na burudani na serious issues! Fergie pale anakuwa michezoni ambapo kutafuna Big-G ni jambo la kawaida. Pia hadhi ya wachezaji kwa kocha wao inaweza kufananishwa sana na watoto wake tu, hivyo kuzungumza nao au kuwaelekeza huku akitafuna bazoka ni jambo la kawaida. Kuzungumza na waandishi wa habari ni tofauti kwa kuwa wao wako pale kwa serious issues na kwa niaba ya jamii, na unapowaita na kuwaonyesha dharau, ni moja kwa moja unaidharau jamii wanayoiwakilisha. Huo ndio mtazamo wangu na ni demokrasia kutofautiana!