Mfumo wa kulea watu na baadae kuwapa uongozi kwa vigezo vya "tunamjua na kumuamini" ndiyo shida kubwa inayotukabili kama Taifa

Mfumo wa kulea watu na baadae kuwapa uongozi kwa vigezo vya "tunamjua na kumuamini" ndiyo shida kubwa inayotukabili kama Taifa

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,620
Reaction score
6,510
Siku Tanzania ilipoamua kuwa yoyote anaweza kulelewa na baadae kupewa uongozi halafu akili atazipata huko huko katika uongozi, ndiyo siku tuliyoanguka kama taifa.

Mfumo wa nchi na wananchi kwa ujumla wanachanganya uzoefu na akili. Mtu yoyote ukimpa afanye jambo kwa muda wa kutosha, uzoefu utambeba ila ufanisi wake unaweza usiwe mzuri.

Viongozi wana access na taarifa muhimu. Wanapewa siri za watu, siri za taasisi mbalimbali na siri za nchi. Hizo taarifa haziwafanyi wawe bora zaidi ya watu ambao hawana hizo taarifa. Kwanza inaonyesha mfumo mzima wa kuzichakata na kuzitumia hizo taarifa kwa manufaa ya nchi haufanyi kazi. Taarifa zipo tu, inajulikana fulani mwizi, fulani kahaba, fulani fisadi, fulani tapeli, fulani muuaji, fulani mshirikina, ila tunaangaliana tu. Mara moja moja vidagaa vinadhalilishwa majukwaani baasi tunaona tuna viongozi.

Ukitaka kupima ufanisi, na hapa ndiyo akili ya mtu inapoingia, mpime wakati wa kufanya maamuzi yanayohitaji tafakuri ya kutosha. Hapo ndiyo utaona majigambo, utaona maamuzi ya kimhemko na kutishana tishana.

Ingekuwa mtu mmoja au watu wachache wala nisingeongea ila shida kubwa ni kwamba mfumo mzima umejaa watu waliochaguliwa kwa sababu tofauti na uwezo, wakalelewa baadae wakapewa nyadhfa na uongozi ikiaminiwa akili watazipata wakishaitwa waheshimiwa. Ndipo hapa tulipo.
 
Siku Tanzania ilipoamua kuwa yoyote anaweza kulelewa na baadae kupewa uongozi halafu akili atazipata huko huko katika uongozi, ndiyo siku tuliyoanguka kama taifa.

Mfumo wa nchi na wananchi kwa ujumla wanachanganya uzoefu na akili. Mtu yoyote ukimpa afanye jambo kwa muda wa kutosha, uzoefu utambeba ila ufanisi wake unaweza usiwe mzuri.

Viongozi wana access na taarifa muhimu. Wanapewa siri za watu, siri za taasisi mbalimbali na siri za nchi. Hizo taarifa haziwafanyi wawe bora zaidi ya watu ambao hawana hizo taarifa. Kwanza inaonyesha mfumo mzima wa kuzichakata na kuzitumia hizo taarifa kwa manufaa ya nchi haufanyi kazi. Taarifa zipo tu, inajulikana fulani mwizi, fulani kahaba, fulani fisadi, fulani tapeli, fulani muuaji, fulani mshirikina, ila tunaangaliana tu. Mara moja moja vidagaa vinadhalilishwa majukwaani baasi tunaona tuna viongozi.

Ukitaka kupima ufanisi, na hapa ndiyo akili ya mtu inapoingia, mpime wakati wa kufanya maamuzi yanayohitaji tafakuri ya kutosha. Hapo ndiyo utaona majigambo, utaona maamuzi ya kimhemko na kutishana tishana.

Ingekuwa mtu mmoja au watu wachache wala nisingeongea ila shida kubwa ni kwamba mfumo mzima umejaa watu waliochaguliwa kwa sababu tofauti na uwezo, wakalelewa baadae wakapewa nyadhfa na uongozi ikiaminiwa akili watazipata wakishaitwa waheshimiwa. Ndipo hapa tulipo.
Uchambuzi sahihi. Na hili tatizo kwa sasa ni kama limeshika kasi.
 
CCM wanaimomonyoa hii nchi bila huruma kwa mifumo yao ya kipuuzi.

Usije kushangaa mtoto wa mwigulu akaja kuwa kiongozi mkubwa nchini.

Bila kuiondosha CCM na mifumo yao kama nchi hatutafika popote.
 
Ingekuwa mtu mmoja au watu wachache wala nisingeongea ila shida kubwa ni kwamba mfumo mzima umejaa watu waliochaguliwa kwa sababu tofauti na uwezo, wakalelewa baadae wakapewa nyadhfa na uongozi ikiaminiwa akili watazipata wakishaitwa waheshimiwa. Ndipo hapa tulipo
"Huyu ni Mwenzetu"

Kwanza niseme hili: umejitokeza kuwa mmoja wa wachangiaji na waanzisha mada zinazofikirisha humu JF, na kuzijengea hoja; lakini mada za aina hii humu JF hazina soko sana, kama zile za Samia Suluhu Hassan kufan kutumia taaluma yake ya usanii; kama vile kumwokota mtoto.

Mada yako inawahusu wote waliotufikisha hapa tulipo sasa. Mfano mzuri ni Jakaya Mrisho Kikwete; ambaye ndiye hasa baba wa mfumo ulioiteka CCM na kuifanya mali ya kundi la watu waovu wasioguswa kabisa na hali ya wananchi wengi wa taifa hili.
 
Siku Tanzania ilipoamua kuwa yoyote anaweza kulelewa na baadae kupewa uongozi halafu akili atazipata huko huko katika uongozi, ndiyo siku tuliyoanguka kama taifa.
Mada yako ni muhimu sana na ni nzito. Kwa hiyo tutaendeleza kwa kuingiza uchokonozi.

Kwani hali hiyo ilianza lini; hiyo ya "kulelewa ndani ya mfumo" na baadae kuamininiwa?

Hili la "kulelewa" siyo jambo baya; kwa sababu ni sehemu ya mafunzo. Kote duniani ndani ya vyama vya siasa hali hiyo ipo.

Lakini kuna tofauti; sisi tumeichukulia hali ya kulelewa na kuifanya iwe ya fursa, badala ya utumishi kutoa huduma bora kwa nchi na wananchi wake.

Tanzania imetumia huko kuleana na kuvuruga taratibu za uongozi. Miaka ya hivi karibuni tunaleana kwa misingi ya makundi ya kidini, kabila na tofauti nyinginezo

Udhaifu mkubwa unaodumisha na kufanya hali hiyo iwe mbaya zaidi ni wakati kiongozi wa juu kabisa wa nchi anapokuwa mbovu zaidi, kuliko hata hao wa chini yake.

Akitokea kiongozi anayejali ufanisi wa uongozi wake kwa nchi, na kufanya jitihada za kubadili hali hiyo katika uongozi wake, inawezekana sana kuibadili, na wananchi watamtambua kiongozi kama huyo.

Bahati yetu mbaya, hatujui atapatikana wapi na lini kiongozi wa aina hiyo

Kuna mfano wa hivi karibuni; hata kama mfano huu siyo kamilifu.
Ungeondoa kupenda misifa na majigambo kama hayo uliyoeleza wewe, pamoja na tabia zake mbaya za kibinaadam (kutofuata taratibu/sheria); Magufuli angeweza kuwa mmoja wa viongozi wa namna hiyo.

Kwa miaka ya mbali kidogo, Edward Sokoine; na bila ya shaka yoyote Mwalimu Nyerere.

Naamini kwa waliopo sasa miongoni mwetu na wanajulikana, Tundu Lissu ni miongoni mwao.
 
Tujikumbushe ya
Ridhiwani kikwete
Wenu hafidhi
Mchengerwa
Sitta
Kombo
Mwinyi
Magufuli
Maghembe
Pinda
Lowasa
Ngasongwa
Kutaja wachache .
Wakina siye utatukuta halmashauri . Kule ambako hata kuhama ni ngumu achilia mbali kupanda cheo
 
Tujikumbushe ya
Ridhiwani kikwete
Wenu hafidhi
Mchengerwa
Sitta
Kombo
Mwinyi
Magufuli
Maghembe
Pinda
Lowasa
Ngasongwa
Kutaja wachache .
Wakina siye utatukuta halmashauri
Makamba Yusuph na january

Magufuli yupi?
Yule wa mwanzo, ukiondoa "ushetan"i wake mwingi, utendaji wake katika nyadhifa alizoshika unajieleza tofauti na hao wengine. Na kama aliigiza 'uzalendo', uigizaji huo ni tofauti na wa akina Kikwete na Samia Mhalifu.

Magufuli hakuingizwa kwa vigezo vya "huyu ni mwenzetu".
 
Siku Tanzania ilipoamua kuwa yoyote anaweza kulelewa na baadae kupewa uongozi halafu akili atazipata huko huko katika uongozi, ndiyo siku tuliyoanguka kama taifa.

Mfumo wa nchi na wananchi kwa ujumla wanachanganya uzoefu na akili. Mtu yoyote ukimpa afanye jambo kwa muda wa kutosha, uzoefu utambeba ila ufanisi wake unaweza usiwe mzuri.

Viongozi wana access na taarifa muhimu. Wanapewa siri za watu, siri za taasisi mbalimbali na siri za nchi. Hizo taarifa haziwafanyi wawe bora zaidi ya watu ambao hawana hizo taarifa. Kwanza inaonyesha mfumo mzima wa kuzichakata na kuzitumia hizo taarifa kwa manufaa ya nchi haufanyi kazi. Taarifa zipo tu, inajulikana fulani mwizi, fulani kahaba, fulani fisadi, fulani tapeli, fulani muuaji, fulani mshirikina, ila tunaangaliana tu. Mara moja moja vidagaa vinadhalilishwa majukwaani baasi tunaona tuna viongozi.

Ukitaka kupima ufanisi, na hapa ndiyo akili ya mtu inapoingia, mpime wakati wa kufanya maamuzi yanayohitaji tafakuri ya kutosha. Hapo ndiyo utaona majigambo, utaona maamuzi ya kimhemko na kutishana tishana.

Ingekuwa mtu mmoja au watu wachache wala nisingeongea ila shida kubwa ni kwamba mfumo mzima umejaa watu waliochaguliwa kwa sababu tofauti na uwezo, wakalelewa baadae wakapewa nyadhfa na uongozi ikiaminiwa akili watazipata wakishaitwa waheshimiwa. Ndipo hapa tulipo.
Na kwa taarifa yako... Hao wanaolelewa kimsingi ndo wanaifaidi Tanganyika!
 
Makamba Yusuph na january

Magufuli yupi?
Yule wa mwanzo, ukiondoa "ushetan"i wake mwingi, utendaji wake katika nyadhifa alizoshika unajieleza tofauti na hao wengine. Na kama aliigiza 'uzalendo', uigizaji huo ni tofauti na wa akina Kikwete na Samia Mhalifu.

Magufuli hakuingizwa kwa vigezo vya "huyu ni mwenzetu".
Magufuli uzalendo wake hauna shaka
 
Uko sahihi, lakini alikuwa kiongozi mkatili, na amechangia sana kurudisha demokrasia ya nchi hii hatua nyingi nyuma. Hata mauaji ya mo29 yalichangiwa sana na mbegu chafu alizopanda akiwa rais.
Ni kwa vile tu watu hawatumii muda kutafakari maoni wanayosoma humu jukwaani.
Samia alifikiri kuua waTanzania kikatili ndiyo njia ya kuwatia uoga watu, akitumia mfano huo huo ulioutumia hapa.

Magufuli alifanya mambo mengi kwa mabavu kutisha watu; Samia kaona hiyo ndiyo njia itakayombakisha kwenye madaraka bila kuhojiwa na watu wenye hofu.

Magufuli na Samia ni watu wawili tofauti kabisa; angalau mwenzake aliweza kuigiza uwepo wa "wanyonge" na kutumia njia hiyo kujionyesha kuwa yeye yupo kwa minajiri ya hao anaowapigania..

Samia hana chochote upande huo; na mbaya zaidi anafanya juhudi za kuwafanya anaowatawala kuwa watwana.
 
Uchambuzi sahihi. Na hili tatizo kwa sasa ni kama limeshika kasi.

wanalea watu wakulinda walivyokwisha kukwapua na kukwapua vingine

Hata zero brain wa kizimkazi kapatikana kwa style hiyohiyo

Na kwa taarifa yako... Hao wanaolelewa kimsingi ndo wanaifaidi Tanganyika!

Wamejaza watu wasio na weledi katika kila taasisi muhimu ili kulinda maslahi yao na ya vizazi vyao.

Unalelewa, unahamishwa hamishwa idara na wizara ili ujuejue vichochoro vya utawala, baadae unapewa uongozi kumbe kichwani ni mtupu. Uzoefu, kaunda suti na cheo vinakubeba.

Hili tatizo lina miaka 20 sasa, nadhani sasa limeota tu mizizi na ndiyo tunaanza kuona athari zake.
 
Tujikumbushe ya
Ridhiwani kikwete
Wenu hafidhi
Mchengerwa
Sitta
Kombo
Mwinyi
Magufuli
Maghembe
Pinda
Lowasa
Ngasongwa
Kutaja wachache .
Wakina siye utatukuta halmashauri . Kule ambako hata kuhama ni ngumu achilia mbali kupanda cheo

Makamba Yusuph na january

Magufuli yupi?
Yule wa mwanzo, ukiondoa "ushetan"i wake mwingi, utendaji wake katika nyadhifa alizoshika unajieleza tofauti na hao wengine. Na kama aliigiza 'uzalendo', uigizaji huo ni tofauti na wa akina Kikwete na Samia Mhalifu.

Magufuli hakuingizwa kwa vigezo vya "huyu ni mwenzetu".
Kuna wakati tunafanya makosa ya kudhani hawa viongozi wakubwa wenye majina tu ndiyo waliolelewa na kubebwa. Hata kwenye idara mbalimbali, wapo wengi sana wa aina hiyo na ndiyo wanaanzishiwa huko ili wapate pate uzoefu, ndiyo baadae wanapandishwa pandishwa wanapewa vyeo vikubwa ila msingi ukiwa mbovu wote tunajua utapata nyumba ya aina gani.
 
CCM wanaimomonyoa hii nchi bila huruma kwa mifumo yao ya kipuuzi.

Usije kushangaa mtoto wa mwigulu akaja kuwa kiongozi mkubwa nchini.

Bila kuiondosha CCM na mifumo yao kama nchi hatutafika popote.
Sahihi kabisa
 
"Huyu ni Mwenzetu"

Kwanza niseme hili: umejitokeza kuwa mmoja wa wachangiaji na waanzisha mada zinazofikirisha humu JF, na kuzijengea hoja; lakini mada za aina hii humu JF hazina soko sana, kama zile za Samia Suluhu Hassan kufan kutumia taaluma yake ya usanii; kama vile kumwokota mtoto.

Mada yako inawahusu wote waliotufikisha hapa tulipo sasa. Mfano mzuri ni Jakaya Mrisho Kikwete; ambaye ndiye hasa baba wa mfumo ulioiteka CCM na kuifanya mali ya kundi la watu waovu wasioguswa kabisa na hali ya wananchi wengi wa taifa hili.

Mada yako ni muhimu sana na ni nzito. Kwa hiyo tutaendeleza kwa kuingiza uchokonozi.

Kwani hali hiyo ilianza lini; hiyo ya "kulelewa ndani ya mfumo" na baadae kuamininiwa?

Hili la "kulelewa" siyo jambo baya; kwa sababu ni sehemu ya mafunzo. Kote duniani ndani ya vyama vya siasa hali hiyo ipo.

Lakini kuna tofauti; sisi tumeichukulia hali ya kulelewa na kuifanya iwe ya fursa, badala ya utumishi kutoa huduma bora kwa nchi na wananchi wake.

Tanzania imetumia huko kuleana na kuvuruga taratibu za uongozi. Miaka ya hivi karibuni tunaleana kwa misingi ya makundi ya kidini, kabila na tofauti nyinginezo

Udhaifu mkubwa unaodumisha na kufanya hali hiyo iwe mbaya zaidi ni wakati kiongozi wa juu kabisa wa nchi anapokuwa mbovu zaidi, kuliko hata hao wa chini yake.

Akitokea kiongozi anayejali ufanisi wa uongozi wake kwa nchi, na kufanya jitihada za kubadili hali hiyo katika uongozi wake, inawezekana sana kuibadili, na wananchi watamtambua kiongozi kama huyo.

Bahati yetu mbaya, hatujui atapatikana wapi na lini kiongozi wa aina hiyo

Kuna mfano wa hivi karibuni; hata kama mfano huu siyo kamilifu.
Ungeondoa kupenda misifa na majigambo kama hayo uliyoeleza wewe, pamoja na tabia zake mbaya za kibinaadam (kutofuata taratibu/sheria); Magufuli angeweza kuwa mmoja wa viongozi wa namna hiyo.

Kwa miaka ya mbali kidogo, Edward Sokoine; na bila ya shaka yoyote Mwalimu Nyerere.

Naamini kwa waliopo sasa miongoni mwetu na wanajulikana, Tundu Lissu ni miongoni mwao.
Uko sahihi, kulea watu kwa ajili ya kuja kuwa watumishi na viongozi kulianza zamani, inawezekana labda toka enzi za Nyerere. Ila kipindi kile nchi ilikuwa na uhaba wa watu waliosoma na bado tulikuwa tunajenga misingi ya kiuongozi.

Sioni haja ya hayo kufanyika sasa, labda kwa idara nyeti ila element za unduguzatio labda zilikuwepo kwa kiwango tofauti toka enzi hizo.

Badala yake kwa sasa kuna watu wametumia mfumo huo, kupenyeza watu wao, kuanzia watoto, ndugu na jamaa maeneo mbalimbali ili baadae waje walinde maslahi yao na kuendeleza utawala ndani ya koo zao. Tatizo huu uchaguzi wa watu hawa haubase kwenye akili au uwezo.

Hali inakuwa mbaya na hatari zaidi kwa ustawi na usalama wa nchi, pale mfumo mzima unapokuwa umejengwa katika misingi hiyo ya kubebana na kujuana bila kujali weledi wa watu.

Mwisho wa siku, unakutana na wimbi la watu wako nje ya serikali ambao wana akili, mawazo mazuri, na uwezo wa kufikiri kuliko walioko ndani. Ukiwadanganya, hawadanganyiki. Wanaishia tu kusema "Watanzania siyo wajinga"
 
Kuna wakati tunafanya makosa ya kudhani hawa viongozi wakubwa wenye majina tu ndiyo waliolelewa na kubebwa. Hata kwenye idara mbalimbali, wapo wengi sana wa aina hiyo na ndiyo wanaanzishiwa huko ili wapate pate uzoefu, ndiyo baadae wanapandishwa pandishwa wanapewa vyeo vikubwa ila msingi ukiwa mbovu wote tunajua utapata nyumba ya aina gani.
Ku-'corrupt' mfumo kunaanzia huko huko juu na kurutubiswa huko ndani unakokuzungumzia wewe.

Hao wajuu ndio watengeneza sera na maamuzi yanayotekelezwa kila mahali.

Huko juu kukiwa na mtu/watu wasiovumilia ubovu wa namna hii , huko chini huwezi kuuona, na ukitokea unazimwa haraka..

Ngoja nikupe mfano, hata kama siyo mfano mzuri sana.
Wakati wa Magufuli na urasimu wa wafanyakazi huko maofisini..

Ninayo mifano mingi mingine tokea enzi za Mwalimu Nyerere. Ukitaka nitaitoa.
 
Uko sahihi, kulea watu kwa ajili ya kuja kuwa watumishi na viongozi kulianza zamani, inawezekana labda toka enzi za Nyerere. Ila kipindi kile nchi ilikuwa na uhaba wa watu waliosoma na bado tulikuwa tunajenga misingi ya kiuongozi.
Inawezekana neno "kulea" likawa siyo sahihi katika maana halisi katika maana inayolengwa hapa.

Chukulia maana hiyo kuwa ni kama 'apprenticeship'; na siyo kulea kwa kupeana shavu.kwa upendeleo.

Chama kuwa na vijana wanaojifunza yanayosimamiwa na chama chao na kuwaandaa kuwa viongozi wa baadae siyo tatizo; tatizo linaanza wakati utaratibu huo unapogeuzwa kuwa wa kuandaa kwa upendeleo kundi la watu maalum, mara nyingi wakiwa na uhusiano na viongozi wa juu wa chama/serikali au nafasi yoyote ya maamuzi.

Akina Kikwete wameingizwa kwenye chama wakiwa watoto bila ya kujali wanatokea kundi gani; wao waliposhika hatamu, wakawa ndio watu wa kuingiza makundi wanayoyataka kwa upendeleo.
 
Back
Top Bottom