Membe akwama kutangaza nia

Membe akwama kutangaza nia

mleta uzi ingependeza ungeweka hapa copy ya hiyo hotuba ya kutangaza nia ili watu waamini kile ulichoandika. Wachangiaji wengi wanaona kama hii habari ni umbeya Fulani toka kwa team nyingine ya mgombea. Ungeondoa huo utata kwa kuweka copy ya hotuba iliyowekwa kwapani


Nataka nikuhakikishie ndugu yangu hapa kuna paradox ya hali ya juu. Watu wanayodai kwamba wamebung'aa wajumbe 1900 wa mkutano Mkuu na wajumbe 270 wa NEC ndiyo hawa unaowaona wanaokota thread chovu na kujaribu kutengeneza uongo ambao hata bure watu hawaupokei. Membe jana hakuwa na mpango wa kutangaza nia, LABDA KAMA WANAZUNGUMZIA NIA YA KUOKOKA maana kwa mwenye akili anajua kwamba mkusanyiko ule ulikuwa ni maalum kwa ajili ya kumtukuza Mungu na siyo kupiga siasa uchwara kama wao ambao pre-occupation yao ni siasa hata kama wako makaburini. Ndiyo maana wanaandaa birthday na kugeuza jukwaa la kujitakasa na kupiga siasa.

wangetuonyesha hiyo hotuba ili kweli tuone kama ili lengo jambo hilo. Lakini hupati shida kuona kwamba Uzi huu ni matokeo ya hasira na ghadhabu za kualikwa Membe kwenye tamasha hili wakidhani kwamba angelitumia kisiasa. Ndo maana walikusanya waganga ili mvua inyeshe shoo iharibike baada ya jaribio Lao la kutaka kuleta vurugu kudhibitiwa ndo wanahamishia hasira zao jukwaani.

Jamani nyie si washindi? Malalamiko na spinning ya kijinga ya nini? Wenye akili wanajua!
 
Jukwaa hili sasa lina watu wanakumbakumba tu habari na kutupia. Kambi zenu za kutafuta u-rais zisituvurugie jukwaa.
 
Hii habari imepikwapikwa sana...ila ukweli ni kwamba membe hakubaliki na hafai kuwa rais
 
Lowasa na Membe wanapoteza muda CCM imemuandaa Stephen Wasira, wako nae busy wanaandaa Ilani ya Chama. Wakizinduka wanakuta Kamati Kuu imemaliza kazi yake.
 
Kazi waliyo nayo CCM mwaka huu anaeijua mwanzo na mwisho wake ni shetani peke yake.
 
Yaan huu Ni upuuzi mtupu maana kama Ni chuki mmezidi nyie team mafisadi maana unachopost Ni upuuzi
 
Mara saa 9, mara saa 10...anyway labda uko sahihi!

Enhee tuambie habari hii inatufundisha nini!!??
 
* Hotuba ilibadilishwa uwanjani

* Makonda aficha kwapani hotuba

Kweli alipangalo Mungu sio alipangalo mwanadamu na siku zote mipango sio matumizi. Hii imekuja kujidhirisha katika tamasha la pasaka lililofanyika jana ambapo lengo mficho la tamasha limeshindwa kutimia.

Tamasha hilo ambalo lilifanyiwa promosheni ya nguvu liliishia kupata watu kidogo, hali iliyopelekea mgeni rasmi kuchelewa kuingia uwanjani badala ya kuingia saa 9 aliingia saa 11 jioni.

Mgeni rasmi ambaye alikuwa Waziri Membe alipanda jukwaani saa 11 na robo badala ya saa 10 kamili kama ilivyokuwa imepangwa kwenye ratiba.

Vituko vilijitokeza wakati wa kumuita mgeni rasmi jukwaani ambapo aliitwa mgeni rasmi Membe na wakati huo huo kukiendelea na maonyesho ya sarakasi ambapo watu waliishia kuangalia sarakasi na hivyo kumlazimu mgeni rasmi Membe kusimamishwa kwa zaidi ya dakika 20 jukwaani bila ya utaratibu wowote.

Mambo yalizidi kuwa mabaya zaidi kwa mgeni rasmi Membe ambaye aliambatana na Dc wa kinondoni, Paul Makonda kwa kutoshangiliwa wakati wakitambulishwa hali iliyomlazimu Membe kubadili mwelekeo wa dhamira mficho wa shughuli hiyo.

Membe alishauriwa na Makonda asitishe zoezi lake la kutangaza nia na hapo ndipo Membe alipoamua kubadilisha hotuba yake na kubuni ya amani kwa vijana badala ya ile ya kutangaza nia na kuishia kula keki ambayo iliandaliwa kwa ajili ya kujipongeza kwa tukio la kutangaza nia lililo gonga ukuta.

Kitendo kile cha kushindwa kutangaza nia kutokana na uwepo wa watu wachache uwanjani pamoja na kukosekana kwa shangwe nyingi kwa Membe uwanjani vilimnyima sana raha Membe na wakati wote alikuwa amepooza na mwenye msongo wa mawazo hadi kushindwa kwenda kuungana kucheza na mwimbaji wa kimataifa Rebecca Malope kama alivyokuwa akiombwa mara kwa mara na mc wa shughuli hiyo.

Membe alitumia jumla ya Tsh. milioni 30 kwa tamasha hilo ili aje atangaze nia lakini akagonga ukuta na haijajulikana ni lini tena atapanga kutangaza nia kwani mpaka sasa upepo wa kisiasa sio mzuri kwake.
Hivi kweli membe anawashauri kweli jamani huyu membe mropokaji anataka urais uwiiiiiiii, hakika Lowasa atosha
 
Yaani..nani anamdanganya Membe kuwa atapata URAIS...!? Namwonea huruma...hv hata yeye Membe hajaona upepo unaelekea wapi...!? OMG....

Nampa pole...bcoz he has no even qualities and abilities to LEAD.....hata kidogo...!!!

Anadanganywa tu, pole yake...!!!
 
nyie mnashangaa hili, mbona dogo

CCM huwa inalipa watu wakalie msibani
 
Team Membe mnatia Huruma sana! Yaani Makonda na Nape ndo vipanga wenu? Aisee... Sikujua kama game litaishia kwenye sekunde za Mwanzo tu ... !!!!
Si kweli kwamba Membe angeweza kutangaza urais pale wakati inafahamika kuwa kwa yeye kufanya hivyo kungefungua kifungo cha Lowasa.

Mtazamo huo ni wa watu dhaifu.
Tafuta kitu kingine cha kumsema Membe

Ukweli ni kwamba Membe hana sifa za Urais wala Lowasa hana sifa za urais
Vita hii ya Lowasa ma Membe inawafanya watu washindwe kufikiria mtu wa kulikomboa taifa.

Kwa sasa mtu akitaka pesa lazima amuunge mkono Lowasa!!
 
Mkuu hebu tupe ukweli wa kilichojiri huko tamashani, hapo ndo utakuwa umepinga post ya jamaa kwa busara zaidi.
Haihitaji ushahidi hapo .
Mtu yoyote mwenye kili atajua kuwa thread hii ni ya ushabiki na kuna malipo ya Lowasa.
Mimi nashangaa Lowasa kutumia nguvu kubwa kupambana na Membe wakati Membe hana kitu
 
* Hotuba ilibadilishwa uwanjani

* Makonda aficha kwapani hotuba

Kweli alipangalo Mungu sio alipangalo mwanadamu na siku zote mipango sio matumizi. Hii imekuja kujidhirisha katika tamasha la pasaka lililofanyika jana ambapo lengo mficho la tamasha limeshindwa kutimia.

Tamasha hilo ambalo lilifanyiwa promosheni ya nguvu liliishia kupata watu kidogo, hali iliyopelekea mgeni rasmi kuchelewa kuingia uwanjani badala ya kuingia saa 9 aliingia saa 11 jioni.

Mgeni rasmi ambaye alikuwa Waziri Membe alipanda jukwaani saa 11 na robo badala ya saa 10 kamili kama ilivyokuwa imepangwa kwenye ratiba.

Vituko vilijitokeza wakati wa kumuita mgeni rasmi jukwaani ambapo aliitwa mgeni rasmi Membe na wakati huo huo kukiendelea na maonyesho ya sarakasi ambapo watu waliishia kuangalia sarakasi na hivyo kumlazimu mgeni rasmi Membe kusimamishwa kwa zaidi ya dakika 20 jukwaani bila ya utaratibu wowote.

Mambo yalizidi kuwa mabaya zaidi kwa mgeni rasmi Membe ambaye aliambatana na Dc wa kinondoni, Paul Makonda kwa kutoshangiliwa wakati wakitambulishwa hali iliyomlazimu Membe kubadili mwelekeo wa dhamira mficho wa shughuli hiyo.

Membe alishauriwa na Makonda asitishe zoezi lake la kutangaza nia na hapo ndipo Membe alipoamua kubadilisha hotuba yake na kubuni ya amani kwa vijana badala ya ile ya kutangaza nia na kuishia kula keki ambayo iliandaliwa kwa ajili ya kujipongeza kwa tukio la kutangaza nia lililo gonga ukuta.

Kitendo kile cha kushindwa kutangaza nia kutokana na uwepo wa watu wachache uwanjani pamoja na kukosekana kwa shangwe nyingi kwa Membe uwanjani vilimnyima sana raha Membe na wakati wote alikuwa amepooza na mwenye msongo wa mawazo hadi kushindwa kwenda kuungana kucheza na mwimbaji wa kimataifa Rebecca Malope kama alivyokuwa akiombwa mara kwa mara na mc wa shughuli hiyo.

Membe alitumia jumla ya Tsh. milioni 30 kwa tamasha hilo ili aje atangaze nia lakini akagonga ukuta na haijajulikana ni lini tena atapanga kutangaza nia kwani mpaka sasa upepo wa kisiasa sio mzuri kwake.
Mbona Udaku tu..Jamani tutafika kwa style hii??
 
Weka rekodi sahihi ... Hakuna vita kati ya Membe na Lowassa... Pili si heshima kumlinganisha Membe na Lowassa!!! wote tunajua Lowassa ameweza sana kuisaidia nchi hii kwenye Elimu kupitia shule za kata na UDOM, ameweza sana kuwapatia wananchi wa shinyanga na kahama maji safi na salama, ameweza sana kurejesha mnazi mmoja...ameweza kufuta mkataba wa City water ... So far membe amelifanyia nini Taifa hili? Mbona tunapigwa bit kila angle? ...

Si kweli kwamba Membe angeweza kutangaza urais pale wakati inafahamika kuwa kwa yeye kufanya hivyo kungefungua kifungo cha Lowasa.

Mtazamo huo ni wa watu dhaifu.
Tafuta kitu kingine cha kumsema Membe

Ukweli ni kwamba Membe hana sifa za Urais wala Lowasa hana sifa za urais
Vita hii ya Lowasa ma Membe inawafanya watu washindwe kufikiria mtu wa kulikomboa taifa.

Kwa sasa mtu akitaka pesa lazima amuunge mkono Lowasa!!
 
Nilisoma mahali kwamba marais wastaafu Benjamin Mkapa na Ali Hassan Mwinyi walialikwa. Je walihudhuria?
 
Back
Top Bottom