Meya Arusha

Meya Arusha

Mumwi

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2011
Posts
592
Reaction score
122
Leo katika ibada ya ijumaa kuuya moja wa madhehebu iliyofanyika katika uwanja wa shekh Abed jijini Arusha na mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa mkoa wa Arusha Isidori Shirima pia kulikuwa na viongozi mbalimbali wa serikali, vyama vya siasa, maaskofu na wachungaji.
Cha kushangaza ni kwamba meya wa Arusha alikuwepo lakini hata kutambulishwa hakutambulishwa wakati viongozi wengine walitambulishwa kwa majina kweli inaonyesha ni jinsi gani huyu meya hakubaliki yaani ni afadhali angekaa nyumbani kuliko kuja hapo maana watu wasiomjua hawakujua Kama meya alikuwepo na alikaa meza kuu nawailisha.
 
UNAJUA PORTI he knows very well that where he is does not belong to him kwa hivyo anaongopa sana. Wa Arusha watammaliza.

Hawezi kabisa kwanza hapo alipo anahakika na maisha yake. ATOKE TUU kama anajipenda maisha yake. Atakufa kisilensa tuu huyo MEYA wa Arusha. Mchagga anakiburi sana. ALINDE TUU KITI CHA CCM LAKINI ATAKUFA TUU KISILENSA MUDA SIO MREFU Subiri uone.
 
Uungwana ni kutambua hali ikoje, ajiuzulu kisha agombee tena ili Kama atapata kwa njia halali heshima yake itarudi. Kibiri cha ki CCM kitaendelea kumnyima heshima.
 
Leo katika ibada ya ijumaa kuuya moja wa madhehebu iliyofanyika katika uwanja wa shekh Abed jijini Arusha na mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa mkoa wa Arusha Isidori Shirima pia kulikuwa na viongozi mbalimbali wa serikali, vyama vya siasa, maaskofu na wachungaji.
Cha kushangaza ni kwamba meya wa Arusha alikuwepo lakini hata kutambulishwa hakutambulishwa wakati viongozi wengine walitambulishwa kwa majina kweli inaonyesha ni jinsi gani huyu meya hakubaliki yaani ni afadhali angekaa nyumbani kuliko kuja hapo maana watu wasiomjua hawakujua Kama meya alikuwepo na alikaa meza kuu nawailisha.

Watu wenye akili zao wanajua kuwa kumtabulisha huyu jamaa kungeharibu shughuli yote. Nafikiri hali hii aliyonayo huyu meya ndiyo inayomkuba mkuu wa nchi hasa ukiwa unajua fika kuwa hukupatikana kihalali, yaani wewe ni product ya chakachua. Uongozi ni kuongoza watu, katika nchi za demokrasia ya kweli huyu meya angekaa pembeni kwa sababu hana public support, ila katika nchi ya kuone vyeo ni ulaji ni dhahiri anang'ang'ania kwa masilahi binafsi tu. Ndiyo maana Tanzania under CCM hatutaenda popote zaidi ya kurudia pre-colonial era stage, maana kuna baadhi ya barabara za rami mijini zilijengwa na wakoloni na tokea waondoke zimeachwa na kurudia hali yake ya kabla ya kujengwa.
 
Alikuwa nyuma ya viongozi wengine ndo maana alikaa meza kuu.

Anasubili nguvu ya umma ije imuwajibishe? Asubili tu, siku zake za kung'oka mbona za-hesabika.
 
Hahahaha Hiyo kali wanaogopa angezomewa na shughuli yote ingetibuka inaelekea mkoa wanataka mambo yawekwe swa ni wakubwa na UVCCM na CCM wanlazimisha maskini anaishi maisha magumu sana,anaonekana ana hofu kuu ya maisha yake na familia vake
 
Mi simtambui km meya, then nawasiwasi na siasa zake!
 
Nimemkumbuka mwalimu wangu alipenda kusema "soma usisome, sikiliza usisikilize lakini mshahara wangu uko palepale"!
Huyu meya anapokea mshahara na posho za vikao na 2015 atapata marupurupu yote ya meya mstaafu!! Ila hatafanya kazi yoyote kama meya.
 
Huyu meya kawekwa na vigogo kwa maslahi yao, hivyo kujiondoa hawezi maana anaweza kuuawa na hawa jamaa kama walivyofanya kule Iringa.
 
Huyu Meya hakuchaguliwa kihalali,ss Kama angetambulishwa mbele ya wananchi mambo yangeharibika wangebaki wenyewe.Tulio Arusha tunataka uchaguzi wa Meya mjini Arusha urudiwe sivyo tutafanya vile tunafikiri.Na huyu Nape kusema uchaguzi hautarudiwa yeye ni nani hata aishinde nguvu ya umma iliyochoshwa na viongozi wabovu!?Tena hatutaki kumuona huku.
 
Suala la umeya wa Arusha limefkia mwisho. Cdm mlichemsha kwa kususia mkutano halali. Hanna la kufanya maana hata mahakamani mmechelewa poleni.
 
Watu wenye akili zao wanajua kuwa kumtabulisha huyu jamaa kungeharibu shughuli yote. Nafikiri hali hii aliyonayo huyu meya ndiyo inayomkuba mkuu wa nchi hasa ukiwa unajua fika kuwa hukupatikana kihalali, yaani wewe ni product ya chakachua. Uongozi ni kuongoza watu, katika nchi za demokrasia ya kweli huyu meya angekaa pembeni kwa sababu hana public support, ila katika nchi ya kuone vyeo ni ulaji ni dhahiri anang'ang'ania kwa masilahi binafsi tu. Ndiyo maana Tanzania under CCM hatutaenda popote zaidi ya kurudia pre-colonial era stage, maana kuna baadhi ya barabara za rami mijini zilijengwa na wakoloni na tokea waondoke zimeachwa na kurudia hali yake ya kabla ya kujengwa.

Amekuwa nuksi, aindende Ng'ende kwa waganga.:spy:
 
Mimi ni mkazi wa Arusha. Huyo uliyemwona ni Gaudence Lyimo,diwani wa moshono. Sio meya wa Arusha maana hakuna meya huku. Tamko la maaskofu wa hapa Ar walisema hawamtambui na hawatampa ushirikiano. Kwa hiyo wasingeweza kumtambulisha pale..
 
Suala la umeya wa Arusha limefkia mwisho. Cdm mlichemsha kwa kususia mkutano halali. Hanna la kufanya maana hata mahakamani mmechelewa poleni.
Mkutano gani tulisusia?,mbona unakurupuka?Chadema walielekezwa sehemu tofauti ya uchaguzi na kwingine ccm wakafanya uchaguzi peke yao bila kufuata utaratibu. Usiandike kitu huna uhakika nacho
 
Back
Top Bottom