Meya Arusha

Namsikitikia na kumuonea sana huruma bwana gaudens Lyimo..........hata mimi jana kwenye uwanja wa stadium arusha nilishuhudia alivyodhalilika.......baada ya watu wote meza kuu kutambulishwa na yeye akiwa meza hiyohiyo akaachwa.......ni aibu kwani Meya ni mtu mkubwa sana ndani ya manispaa. hili nilishaliona tena mahali pengine.......alitambulisho kwa cheo cha diwani tu na si meya, siku hiyo alihuzunika sana na ikabidi akaondoka kabla ya wakati. Huyu jamaa anateseka kwa ajili ya maslahi ya wengine............lakini ajue kwamba yeye ni Gaudens na wengine ni wao........kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe!!!
 
UNAJUA PORTI he knows very well that where he is does not belong to him kwa hivyo anaongopa sana. Wa Arusha watammaliza.

Hawezi kabisa kwanza hapo alipo anahakika na maisha yake. ATOKE TUU kama anajipenda maisha yake. Atakufa kisilensa tuu huyo MEYA wa Arusha. Mchagga anakiburi sana. ALINDE TUU KITI CHA CCM LAKINI ATAKUFA TUU KISILENSA MUDA SIO MREFU Subiri uone.

Ndugu yangu, mbona unazungumza kwa ukali kana kwamba hatima ya maisha yake i mikononi mwako!
 
Nchi ikiongozwa na mafisadi ndio matatizo yake. Hivi kweli huyu meya bado anatafuna pesa za walipa kodi wakati hakuchaguliwa kihalali, je, serikali inahitaji raia wachukue sheria mikononi mwao?
 
Wanafunzi Suye hatarini


na Grace Masha, Arusha


amka2.gif
CHOO katika shule ya Msingi Suye kata ya Kimandolu jijini Arusha kiko hatarini kudidimia baada ya kuchakaa na kuta zake kuweka ufa hali inayohatarisha maisha ya wanafunzi wanaokitumia.
Hali hiyo imesababisha wazazi katika kikao chao cha Machi 30, mwaka huu, kuomba shule hiyo ifungwe mpaka kitakapokamilika choo kingine kilichokuwa kikijengwa na kampuni ya ukandarasi ya Gaimo inayomilikiwa na Meya wa jiji hilo, Gaudense Lyimo, ambacho ujenzi wake umesimama tokea mwezi Desemba mwaka jana.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Geoge Peter akizungumza na gazeti hili alithibitisha kuwepo kwa hali hiyo ambapo alisema kuwa amekuwa akiwasiliana na uongozi wa halmashauri ili kulipatia ufumbuzi hasa baada ya ujenzi huo kusimama.
Alisema kuwa mwezi Agosti mwaka jana alitoa taarifa kwenye ofisi ya mkurugenzi juu ya uchakavu wa choo hicho ambapo mhandisi wa Majengo, J. Nguvumali alifika kukikagua na kuthibitisha kwa maandishi kuwa choo hicho kimeanza kudidimia kutokana na uchakavu hivyo akaamuru wasikitumie.
Peter alisema kuwa baada ya hapo ilipatikana kampuni ya ukandarasi ya Gaimo ambayo ilianza ujenzi wa choo kingine mwishoni mwa mwezi Agosti lakini tangu mwezi Desemba mwaka jana ujenzi umesimama ukiwa umefikia hatua ya kuanza kupauliwa ambapo alipofuatilia aliambiwa anasubiri malipo ili aweze kumalizia ujenzi huo.
Alisema kuwa walikifunga choo hicho mwezi Agosti mwaka jana ambapo walimu na wanafunzi walikuwa wakitumia choo cha kimoja chenye matundu manne lakini hali ilikuwa mbaya wanafunzi walikuwa wakijisaidia kwenye maeneo mbalimbali ya shule jambo alilohofia kuwa linaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa.
Mwalimu mkuu huyo alisema kuwa ilipofika Januari mwaka huu baada ya kuona ujenzi umesimama waliamua kufungua baadhi ya vyoo hivyo ili wanafunzi wavitumie ingawa ni hatari sana lakini wanafunzi 1,042 kutumia matundu manne ni vigumu.
Kwa upande wake mkurugenzi wa jiji la Arusha, Estomih Chang’a, alikiri kufahamu tatizo hilo ambapo alisema kuwa kwa sasa wako kwenye mchakato wa kulishughulikia huku akikataa kuzungumzia suala hilo kwa undani.
Hata hivyo mhandisi wa majengo, Nguvumali akizungumza na gazeti hili alikiri kufahamu juu ya uchakavu wa choo na kuwa tayari kuna ujenzi wa choo kingine cha matundu 10 kitakachogharimu kiasi cha shilingi milioni 35 hadi kukamilika.


:whoo::whoo::whoo::whoo::angry:
 
Wewe ndiye unakurupuka kwa kutokuwa na taarifa sahihi.mkutano wa kwanza wa manispaa ulifanyika tarehe 17. 12 .2010. Madiwani wote wa CCM, CDM waliapishwa . Walipotaka kuanza agenda ya uchaguzi, ulizuka mjadala kuhusu uhalali wa Mary Chatanda wa CCM na Mgodo wa Chadema. Ilimchukua hadi jioni kupata ufafanuzi kuhusu uhalali wa hao madiwani wawili. Ilipotimia saa mojarra usiku na taa kuzimika, mkutano uliahirishwa hadi tarehe 18 Yaani kesho Yale na kola diwani alipewa barua yenye kueleza saa na mahali. Siku ya siku madiwani wa ccm na wa tlp walihudhulia. Madiwani wa cdm walisusia wakidhani wanawakomoa wenzao wa ccm kumbe wanajikomoa wenyewe. Cdm wanaujua ukweli huu ndiyo maana hawakwenda mahakamani, kwa kujia kuwa watashindwa. Ni vizuri kabla hujajibu hoja ni vizuri ukafanya utafiti, vinginevyo utabaki kuutukana ukweli. No research no right to speak!
 
Wewe ndiye unakurupuka kwa kutokuwa na taarifa sahihi.mkutano wa kwanza wa manispaa ulifanyika tarehe 17. 12 .2010. Madiwani wote wa CCM, CDM waliapishwa . Walipotaka kuanza agenda ya uchaguzi, ulizuka mjadala kuhusu uhalali wa Mary Chatanda wa CCM na Mgodo wa Chadema. Ilimchukua hadi jioni kupata ufafanuzi kuhusu uhalali wa hao madiwani wawili. Ilipotimia saa mojarra usiku na taa kuzimika, mkutano uliahirishwa hadi tarehe 18 Yaani kesho Yale na kola diwani alipewa barua yenye kueleza saa na mahali. Siku ya siku madiwani wa ccm na wa tlp walihudhulia. Madiwani wa cdm walisusia wakidhani wanawakomoa wenzao wa ccm kumbe wanajikomoa wenyewe. Cdm wanaujua ukweli huu ndiyo maana hawakwenda mahakamani, kwa kujia kuwa watashindwa. Ni vizuri kabla hujajibu hoja ni vizuri ukafanya utafiti, vinginevyo utabaki kuutukana ukweli. No research no right to speak!

Sawa akidi ilitimia, alipata kuwa ngapi kati ya hiyo akidi?
 
hata mimi niliona jamani ilikuwa mbaya sana. sijui kwanni diwani wetu mzuri hivyo anakubali kudhalilika namna hiyo na wakati alikuwa anakubalika kwenye jamii sana tuna. shida inakuja baada ya kuchakachuliwa tu ninaimani angepata kialali umeya leo hii angefurahia kiti chake. ingekuwa vipi ningemshauri haachane na hicho kiti kabisa ili awe huru.
 
Mimi ni mkazi wa Arusha. Huyo uliyemwona ni Gaudence Lyimo,diwani wa moshono. Sio meya wa Arusha maana hakuna meya huku. Tamko la maaskofu wa hapa Ar walisema hawamtambui na hawatampa ushirikiano. Kwa hiyo wasingeweza kumtambulisha pale..

Gaudence Lymo Diwani wa Oloirien na sio wa Moshono.
 
Uungwana ni kutambua hali ikoje, ajiuzulu kisha agombee tena ili Kama atapata kwa njia halali heshima yake itarudi. Kibiri cha ki CCM kitaendelea kumnyima heshima.
Kama CCM wangelikuwa werevu wa kufahamu mema na mabaya wengi wangejiuzulu kama EL na leo hii tusingekuwa tunalalamikia kero na matatizo ya serikali yetu. Tanzania isingekuwa na mabonde ya uvuli wa mauti kama ilivyo sasa.
 
Back
Top Bottom