Heaven Ambassador
Member
- Oct 27, 2017
- 92
- 94
Umasikini ukizidi hazaa waasi wenye uzalendo~ alisema babu yule. Hakika meli ikipoteza dira mwisho wake sio mwema labda iokolewe na wasamalia wema na vipi Kama wasamalia huonekana ni waasi.
Taifa langu Tanzania~ Namkumbuka Zitto Kabwe akiwa BBC aliwahi sema ni vyema wanafunzi wajawazito wapewe nafasi ya kusoma Tena, aliekuwa raisi wakati huo alilipinga Hilo na spika wa bunge wakati huo alimuita Zitto Ni msaliti na amefanya uhaini. Hakika Zitto alionekana mbaya leo Spika huyo huyo na waziri wa juu anaunga swala Hilo nini tunajifunza hapo?
Gesi inachimbwa mtwara inasafirishwa mpaka Dar es salaam hatujaweza kuitumia kwenye mitungi kwasababu ni nyepesi mno na grade ya juu swali ni kwamba ni kweli natuwezi kuja na mfumo wa kuweza tumia gesi ile kwenye mitungi au mpaka mataifa ya nje yakaichakate huko nje wake watuuzie Tena. Kitaalamu gesi naijua na designing naifahamu nadhani hatujawekeza vya kutosha kulitatua hili na huenda hata ambao wana nafasi ya kufanya hili hawataki sumbua vichwa vyao kwani mshahara unaingia.
Mbeya Kuna madini ya niobium ambayo hutumika katika utengenezaji wa rocket, jet engine na Mambo mengine, mpaka Sasa nahakika kampuni iliyoshika kufanya kazi ile Ni ya muingereza na si Tanzania. Swali ni kwamba watalamu tulionao Tanzania wa madini Ni mwengi, kwanini Taifa hili lisiwatumie lichimbe lenyewe liuze kwa mataifa mengine?
Hakika Nyerere aliesema wazawa wasome wakomboe Taifa mnamsaliti halafu tunasherehekea uhuru, uhuru wanini?
Tunapanga kusomesha wenye Mimba ilihali Kuna sehemu Hakuna shule za msingi kwa watoto, tunadakia hili tunarukia lile. Taifa halina dira.
Kuna haja ya watu wenye uchungu na nchi hii kuangalia namna ya kufanya japo huenda ukaitwa Mhaini.
Kiwanda Cha general Tyre kiko wapi?
Kwenye dhahabu tunapigwa, gesi tunapigwa, niobium tutapigwa, mikopo ya riba tunapokea na tunatumia hovyo tutafika.
Nawambia mtaani kuna njaa Kali ikizidi Kuna kundi la Simba litatafuna kondoo wanaoongoza.
Naomba viongozi wawe na uchungu na nchi hii na ipo haja ya kuwa na mpango wa Taifa wa miaka kumi au kumi na mitano sio Kila mwaka mnapanga bajeti na Kila kiongozi anakuja na dira yake. Meli ya thamani Hakika inazama.
Siku moja njaa itazaa chuki na chuki itazaa waasi. Tuipende Tanzania.
Pumzika Mwl. Nyerere
Taifa langu Tanzania~ Namkumbuka Zitto Kabwe akiwa BBC aliwahi sema ni vyema wanafunzi wajawazito wapewe nafasi ya kusoma Tena, aliekuwa raisi wakati huo alilipinga Hilo na spika wa bunge wakati huo alimuita Zitto Ni msaliti na amefanya uhaini. Hakika Zitto alionekana mbaya leo Spika huyo huyo na waziri wa juu anaunga swala Hilo nini tunajifunza hapo?
Gesi inachimbwa mtwara inasafirishwa mpaka Dar es salaam hatujaweza kuitumia kwenye mitungi kwasababu ni nyepesi mno na grade ya juu swali ni kwamba ni kweli natuwezi kuja na mfumo wa kuweza tumia gesi ile kwenye mitungi au mpaka mataifa ya nje yakaichakate huko nje wake watuuzie Tena. Kitaalamu gesi naijua na designing naifahamu nadhani hatujawekeza vya kutosha kulitatua hili na huenda hata ambao wana nafasi ya kufanya hili hawataki sumbua vichwa vyao kwani mshahara unaingia.
Mbeya Kuna madini ya niobium ambayo hutumika katika utengenezaji wa rocket, jet engine na Mambo mengine, mpaka Sasa nahakika kampuni iliyoshika kufanya kazi ile Ni ya muingereza na si Tanzania. Swali ni kwamba watalamu tulionao Tanzania wa madini Ni mwengi, kwanini Taifa hili lisiwatumie lichimbe lenyewe liuze kwa mataifa mengine?
Hakika Nyerere aliesema wazawa wasome wakomboe Taifa mnamsaliti halafu tunasherehekea uhuru, uhuru wanini?
Tunapanga kusomesha wenye Mimba ilihali Kuna sehemu Hakuna shule za msingi kwa watoto, tunadakia hili tunarukia lile. Taifa halina dira.
Kuna haja ya watu wenye uchungu na nchi hii kuangalia namna ya kufanya japo huenda ukaitwa Mhaini.
Kiwanda Cha general Tyre kiko wapi?
Kwenye dhahabu tunapigwa, gesi tunapigwa, niobium tutapigwa, mikopo ya riba tunapokea na tunatumia hovyo tutafika.
Nawambia mtaani kuna njaa Kali ikizidi Kuna kundi la Simba litatafuna kondoo wanaoongoza.
Naomba viongozi wawe na uchungu na nchi hii na ipo haja ya kuwa na mpango wa Taifa wa miaka kumi au kumi na mitano sio Kila mwaka mnapanga bajeti na Kila kiongozi anakuja na dira yake. Meli ya thamani Hakika inazama.
Siku moja njaa itazaa chuki na chuki itazaa waasi. Tuipende Tanzania.
Pumzika Mwl. Nyerere