OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 437
* Hotuba ilibadilishwa uwanjani
* Makonda aficha kwapani hotuba
Kweli alipangalo Mungu sio alipangalo mwanadamu na siku zote mipango sio matumizi. Hii imekuja kujidhirisha katika tamasha la pasaka lililofanyika jana ambapo lengo mficho la tamasha limeshindwa kutimia.
Tamasha hilo ambalo lilifanyiwa promosheni ya nguvu liliishia kupata watu kidogo, hali iliyopelekea mgeni rasmi kuchelewa kuingia uwanjani badala ya kuingia saa 9 aliingia saa 11 jioni.
Mgeni rasmi ambaye alikuwa Waziri Membe alipanda jukwaani saa 11 na robo badala ya saa 10 kamili kama ilivyokuwa imepangwa kwenye ratiba.
Vituko vilijitokeza wakati wa kumuita mgeni rasmi jukwaani ambapo aliitwa mgeni rasmi Membe na wakati huo huo kukiendelea na maonyesho ya sarakasi ambapo watu waliishia kuangalia sarakasi na hivyo kumlazimu mgeni rasmi Membe kusimamishwa kwa zaidi ya dakika 20 jukwaani bila ya utaratibu wowote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya zaidi kwa mgeni rasmi Membe ambaye aliambatana na Dc wa kinondoni, Paul Makonda kwa kutoshangiliwa wakati wakitambulishwa hali iliyomlazimu Membe kubadili mwelekeo wa dhamira mficho wa shughuli hiyo.
Membe alishauriwa na Makonda asitishe zoezi lake la kutangaza nia na hapo ndipo Membe alipoamua kubadilisha hotuba yake na kubuni ya amani kwa vijana badala ya ile ya kutangaza nia na kuishia kula keki ambayo iliandaliwa kwa ajili ya kujipongeza kwa tukio la kutangaza nia lililo gonga ukuta.
Kitendo kile cha kushindwa kutangaza nia kutokana na uwepo wa watu wachache uwanjani pamoja na kukosekana kwa shangwe nyingi kwa Membe uwanjani vilimnyima sana raha Membe na wakati wote alikuwa amepooza na mwenye msongo wa mawazo hadi kushindwa kwenda kuungana kucheza na mwimbaji wa kimataifa Rebecca Malope kama alivyokuwa akiombwa mara kwa mara na mc wa shughuli hiyo.
Membe alitumia jumla ya Tsh. milioni 30 kwa tamasha hilo ili aje atangaze nia lakini akagonga ukuta na haijajulikana ni lini tena atapanga kutangaza nia kwani mpaka sasa upepo wa kisiasa sio mzuri kwake.
* Makonda aficha kwapani hotuba
Kweli alipangalo Mungu sio alipangalo mwanadamu na siku zote mipango sio matumizi. Hii imekuja kujidhirisha katika tamasha la pasaka lililofanyika jana ambapo lengo mficho la tamasha limeshindwa kutimia.
Tamasha hilo ambalo lilifanyiwa promosheni ya nguvu liliishia kupata watu kidogo, hali iliyopelekea mgeni rasmi kuchelewa kuingia uwanjani badala ya kuingia saa 9 aliingia saa 11 jioni.
Mgeni rasmi ambaye alikuwa Waziri Membe alipanda jukwaani saa 11 na robo badala ya saa 10 kamili kama ilivyokuwa imepangwa kwenye ratiba.
Vituko vilijitokeza wakati wa kumuita mgeni rasmi jukwaani ambapo aliitwa mgeni rasmi Membe na wakati huo huo kukiendelea na maonyesho ya sarakasi ambapo watu waliishia kuangalia sarakasi na hivyo kumlazimu mgeni rasmi Membe kusimamishwa kwa zaidi ya dakika 20 jukwaani bila ya utaratibu wowote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya zaidi kwa mgeni rasmi Membe ambaye aliambatana na Dc wa kinondoni, Paul Makonda kwa kutoshangiliwa wakati wakitambulishwa hali iliyomlazimu Membe kubadili mwelekeo wa dhamira mficho wa shughuli hiyo.
Membe alishauriwa na Makonda asitishe zoezi lake la kutangaza nia na hapo ndipo Membe alipoamua kubadilisha hotuba yake na kubuni ya amani kwa vijana badala ya ile ya kutangaza nia na kuishia kula keki ambayo iliandaliwa kwa ajili ya kujipongeza kwa tukio la kutangaza nia lililo gonga ukuta.
Kitendo kile cha kushindwa kutangaza nia kutokana na uwepo wa watu wachache uwanjani pamoja na kukosekana kwa shangwe nyingi kwa Membe uwanjani vilimnyima sana raha Membe na wakati wote alikuwa amepooza na mwenye msongo wa mawazo hadi kushindwa kwenda kuungana kucheza na mwimbaji wa kimataifa Rebecca Malope kama alivyokuwa akiombwa mara kwa mara na mc wa shughuli hiyo.
Membe alitumia jumla ya Tsh. milioni 30 kwa tamasha hilo ili aje atangaze nia lakini akagonga ukuta na haijajulikana ni lini tena atapanga kutangaza nia kwani mpaka sasa upepo wa kisiasa sio mzuri kwake.