Kingcobra
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 1,000
- 309
Wakubwa,
Katika mahojiano niliyoyasikia kupitia Kituo cha ITV Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Uhusiano wa Kimataifa Mhe. Membe alieleza pamoja na mambo mengine kusikitishwa kwake na namna baadhi ya watu wanavyodharau na kuiita dhaifu serikali ya awamu ya nne ambayo anadai imechaguliwa na wananchi. Mhe. Membe alisema ni kosa kubwa kufanya hivyo na akapinga tabia ya kuihusisha serikali na kila udhaifu au hali mbaya ya kimaisha inayoikumba nchi na wanachi wake.
My take:
(1) Heshima ya serikali kutoka kwa wanachi inatokana na matendo ya serikali yenyewe kwa wanachi wake. Heshima kamwe hailazimishwi kutolewa. Na kama ikilazimishwa hiyo siyo heshima. Neno dhaifu halikuwahi kutumika kwa marais wa awamu ya kwanza, pili na ya tatu. Hali inayoashiria kwamba awamu hii imevuka kiwango cha kutowajibika kwa kiwango stahili.
(2) Serikali iliyopo madarakani ndiyo inaweka mipango na kuamua viwango vya kodi wanayotozwa wananchi kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo ya wananchi wanaochangia kodi. Wananchi wanapoona maendeleo hayapatikani pamoja na rasilimali zilizopo wamlaumu nani kama siyo serikali!!? Kwa ujumla, ni vigumu kutenganisha hali ngumu ya maisha na utendaji wa serikali.
Katika mahojiano niliyoyasikia kupitia Kituo cha ITV Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Uhusiano wa Kimataifa Mhe. Membe alieleza pamoja na mambo mengine kusikitishwa kwake na namna baadhi ya watu wanavyodharau na kuiita dhaifu serikali ya awamu ya nne ambayo anadai imechaguliwa na wananchi. Mhe. Membe alisema ni kosa kubwa kufanya hivyo na akapinga tabia ya kuihusisha serikali na kila udhaifu au hali mbaya ya kimaisha inayoikumba nchi na wanachi wake.
My take:
(1) Heshima ya serikali kutoka kwa wanachi inatokana na matendo ya serikali yenyewe kwa wanachi wake. Heshima kamwe hailazimishwi kutolewa. Na kama ikilazimishwa hiyo siyo heshima. Neno dhaifu halikuwahi kutumika kwa marais wa awamu ya kwanza, pili na ya tatu. Hali inayoashiria kwamba awamu hii imevuka kiwango cha kutowajibika kwa kiwango stahili.
(2) Serikali iliyopo madarakani ndiyo inaweka mipango na kuamua viwango vya kodi wanayotozwa wananchi kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo ya wananchi wanaochangia kodi. Wananchi wanapoona maendeleo hayapatikani pamoja na rasilimali zilizopo wamlaumu nani kama siyo serikali!!? Kwa ujumla, ni vigumu kutenganisha hali ngumu ya maisha na utendaji wa serikali.