Embu tujaribu kuzi'mordenize' kidogo ziendane na maisha ya kileo.
. . . Lisemwalo lipo kama halipo . . . HALIPO.
. . . Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu, lakini hakosi KUJINASUA.
. . . Pole pole YACHELEWESHA.
. . . Dawa ya moto ni MAJI.
. . . Fuata nyuki UTOLEWE MANUNDU.
. . . Kawia UCHELEWE.
. . . Mgeni njoo MWENYEJI AINGIE GHARAMA.
. . . Samaki mmoja akioza MTUPE.
. . . Ukitaka uzuri SHARTI ULIPIE.
. . . Ukitaka cha uvunguni SOGEZA KITANDA.
. . . .
nazi advance mordenize hizi zako lol
lisemwalo lipo kama halipo...huo ni umbea
ndege mjanja akinaswa na tundu bovu si mjanja tena.
dawa ya moto ni fire extinguisher maji huzidisha moto.
Fuata nyuki ukajifunze kuchangarika.
ukitaka uzuri ni sawa ila usiwe wa kichina.
Lol
Bandu Bandu ndugu yake Patel Sasa Yuko India
Zimwi likujualo Hilo lazima linafugwa na mzee wa busara nyumba ya pili
Asiyefunzwa na mamaye.. Mama yake ni kilaza
samaki mkunje mpaka akome
kidole kimoja kikiwa cha Kati ni matusi