Mkuu nadhani hujanielewa. Issue sio kukojoa isu ni kushindwa kudumu na msichana jamani. Nifanyeje nisimchoke?
Well,...
sometimes yawezekana tatizo haliko kwako......
Labda wao ndo wanajiweka katika hali za kuchokwa,...sio wabunifu,....wana bweteka.......etc.
Lakini kwa upande mwingine ni wewe mwenyewe,
haujawahi penda bali unatamani tu.
Ndo maana ukisha maliza hamu yako unahisi kumchoka na haraka unaona mwingine na kutamani
kuwa nae ukizani atakuwa wa tofauti.
Nimekuwa na mchumba wangu tunae tarajia kufunga ndoa karibuni kwa miaka 6 sasa,...
ana mapungufu mengi kama vile nilivo na mapungufu mengi vile vile lakini tume vumiliana
maana UPENDO WA KWELI HUVUMILIA.
Napenda kutumia biblia kama kiongozi wangu katika kujenga hoja hapa.
1Wakorinto 4-8:
Mungu anaongelea kuhusu upendo wa kweli,.....
Mwenye upendo huvumilia,hufadhili,mwenye upendo hana wivu,hajidai,wala hajivuni.
Mwenye upendo hakosi adabu,hatafuti faida yake binafsi,wala hana wepesi wa hasira; haweki kumbukumbu ya mabaya
,hafurahii uovu,bali hufurahia ukweli.
Mwenye upendo wa kweli huvumilia yote,huamini yote,na hustahimili yote.
Upendo hauna kikomo kamwe.................
2Timetheo 2:22
Jiepushe na tamaa za ujana,fuata uadilifu,imani,upendo,amani pamoja na watu
wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo msafi
Yako meeengi ya kuongelea,ila kutokana na wewe mwenyewe naweza sema hayo mawili.
Ila kwa kiwango kikubwa wewe ndo utakuwa chanzo.
Lakini yawezekana pia umri wako ukawa mdogo ndo maana unashindwa kumvumilia mtu maana
ukipiga mahesabu hata mda wako wa kuoa bado uko mbali sana.
Ukiona hivo tulia,usiwe na haraka ya kumtafuta umpendae na ukimpata kubali
kwanza kabisa kwama HANA KILA UNACHO TAKA,....lakini ukumbuke pia kwamba
HAUNA KILA ANACHO TAKA.
Jifunze kumzoea,mvumilie,....onyaneni,...fundishaneni,....pongezaneni na
mwisho wa siku utajikuta unakuwa na mke mwema ambae anakujua vyema na
una mjua vyema pia.
Nionavyo mimi,ukiendelea hivyo unaweza kufika mda wako wa kuoa na kwakua
hautakua na mtu uliye kuwa nae karibu aka kufahamu vyema na ukamfahamu,...
unaweza kutana na mtu MIEZI MITATU (3) na kutangaza ndoa..........
Ndoa kama hizi mmmmmh,sidhani kama zinadumu maana umekutana na mtu
aliye ishi miaka 25 hukooooo anako jua yeye,na unajidai ndani ya miezi mi3
ume mfahamu na unataka kumuamini mkae nae kweli?
Tulia kaka,tengeneza future yako sasa.
Nita kutafuta kwa ukaribu zaidi pia,if you don't mind me disturbing you.