Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,187
- 670
hivi kweli haya yanaweza kutokea ndani ya nchi yetu?
hivi watanzania kudhalilishwa na kugeuzwa panya wa maabara ndani ya nchi yao ndani ya hospitali tunazoziheshimu tena bila ya haya mchana ni uungwana huu?
jee serikali imepanga kuwachukulia hatua gani hawa waliohusika na haya?
au ndio limeisha ?
Wajaribiwa dawa ya UKIMWI kinyume na maadili
Habari Zinazoshabihiana
Na Joseph Lugendo
MBUNGE wa Karatu, Dkt. Wilbroad Slaa (CHADEMA), amesema Watanzania 64 walifanyiwa majaribio ya utafiti wa dawa ya UKIMWI aina ya Virodene Po 58, katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam na kwenye zahanati iliyokuwa inamilikiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu, Bw. Omar Mahita kinyume na maadili.
Dkt. Slaa jana bungeni aliitaka Serikali kutaja chombo ambacho kilitoa kibali cha majaribio ya aina hiyo kwa Watanzania, wakati dawa hiyo ilikuwa imepigwa marufuku Afrika Kusini ilikotengenezwa.
Aidha, Mbunge huyo pia aliitaka Serikali kueleza hatua ambazo zimechukuliwa dhidi ya Watanzania wakiwamo wanajeshi walioingiza dawa hizo na kufafanua kama waliofanyiwa majaribio hayo walilipwa
fidia.
Akijibu hoja hizo, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Aisha Kigoda, alikiri kufanyika kwa majaribio hayo na kufafanua kwamba yalifanyika kinyume na taratibu za utafiti.
Dkt. Kigoda alisema ombi la kibali cha kufanya utafiti huo liliwasilishwa katika Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Julai 2000 na baada ya tathmini ya taasisi hiyo, ombi hilo likakataliwa.
Alisema kukataliwa kwa ombi hilo kulisababishwa na matokeo ya tathmini hiyo yaliyoonesha kuwa utafiti huo ulikuwa na upungufu wa kisayansi na kimaadili.
Kwa mujibu wa Dkt. Kigoda, baada ya kukataliwa kwa ombi hilo, wanasayansi hao waliamua kuingiza dawa hizo bila kibali cha Serikali na kufanya utafiti katika Hospitali ya Lugalo na wakati huo huo kuanza kuziuza dawa hizo kiholela.
Dkt. Kigoda alisema Agosti, 2001 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ilipata habari ya kufanyika kwa vitendo hivyo na kuamua kutoa agizo la kusitisha utafiti, kuwafukuza watafiti wahalifu, kuzuia uingizwaji wa dawa hizo na kuzirejesha dawa zilikotoka.
Hata hivyo, Dkt. Kigoda hakufafanua zaidi juu ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya Watanzania wakiwamo wanajeshi ambao walihusika kuingiza dawa hizo na kufanya utafiti huo, lakini akashauri Watanzania waliohusishwa katika utafiti huo, kufuata taratibu za sheria iwapo watataka kulipwa
fidia.
majira
hivi watanzania kudhalilishwa na kugeuzwa panya wa maabara ndani ya nchi yao ndani ya hospitali tunazoziheshimu tena bila ya haya mchana ni uungwana huu?
jee serikali imepanga kuwachukulia hatua gani hawa waliohusika na haya?
au ndio limeisha ?
Wajaribiwa dawa ya UKIMWI kinyume na maadili
Habari Zinazoshabihiana
Na Joseph Lugendo
MBUNGE wa Karatu, Dkt. Wilbroad Slaa (CHADEMA), amesema Watanzania 64 walifanyiwa majaribio ya utafiti wa dawa ya UKIMWI aina ya Virodene Po 58, katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam na kwenye zahanati iliyokuwa inamilikiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu, Bw. Omar Mahita kinyume na maadili.
Dkt. Slaa jana bungeni aliitaka Serikali kutaja chombo ambacho kilitoa kibali cha majaribio ya aina hiyo kwa Watanzania, wakati dawa hiyo ilikuwa imepigwa marufuku Afrika Kusini ilikotengenezwa.
Aidha, Mbunge huyo pia aliitaka Serikali kueleza hatua ambazo zimechukuliwa dhidi ya Watanzania wakiwamo wanajeshi walioingiza dawa hizo na kufafanua kama waliofanyiwa majaribio hayo walilipwa
fidia.
Akijibu hoja hizo, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Aisha Kigoda, alikiri kufanyika kwa majaribio hayo na kufafanua kwamba yalifanyika kinyume na taratibu za utafiti.
Dkt. Kigoda alisema ombi la kibali cha kufanya utafiti huo liliwasilishwa katika Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Julai 2000 na baada ya tathmini ya taasisi hiyo, ombi hilo likakataliwa.
Alisema kukataliwa kwa ombi hilo kulisababishwa na matokeo ya tathmini hiyo yaliyoonesha kuwa utafiti huo ulikuwa na upungufu wa kisayansi na kimaadili.
Kwa mujibu wa Dkt. Kigoda, baada ya kukataliwa kwa ombi hilo, wanasayansi hao waliamua kuingiza dawa hizo bila kibali cha Serikali na kufanya utafiti katika Hospitali ya Lugalo na wakati huo huo kuanza kuziuza dawa hizo kiholela.
Dkt. Kigoda alisema Agosti, 2001 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ilipata habari ya kufanyika kwa vitendo hivyo na kuamua kutoa agizo la kusitisha utafiti, kuwafukuza watafiti wahalifu, kuzuia uingizwaji wa dawa hizo na kuzirejesha dawa zilikotoka.
Hata hivyo, Dkt. Kigoda hakufafanua zaidi juu ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya Watanzania wakiwamo wanajeshi ambao walihusika kuingiza dawa hizo na kufanya utafiti huo, lakini akashauri Watanzania waliohusishwa katika utafiti huo, kufuata taratibu za sheria iwapo watataka kulipwa
fidia.
majira