Mfano wa nchi itakayopigwa mnada

Mfano wa nchi itakayopigwa mnada

Mstahiki Mea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
5,582
Reaction score
10,112
Hii kuwa mfano wa nchi itakayopigwa mnada? ZIDISHA MARA 20 ILI UPATE IN TSH

Serikali ya Kenya imetangaza kwamba deni la nchi hiyo limefikia shillingi trilioni 10, kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa katika historia ya nchi hiyo, huku waziri wa fedha John Mbadi akidai kwamba thuluthi mbili za mapato ya kila mwaka ya nchi hiyo yanatumika kulipa madeni.

Mbadi amewataka Wakenya sasa wachukue msimamo mkali dhidi ya ufisadi, ambao unadaiwa kuwa na dhima kubwa katika kuiweka Kenya kuwa katika hali ya kiuchumi iliyoko sasa. Waziri huyo wa fedha anasema mzigo wa deni la taifa unazidi kuongezeka. DW
 

Attachments

  • 1743088434578.jpg
    1743088434578.jpg
    1 MB · Views: 13
sisi ni trion 97 sajajua ni kwa USD au kwa shilingi.TZ watatuuza mpaka vijambio vyetu
 
Halafu hakuna siku deni linashuka kila awamu linapanda!, hii nchi tunahitaji viongozi watakaotutafutia pesa na sio kila siku kukopa tu!
 
Utabiri wa Job mpaka kufikia 2030, utakuwa umetimia kitambo tu. Waarabu, Wachina, Wakorea, Mabeberu wengine wa kizungu na vibaraka wao wenye ngozi nyeusi watakuwa wameshagawana kila kitu ndani ya hii nchi yetu ya kusadikika.
 
Back
Top Bottom