PreGE2025 Meya jiji la Arusha: Mrisho Gambo ndiye anayemchokoza Makonda, ni mgomvi kwa kila mtu

PreGE2025 Meya jiji la Arusha: Mrisho Gambo ndiye anayemchokoza Makonda, ni mgomvi kwa kila mtu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
“Si kwamba namtetea Makonda lakini katika sakata lao hili, Gambo ndie anaemchokoza Makonda, Gambo ana ugomvi na kila kiongozi anayekuja Arusha, alikuwa na ugomvi na viongozi waliopita wakina John Mongela, Kennani Kihongozi hata mimi hayuko sawa na mimi” Maximilian Iranqhe - MEYA JIJI LA ARUSHA.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
“Si kwamba namtetea Makonda lakini katika sakata lao hili, Gambo ndie anaemchokoza Makonda, Gambo ana ugomvi na kila kiongozi anayekuja Arusha, alikuwa na ugomvi na viongozi waliopita wakina John Mongela, Kennani Kihongozi hata mimi hayuko sawa na mimi” Maximilian Iranqhe - MEYA JIJI LA ARUSHA.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
View attachment 3317260

Kwa kauli hizi, inathibitisha wazi kabisa kwamba Mbunge wa Arusha Mjini Bw. Mrisho Gambo atakuwa amekuwa akiwabana Sana hawa Watu kwenye madili yao haramu ya Ufisadi.
Japokuwa Mimi binafsi siwakubali hawa Watu wote wawili, Gambo na Paul Makonda, lakini kutokana na hizo kauli zao inaonyesha wazi kabisa kwamba hawa Watu Wana ajenda zao za Siri zilizofichwa nyuma ya pazia. Kwa kawaida kwenye Ofisi nyingi sana za Umma (Ofisi za Serikali) yule mtu ambaye anapinga Ufisadi, mfichua maovu au asiyetaka kuungana na Magenge haramu ya Wapiga madili huwa anahesabika kuwa ni Mtu mkorofi, mtu mgomvi, Mtu asiyekuwa na ushirikiano na wenzake, n.k. Watu wa namna hii kwa kawaida huwa wanabambikiwa tuhuma mbalimbali za uwongo na kuwapachika au kuwa-brand Majina mabaya mabaya ili waonekane kuwa ni Watu wasiofaa mbele ya Jamii. Hii ni kawaida kabisa kutokea huko kwenye Ofisi za Serikali. Ni Ugomvi wa maslahi binafsi!
Mrisho Gambo awe makini Sana kwenye Mgogoro huu, asipokuwa mwangalifu anaweza akahujumiwa hata kwa kuwekewa sumu. Magenge ya Wahalifu Wapiga Madili kwenye Ofisi za Serikali huwa yanakuwa yana nguvu kubwa sana, pia huwa yanakuwa na mitandao mikubwa Sana ya Watu.

Siyo Watu wote kabisa wanaomchukia Marehemu Rais Magufuli walikuwa Watu Wasafi, la hasha, kundi kubwa zaidi la Watumishi wa Umma ambao wamekuwa wakimchukia JPM hasa ni wale Wahalifu, Mafisadi, wezi na wapiga madili ya Ufisadi ambao walizigeuza Ofisi za Umma kuwa Pango la Walanguzi!
 
Kwa kauli hizi, inathibitisha wazi kabisa kwamba Mbunge wa Arusha Bw. Mrisho Gambo atakuwa amekuwa akiwabana Sana hawa Watu kwenye madili yao haramu ya Ufisadi.
Japokuwa Mimi binafsi siwakubali hawa Watu wote wawili, Gambo na Paul Makonda, lakini kutokana na hizo kauli zao inaonyesha wazi kabisa kwamba hawa Watu Wana ajenda zao za Siri zilizofichwa nyuma ya pazia.
Kwa nini sasa kaomba radhi bungeni baada ya kuambiwa aende mbele ya kamati ya maadili kuonesha huo ufisadi na uongo wa waziri?
 
Ka Gambo ni kaswahili sana kale kajamaa,Sema Makonda nae niyeye anateswa na Jimbo hana lolote..
 
“Si kwamba namtetea Makonda lakini katika sakata lao hili, Gambo ndie anaemchokoza Makonda, Gambo ana ugomvi na kila kiongozi anayekuja Arusha, alikuwa na ugomvi na viongozi waliopita wakina John Mongela, Kennani Kihongozi hata mimi hayuko sawa na mimi” Maximilian Iranqhe - MEYA JIJI LA ARUSHA.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
View attachment 3317260
Hawa wote wamekutana ni wapuuzi na upuuzi wao wanauthibisha hadharani kwani wangeweza kuitana kwenye vikao lakini wanaviziana kuaibishana kenye mikutano ya hadhara.
 
Kwa nini sasa kaomba radhi bungeni baada ya kuambiwa aende mbele ya kamati ya maadili kuonesha huo ufisadi na uongo wa waziri?

Ukisoma vizuri na kwa umakini hiyo comment yangu uliyonukuu utaweza kunielewa vizuri. Nimesema kwamba Magenge ya Wapiga madili ya Ufisadi yana mtandao wao mkubwa sana. Elewa maana ya 'kuwa na Mtandao mkubwa sana!'
 
Ukisoma vizuri na kwa umakini hiyo comment yangu uliyonukuu utaweza kunielewa vizuri. Nimesema kwamba Mitandao ya Wapiga madili ya Ufisadi yana mtandao wao mkubwa sana. Elewa maana ya 'kuwa na Mtandao mkubwa sana!'
Kama hawezi mapambano akae kimya sasa anajidhalilisha tu!
 
Kama hawezi mapambano akae kimya sasa anajidhalilisha tu!

Kupambana na Magenge ya Wapiga madili ya Ufisadi katika Ofisi za Serikali ni kazi ngumu Sana, tena ni kazi yenye hatari kubwa sana kupita kiasi. JPM yuko wapi leo hii??

JPM enzi za Utawala wake akiwa bado yupo hai, mara kwa mara alisikika akilalamika Sana kwamba "waTanzania mniombee, kuna Watu wanaona kuwa Mimi ninakwamisha mambo yao." Usifikiri kwamba malalamiko haya ya Rais JPM yalikuwa ni ya uwongo, yana Ukweli kwa kiasi kikubwa Sana.
 
Ukiwa huna akili kubwa huwezi jua kuwa Gambo anaonewa na hao wezi. Gambo anasimamia haki za wananchi
 
Kwa nini sasa kaomba radhi bungeni baada ya kuambiwa aende mbele ya kamati ya maadili kuonesha huo ufisadi na uongo wa waziri?
Gambo kaomba radhi kwa woga wa kuikabili kamati kwa sababu wote wanaokwenda huko wanaangukia pua, lazima Kamati itaegemea upande wa Serikali tu kama ilivyokuwa kwenye sakata la Bashe na Luhaga Mpina, na pia kumbuka kupambana na mkwe wa Rais ni kujiweka katika mazingira magumu kuelekea mchakato wa kupitisha majina ya wagombea Ubunge.
 
Back
Top Bottom