Melchizedek na utata unaomzunguka

Siku ukielewa kuwa Agano la kale ni kivuli cha Agano jipya utafunguka ufahamu. Hata hivyo nakushangaa wewe kwa sababu Melkizedeki kaandikwa wazi kwenye Biblia. Unakwama wapi?
Mkuu sijui umeelewa mada?? Kinachonitatiza Ni huyo Melchizedek kuelezwa kma Alikua binadamu na mfalme wa Nchi/kuhani then agano jipya anaelezwa kwamba hana baba wala mama na anaishi milele....
*Nakua curious je alikua mtu wa kawaida?
*Je yeye ndio Yesu/Mungu/Malaika fulani?
*Kwanini Yesu afananishwe naye?? Ana kitu gani special zaidi?
* kwanini biblia haijamuongelea kwa undani ilihali ana maana kubwa kiroho??

NNisaidie hapa
 
Mkuu sijui umeelewa mada?? Kinachonitatiza Ni huyo Melchizedek kuelezwa kma Alikua binadamu na mfalme wa Nchi/kuhani then agano jipya anaelezwa kwamba hana baba wala mama na anaishi milele....
*Nakua curious je alikua mtu wa kawaida?
*Je yeye ndio Yesu/Mungu/Malaika fulani?
*Kwanini Yesu afananishwe naye?? Ana kitu gani special zaidi?
* kwanini biblia haijamuongelea kwa undani ilihali ana maana kubwa kiroho??

NNisaidie hapa

Kwa nini usidhani kuwa Melkizedeki ni FATHER na siyo SON( yaani Yesu)?

Au na wewe unadhani kuwa FATHER ndiyo huyohuyo SON (Yaani Jesus)?
 
Hii ni mojawapo ya masomo ambayo nimeyapitia kwa undani kidogo. Sijui kama kuna nafasi ya kutosha. Lakini kwa ufupi niseme tu Mwandishi wa Waebrania, wa Zaburi na yule wa Mwanzo wote wanamzungumzia mtu yule yule; Yesu Kristu. Kumbuka Waebrania ina mstari mmoja muhimu sana Waeb. 13.8 ambayo inasema "Yesu Kristu ni yule yule, Jana, na leo, na hata milele". Na kama unakumbuka katika unabii wa Isaya kuhusu kuzaliwa kwa Yesu tunaambiwa kati ya majina yake mengi mojawapo ataitwa "Mfalme wa Amani"... Mfalme wa Amani ni Mfalme wa Salemu (Salemu ni "amani").

Hii ndio sababu Ibrahim alipokutana na Melkizedek alimpa fungu la kumi (kumbuka hii ilikuwa kabla ya zaka kuingizwa katika sheria za wayahudi). Ukitaka kuelewa hili rejea maneno ya Yesu ambayo anawaambia Wayahudi kuwa "Ibrahim baba yenu aliitamani kuiona siku yangu, aliiona na akafurahi (Yoh 8:56). Na utaona kuwa Yesu hamuiti Ibrahimu "baba yetu" bali "baba yenu"... Lakini pia alitoa dai moja sehemu nyingine (mistari miwili tu chini) ambalo nusura wayahudi wampige. Alisema katika mstari mwingine maarufu "Kweli kweli nawaambia" Yesu akasema, "kabla Ibrahim hajazaliwa mimi Niko" (Yoh 8:58).

Basi hapo kwa ufupi tu; ni sehemu ya tafiti yangu moja ndefu sana; labda siku moja ikimpendeza Mungu nitawashirikisha.
Mkuu kumbe upo vzuri hadi sekta za Imani..... Indeed you are a great thinker.
 
Kwa nini usidhani kuwa Melkizedeki ni FATHER na siyo SON( yaani Yesu)?

Au na wewe unadhani kuwa FATHER ndiyo huyohuyo SON (Yaani Jesus)?
Mkuu ni wapi nimesema melchizedek ni Yesu/Mungu??
Wapi nmeongelea Yesu na Mungu kuwa kitu kimoja?? Hizi assumptions unatoa wapi??

Stick kwenye mada
 
Sasa kama hoja ya uwana wa Mungu wa Yesu unatokana na roho aliye ndani yake kwa nini sasa aitwe GOD'S ONLY BEGOTTEN SON? (John 3:16 )

Nadhani neno Begotten unaelewa maana yake nini kwenye english:(Maana yake KUMZAA)

Kwa mfano hapa tunaelezwa geneology mbali mbali kwenye biblia ya Kiingereza (Mathew 1: 6-9)kwa kutumia neno begot

David the king begot Solomon by her [a]who had been the wife of Uriah. 7 Solomon begot Rehoboam, Rehoboam begot Abijah, and Abijah begot [b]Asa. 8 Asa begot Jehoshaphat, Jehoshaphat begot Joram, and Joram begot Uzziah. 9 Uzziah begot Jotham, Jotham begot Ahaz, and Ahaz begot Hezekiah.

Sasa kama Yesu ni THE ONLY BEGOTTEN SON wewe iweje utafsiri kuwa hiyo ina maanisha kuwa ni SON SIMPLY TU KWA SABABU ANA ROHO WA MUNGU NDANI?

Hoja yako ingekuwa na nguvu kama na Sisi tungekuwa BEGOTTEN SONS WA MUNGU, hiyo tungesema kuwa uSON unaozungumziwa hapa ni huo wa Kuwa na Roho ya Mungu ndani mwetu lakini iweje YESU sasa isemwe ni THE ONLY BEGOTTEN SON?, huO uONLY huohuo maana yake nini?
Inaonekana figurative language ya Bible ni changamoto!! soma 1 Peter 1:23 alafu uniambie umeelewa nini??

Ukimaliza gusia Mathew 12:47-50

Then Ufunuo 14:4

Nataka upate connection ya seed,birth and Baba figuratively
 
Kumbe kabla ya Bikira Maria yupo mwanamke mwingine aliyewahi kumleta Yesu duniani!

Maana Melkizedeki hakuibuka from nowhere lazima kwa maisha ya hapa duniani alizaliwa, hakudondoka from the sky!

Na ukuhani zama zake ulikuwa ni kwa koo, hii inamaanisha watu waliokuwepo enzi za Melkizedeki walikuwa wanaujua ukoo wake vizuri tu!

Guys let me tell you one thing:
Tatizo lilikuwepo hapa ni baadhi ya Wakiristo kuhijack mafundisho ya Kiyahudi na kujaribu kuyaposses na kuyaangalia katika miwani ya theolojia ya Ukiristo. Hata kwa yale maandiko yasiyomhusu Yesu, wanasema yanamhusu Yesu

Ni kweli kwenye Agano la kale kuna utabiri juu ya Yesu, lakini baadhi ya zile prophecy watu wanazozitumia kumhusisha Yesu wala hazimhusu Yesu kabisa

Ni watu wanajaribu kutumia akili zao tu, kutumia logic zao tu kuungaunga vitu ambavyo wala havihusiani

Ishu ya Melkizedeki na sifa alizopewa ni figurative zaidi lakini watu wanachukulia kuwa ndivyo ilivyo literary
1. Labda niulize, ni wakati gani biblia ni figurative na wakati gani bible ni Lateral??

2. Agano la kale lote linamtabiri Kristo na hata hao wayahudi ndio waliofanya hivyo ukisoma new testament imejaa citations za unabii wa Agano la kale juu ya Yesu.

3. Bible inasema melchizedek hakua na baba wala mama je wapi wamesema alikua na ukoo??

4. Book of Enock inadai hakuzaliwa na mama wala Baba sasa wapi atoe ukoo?

5. Hakuna anayetumia akili zake bali wanakusanya dots mfano sifa anazopewa melchizedek anapewa Yesu ndio maana wanajaribu kuweka ulinganisho.
Ni sawa na Yule mtoto wa Ufunuo 12 au Mpanda farasi mweupe wa Ufunuo 6 na 19?? Hajaitwa Yesu ila sifa alizopewa ni za Yesu pekee.
 
Mkuu sijui umeelewa mada?? Kinachonitatiza Ni huyo Melchizedek kuelezwa kma Alikua binadamu na mfalme wa Nchi/kuhani then agano jipya anaelezwa kwamba hana baba wala mama na anaishi milele....
*Nakua curious je alikua mtu wa kawaida?
*Je yeye ndio Yesu/Mungu/Malaika fulani?
*Kwanini Yesu afananishwe naye?? Ana kitu gani special zaidi?
* kwanini biblia haijamuongelea kwa undani ilihali ana maana kubwa kiroho??

NNisaidie hapa
Agano la kale ni kivuli cha Agano jipya. Maana yake yaliyotokea yaliakisi yatakayotokea katika Agano jipya. Mzee Mwanakijiji kaandika vema nami naandika kwa kiasi.

Tuanze na Yohana 8 ambapo Yesu alikuwa akijibizana na mafarisayo kuhusu Yeye ni nani:

Yohana 8
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁵⁶ Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.
⁵⁷ Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
⁵⁸ Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.


Hapa Yesu anatupa dokezo kuwa kuna mahali wakati Ibrahimu akiishi hapa duniani walikutana hivyo basi tukitafuta kwenye Agano la kale tutakuta mahali fulani habari ya Yesu na Ibrahimu. Twende kwenye Agano la kale:

Mwanzo 14
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁸ Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.
¹⁹ Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.
²⁰ Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.


Hapa kuna mambo matatu muhimu kumhusu Melkizedeki:
1. Alikuwa mfalme wa Salem
2. Alileta mkate na divai wakala pamoja
3. Alikuwa kuhani wa Mungu aliye juu

Ikumbukwe kuwa katika Biblia yote hakuna mwanadamu aliyetajwa kuwa mfalme na kuhani kwa wakakati mmoja isipokuwa masihi tu. Tuone andiko moja tu kwa mfano:

Zekaria 6
¹³ Naam, yeye atalijenga hekalu la Bwana; naye atauchukua huo utukufu; ataketi akimiliki katika kiti chake cha enzi; na kutakuwa na kuhani katika kiti chake cha enzi; na shauri la amani litakuwa kati ya hao wawili.


Ok, tukiangalia hayo mambo matatu, salem (shalem kwa kiebrania) sio mahali, bali ni ufafanuzi. Maana yake ni amani, hivyo alikuwa mfalme wa AMANI, sifa ambayo imetajwa kuwa nayo masihi pekee.

Isaya 9
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁶ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.


Alileta mkate na divai ambayo ni komunyo. Angalia jambo hilo lilifanyika pia kwenye Agano jipya.

Tuangalie sasa Waebrania:

Waebrania 7
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;
² ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;


Kumbe hata neno Melkizedeki sio jina kama tulivyodhania, ni maelezo tu. Melkizedeki = mfalme wa haki. Yesu ndiye atakayehukumu kwa haki, yeye ni mfalme wa haki pia mfalme wa amani.

³ hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.


Nadhani umeona parallel iliyopo kati ya Agano la kale na jipya, hicho ndicho kivuli kilichokuja kudhihirika kwa Agano jipya.

Kama hujaelewa uliza.
 
Hii ni mojawapo ya masomo ambayo nimeyapitia kwa undani kidogo. Sijui kama kuna nafasi ya kutosha. Lakini kwa ufupi niseme tu Mwandishi wa Waebrania, wa Zaburi na yule wa Mwanzo wote wanamzungumzia mtu yule yule; Yesu Kristu. Kumbuka Waebrania ina mstari mmoja muhimu sana Waeb. 13.8 ambayo inasema "Yesu Kristu ni yule yule, Jana, na leo, na hata milele". Na kama unakumbuka katika unabii wa Isaya kuhusu kuzaliwa kwa Yesu tunaambiwa kati ya majina yake mengi mojawapo ataitwa "Mfalme wa Amani"... Mfalme wa Amani ni Mfalme wa Salemu (Salemu ni "amani").

Hii ndio sababu Ibrahim alipokutana na Melkizedek alimpa fungu la kumi (kumbuka hii ilikuwa kabla ya zaka kuingizwa katika sheria za wayahudi). Ukitaka kuelewa hili rejea maneno ya Yesu ambayo anawaambia Wayahudi kuwa "Ibrahim baba yenu aliitamani kuiona siku yangu, aliiona na akafurahi (Yoh 8:56). Na utaona kuwa Yesu hamuiti Ibrahimu "baba yetu" bali "baba yenu"... Lakini pia alitoa dai moja sehemu nyingine (mistari miwili tu chini) ambalo nusura wayahudi wampige. Alisema katika mstari mwingine maarufu "Kweli kweli nawaambia" Yesu akasema, "kabla Ibrahim hajazaliwa mimi Niko" (Yoh 8:58).

Basi hapo kwa ufupi tu; ni sehemu ya tafiti yangu moja ndefu sana; labda siku moja ikimpendeza Mungu nitawashirikisha.
Nikajua wewe ni mtaalam wa uchambuzi wa Siasa kumbe uko vizuri sana hata kwenye maswala ya maandiko. Umeelezea vizuri sana
 
Agano la kale ni kivuli cha Agano jipya. Maana yake yaliyotokea yaliakisi yatakayotokea katika Agano jipya. Mzee Mwanakijiji kaandika vema nami naandika kwa kiasi.

Tuanze na Yohana 8 ambapo Yesu alikuwa akijibizana na mafarisayo kuhusu Yeye ni nani:

Yohana 8
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁵⁶ Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.
⁵⁷ Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
⁵⁸ Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.


Hapa Yesu anatupa dokezo kuwa kuna mahali wakati Ibrahimu akiishi hapa duniani walikutana hivyo basi tukitafuta kwenye Agano la kale tutakuta mahali fulani habari ya Yesu na Ibrahimu. Twende kwenye Agano la kale:

Mwanzo 14
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁸ Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.
¹⁹ Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.
²⁰ Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.


Hapa kuna mambo matatu muhimu kumhusu Melkizedeki:
1. Alikuwa mfalme wa Salem
2. Alileta mkate na divai wakala pamoja
3. Alikuwa kuhani wa Mungu aliye juu

Ikumbukwe kuwa katika Biblia yote hakuna mwanadamu aliyetajwa kuwa mfalme na kuhani kwa wakakati mmoja isipokuwa masihi tu. Tuone andiko moja tu kwa mfano:

Zekaria 6
¹³ Naam, yeye atalijenga hekalu la Bwana; naye atauchukua huo utukufu; ataketi akimiliki katika kiti chake cha enzi; na kutakuwa na kuhani katika kiti chake cha enzi; na shauri la amani litakuwa kati ya hao wawili.


Ok, tukiangalia hayo mambo matatu, salem (shalem kwa kiebrania) sio mahali, bali ni ufafanuzi. Maana yake ni amani, hivyo alikuwa mfalme wa AMANI, sifa ambayo imetajwa kuwa nayo masihi pekee.

Isaya 9
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁶ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.


Alileta mkate na divai ambayo ni komunyo. Angalia jambo hilo lilifanyika pia kwenye Agano jipya.

Tuangalie sasa Waebrania:

Waebrania 7
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;
² ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;


Kumbe hata neno Melkizedeki sio jina kama tulivyodhania, ni maelezo tu. Melkizedeki = mfalme wa haki. Yesu ndiye atakayehukumu kwa haki, yeye ni mfalme wa haki pia mfalme wa amani.

³ hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.


Nadhani umeona parallel iliyopo kati ya Agano la kale na jipya, hicho ndicho kivuli kilichokuja kudhihirika kwa Agano jipya.

Kama hujaelewa uliza.
Kunawatu mko deep yani unaelezea hadi unauona utukufu unashuka na kukufunika. Barikiwa
 
Ivi kwa nini lakini hawa waandishi walitumia lugha ya mafumboo..!!??
Vichwa panzi hapa unatoka kapaaa...!!

But why?...Whyyy??
Kusoma neno la Mungu hadi uelewe inahitaji uombe kwanza roho mtakatifu afungue fahamu zako

Hata wale wanafunzi wa Yesu kuna mda walikua hamwelew wakamwomba awatafsirie
 
Agano la kale ni kivuli cha Agano jipya. Maana yake yaliyotokea yaliakisi yatakayotokea katika Agano jipya. Mzee Mwanakijiji kaandika vema nami naandika kwa kiasi.

Tuanze na Yohana 8 ambapo Yesu alikuwa akijibizana na mafarisayo kuhusu Yeye ni nani:

Yohana 8
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁵⁶ Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.
⁵⁷ Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
⁵⁸ Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.


Hapa Yesu anatupa dokezo kuwa kuna mahali wakati Ibrahimu akiishi hapa duniani walikutana hivyo basi tukitafuta kwenye Agano la kale tutakuta mahali fulani habari ya Yesu na Ibrahimu. Twende kwenye Agano la kale:

Mwanzo 14
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁸ Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.
¹⁹ Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.
²⁰ Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.


Hapa kuna mambo matatu muhimu kumhusu Melkizedeki:
1. Alikuwa mfalme wa Salem
2. Alileta mkate na divai wakala pamoja
3. Alikuwa kuhani wa Mungu aliye juu

Ikumbukwe kuwa katika Biblia yote hakuna mwanadamu aliyetajwa kuwa mfalme na kuhani kwa wakakati mmoja isipokuwa masihi tu. Tuone andiko moja tu kwa mfano:

Zekaria 6
¹³ Naam, yeye atalijenga hekalu la Bwana; naye atauchukua huo utukufu; ataketi akimiliki katika kiti chake cha enzi; na kutakuwa na kuhani katika kiti chake cha enzi; na shauri la amani litakuwa kati ya hao wawili.


Ok, tukiangalia hayo mambo matatu, salem (shalem kwa kiebrania) sio mahali, bali ni ufafanuzi. Maana yake ni amani, hivyo alikuwa mfalme wa AMANI, sifa ambayo imetajwa kuwa nayo masihi pekee.

Isaya 9
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁶ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.


Alileta mkate na divai ambayo ni komunyo. Angalia jambo hilo lilifanyika pia kwenye Agano jipya.

Tuangalie sasa Waebrania:

Waebrania 7
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;
² ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;


Kumbe hata neno Melkizedeki sio jina kama tulivyodhania, ni maelezo tu. Melkizedeki = mfalme wa haki. Yesu ndiye atakayehukumu kwa haki, yeye ni mfalme wa haki pia mfalme wa amani.

³ hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.

Nadhani umeona parallel iliyopo kati ya Agano la kale na jipya, hicho ndicho kivuli kilichokuja kudhihirika kwa Agano jipya.

Kama hujaelewa uliza.
Mkuu naona ww na Mzee Mwanakijiji mmetegua hiki kitendawili.

Ubarikiwe sana mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom