Mfumo Tatanishi: Ujasiri Wa Lowassa, Ukiritimba Wa Kisiasa, na Mkakati Wa UKAWA

Nietzsche

JF-Expert Member
Dec 5, 2014
206
391
Ikiwa kama "maamuzi magumu" ya Waziri Mkuu wa zamani, ndugu Lowassa, yalipangwa na ‘kitengo' au la, mimi kwa kweli nimevutiwa na matokeo yake. Hili, kwangu mimi, ni tikisiko la kihistoria katika mienendo ya siasa zetu toka tupate uhuru; kwasababu ya tikisiko hili, kitu chochote kinaweza kutokea sasa hivi. Tofauti na hapo zamani, wigo wa siasa zetu umepanuka sasa hivi, na siasa zetu zimebadilika! Binafsi, nimevutiwa na vuguvugu hili ambalo, kwa maoni yangu, limesababishwa na mfumo tatanishi. Mtikisiko huu umenivutia kwa sababu moja kuu: kuna uwezekano mkubwa sana kwamba matokeo ya mtikisiko huu yatakuwa ni kufumuliwa kabisa kwa mfumo uliopo na kusukwa upya! Jambo ambalo siku zote nimekuwa nikitamani litokee nchini Tanzania.

Lakini kabla sijaendelea, ili sote twende sambamba nafikiri ni vizuri nifafanue, japo kwa ufupi tu, maana hasa ya neno hili ‘mfumo'. Katika mazingira ya kawaida, mfumo ni mkusanyiko wa vitengo (units) mbalimbali vinavyofanya kazi pamoja kama sehemu ya utaratibu au mtandao wa mitandao, kama vile ubadilishanaji wa taarifa. Aidha, tukiingia zaidi katika maudhui ya kisiasa, neno ‘mfumo' huweza kumaanisha mkusanyiko wa kanuni na taratibu anuai za kiitifaki ambazo kwayo maamuzi hufanyika. Aghalabu utumiaji wa neno ‘mfumo' hutegemea muktadha wa jambo linaloongelewa.

Kwa wale ambao, kama mimi, mliwahi kupata nafasi ya kusomea fani ya uhandisi, hasa katika somo la Ubunifu wa Mifumo au Systems Design, mtakubaliana na mimi kwamba mfumo wa vitu au watu unaweza ukaundwa kwa njia mbili: unaweza ukaundwa kama mfumo mmoja unaojitegemea au unaweza ukaundwa kwa kujumuisha mifumo mingine midogo-midogo inayojikita ndani ya mfumo huo. Kimsingi, siku hizi mfumo wetu wa siasa chini ya CCM umechukua mtiririko wa aina hii ya pili kimfumo. Aidha, kwa muda mrefu sasa, Tanzania tumekuwa tukitumia mfumo ule ule wa siasa tulioanza nao toka tulipojipatia uhuru, mfumo uliosukwa na waanzilishi wa taifa hili, hususan Mwalimu Nyerere. Mfumo huu sasa umezeeka, umepitwa na wakati, na umejisokota sana na kuzaa ‘mifumo-butu' inayosababisha ufisadi – unahitaji kuzongolewa au kunasuliwa – umekuwa ‘mfumo tatanishi'.

Hapo mwanzo, mfumo huu ulifanya kazi yake vizuri sana na ukawa na nguvu kuliko hata ulivyokusudiwa na mbunifu wake, Nyerere. Hii ndiyo sababu tuliweza kuepuka matatizo ya vita vya kikabila na balaa nyingine zilizopitiwa na karibu nchi zote zinazotuzunguka barani Afrika. Mfumo wa Mwalimu ulikuwa madhubuti. Hata hivyo, kadri Mwalimu alivyoanza kuchoka, ndivyo mfumo wake nao ulivyodhoofika. Mpaka wakati mauti yanampata, mfumo wake ulikuwa umenyong'onyea, itifaki zake nyingi kama zile za Azimio la Arusha zikiwa zimenyofolewa, huku makundi ndani ya chama chake yakimea. Hali hii ilisababisha ombwe (void) katika mfumo wake alioutengeneza, jambo ambalo lilizaa ‘vimifumo' vingine zaidi ndani ya mfumo, vilivyotumiwa kwa ubinafsi na makundi yaliyoibuka katika mfumo wenyewe. Ule uzalendo wote wa ile miaka ya sabini, enzi za TANU na CCM mpya, ulitoweka! Leo hii, matokeo ya dhima hili yamekuwa ni kukinzana kwa ‘mifumo ndani ya mfumo' kunakoambatana na migogoro isiyoisha, inayosababishwa na makundi ndani ya chama. Jambo ambalo limekuwa jinamizi kuu kwa CCM, ambalo kama lisiporekebishwa, litasababisha kifo chake hivi karibuni, kama ilivyotokea kwa chama cha KANU katika nchi jirani ya Kenya.

Sasa basi, nionavyo mimi, uamuzi wa ndugu Edward Lowassa umekuja katika wakati muafaka kwa sababu sisi sote lengo letu la msingi ni kuuondoa mfumo huu mbovu unaochelewesha maendeleo yetu. Mfumo uliojaa, ubadhirifu, ukiritimba, ubwanyeye na, kibaya zaidi, rushwa katika ngazi zake zote – toka chini hadi juu! Katika hali yoyote ile, kama tunataka demokrasia ya kweli, ni lazima tuuondoe utawala wa kurithishana wa ki-CCM uliosababisha ‘ukiritimba wa kisiasa' nchini mwetu, ili matakwa ya watu wetu yaweze kuheshimiwa. Kimsingi, ndiyo maana ninampongeza Waziri Mkuu wa zamani, ndugu Lowassa, na viongozi wa UKAWA kwa mkakati wao katika sakata lote hili.

Hata hivyo, ningependa kutoa angalizo moja dogo tu hapa. Ninajua kwamba sisi sote nia yetu ni moja: kujikwamua kutoka katika mfumo mbovu wa kiutawala kama nilivyofafanua hapo juu. Lakini pamoja na msisimko huu wa kisiasa, ukweli wa mambo ni kwamba, ndugu Lowassa kama mwanasiasa ni 'wild card.' Katika mifumo ya kitaalamu ya data ijulikanayo kama SQL Database Systems, sisi wataalamu wa mifumo hii hutumia wild cards zilizo kwenye baobonya (keyboard) la tarakilishi, kama vile alama ya asilimia "%", kinyota "*" na alama iitwayo kareti "^", kuweza kuudhibiti na kuuendesha mfumo wa data hata katika hali isiyo ya kawaida, yaani hali ngumu ya mambo. Sasa basi, katika mfumo wa data, wild cards kama hizi zinaweza kuwa nzuri sana katika kufanikisha majukumu ya kimfumo. Hufanya kazi haraka na kwa ufanisi wa hali ya juu. Lakini tatizo lake ni kwamba, kitabia, zina NGUVU KUBWA sana katika mfumo kiasi kwamba usipokuwa mwangalifu na kuzibatilisha ipasavyo, unaweza ukajikuta unauharibu mfumo mzima mara moja! Mfumo uliotumia kipindi cha mwaka mzima kuimarishwa, kwa mfano, wild cards hizi zinaweza zikauharibu kwa muda wa sekunde moja tu! Nikiwa kama mhandisi, ninamfananisha Lowassa na wild cards hizi, and for the love of God, UKAWA inabidi watafute mbinu imara sana ya kimfumo na kiitifaki ya kumweka kwenye mstari ulio wima - Lowassa must be ‘tamed'!

Hata hivyo, ni dhahiri kwamba gharama ya ‘kumbatilisha' Lowassa (the cost of ‘taming') ni ndogo kuliko gharama za UKAWA kupoteza uchaguzi dhidi ya CCM. UKAWA inahitaji kupambana na huu ‘mfumo tatanishi' mkongwe tulio nao kwa njia yoyote ile, hakuna ubaya katika hili kama sheria za nchi hazivunjwi. Lengo kuu ni kuung'oa utawala wa CCM na kuufumua mfumo wote tulionao, kisha kuusuka tena upya tukianza na KATIBA mpya ya taifa! Mfumo uliopo sasa na Katiba yake umeharibiwa sana na haufai tena kuwahudumia watu wetu. Haupo pale kwa ajili ya maslahi ya wananchi bali kwa ajili ya maslahi ya wachache, hasa vibopa wa CCM. CCM imeuharibu kabisa kiasi kwamba imebweteka na inaona kama vile madaraka na fursa ya kutawala ni haki yao ya kuzaliwa (birthright) – hata kama wakiiba pesa ya umma kama walivyofanya katika ile kashfa ya #escrow. Wao bado wanafikiri kwamba wao tu ndio walio na haki ya kutawala nchi! Hizi zote ni kasoro mbovu za kimfumo na tutaweza kuzirekebisha pale tu CCM itakapopumzika ikawa chama cha upinzani japo kwa muongo hata mmoja.

Na kwa sababu hii, ninawapongeza tena UKAWA kwa mikakati yao, na Lowassa kwa ujasiri wake. Kama Lowassa alilazimika kuyachukua maamuzi haya kwa sababu ya ‘vimifumo vidogo-vidogo' vilivyokithiri ndani ya ‘mfumo tatanishi' hilo halijalishi sasa hivi; lililo la muhimu sasa ni kuuona MWISHO wa ‘mzunguko wa ukiritimba wa kisiasa usioisha' – the looping political monopoly - ulioota mizizi ndani ya mfumo wa siasa zetu. CCM sasa basi – imetoshaa!!

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.
 
Mliko lala ndiko tuliko amkia, UKAwa hamjafanikiwa bado, jipeni matumaini tuu
 
11825921_864940273587869_584721516591045598_n.jpg
 
Mwaka huu theory zitakuja na kuondoka, watasema na kugeuza. Tunasubiri mafuriko, na mifumo midogo ije kusaidia.
 
Yote hayo yaategemeana na kitu kimoja tu iwapo Lowasa atakuwa Rais
nacho ni hiki 'Lowassa kawatumia UKAWA au UKAWA wamemtumia Lowassa?

Valid input, The Boss. Lakini mimi nafikiri, kama CHADEMA na UKAWA kwa ujumla, waki-manage kumwekea protocols za kimkakati - or constitutional demarcations, if you like - inawezekana kabisa kupata vyote, yaani victory against CCM and good governonce. It's all about good organisation, ethics, and having effective leaders who understand the ethics of leadership.

​Nietzsche.
 
Yote hayo yaategemeana na kitu kimoja tu iwapo Lowasa atakuwa Rais
nacho ni hiki 'Lowassa kawatumia UKAWA au UKAWA wamemtumia Lowassa?

Wote "wametumiana" mkuu! UKAWA kumtumia Lowassa kuibwaga ccm na kuuvunja "mfumo" na Lowassa kuwatumia UKAWA kuifikia ndoto yake ya kuwa Rais wa JMT! Faida kwa UKAWA ni kubwa kwani Lowassa ni mmoja na kwa sasa hana mfumo utakaomwezesha kuwabeba wale "watu/rafiki zake" kama ambavyo ingekuwa angalikuwa Rais kupitia ccm! Kama alivyosema mtoa mada ni muhimu kum-"tame" Lowassa vizuri na mapema hii ili aweze kucheza mdundo/ngoma ya chadema/ukawa na kusahau mdundo/ngoma alozoea ndani ya ccm!
 
Wote "wametumiana" mkuu! UKAWA kumtumia Lowassa kuibwaga ccm na kuuvunja "mfumo" na Lowassa kuwatumia UKAWA kuifikia ndoto yake ya kuwa Rais wa JMT! Faida kwa UKAWA ni kubwa kwani Lowassa ni mmoja na kwa sasa hana mfumo utakaomwezesha kuwabeba wale "watu/rafiki zake" kama ambavyo ingekuwa angalikuwa Rais kupitia ccm! Kama alivyosema mtoa mada ni muhimu kum-"tame" Lowassa vizuri na mapema hii ili aweze kucheza mdundo/ngoma ya chadema/ukawa na kusahau mdundo/ngoma alozoea ndani ya ccm!

Very nice analysis Kindafu, and I agree with you 100% mkuu. Safi kabisa!

Nietzsche.
 
kuna mijadala huwa naona raha sana ninapoisoma na vile inavochangiwa na wadau. huu ni mmoja wapo. a very good analysis and contributions ukiondoa mlevi mmoja alocomment ati tulikolala ndo walikoamkia wao ccm

Asante sana mkuu Leo two. Unajua, imefikia wakati sasa Watanzania wote tuwe tunafikiri kwanza kabla ya kutoa mawazo yetu! Tukumbuke kwamba hiki ni kipindi kigumu sana kwa nchi yetu. This country belongs to all of us after all. Let us do our part - inawezekana!

Mimi huwa nasononeka sana ninapokutana na sarcastic comments kama hizo hapo juu, kwani hilo hunionyesha ni jinsi gani baadhi yetu wamebweteka na 'status qou'. Lakini pia huwa ninafarijika sana ninapokutana na wadau wenye moyo wa kizalendo kama wako, kwani hilo hunionyesha ni jinsi gani nimezungukwa na makomredi wenye hamu ya ukombozi nchini mwangu kama mimi. Asante kamanda!

You know, I really LOVE my country, and I know that my country is rich enough to advance to the likes of Malaysia and even Singapore, because, all these countries don't have what we have in terms of resources, and yet, look at where they are now! It's time we, the young generation, take back the control of our country from these myopic hooligans who are imprudently driving it in a ditch!

Thanks again, Leo two, I am humbled!
:hail:

Nietzsche.
 
Mliko lala ndiko tuliko amkia, UKAwa hamjafanikiwa bado, jipeni matumaini tuu

Huh?! How do you justify that statement? Ngoja nikwambie hili: uliona matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa yalivyokuwa? Basi kwa taarifa yako, hayo yalikuwa "manyunyu" tu. Mafuriko yenyewe subiri utayaona October the 25th!

​Nietzsche.
 
Ikiwa kama “maamuzi magumu” ya Waziri Mkuu wa zamani, ndugu Lowassa, yalipangwa na ‘kitengo’ au la, mimi kwa kweli nimevutiwa na matokeo yake. Hili, kwangu mimi, ni tikisiko la kihistoria katika mienendo ya siasa zetu toka tupate uhuru; kwasababu ya tikisiko hili, kitu chochote kinaweza kutokea sasa hivi. Tofauti na hapo zamani, wigo wa siasa zetu umepanuka sasa hivi, na siasa zetu zimebadilika! Binafsi, nimevutiwa na vuguvugu hili ambalo, kwa maoni yangu, limesababishwa na mfumo tatanishi. Mtikisiko huu umenivutia kwa sababu moja kuu: kuna uwezekano mkubwa sana kwamba matokeo ya mtikisiko huu yatakuwa ni kufumuliwa kabisa kwa mfumo uliopo na kusukwa upya! Jambo ambalo siku zote nimekuwa nikitamani litokee nchini Tanzania.

Lakini kabla sijaendelea, ili sote twende sambamba nafikiri ni vizuri nifafanue, japo kwa ufupi tu, maana hasa ya neno hili ‘mfumo’. Katika mazingira ya kawaida, mfumo ni mkusanyiko wa vitengo (units) mbalimbali vinavyofanya kazi pamoja kama sehemu ya utaratibu au mtandao wa mitandao, kama vile ubadilishanaji wa taarifa. Aidha, tukiingia zaidi katika maudhui ya kisiasa, neno ‘mfumo’ huweza kumaanisha mkusanyiko wa kanuni na taratibu anuai za kiitifaki ambazo kwayo maamuzi hufanyika. Aghalabu utumiaji wa neno ‘mfumo’ hutegemea muktadha wa jambo linaloongelewa.

Kwa wale ambao, kama mimi, mliwahi kupata nafasi ya kusomea fani ya uhandisi, hasa katika somo la Ubunifu wa Mifumo au Systems Design, mtakubaliana na mimi kwamba mfumo wa vitu au watu unaweza ukaundwa kwa njia mbili: unaweza ukaundwa kama mfumo mmoja unaojitegemea au unaweza ukaundwa kwa kujumuisha mifumo mingine midogo-midogo inayojikita ndani ya mfumo huo. Kimsingi, siku hizi mfumo wetu wa siasa chini ya CCM umechukua mtiririko wa aina hii ya pili kimfumo. Aidha, kwa muda mrefu sasa, Tanzania tumekuwa tukitumia mfumo ule ule wa siasa tulioanza nao toka tulipojipatia uhuru, mfumo uliosukwa na waanzilishi wa taifa hili, hususan Mwalimu Nyerere. Mfumo huu sasa umezeeka, umepitwa na wakati, na umejisokota sana na kuzaa ‘mifumo-butu’ inayosababisha ufisadi – unahitaji kuzongolewa au kunasuliwa – umekuwa ‘mfumo tatanishi’.

Hapo mwanzo, mfumo huu ulifanya kazi yake vizuri sana na ukawa na nguvu kuliko hata ulivyokusudiwa na mbunifu wake, Nyerere. Hii ndiyo sababu tuliweza kuepuka matatizo ya vita vya kikabila na balaa nyingine zilizopitiwa na karibu nchi zote zinazotuzunguka barani Afrika. Mfumo wa Mwalimu ulikuwa madhubuti. Hata hivyo, kadri Mwalimu alivyoanza kuchoka, ndivyo mfumo wake nao ulivyodhoofika. Mpaka wakati mauti yanampata, mfumo wake ulikuwa umenyong’onyea, itifaki zake nyingi kama zile za Azimio la Arusha zikiwa zimenyofolewa, huku makundi ndani ya chama chake yakimea. Hali hii ilisababisha ombwe (void) katika mfumo wake alioutengeneza, jambo ambalo lilizaa ‘vimifumo’ vingine zaidi ndani ya mfumo, vilivyotumiwa kwa ubinafsi na makundi yaliyoibuka katika mfumo wenyewe. Ule uzalendo wote wa ile miaka ya sabini, enzi za TANU na CCM mpya, ulitoweka! Leo hii, matokeo ya dhima hili yamekuwa ni kukinzana kwa ‘mifumo ndani ya mfumo’ kunakoambatana na migogoro isiyoisha, inayosababishwa na makundi ndani ya chama. Jambo ambalo limekuwa jinamizi kuu kwa CCM, ambalo kama lisiporekebishwa, litasababisha kifo chake hivi karibuni, kama ilivyotokea kwa chama cha KANU katika nchi jirani ya Kenya.

Sasa basi, nionavyo mimi, uamuzi wa ndugu Edward Lowassa umekuja katika wakati muafaka kwa sababu sisi sote lengo letu la msingi ni kuuondoa mfumo huu mbovu unaochelewesha maendeleo yetu. Mfumo uliojaa, ubadhirifu, ukiritimba, ubwanyeye na, kibaya zaidi, rushwa katika ngazi zake zote – toka chini hadi juu! Katika hali yoyote ile, kama tunataka demokrasia ya kweli, ni lazima tuuondoe utawala wa kurithishana wa ki-CCM uliosababisha ‘ukiritimba wa kisiasa’ nchini mwetu, ili matakwa ya watu wetu yaweze kuheshimiwa. Kimsingi, ndiyo maana ninampongeza Waziri Mkuu wa zamani, ndugu Lowassa, na viongozi wa UKAWA kwa mkakati wao katika sakata lote hili.

Hata hivyo, ningependa kutoa angalizo moja dogo tu hapa. Ninajua kwamba sisi sote nia yetu ni moja: kujikwamua kutoka katika mfumo mbovu wa kiutawala kama nilivyofafanua hapo juu. Lakini pamoja na msisimko huu wa kisiasa, ukweli wa mambo ni kwamba, ndugu Lowassa kama mwanasiasa ni ‘wild card.’ Katika mifumo ya kitaalamu ya data ijulikanayo kama SQL Database Systems, sisi wataalamu wa mifumo hii hutumia wild cards zilizo kwenye baobonya (keyboard) la tarakilishi, kama vile alama ya asilimia “%”, kinyota “*” na alama iitwayo kareti “^”, kuweza kuudhibiti na kuuendesha mfumo wa data hata katika hali isiyo ya kawaida, yaani hali ngumu ya mambo. Sasa basi, katika mfumo wa data, wild cards kama hizi zinaweza kuwa nzuri sana katika kufanikisha majukumu ya kimfumo. Hufanya kazi haraka na kwa ufanisi wa hali ya juu. Lakini tatizo lake ni kwamba, kitabia, zina NGUVU KUBWA sana katika mfumo kiasi kwamba usipokuwa mwangalifu na kuzibatilisha ipasavyo, unaweza ukajikuta unauharibu mfumo mzima mara moja! Mfumo uliotumia kipindi cha mwaka mzima kuimarishwa, kwa mfano, wild cards hizi zinaweza zikauharibu kwa muda wa sekunde moja tu! Nikiwa kama mhandisi, ninamfananisha Lowassa na wild cards hizi, and for the love of God, UKAWA inabidi watafute mbinu imara sana ya kimfumo na kiitifaki ya kumweka kwenye mstari ulio wima - Lowassa must be ‘tamed’!

Hata hivyo, ni dhahiri kwamba gharama ya ‘kumbatilisha’ Lowassa (the cost of ‘taming’) ni ndogo kuliko gharama za UKAWA kupoteza uchaguzi dhidi ya CCM. UKAWA inahitaji kupambana na huu ‘mfumo tatanishi’ mkongwe tulio nao kwa njia yoyote ile, hakuna ubaya katika hili kama sheria za nchi hazivunjwi. Lengo kuu ni kuung’oa utawala wa CCM na kuufumua mfumo wote tulionao, kisha kuusuka tena upya tukianza na KATIBA mpya ya taifa! Mfumo uliopo sasa na Katiba yake umeharibiwa sana na haufai tena kuwahudumia watu wetu. Haupo pale kwa ajili ya maslahi ya wananchi bali kwa ajili ya maslahi ya wachache, hasa vibopa wa CCM. CCM imeuharibu kabisa kiasi kwamba imebweteka na inaona kama vile madaraka na fursa ya kutawala ni haki yao ya kuzaliwa (birthright) – hata kama wakiiba pesa ya umma kama walivyofanya katika ile kashfa ya #escrow. Wao bado wanafikiri kwamba wao tu ndio walio na haki ya kutawala nchi! Hizi zote ni kasoro mbovu za kimfumo na tutaweza kuzirekebisha pale tu CCM itakapopumzika ikawa chama cha upinzani japo kwa muongo hata mmoja.

Na kwa sababu hii, ninawapongeza tena UKAWA kwa mikakati yao, na Lowassa kwa ujasiri wake. Kama Lowassa alilazimika kuyachukua maamuzi haya kwa sababu ya ‘vimifumo vidogo-vidogo’ vilivyokithiri ndani ya ‘mfumo tatanishi’ hilo halijalishi sasa hivi; lililo la muhimu sasa ni kuuona MWISHO wa ‘mzunguko wa ukiritimba wa kisiasa usioisha’ – the looping political monopoly - ulioota mizizi ndani ya mfumo wa siasa zetu. CCM sasa basi – imetoshaa!!

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.

Hii nimeipenda sana!! yaani haichoshi kusoma. Wewe ndugu uliyetoa mada ni kichwa si mchezo. Hapa kuna vitu vingi sana nimejifunza. Kwa mfano hilo neno mfumo hivi karibuni naona limekuwa likitumika sana mpaka likawa linanichanganya kuliwelewa lakini leo mkuu umelidadavua vizuri kabisa. Du Kweli Jamii forum mna kila kitu!!!
 
Hii nimeipenda sana!! yaani haichoshi kusoma. Wewe ndugu uliyetoa mada ni kichwa si mchezo. Hapa kuna vitu vingi sana nimejifunza. Kwa mfano hilo neno mfumo hivi karibuni naona limekuwa likitumika sana mpaka likawa linanichanganya kuliwelewa lakini leo mkuu umelidadavua vizuri kabisa. Du Kweli Jamii forum mna kila kitu!!!

Shukrani sana mkuu. Really appreciate that! Tuko pamoja mkuu wangu.

​Nietzsche.
 
Back
Top Bottom