Ahsante kwa ushauri mzuri dada Lizzy.
Ahsante sana.
Ningependa kukusahisha kuwa silalamiki juu ya tatizo langu anymore,kuna kipindi fulani nililalamika lakini sasa najitambua hivyo katika thread hii sijalalamika pia.
Ni kweli Volunteer,field na ajira nimeshindwa kupata kutokana na tatizo langu.
Nataka kukomboa cheti baada ya kupata watu wenye uelewa juu ya ajira maalumu za serikali,ambapo wapo willing kunisaidia kuapply ajira hizo ndiyo maana nataka nipate cheti niweze kufanya mchakato huo,hatimaye ajira iweze kunikomboa kimaisha.
Vilevile kujiendeleza kielimu nitahitaji cheti hiko pia.
Mimi si mnyonge,nina amani sana even licha ya kuwa na hili tatizo nilipata marafiki wenye busara walionisaidia kujitambua zaidi na najitambua sana.
Kipindi fulani nilikata tamaa ya kuendelea na masomo,it was Wakonta na Aneth gerana walioniinspire kukaza moyo hadi nikarudi shuleni na kumaliza masomo.
Nakiri Wakonta hakuwahi kuwa mnyonge,she was always bright,thats why aliniinspire sana.
Wakati mwingine maisha yalinisukuma kulalamika na kuwa mnyonge kwa sababu...katika hali ya kawaida kuwa rejected kwa kosa ambalo halikuwa kusudi lako inaumiza pia,mimi ni binadamu tu hisia ninazo.
.hali halisi ya maisha mfano kulala na njaa,kula mlo mmoja,kulala sehemu isiyo salama,kuugua na kuonekana like si kitu si mtu hata kwa familia yako mwenyewe haya yalipelekea kuwa dhaifu sana kiasi nisimudu vibarua vya kutumia nguvu,miguu inaishiwa nguvu,kutetemeka mikono na kizunguzungu kikali.
Hivyo ni baadhi ya vitu vilivyoninyima amani na kunifanya niwe vile(kulalamika sana) lakini sasa silalamiki tena.
Suala la kujiajiri ni kipaumbele changu pia,lakini sina kitu kwa sasa kuweza kujiajiri nimefanya juhudi nyingi na jitihada nyingi sana lakini sijafanikiwa.
Kadhalika napambana sana dada natamani mafanikio ya watu kama Wakonta na Aneth,wapo wengi wa aina hii waliofanikiwa na wanaoendelea na mapambano.
Lakini hawakufanikiwa peke yao,kama ilivyo kwangu nipo peke yangu si ndugu si marafiki,hii inaniwia ugumu lakini si sababu ya mimi kuacha kupambana,bado najaribu.
Ndio maana nipo hapa leo,silalamiki bali najaribu kujikwamua.