Hii umeitoa wapi?sehemu zingine duniani? Sehemu zote siku inaanza saa 6 (0000) usiku lakini kwetu inaanza saa 1 (0700)
Hii umeitoa wapi?
Umetumia kigezo gani kufikia hili hitimisho?
-
je wazungu saasita kamili usiku wanatamkaje?Sio hitimisho ni swali, toa uelewa wako kiongozi! Dunia ina mambo mengi sana hamna mjuvi wa kila kitu. Asubuhi sisi tunasema ni saa moja wenzetu wanasema ni Seven lakini pia saa zetu zinasoma 7 sio 1
Kwakuwa sisi ni special sana?
Mfumo ni ule ule sema tunaandika masaa kwa kuzingatia swahili kama tuavyoyatamka, kwa kuzingatia mawio na machweo ya jua
Saa la kwanza la asubuhi - saa 1 asubuhi
Saa la kwanza la usiku - saa 1 usiku
Tarehe bado inabadilika saa 6 usiku kama mfumo ulivyo
twelve pm? saasita mchana je?Twelve pm au Midnight
Wao wanatumia am pmNdio najiuliza mimi ngumbaru, nikaona nishirikishe na wajuzi wa mambo hapa jamvini! Kwa nini hiyo saa 7 tusingeita saa 1 tu kama ndio siku inaanzia? Bado ingekuwa kiswahili tu pia
Wao wanatumia am pm
Sisi tunatumia alfajiri/adhuhuri asubuhi mchana jioni/alasiri usiku
Hiyo saa 7 usiku ingekuwa saa 1 which ili ileleweke? Lengo ni kueleweka. Utasema iwe saa 1 nini?