Mipango yote ya kiserikali inafanywa na wataalamu wa sekta husika (kama nishati,n.k) walioko wizarani. Lakini wengi wa wataalamu wetu wamepanda mpaka kufika vyeo vya juu kabisa bila ya kuwa na uelewa wa mambo halisi yalivyo katika fani hizo kwani huajiriwa baada ya kuhitimu masomo na kupandishwa vyeo serikalini kwa kufuata muda wa utumishi wa umma na mtandao ulio nao ndani ya wizara. Ni vizuri nafasi hizo zikawa zinatangazwa na kuombwa na watu wenye ujuzi (practical experience) kuliko kukaliwa na watu wenye utaalamu wa mezani tu! Ndio maana hakuna mipango madhubuti inayokamilika (mfano changamoto za nishati) kwa sababu inafanywa na watu wasiokuwa na uwezo halisi wa mambo. Ni muhimu tubadilishe mfumo.