Membe: Ngeleja ni tishio urais 2015

Membe: Ngeleja ni tishio urais 2015

Kwani amelipa deni analodaiwa na umma la escrow??? anapesa yetu yule alipe kwanza na achukue form.bring back our money ngeleja
 
kama unawaza Ngeleja kuwa Rais; basi wewe sio MTANZANIA SAFI kama unavyojiita
 
Tunakoelekea hata Chenge na yeye ataomba kugombea uraisi.
 
Kama kweli wewe ni Mtanzania Safi basi nilitegemea umnadi mtu msafi. Nilitegemea umnadi rais mtarajiwa mwenye kufuata sheria na taratibu. Nilitegemea umnadi mtu mwenye kuheshimu taratibu na watu wengine. Si huyu huyu Ngeleja unayempigia debe leo aliyekataa kufuata utaratibu wa foreni kwenye ATM na hata alipofuatwa na mlinzi akimwelezea kuwa ni vema awasubiri waliotangulia alimtukana na kusababisha mlinzi kufukuzwa kazi na boss wake. Kweli huyu ndo unataka tumpe uraisi. Mtu asiyeheshimu wenzake. Mtu asiye heshimu taratibu. Mtu asiyeajari wenzie tena walioonesha kufuata sheria za kazi na ufanya kazi uliotukuka. Kwasababu ya cheo unamwambia boss wake kama hatamfukuza yeye ataona kitakachompata. Asiye jua kuwa cheo ni dhamana. Endelea kupiga debe ila sidhani kama hilo litawezekana kwa 2015.
 
Last edited by a moderator:
His excellency president William mganga ngeleja.watanzania Haaaaaaaahaaaaa.mwambie achukue fomu asiogope akili za watanzania ni dynamics
 
Ama kweli nchi hii haina mwenyewe (unclaimed property) mwandishi wa hii post unaweza kutusaidia Ngeleja alipokuwa waziri wa nishati na madini kwa karibu miaka mitano alitufanyia nini Watanzania cha kutufanya tumkumbuke. Kwa kipindi chote alichokuwepo pale alitusaidia nini katika sekta ya madini na alitusaidia lipi katika sekta ya nishati hata leo tufikirie kumpa nafasi ya juu kabisa katika nchi. Tusileteane utani hapa Urais si lele mama, Urais ni zaidi ya ving'ola na misururu ya magari, Urais ni zaidi ya kukagua gwaride na kuchezewa ngonjera. Urais ni pamoja na kuumia wananchi wanapokwenda hospitali na kukosa dawa, Urais ni pamoja na kusononeka pale basi linapo pata ajali na kuua watu zaidi ya 30 kwa mara moja, Urais ni pamoja na kuumia pale Albino wanapouawa hovyo na kukatwa viungo vyao. Urais ni pamoja na kutegua kitendawili cha wafadhili wanapoamua kusitisha misaada ya kibajeti, Urais ni pamoja na kukabiliana na mafisadi na wala rushwa wakubwa wanaoiteketeza nchi. Urais ni mzigo mzito unaohitaji busara za ziada.

MH.WILLIUM MGANGA NGELEJA SULUHISHO BORA MADINI

Itakumbukwa kuwa sekta ya nishati na madini ilishawah kukaliwa na nawazir wengi mno wakuwemo kina Mzee Msabaha,Mzee Daniel Yona na wengine wengi tuu,lakini hao wote walikuwa wanaishia kuwa katika wizara hiyo kwa muda wa miaka 2 na nusu na muda mwingine miwili kamili, ni mawazir watatu tuu akiwemo mh.Rais Kikwete pamoja na mh.Willium Mganga Ngeleja ndio waliokaa kwa muda mrefu kulingana na ugumu wa wizara hiyo,Mh.Kikwete alikaa miaka 6 na mh.Willium Mganga Ngeleja alikaaa miaka 5 na miez 8 kitu kinachoonyesha upambanaj mkubwa kwenye wizara hii na mh.Ngeleja, kwaukweli mambo aliyoyafanya yatabaki kuwa msaada mkubwa kwa Tanzania yetu,yafuatayo ni baadhi ya mambo ambayo mh.Ngeleja aliyafanya alipokuwa ktk wizara ya Nishat na Madini ikiwa ni kwa muda wa miaka 5 na miez 8,:-

1.Itakumbukwa kuwa Ngeleja ndiye aliyepambana kwa hali na mali mpk kuhskikisha kunapatikana maeneo zaidi kwa ajili ya wachimbaji wadogowadogo.

2.Itaendelea kukumbukwa kuwa ngeleja ndie muasisi wa utaratibu wa mfuko maalum wa kuwasaidia wadogo nchini kitu ambacho kinazungumzwa na wachimbaji wadogo mpaka leo,na hata juzi nilipokuwa ziarani Geita nilipata kutembelea maeneo ya wachimbaji wadogo na walimtaja Ngeleja kama mkombozi wao,na daima wataendelea kumtukuza kwa anachokifanya kwani anafanya mambo mazur anapokabiziwa majukum ya kijamii.

3.Mwezi April 2010 mh.Ngeleja alipiga marufuku usafirishaji nje ya nchi wa madini ghafi ya Tanzanite yenye ukubwa unaozidi gramu1,kitu ambacho juzi nilivyokuwa nazungumza na baadhi ya mawazir na baadhi ya viongoz wa juu wa chama walikipenda na kusema Ngeleja anafaa kuingia wazir mkuu wa Tanzania au hata Raisi kama akiamua kugombea

4.Mh.Ngeleja ndie muasisi wa utaratibu wa kutoa hati ya uasili(certificate of origin) kwa wanaouza madini ya Tanzanite nje ya nchi ikiwa ni mkakati wa serikali kudhibiti uuzwaji haramu wa madini ya Tanzanite,kitu amabcho hata Prof.Muhongo anajivunia sasa na kipindi fulani hivi ktk ziara yake mererani yanapopatikana madini ya Tanzanite mh.Muhongo alimtaja Ngeleja kama msaada mkubwa katika hilo...

Mwisho
Watanzania tunapaswa kuwasemea watu kwa mabaya yao na mazuri yao yalio mengi kwani hakuna mwanadam aliye kamili,..Ngeleja kafanya mengi sana sekta ya madini na hayo hapo juu ni kwa uchache wake.
 
MTOA MADA APELEKWE MIREMBE KWA SABABU hata si mtanzania. kama angekuwa mtanzania angejua Ngeleja huyu ni mwizi wa ESCROW KULINGANA NA TAARIFA YA CAG. HATA HUYU MTOA MADA HAKUMBUKI HUYU JAMAA ALIKUWA WAZIRI WA NISHATI NA ALIFANYA MGAWO KUWEPO NCHI NZIMA. AT LEAST MUHONGO. MPAKA AKAFUKUZWA UWAZIRI HETI NDIO UNAMPENDEKEZA TENA? UMECHOKA SANA NA WEWE NINA UHAKIKA NI FEKI NA HUNA NDOTO NA NCHI YETU.
 
Ngeleja yupi? Huyu huyu wa escrow au mwingine? Huyu ni fisadi aliyekubuhu kuanzia wakati wa Jairo hadi sasa. Hafai. Hafai. Hafai. Period!
 
Jamani ivi kweli kuna watu km hawa Tz anamuingelea Ngeleja yupi huyu? Ila mu naona ameleta huu uzi ili aone watu wanasemaje na yawezakuwa ni ndugu wa ngeleja hivyo nimwambie tu aende akamwambie ndugu yake asijaribu hata kujisumbua,alikuwa waziri nishati na madini Kang'atuka kwa kashfa,esrow yumo ivi vp huyu ebu tujaribu kupima kabla ya kuleta uzi binafsi simtaki kwa gharama yoyote!!!
 
Hata kama ndio ulitumwa au tumiwa na timu Ngeleja ulete ujumbe hapa JF ungekuwa na wewe uko smart kidogo basi ungechanganya na akili zako badala ya kusikika kama kasuku tu.

Watu wengine bwana mbona mnapenda kujivua nguo wenyewe mbele ya khadham nasi kubwa kama hii ya JF? Hata kama ndio kuwa umepokea mshiko wa watu? Hovyooo!
 
Back
Top Bottom