nyumbamungu
JF-Expert Member
- Mar 3, 2017
- 997
- 828
Kuna taarifa nimezisikia kuna Mfanyabiashara mwenye asili ya Yemen anataka kutoa Sh 2 Milion hadi 3 Milion kwa wale wanaozika waathirika wa Covid 19.
Aliandika barua kwenda kwenye Baraza la Dhehebu la Dini yake kwamba Baraza liiombe Serikali waumini wa Dhehebu hilo wasizikwe kwa utaratibu waliouweka Serikali, bali Baraza likabidhiwe Mwili wakishafanya taratibu zote za Dini ikiwemo Kumuosha, Kumsitiri na Kumuombe Du'wa ndio wapewe.
Kwa upande wa Kuzika Baraza liteuwe Walimu wa Nne hadi Sita na wapewe mafunzo na Wizara ya Afya jinsi ya kumzika Marehemu aliyefariki kwa ugonjwa wa mlipuko usio na kinga wala tiba, kwaajili ya kuupokea mwili na kuuhifadhi Kaburini, kwa utaratibu unaotakiwa na WHO.
Katika barua yake alisema kama atakubaliwa ataoa posho kwa hao wahusika ambao wanne hadi sita kwa kila marehemu watakaomzika atawapa Sh 500,000. Dhumuni la kufanya hivyo "Kila Marehemu anastahiki kutendewa yaliyomema pindi anapofariki"
ANGALIZO: Huyo Mfanyabiashara ajiridhishe kwa kufanya uchunguzi wake binafsi kufahamu ni wastani wa Wagonjwa wangapi wanaodhaniwa kufariki kwa dalili za Covid 19, asiangalie takwimu inayotolewa na Wizara ya Afya akafikiri ni hao 11 waliotangazwa.
Aliandika barua kwenda kwenye Baraza la Dhehebu la Dini yake kwamba Baraza liiombe Serikali waumini wa Dhehebu hilo wasizikwe kwa utaratibu waliouweka Serikali, bali Baraza likabidhiwe Mwili wakishafanya taratibu zote za Dini ikiwemo Kumuosha, Kumsitiri na Kumuombe Du'wa ndio wapewe.
Kwa upande wa Kuzika Baraza liteuwe Walimu wa Nne hadi Sita na wapewe mafunzo na Wizara ya Afya jinsi ya kumzika Marehemu aliyefariki kwa ugonjwa wa mlipuko usio na kinga wala tiba, kwaajili ya kuupokea mwili na kuuhifadhi Kaburini, kwa utaratibu unaotakiwa na WHO.
Katika barua yake alisema kama atakubaliwa ataoa posho kwa hao wahusika ambao wanne hadi sita kwa kila marehemu watakaomzika atawapa Sh 500,000. Dhumuni la kufanya hivyo "Kila Marehemu anastahiki kutendewa yaliyomema pindi anapofariki"
ANGALIZO: Huyo Mfanyabiashara ajiridhishe kwa kufanya uchunguzi wake binafsi kufahamu ni wastani wa Wagonjwa wangapi wanaodhaniwa kufariki kwa dalili za Covid 19, asiangalie takwimu inayotolewa na Wizara ya Afya akafikiri ni hao 11 waliotangazwa.