Mfumo wa kupeana majina nchini Korea Kusini

Krikichino

JF-Expert Member
Oct 5, 2019
651
1,097
Asante mno kwa kuweza kufungua uzi huu. Naomba niende moja kwa moja kwenye mada.

Wakorea huwa wanatumia mfumo wa tofauti sana katika kupeana majina. Kwa hapa Tanzania kwa mfano mtu anaitwa JOHN SULUHU KIKWETE.

Maana yake hapo JINA LAKE ni JOHN, SULUHU ni JINA LA BABA alafu KIKWETE ni jina la ukoo. Hiyo inaeleweka sina haja ya kukazia sana.

Sasa kwa upande wa Korea kuna utofauti kidogo.

1. JINA LA FAMILIA LINAKUA LA KWANZA

Yes. Kwa mfano mtu anaitwa LEE MIN HO. Maana yake hapo LEE ni jina la familia au la ukoo alafu MIN HO ndio jina lake alilopewa.
Au tuseme PARK GEUN HYE maana yake hapo PARK ni jina la familia alafu GEUN HYE ndio jina lake.

2. WAKOREA WANA MAJINA MAWILI TU.
Wabongo mtu huwa na majina matatu. Mfano Ali Salehe Kiba. Kwa Korea majina ni mawili ni mawili tu. Mfano KIM YOUNG SAM hapo majina ni Kim la kwanza na Young Sam la pili.

Hawana haya mambo ya jina la baba. Ni jina la mtu na la familia basi.

Sasa kama umeangalia series au movies nyingi za Kikorea utafahamu kuwa wakorea wengi huitwa KIM, LEE, PARK, CHOI na JUNG.

Ukweli uliopo ni kwamba by 2015, watu takribani 10.6 Milion wanatumia jina la KIM hiyo ni sawasawa na 21.5% ya wakorea wote wanatumia jina la KIM.

Maana yake ni kwamba KIM ndio jina linalotumiwa sana na wakorea kama Surname likifuatiwa na LEE pamoja na PARK ambapo kulingana na sensa iliyofanyika 2015 takribani nusu ya wakorea wanatumia majina ya KIM, LEE na PARK.

Sasa kuna kitu kimoja lazima tukielewe haimaanishi kuwa KIM au LEE wote ni ndugu. Maana yake ni kwamba staa LEE MIN HO na LEE SEUNG GI pamoja na kwamba wote ni kina Lee lakini sio ndugu maana Koo zao ni tofauti.

Pia kutokana na sensa y mwaka 2000 kwenye Jina KIM kuna koo kama 348 ikiwemo ANDONG KIM, NAGAN KIM na YASEONG KIM.
Kwenye Jina La LEE pia kuna Koo kama PYEONGCHANG na GYEONGJU watu walioko kwenye Koo hizi, wote hawa wanaitwa Lee .

Muanzilishi wa kampuni ya Samsung LEE BYUNG CHUL, Mkurugenzi wa zamani wa Samsung LEE KUN HEE pamoja na Rais wa zamani wa korea kusini LEE MYUNG BAK wote wanatoka ukoo moja wa GYEONGJU.

Kulingana na sensa ya watu na makazi ya mwaka 2000 huko Korea Kusini inasema kuna jumla ya SURNAMES 286 huku Koo zote jumla.

4,179

byung-chul-lee.jpg
maxresdefault(0).jpg
Screenshot_20210508-204810.jpg
lee-byung-hun.jpg
 
"Wabongo mtu huwa na majina matatu".
"Hawana haya mambo ya jina la baba. Ni jina la mtu na familia basi"



Kwa hiyo unaona mfumo wetu ni wa hovyo na wao ndio bora.?
Mental slavery ni mbaya sana. Yaani mtu anakosa kujiamini na kujithamini hadi anajidharau.

Kuna bwana aliulizwa. 'sisi huku Tanzania sasa hivi ni saa 2 usiku na Marekani ni saa 7 mchana, wapi bora zaidi?'. Akajibu marekani ni bora zaidi. Yaani mtu unajidharau hadi mfumo wako wa majina. Tuna shida sisi waafrika.
 
"Wabongo mtu huwa na majina matatu".
"Hawana haya mambo ya jina la baba. Ni jina la mtu na familia basi"



Kwa hiyo unaona mfumo wetu ni wa hovyo na wao ndio bora.?
Mental slavery ni mbaya sana. Yaani mtu anakosa kujiamini na kujithamini hadi anajidharau.

Kuna bwana aliulizwa. 'sisi huku Tanzania sasa hivi ni saa 2 usiku na Marekani ni saa 7 mchana, wapi bora zaidi?'. Akajibu marekani ni bora zaidi. Yaani mtu unajidharau hadi mfumo wako wa majina. Tuna shida sisi waafrika.
Soma vizuri uelewe mbona hakuna sehemu mtoa maada kadharau mfumo wetu? hii tabia ya kulalamika inataka kuota mizizi
 
"Wabongo mtu huwa na majina matatu".
"Hawana haya mambo ya jina la baba. Ni jina la mtu na familia basi"



Kwa hiyo unaona mfumo wetu ni wa hovyo na wao ndio bora.?
Mental slavery ni mbaya sana. Yaani mtu anakosa kujiamini na kujithamini hadi anajidharau.

Kuna bwana aliulizwa. 'sisi huku Tanzania sasa hivi ni saa 2 usiku na Marekani ni saa 7 mchana, wapi bora zaidi?'. Akajibu marekani ni bora zaidi. Yaani mtu unajidharau hadi mfumo wako wa majina. Tuna shida sisi waafrika.
We mjinga KUNA SEHEM MTOA MADA KADHARAU

KWAN ULIPO SOMAGA MAMBO YA SHAKA ZULU WALIDHARAU TAMADUNI ZETU?
 
"Wabongo mtu huwa na majina matatu".
"Hawana haya mambo ya jina la baba. Ni jina la mtu na familia basi"



Kwa hiyo unaona mfumo wetu ni wa hovyo na wao ndio bora.?
Mental slavery ni mbaya sana. Yaani mtu anakosa kujiamini na kujithamini hadi anajidharau.

Kuna bwana aliulizwa. 'sisi huku Tanzania sasa hivi ni saa 2 usiku na Marekani ni saa 7 mchana, wapi bora zaidi?'. Akajibu marekani ni bora zaidi. Yaani mtu unajidharau hadi mfumo wako wa majina. Tuna shida sisi waafrika.
Asee ndugu vipi mbona kama uzi huu na hii Comment haviendani
 
Back
Top Bottom