Mbatizaji Mkuu
Member
- Jul 19, 2020
- 39
- 128
MEYA JUMA RAIBU MWIBA MKALI KISIASA MOSHI
Nilianza kumfuatilia huyu kijana, Mwanasiasa machachari na mpenda maendeleo Ndugu Juma Raibu ambaye ni Diwani wa Kata ya Bomambuzi iliyopo Manispaa ya Moshi na ni Mstahiki Meya wa Moshi Mjini.
Ngoja nimzungumzie kidogo, Huyu kijana ana nyota ya kipekee, Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kilimanjaro na kisha akagombea Udiwani Kata ya Bomambuzi na kushindwa Uchaguzi wa Udiwani mwaka 2015 akakata rufaa na baada ya kipindi kifupi akashinda rufaa na Uchaguzi ukaitishwa tena Akashinda kwa Kishindo.
Katika kipindi hiko madiwani wa CCM walikua watatu tu. Kati ya Madiwani 27 wa Chadema ambapo madiwani hao wa CCM ni Ndugu Priscus Tarimo ambaye kwa Sasa ni Mbunge, Ndugu Masiu ambaye kwa sasa ni Mjumbe wa Kamati ya fedha na Uchumi katika Baraza la Madiwani, na Juma Raibu ambaye kwa Sasa ni Meya wa Manispaa ya Moshi.
Baada ya hapo alitumikia wananchi na wakamuelewa akapata nafasi ingine kwa awamu ingine ya 2020.
Wakati wa kuomba Ridhaa ya kuteuliwa kuwa Meya waliomba wanachama 7 na jina lake pekee ndilo lilirudi na kutawadhwa kuwa Meya. Ambapo pia Mikoa kama Dar, Dodoma na Arusha wapo wagombea walirudishwa pekee katika uchaguzi huo kwa historia yao ya Uchapaji wa kazi.
Juma Raibu yupo katika vita kubwa sana, Vita ya kumuangusha kisiasa, Juma ni mwiba mkali sana kwa watu wanaocheza na mali za umma. Kwa aina yake ya Uongozi na Misismamo yake kwa wananchi hatobaki salama. Ni dhahiri ukichagua upande wa wanyonge na ukasimama katika haki zao wanyonyaji watakuondoa tu,
Na sasa Juma Raibu anapitia katika njia hiyo. Chama cha Mapinduzi na Serikali ambayo ndio waajiri wake inapaswa kumlinda na kumtia moyo kwa maana huyu kiongozi ni Hazina ya nchi.
Juzi nimeona Gazeti moja likiandika "MEYA AKALIA KUTI KAVU" Tena ukurasa wa mbele kwa maandishi Makubwa. Niliposoma niliona ni hadithi ya Kufikirika. Eti Meya ashiriki sherehe ya mashoga. (Wanaume wanaoshiriki mapenzi ya jinsia Moja) Mwandishi hajathibitisha hiyo sherehe ilikua ni ya Mashoga, Mwandishi amehoji watu kwa maswali ya close ended question (Swali linalohitaji jibu bila Maelezo) Unamuuliza shekh "Ikiwa Meya na ni Muislam kashiriki hafla ya Mashoga je ni sahihi?" Je jibu la huyo Shekh unategemea liweje?
Nimefuatilia juu ya Sherehe hii nilichogundua Sherehe ilikua ni ya Mfanyabishara anayetambulika kwa Jina la Faustin Kolesia Maarufu kama Msukuma, Huyu ni Msukuma Mwenyeji wa Geita. Alikua anafanya sherehe ya kufungua mwaka wa Biashara zake ikiambatana na sherehe yake ya kuzaliwa.
Ok embu tuseme Sherehe ni ya mashoga. Katika hiyo sherehe Alialikwa Diwani wa eneo hili anayetambulika kwa jina la Masiu na alimtuma mwakilishi wake, Je Diwani naye ni Mshiriki wa Mashoga? Na je mwakilishi wake ni Shoga?
Alialikwa Mwenyekiti wa Mtaa huo anayetambulika kwa jina la Kideko na alitoa Salamu katika sherehe hiyo je? Mwenyekiti huyo naye ni Shoga?
Alialikwa Katibu wa CCM wa Eneo hlo aitwaye Tedy, Je katibu huyo naye ni Mshiriki wa Mashoga? Pia alikuwepo mjumbe wa Serikali za mitaa wa mtaa huo na wananchi mbalimbali.
Juma Raibu alishiriki Sherehe hiyo kama mwananchi na si kama Meya, Je Gazeti hilo lilithibitisha wapi kuwa Meya kaalikwa kwenye Birthday kwa kofia ya Meya. Juma Raibu ni kawaida yake kuhudhuria sherehe za watu katika Jamii.
Kwanza mimi ningekua mmoja wa Madiwani wa Manispaa ya Moshi ningeshinikiza kufunguliwe kesi dhidi ya Gazeti hilo kwa kudhalilisha Ofisi ya Meya. Haiingii akilini Gazeti liandike story ya kuchafua taswira ya kiongozi halafu wakae kimya.
Pili Shekh aliyetajwa katika Gazeti hilo na kuzungumza kama Bakwata inabidi athibitishe aliyoongea kama alithibitisha hilo au aombe Radhi kwa kutumia Taasisi ya Dini kwa Maslahi ya watu wengine. Kwa maaba hata Dini yake imezungumzia juu ya kuhukumu kwa kuthibitisha.
Kilochonishangaza Gazeti la Jana limeandika tena Viongozi wa Dini wa Kikristo wamezungumzia hili, Na niliposoma ndani amehojiwa mchungaji wa Mtaani na kusimama kuzungumzia kwa niaba ya viongozi wa Dini. Hii ni mbaya kwa kuhusisha viongozi wadini katika mpango wa Ovu. Baraza la Viongozi wa Dini za kikristo tazameni hili linaharibu Taswira ya Kanisa.
Nimejaribu kutafuta hata kipande cha Video cha sherehe hiyo ili nione hao mashoga mpaka sasa sijakipata kama kuna mwenye nacho nakihitaji kwa gharama yeyote. Nataka kumuona huyu Meya akiunga mkono hao Mashoga kama inavyoandikwa.
Mwisho niseme kwamba, Mungu akiamua kumsimamisha mtu wake katikati ya watu wengi hakuna wa kumuondoa.
Nikiri Juma Raibu ni Mwiba mkali kisiasa na kwa wafujaji wa mali za umma ndani ya Moshi.
Jacob Marewa
Mchambuzi wa Siasa na Uchumi.
Nilianza kumfuatilia huyu kijana, Mwanasiasa machachari na mpenda maendeleo Ndugu Juma Raibu ambaye ni Diwani wa Kata ya Bomambuzi iliyopo Manispaa ya Moshi na ni Mstahiki Meya wa Moshi Mjini.
Ngoja nimzungumzie kidogo, Huyu kijana ana nyota ya kipekee, Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kilimanjaro na kisha akagombea Udiwani Kata ya Bomambuzi na kushindwa Uchaguzi wa Udiwani mwaka 2015 akakata rufaa na baada ya kipindi kifupi akashinda rufaa na Uchaguzi ukaitishwa tena Akashinda kwa Kishindo.
Katika kipindi hiko madiwani wa CCM walikua watatu tu. Kati ya Madiwani 27 wa Chadema ambapo madiwani hao wa CCM ni Ndugu Priscus Tarimo ambaye kwa Sasa ni Mbunge, Ndugu Masiu ambaye kwa sasa ni Mjumbe wa Kamati ya fedha na Uchumi katika Baraza la Madiwani, na Juma Raibu ambaye kwa Sasa ni Meya wa Manispaa ya Moshi.
Baada ya hapo alitumikia wananchi na wakamuelewa akapata nafasi ingine kwa awamu ingine ya 2020.
Wakati wa kuomba Ridhaa ya kuteuliwa kuwa Meya waliomba wanachama 7 na jina lake pekee ndilo lilirudi na kutawadhwa kuwa Meya. Ambapo pia Mikoa kama Dar, Dodoma na Arusha wapo wagombea walirudishwa pekee katika uchaguzi huo kwa historia yao ya Uchapaji wa kazi.
Juma Raibu yupo katika vita kubwa sana, Vita ya kumuangusha kisiasa, Juma ni mwiba mkali sana kwa watu wanaocheza na mali za umma. Kwa aina yake ya Uongozi na Misismamo yake kwa wananchi hatobaki salama. Ni dhahiri ukichagua upande wa wanyonge na ukasimama katika haki zao wanyonyaji watakuondoa tu,
Na sasa Juma Raibu anapitia katika njia hiyo. Chama cha Mapinduzi na Serikali ambayo ndio waajiri wake inapaswa kumlinda na kumtia moyo kwa maana huyu kiongozi ni Hazina ya nchi.
Juzi nimeona Gazeti moja likiandika "MEYA AKALIA KUTI KAVU" Tena ukurasa wa mbele kwa maandishi Makubwa. Niliposoma niliona ni hadithi ya Kufikirika. Eti Meya ashiriki sherehe ya mashoga. (Wanaume wanaoshiriki mapenzi ya jinsia Moja) Mwandishi hajathibitisha hiyo sherehe ilikua ni ya Mashoga, Mwandishi amehoji watu kwa maswali ya close ended question (Swali linalohitaji jibu bila Maelezo) Unamuuliza shekh "Ikiwa Meya na ni Muislam kashiriki hafla ya Mashoga je ni sahihi?" Je jibu la huyo Shekh unategemea liweje?
Nimefuatilia juu ya Sherehe hii nilichogundua Sherehe ilikua ni ya Mfanyabishara anayetambulika kwa Jina la Faustin Kolesia Maarufu kama Msukuma, Huyu ni Msukuma Mwenyeji wa Geita. Alikua anafanya sherehe ya kufungua mwaka wa Biashara zake ikiambatana na sherehe yake ya kuzaliwa.
Ok embu tuseme Sherehe ni ya mashoga. Katika hiyo sherehe Alialikwa Diwani wa eneo hili anayetambulika kwa jina la Masiu na alimtuma mwakilishi wake, Je Diwani naye ni Mshiriki wa Mashoga? Na je mwakilishi wake ni Shoga?
Alialikwa Mwenyekiti wa Mtaa huo anayetambulika kwa jina la Kideko na alitoa Salamu katika sherehe hiyo je? Mwenyekiti huyo naye ni Shoga?
Alialikwa Katibu wa CCM wa Eneo hlo aitwaye Tedy, Je katibu huyo naye ni Mshiriki wa Mashoga? Pia alikuwepo mjumbe wa Serikali za mitaa wa mtaa huo na wananchi mbalimbali.
Juma Raibu alishiriki Sherehe hiyo kama mwananchi na si kama Meya, Je Gazeti hilo lilithibitisha wapi kuwa Meya kaalikwa kwenye Birthday kwa kofia ya Meya. Juma Raibu ni kawaida yake kuhudhuria sherehe za watu katika Jamii.
Kwanza mimi ningekua mmoja wa Madiwani wa Manispaa ya Moshi ningeshinikiza kufunguliwe kesi dhidi ya Gazeti hilo kwa kudhalilisha Ofisi ya Meya. Haiingii akilini Gazeti liandike story ya kuchafua taswira ya kiongozi halafu wakae kimya.
Pili Shekh aliyetajwa katika Gazeti hilo na kuzungumza kama Bakwata inabidi athibitishe aliyoongea kama alithibitisha hilo au aombe Radhi kwa kutumia Taasisi ya Dini kwa Maslahi ya watu wengine. Kwa maaba hata Dini yake imezungumzia juu ya kuhukumu kwa kuthibitisha.
Kilochonishangaza Gazeti la Jana limeandika tena Viongozi wa Dini wa Kikristo wamezungumzia hili, Na niliposoma ndani amehojiwa mchungaji wa Mtaani na kusimama kuzungumzia kwa niaba ya viongozi wa Dini. Hii ni mbaya kwa kuhusisha viongozi wadini katika mpango wa Ovu. Baraza la Viongozi wa Dini za kikristo tazameni hili linaharibu Taswira ya Kanisa.
Nimejaribu kutafuta hata kipande cha Video cha sherehe hiyo ili nione hao mashoga mpaka sasa sijakipata kama kuna mwenye nacho nakihitaji kwa gharama yeyote. Nataka kumuona huyu Meya akiunga mkono hao Mashoga kama inavyoandikwa.
Mwisho niseme kwamba, Mungu akiamua kumsimamisha mtu wake katikati ya watu wengi hakuna wa kumuondoa.
Nikiri Juma Raibu ni Mwiba mkali kisiasa na kwa wafujaji wa mali za umma ndani ya Moshi.
Jacob Marewa
Mchambuzi wa Siasa na Uchumi.