PreGE2025 Meya Kinondoni, Songolo: Nchi ina Katiba na Tume Huru ya Uchaguzi, No Reforms No Election haina maana

PreGE2025 Meya Kinondoni, Songolo: Nchi ina Katiba na Tume Huru ya Uchaguzi, No Reforms No Election haina maana

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Songolo Mnyonge, amewataka viongozi wa CHADEMA kuacha chokochoko za kisiasa ambazo zinaweza kuhatarisha amani ya nchi, hasa kipindi hiki taifa linapoelekea kwenye uchaguzi. Akizungumza na waandishi wa habari leo baada ya kumaliza uzinduzi wa vijana kuelekea siku ya mapokezi ya mwenge, Meya Mnyonge amesema kuwa madai ya CHADEMA ya kutoshiriki uchaguzi bila mabadiliko ya kisiasa hayana mashiko kwa kuwa nchi tayari ina Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.

Soma, Pia: Tundu Lissu: Hatutasusia Uchaguzi, tutazuia uchaguzi kwa nguvu ya Umma, sio bila mabadiliko hatutashiriki uchaguzi

"Siioni maana ya kauli ya No Reforms, No Election wakati wabunge wao wa zamani walitokana na Katiba hii hii wanayoikataa leo. Huu ni unafiki wa kisiasa," alisema Mnyonge. Ameongeza kuwa ni muhimu kwa vyama vyote vya siasa kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi kwa njia ya amani na kuheshimu utaratibu wa kidemokrasia uliowekwa

Caw.
 
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Songolo Mnyonge, amewataka viongozi wa CHADEMA kuacha chokochoko za kisiasa ambazo zinaweza kuhatarisha amani ya nchi, hasa kipindi hiki taifa linapoelekea kwenye uchaguzi. Akizungumza na waandishi wa habari leo baada ya kumaliza uzinduzi wa vijana kuelekea siku ya mapokezi ya mwenge, Meya Mnyonge amesema kuwa madai ya CHADEMA ya kutoshiriki uchaguzi bila mabadiliko ya kisiasa hayana mashiko kwa kuwa nchi tayari ina Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.

Soma, Pia: Tundu Lissu: Hatutasusia Uchaguzi, tutazuia uchaguzi kwa nguvu ya Umma, sio bila mabadiliko hatutashiriki uchaguzi

"Siioni maana ya kauli ya No Reforms, No Election wakati wabunge wao wa zamani walitokana na Katiba hii hii wanayoikataa leo. Huu ni unafiki wa kisiasa," alisema Mnyonge. Ameongeza kuwa ni muhimu kwa vyama vyote vya siasa kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi kwa njia ya amani na kuheshimu utaratibu wa kidemokrasia uliowekwa

OLE WAKE MWANANCHI ATAKAYE ENDA KUPIGA KURA MWAKA HUU.

OLE WAKE MWALIMU ATAKAYE SIMAMIA UCHAGUZI MWAKA HUU
 
Kwani hajui alishinda vipi uchaguzi?
 
Back
Top Bottom