#COVID19 Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani, Tumbi Hospital adaiwa kulazimisha watumishi kuchanjwa kinyume na hiari yao

Jana na leo zinafanana!!???
 
Itakuwa upumbavu kwa watumishi wa sekta ya afya kukataa kuchanja wakati wao wapo katika mazingira hatarishi ya kuambukizwa Covid-19 kuliko kada yoyote. Ilipaswa iwe lazima.
Kweli mimi mwenye nililazimika kuchanja kwa kuwa mke ni muuguzi (amechanja) na ameshahudumia wagonjwa wa uviko na baadhi walipona kwa kuwekewa oksijeni na baadhi walifariki.Watu waache hofu sijaona badiliko lolote upungufu wowote leo ni siku 52 toka nichanjwe.
 
Matokeo ya side effects za Johnson & Johnson utaziona kuanzia mwaka 2023- 2025! We subiri tu!!!
 
Pamoja na kuwepo kwao katika mazingira hatarishi kuambukizwa, itakuaje upumbavu kwa kutochanjwa kama kuchanjwa kwenyewe hakuzuii maambukizi???
 
Subiri wakianza uploading!! Mkuu una nano-chip tayari!! They can trace you whenever they want!! They can upload whatever data they want! They can even influence your thinking! Pole!! Tuache hayo corona ni ugonjwa wa kufikirika! Ukiamini upo unakuwepo kweli!! Ukiamini haupo, haupo kweli!! Wanaoathirika ni wale wanaoamini juu ya corona!!
 
Mganga mkuu wa Tumbi pole, huu muziki hautauweza!! Huna uba u wa kulazimisha watu wachanjwe!! Yawezekana kabisa nyuma ya pazia mnashinikizwa mlazimishe watumishi kuchanja na ngazi za juu lakini mambo yakikudodea jiandae kufanywa KONDOO WA KAFARA!! Huu muziki hauuwezi, POLE!!! Achana na kulazimisha watu vinginevyo lazima utumbuliwe na WATAKURUKA!!
 
Nguvu ya beberu sio poa hata kidogo, beberu kahakikisha tunachanja, lazima tuchanje coz tunapewa pesa za bure na mikopo nafuu. Jiulize beberu ana interest gani na mwafrika, kumlazimisha mambo yake ya ndani kabisa?

These mofos are imbeciles!
Mkuu usiwatishe watu.
Acha wenye kuhitaji wachanje.
 

Kama wewe ni muhudumu wa Afya na badala ya kuamini chanjo una mwamini askofu gwajima katafute kazi nyingine. Wahudumu ndiyo waambukizaji wakubwa wa Corona tena kwa watu walio hatarini kiafya. Huyu anajaribu kuokoa maisha ya watu sio kupokea rushwa lakini bado kuna watu hawapendi!!
 
Itakuwa upumbavu kwa watumishi wa sekta ya afya kukataa kuchanja wakati wao wapo katika mazingira hatarishi ya kuambukizwa Covid-19 kuliko kada yoyote. Ilipaswa iwe lazima.
In medical issues hakuna kitu inayoitwa "kushurutisha/kulazimisha". Kinachotakiwa ni kutoa taarifa sahihi ya huduma na mlengwa aamue kuridhia kupata huduma paswa kupitia taarifa sahihi alizopatiwa (Informed consent). Huo ndio UTABIBU.
 
Wapi umeona hiyo chanjo moja imeokoa maisha!! Aende kuokoa mama yake, mke wake watoto wake nk!!
 
Chip unaijua acheni kupotosha.wanitrace kwa faida gani.Shida baadhi ya watanzania ni kuamini watu wasio na elimu ya tiba.Wengi walikimbilia Samunge eti tiba ya ukimwi wakaacha ARV wakapukutika.Tusubiri hiyo 2023 yenu mnaodanganywa na Gwajiboy tapeli wa mimbarini.
 
Bila shaka wanajikinga la sivyo wangekuwa wameshaambukizwa na wengine wengi kufa
 
Sasa na wale wahudumu wa afya kule Marekani waliyofukuzwa kazi kwa kutokubali kuchanjwa nao watakuwa wamemsikiliza Gwajima pia? Ni upumbavu kufikiria kwamba kila asiyetaka kuchanja hapa Tz ni kwa sababu ya Magufuli au Gwajima.
 
Zoezi kuzuia kuambukizana limeshindikana mfano hapa Dar tu level seat imewashinda kusimamia halafu et tunataka kulazimishana hivyo vichanjo milioni moja et kwa ajili ya kinga!
Wenzetu huko waliweka hadi Lockdown ili kudhibiti maambukizi wamekuja kufungua baada ya kuchanja watu wao kwa wingi ila sisi tumeachia watu waambukizane watakavyo halafu et tunataka kulazimishana hivyo vichanjo vichache et kwa ajili ya kinga, waseme tu wameona zinakaribia ku expire basi ndio maana wanataka kuzimaliza.
 
Tatizo hili ni global,watumishi wa afya wapo kwenye risk kubwa ya kupata UVIKO 19,hivyo kuchanjwa ni muhimu sana,huyo kiongozi anawataka watumishi kuchanja anastahili pongezi badala ya majungu,UVIKO 19 ni jirani yetu anaetutesa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…