Meli ya wachina yaibua Matapeli

Meli ya wachina yaibua Matapeli

View attachment 635610
WAKATI upimaji wa afya bure ukiendelea katika meli maalumu kutoka China, baadhi ya wananchi jijini Dar es Salaam wamegeuza shughuli hiyo kuwa mtaji baada ya kuanza kuuza namba za kadi wanazopatiwa.

Aidha, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk Grace Maghembe amesema tayari watu 6,000 wamepata namba kuwawezesha kuwaona madaktari hao kwa utaratibu unaofaa.

Dk Maghembe alitoa mwito kwa wananchi ambao hawajapewa namba, kusubiri hadi waliopata namba hizo watakapohudumiwa. “Tunawaomba msiendelee kusongana; tumeshagawa namba hadi 6,000, hivyo subirini hawa wapate huduma ndipo tutaangalia kama tutaendelea kugawa namba nyingine kulingana na uwezo wa madaktari hawa,”alisema Maghembe.

Meli hiyo yenye madaktari na wataalamu wa afya zaidi ya 380 iliwasili nchini Novemba 19 na inatarajiwa kutoa huduma hiyo kwa siku tano kwa wagonjwa 600 kwa siku. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alisema amepata taarifa juu ya uwepo wa watu hao wanaofika kwenye meli hiyo kama wagonjwa wanaotaka kuhudumiwa, lakini wakipatiwa namba hizo hugeuka na kuziuza kwa Sh 5,000 hadi Sh 50,000, jambo ambalo ni kosa na kinyume na makusudio.

“Upimaji huo tulisema ni bure na ni makosa kwa mtu kununua au kuuza namba,” alisema. Alibainisha kuwa, baadhi ya wagonjwa wamebainika kutakiwa kusafirishwa kwenda China kupatiwa huduma zaidi hivyo ofisi yake itaandaa utaratibu wa kuwawezesha kusafiri.

Akaongeza, “wagonjwa hawa wanaotakiwa kusafirishwa tutaangalia utaratibu wa kuwasaidia baada ya kupata idadi kamili tutawasaidia kupata hati za kusafiria pamoja na kuangalia utaratibu wa kuwawezesha wakiwa huko kwa matibabu.”


Muungwana
Meli itakwepo kwa siku tano,madaktari kwa siku wanahudumia wagonjwa 600,Waliopata namba wapo 6000, naona hapa Hesabu imekaa vibaya maana 600×5=3000
Kwa hiyo kuanzia namba 3001 Na kuendelea warudi tu walikokuwa wanapata matibabu wakaendelee Na shughuli zao
 
TAPELI namba ni makonda na CCM
Ndio kabisa! Kaanza kwa kutapeli kuwa meli hiyo imeletwa na yeye na Magufuli ndio kalipia gharama za matibabu hayo ya bure. Huo ndio utapeli namba moja, hao wengine wanafanya vijiutapeli tuu. Ajabu mpaka leo hakuna aliye kanusha kuwa Magu kalipia matibabu hayo hivyo kiwango cha utapeli kimepanga kwenda juu zaidi
 
Meli itakwepo kwa siku tano,madaktari kwa siku wanahudumia wagonjwa 600,Waliopata namba wapo 6000, naona hapa Hesabu imekaa vibaya maana 600×5=3000
Kwa hiyo kuanzia namba 3001 Na kuendelea warudi tu walikokuwa wanapata matibabu wakaendelee Na shughuli zao
Za kuambiwa,........... bure ghari
 
Msione watu wanatembea tuu, kumbe wagonjwa wengi. Wangekuja huku mtaani wapime akili ile ya 1/4 siiamin pengne ni 5/4 kbsa
 
BINADAMU HAWANA WEMA ,PAMOJA NA JITIHADA ZOTE ANAZOFANYA MKUU WA MKOA BADO UNAMWITA TAPELI? MNYONGE MNYONGENI, HAKI YAKE MPENI ! ANASTAHILI PONGEZI KWA HILI
Kafanya jitihada gani huyo makonda zaidi ya visasi?
Unadhani hiyo meli ameileta makonda na magufuli?acheni kupotosha watu
 
BINADAMU HAWANA WEMA ,PAMOJA NA JITIHADA ZOTE ANAZOFANYA MKUU WA MKOA BADO UNAMWITA TAPELI? MNYONGE MNYONGENI, HAKI YAKE MPENI ! ANASTAHILI PONGEZI KWA HILI
Wewe kweli ngedere wachina wanasema matbabu bure Grace Mugabe anasema JPM kalipia pesa which is which
 
A
Arusha inakuja lini?? Au mnatulipiza tulivyowapiga bao kwenye Kikombe cha loliondo? Kile ndo kilikuwa chenyewe! Hadi Mugabe (jina kwa hisani ya askofu Shio wa jimbo la Zanzibar) naye hakubaki nyuma
Hiyo meli huko Arusha itapita wapi?
 
Back
Top Bottom