Mfuko wa LAPF, huu ni ubabaishaji

Mfuko wa LAPF, huu ni ubabaishaji

ibontoko

Member
Joined
Oct 31, 2011
Posts
62
Reaction score
14
Mimi ni muhanga wa huu mfuko wa LAPF kwa mafao ya mirathi na ndio msimamizi wa mirathi.

Nimekamilisha kila kinachohitajika na nasubiri kupewa pesa tu. Lakini huu ni mwezi wa 6 wananiambia benki kuna matatizo hivyo nisubiri.

Wasiwasi wangu ni kwamba huyu mhasibu ni huyu muhasibu anaifanyia biashara hii fedha na kusababisha kuchelewa kwa malipo.

Naomba mnishauri nitawezaje kutatua hili tatizo?
 
Ndio michezo inayofanyika ktk hizo taasisi za fedha...wafanyakazi wamekua na njaa hadi kufikia kudhurumu haki za watu.
 
Hivi kwenye fao la Uzazi huwa inachukua muda gani kupata pesa? Maana documents zote zilijazwa zikapelekwa wakasema ndani ya mwezi hela itakuwa tayari lkn kila siku wanakuja na hadithi mpya,hawa LAPF bure kabisa
 
Mimi waliniambia hivyo hivyo kwamba ndani ya mwezi mmoja utakua umelipwa..... Lakini kilichotokea kila siku story..... Mara michango? Mara network hakuna.... Mara wafanyakazi wachache..... Sababu haziishi...... Kiukweli Lapf majanga.... nadhani bora NSSF bt not sure....
 
Na siku hizi hii mifuko wanavyojipigia promo kwa matangazo ya maneno matamu na ya kilaghai ya kila aina mbona watu watalia sana.
 
Nikiwa kama Mfanyakazi wa Mfuko sio huo nakushauri yafuatayo:
-Jaribu kwenda wa wahusika mhakikishimane kwamba document zinazotakiwa zipo
-Omba hesabu za michango za marehemu na kujihakikishia kwamba fao la warithi li aendana na formula ya ukokotoaji ya fao lako .tacuta wadau wanaojua formula ya LAPF ya ukokotoaji mafao wakusaidie hapa
Kama kila kitu kiko sawa na unacheleweshewa makusudi fikisha tatizo lako kwa Mkurugenzi Mkuu.Hakuna mfuko unaokusudia kuchelewesha mafao pasipo sababu
 
Hesabu zote zipo sawa.. Hatua iliyopo ni kulipwa tu.....na hakuna kitu ambacho kimekosekana...... Maana huwa nawasiliana nao mara kwa mara....
 
Back
Top Bottom