Mfumo wa elimu Tanzania

Mfumo wa elimu Tanzania

saopaul

New Member
Joined
Mar 14, 2026
Posts
1
Reaction score
4
Nimejaribu kupitia mtaala huu mpya wa elimu ya msingi Hadi kidato Cha nne sijaona suluhisho la mtaala huu kuwaandaa watoto wetu kushindana na nchi zingine au watoto kujitegemea.

Mfano historia ya Tanzania mtoto anafundishwa teknolojia ya asili ya uvuvi, uhunzi, kilimo wakati watoto wa huko china Wanajifunza kwenda mwezini hii habari ya teknolojia ya asili inamsaidia vipi mtoto wa kitanzania??

Wizara ilete mitaala kutokana na ulimwengu wa Sasa hasa utandawazi na ujasiria mali
 
Kila siku tutawaza kutekeleza mtaala
Mkuu inasikitisha sana 😢 ifike mahala
Unapozungumzia mstakabali wanchi
Elimu haiwezi kutenganishwa swala la msingi wakae na wataalamu kwakina
Wapange mpango mkakati tutoke
Hapa tulipo na wahakikishe isijurudie
Tenha kubadili mtaala kwa kipindi
Cha muda mfupi baada ya mtaala
Kutoka walau miaka 30 hivi inaweza
Kuwa na mantiki .
Tuitazame Dunia mpka miaka
30 ijayo inahitji nn na mtaala
Ukae kwa namna hio sio
Leo huuu mwaka hujaisha
Huu tutakuwa tunafanya nn
Sasa
 
Kuna vitabu vya kichina, kiarabu huko kwenye mitaala ya shule za primarily na secondary school's Yan 😂 watoto watu ss ivi wanafundishwa kichina na kiarabu.
Ni kama serikali inasaidia kueneza ukoloni Mambo Leo,Sasa sijui wanajua au Ndio Kuna MTU kala cha juu,
 
Mfano historia ya Tanzania mtoto anafundishwa teknolojia ya asili ya uvuvi, uhunzi, kilimo wakati watoto wa huko china Wanajifunza kwenda mwezini hii habari ya teknolojia ya asili inamsaidia vipi mtoto wa kitanzania??
Sasa historia ya Tanzania ulitaka wafundushe vitu gani?
 
Kuna vitabu vya kichina, kiarabu huko kwenye mitaala ya shule za primarily na secondary school's Yan 😂 watoto watu ss ivi wanafundishwa kichina na kiarabu.
Ni kama serikali inasaidia kueneza ukoloni Mambo Leo,Sasa sijui wanajua au Ndio Kuna MTU kala cha juu,
Wachina na waarabu ndo washirika wakubwa wa maendeleo ya hii nchi, kujua hizo lugha ni muhimu.
 
Elimu ya shule ya msingi mpaka sekondari ni ya kiujumla tu, lazima watoto wasome vitu vingi.

Hata hao wachina wanasoma historia, tena ni lazima.

Elimu yenye shida nafikiri ni ya vyuoni. Vyuo havitoi ujuzi unaosaidia moja kwa moja kazini.
 
Wachina na waarabu ndo washirika wakubwa wa maendeleo ya hii nchi, kujua hizo lugha ni muhimu.
Ili watoto wetu wawe wachuuzi wa bidhaa zao.

Unafikiri basi ni malengo ya serikali kufundhishwa hizo lugha, ni china na nchi za kiarabu ndio wanao finance hiyo mitaala Yan 😂 serikali inapelekwesha kwenye shughuli zake, kisa dollars
 
Back
Top Bottom