Memory

Memory

Comment yako imenipa majonzi. Maskini njoo mama nikufariji ndugu yangu
Ndio hali yangu kila siku
Furaha kidogo majonzi na mawazo mengi...
Kwakweli sikuwahi kuwaza kama kweli angekufa hivi karibuni japo nlijua kifo kipo.
Jumamosi kuna mtu alinionea na kunishout sana bila sababu za msingi yaaani sijui hata niliwaza nini nikamkumbuka mama yangu kwamba angekuwepo tungeongeaaaa angenipozaa hadi niwe poa... ila ndo hvo hayupo tena....nililia siku nzima.
 
Me machoz yangu kila siku ni kwa mama yangu... sikuwah kudhani mama yangu angeniacha mapema yote hii. Na kero zote hizi za dunia Leo sina pa kufafijiwa bila unafiki najifariji mwenyewe
Pole sana mpendwa
 
Mtoto wa baba. wengine hawaelewi how you feel kwa kuwa wanahisi baba hana thamani kama ya mama ila me nakuelewa kwa kuwa nimelelewa na baba, Pole mkuu

Kwa wale waliopatwa na hali hiyo nadhani wana picha hali jinsi inavyokuwa. Lakini nalo nadhani inategemea unaachwa na wazazi ktk umri gani.

Hebu fikiria unafiwa na mzazi mmoja wapo ukiwa labla shule au chuo ni tofauti na yule aliyefiwa na mzazi wake wakati akiwa mtu mzima ana kazi yake na maisha yake.

Hebu fikiria ukaondokewa na baba yako mzazi aliyekuwa anakupenda sana hadi wewe mwenyewe ukajua unapendwa. Unabaki na mama ambaye sasa ni mjane na siku moja anakuomba pesa (na sio kawaida yake kukuomba pesa) na wewe ukawa huna pesa hizo kwa wakati huo utajisikiaje
 
Ndio hali yangu kila siku
Furaha kidogo majonzi na mawazo mengi...
Kwakweli sikuwahi kuwaza kama kweli angekufa hivi karibuni japo nlijua kifo kipo.
Jumamosi kuna mtu alinionea na kunishout sana bila sababu za msingi yaaani sijui hata niliwaza nini nikamkumbuka mama yangu kwamba angekuwepo tungeongeaaaa angenipozaa hadi niwe poa... ila ndo hvo hayupo tena....nililia siku nzima.
Hali kama hiyo ikikukuta swali au sali Mungu atakutia nguvu. Mimi nilikuwa nikilia kuna watoto waliachwa wadogo na mama yao kwa ajali ya mv.bukoba wakawa wananiambia unalia nini umeachwa na una familia? Toka wakati huo huwa namshukuru Mungu kwa kila jambo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom