Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,948
- 62,768
Yesu alipokuja duniani alikuja katika 4m ya mwili
Na utukufu na baadhi ya mamlaka yake aliyaacha Mbinguni...
Na hapo tunapata sababu ya yeye kujibu vile
Kwa hiyo majibu yatapatikana kwa kuweka vituo?Biblia imeandikwa kimafumbo sana...
kupata jibu la moja kwa moja ni kazi sana!
Kumbe kuna uwezekano hata hizo amri kumi zilizoandikwa ni mafumbo tofauti na tunavyozielewa?Biblia imeandikwa kimafumbo sana...
kupata jibu la moja kwa moja ni kazi sana!
Na pia kwa haraka haraka unaweza ukasema Merikizedeck ndio baba wa yesu.Hivi kwa mujibu wa maandiko Yesu si ni mwana wa Mungu, vipi tena inakuwaje mnasema hana baba?
Mfano maandiko yanasema:
"Na kwa namna hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa MWANA WAKE WA PEKEE ili kila atakayemuamini asipotee"
"Mahali pengine yanasema:
Baba mtukuze Mwanao na mwanao naye akutukuze....."
"Sehemu nyingine panasema, Huyu ni MWANANGU mpendwa niliyependezwa naye.."
Sasa ni andiko gani kwenye Biblia linasema Melkizedeki ana baba?
Kama Yesu ndiye Melkizedeki basi Yesu hana baba kwa hiyo dhana ya Kuwa Yesu ni mwana wa Mungu inavunjika
Na kama Yesu ni mwana Pekee wa Mungu basi Yesu siyo Melkizedeki maana Melkizedeki hana baba
Kwa hiyo unamaanisha kuna raia zinapoteza muda kukesha makanisani na kushinda misikitini bila kujua kuwa huo ufalme hauwahusu?Mathayo 13
Wakaja wanafunzi, wakamwambia, Kwa nini wasema nao kwa mifano (Mafumbo)?
11 Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa.
12 Kwa maana ye yote mwenye kitu atapewa, naye atazidishiwa tele; lakini ye yote asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang?anywa.
13 Kwa sababu hii nasema nao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa.
14 Na neno la nabii Isaya linatimia kwao, likisema,Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa;Kutazama mtatazama, wala hamtaona.
JIBU: Ili kuficha siri za ufalme wa mbingu kwa watu wasio wake
Ni sawa tu na mashirika ya usalama/Jasusi hutumia mafumbo kuwasiliana ili watu msio wa shirika lao msigundue wanachoongelea yaani siri zao!!
Eliya inasemekana alienda mbinguni na usafiri kabisa wa gari ya moto. Hapa pia napata maswali mengi kuwa huko mbinguni kuna parking ya magari pia au hilo nalo ni fumbo la mwandishi?Mkuu , huyo mwizi aliyekuwa msalabani pembeni mwa Yesu alipopewa ahadi kuwa angekuwa peponi na Yesu jioni ile humo peponi angekuwemo bila kujitambua?. Maana naye aliuliwa msalabani na alizikwa kama wanavyozikwa wafu wengine.
Pili Elia huko aliko yuko vague?
Maana Elia hajawahi kufa
Kwa hiyo kuna Mungu wangapi kwa mujibu wa Bible?Kwa mujibu wa quran sawa, la kibiblia ni Mungu.
Yani mimi katika kitu ambacho siwezi kukielewa ni yesu kuwa mungu ili uamini hiki inabidi ujitoe akili na usiulize chochote nakubaliana na wewe 100 yesu sio mungu.
Melikzedek ni mmoja Kati ya " brothers" wanao heshimika sana in freemasonry.Habari za masiku wanajukwaa wote, leo ningependa tujadili watu mysterious kwenye vitabu vyetu vya dini kama ilivyo kawaida yetu. Hivyo twendeni pamoja ili tusolve mystery hii, kubwa ya yote tuongeze tu maarifa na kujibu maswali ambayo yameonekana magumu kwenye vitabu hivi.
Niweke rai mapema pamoja na kwamba inaongelea mtu wa kwenye imani zetu ila mada hii isijengwe kidini yaani kukashifiana bali ijikite kwenye mrengo wa kuelemishana. Karibuni
UTANGULIZI
Melchizidek anaongelewa kwa mara ya kwanza ndani ya Biblia kwenye kitabu cha mwanzo 14:18 ambapo baada ya Abraham kutokea vitani alikutana na Mfalme wa eneo la Salem (Jerusalem ya leo) ambapo alimbariki na Adam alimpa kikumi cha kila alichokuwa nacho wakati huo.
Kwahiyo kitabu cha mwanzo kinamueleza kama MFALME WA SALEM na kuhani wa Mungu YAHWEH
View attachment 1176929
AGANO JIPYA
Upande wa agano Jipya Melchizedek anaelezwa kuwa ana uhusiano ma Yesu.
Waebrania 5
6 kama asemavyo mahali pengine,Ndiwe kuhani milele Kwa mfano wa Melkizedeki
Zaburi 110:4, Waebrania 5:10,6:20 zote zinaeleza kuwa Yesu ni kuhani kwa mfuatano na huyu melchizedek. Ikumbukwe Makuhani wengi wamepita hapo kati na Yesu ametokea kwenye uzao wa Abraham sasa iweje afananishwe na melchizedek na sio kuhani yeyote yule??
Je huyu melchizedek ni nani hasa?
UTATA ZAIDI
Utata zaidi unaibuka pale ambapo muandishi wa kitabu cha waebrania (ambaye mpaka leo hafahamiki ni nani) anaandika haya
Waebrania 7
3 hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.
Tunaambiwa huyu ''Jembe'' hakuwa na baba wala mama na anaishi milele hata sasa???
Ukisoma sura yote inamsifia mtu huyu wa ajabu (mysterious) na kusema licha ya ukuu wa Abraham kama Baba wa wayahudi ila haoni ndani kwa huyu Melchizedek!!
Book of Enoch
Muandishi wa kitabu hiki anajaribu kutupa mwanga kidogo kuhusu utata huu. Ukisoma Enoch 2 sura ya 71 inaeleza kuwa Kuhani Nir (Kaka yake Nuhu) alikuwa na mke ambaye hakulala naye toka alipoteuliwa na Mungu kuwa kuhani. Siku moja anagundua mke wake ana mimba, hivyo ukazuka ugomvi mkubwa mwishowe yule mama akapata presha akaanguka akafa, sasa cha ajabu walipotaka kuizika maiti haraka haraka ''kuua soo'' Wakashangaa mtoto ametoka tayari!!!. Yaani maiti imezaa!!!
Hivyo ikawa concluded kuwa kazaliwa bila baba wala mama.
Ikumbukwe alizaliwa kabla ya gharika, hivyo ili unabii utimie kuwa atakuwa kuhani wa makuhani wote ikabidi Malaika Gabriel amchukue na kumficha bustani ya Eden hivyo akapona gharika na akarudishwa baada ya gharika kupita.
HITIMISHO
Katika pekua pekua zangu sijakutana kabisa na maandiko yeyote kwenye biblia na pseudepigrapha (vilivyoachwa) ambacho kinagusia mwisho wake zaidi vyote vinasema anaishi milele ingawa havisemi wapi ama lini aliacha kuwa mfalme wa Salem.
Sasa wajuvi wa Historia na Dini mtusaidie je mtu huyu alikua nani hasa??
Pia kma alikuwa mkuu kuliko Abraham na amefananishwa na Yesu kwanini hajaongelewa sana kwenye Bible??
Je historia yake ni ipi??
Je mwisho wake ni upi hapa duniani? Au bado anaishi na sisi kwa sura tofauti?
Karibuni....
Una uthibitisho wa kimaaandiko kuwa Yesu aliacha "baadhi" ya mamlaka yake mbinguni?
Lete andiko la kuthibitisha hivyo, siyo unaleta "dhana", "fikra zako", "falsafa" au "connecting dots"
Huko mbinguni hayo mamlaka alimwachia nani?, na huyo aliyemwachia unauthibitisho gani kama kakubali kumrudishia au kamkatalia?. Maana kwa mujibu wa bible nyakati nyingine Siyo yote Yesu aliyoomba alipewa kwa mfano aliomba anusuriwe kutoka kwenye kikombe cha kutundikwa msalabani lakini akafungiwa vioo!. Sasa huko mbinguni una uhakika gani kuwa hajafungiwa vioo kurudishiwa mamlaka yake?- Au hayo mamlaka aliyaficha mahali wakazi wa huko wasiyaone ili pindi akirudi tu ajivike fasta?
Wenzako wanakwambia Yesu alipokuwa duniani alikuwa Mungu kamili na Mtu kamili at the same time! wewe unasema la hasha Hapa alikuwa Mungu mwenye mamlaka baadhi tu!.
Sasa basi nikwambie, ukishaexist katika any point ya Universe at any time bila kuwa na mamlaka kamili ya uungu maana yake Hukuwa Mungu wa milele, maana mamlaka ya Mungu ni ya Milele popote pale alipo!.
Hilo peke yake litoshe kukuonyesha kuwa Yesu siyo Mungu bali ni Aliyetumwa na Mungu
Sasa nikwambie kitu?- Huwa hakuna Mungu asiye na mamlaka kamili, ukishakuwa na baadhi ya mamlaka basi wewe si Mungu
Mkuu dadavua hapoMelikzedek ni mmoja Kati ya " brothers" wanao heshimika sana in freemasonry.
Ha ha ha haAdamu na mkewe Hawa
Hapo Yesu alimaanisha kwa watakaomuamini na kumfuata (John 1:12) ndio wataelewa hayo mafumbo yake sababu watajazwa Roho mtakatifu anayejua kila kitu mpaka siri/Mafumbo ya Mungu Baba (1 Cor 2:10).Kwa hiyo unamaanisha kuna raia zinapoteza muda kukesha makanisani na kushinda misikitini bila kujua kuwa huo ufalme hauwahusu?
Hapo Yesu alimaanisha kwa watakaomuamini na kumfuata (John 1:12) ndio wataelewa hayo mafumbo yake sababu watajazwa Roho mtakatifu anayejua kila kitu mpaka siri/Mafumbo ya Mungu Baba (1 Cor 2:10).
Na hii principle ipo kote mkuu hasa mashirika ya kijasusi hawawezi ongea lugha ambayo raia wa kawaida utaelewa hasa inapokua wanajadili siri za uwanja wa vita utaona tu codes nyingi hadi utachanganyikiwa.
So ukitaka kuzijua itakubidi ujiunge nao ili uweze kuwa na access na taarifa hizo hakuna namna nyingine
Huyo roho mtakatifu anabadirikabadirika?
Kama analeta meseji ya aina moja ya wokovu kwa kila mwenye nae mbona kuna madhehebu nyingi tofauti tofauti na hazikubaliani kwenye mambo kadha wa kadha?. Kwa mfano Biblia ya Wakatoliki in vitabu 73, Biblia ya Protestant in vitabu 66, Biblia ya Ethiopia orthodox church ina vitabu 81
Kama roho Mtakatifu ni yuleyule mmoja, na meseji ni ileile moja kutoka kwake kwa nini awafunulie watu kuwa na biblia zenye idadi ya vitabu tofautitofauti?
Jamaa una ufinyu sanaa wa maarifa ya Neno la Mungu hususani (Biblia)
Naomba ukitaka kujadili habari za Ufalme wa Kristo toka kwenye hali ya ushindani na ubishani,kubali kufundishika!!
Ni hayo tu
Mkuu hii mada ni pana kidogo na nlishaijadili huku na great thinkers walitiririka naona kama una querry basi ipitie ujue wapi tofauti ilipoanza. Humu tutahama mjadalaHuyo roho mtakatifu anabadirikabadirika?
Kama analeta meseji ya aina moja ya wokovu kwa kila mwenye nae mbona kuna madhehebu nyingi tofauti tofauti na hazikubaliani kwenye mambo kadha wa kadha?. Kwa mfano Biblia ya Wakatoliki in vitabu 73, Biblia ya Protestant in vitabu 66, Biblia ya Ethiopia orthodox church ina vitabu 81
Kama roho Mtakatifu ni yuleyule mmoja, na meseji ni ileile moja kutoka kwake kwa nini awafunulie watu kuwa na biblia zenye idadi ya vitabu tofautitofauti?
kinachonishangaza ni picha yake hiyo ni wazi inathibitisha kuwa waisraeli halisi ni weusi 'tiiiii'Habari za masiku wanajukwaa wote, leo ningependa tujadili watu mysterious kwenye vitabu vyetu vya dini kama ilivyo kawaida yetu. Hivyo twendeni pamoja ili tusolve mystery hii, kubwa ya yote tuongeze tu maarifa na kujibu maswali ambayo yameonekana magumu kwenye vitabu hivi.
Niweke rai mapema pamoja na kwamba inaongelea mtu wa kwenye imani zetu ila mada hii isijengwe kidini yaani kukashifiana bali ijikite kwenye mrengo wa kuelemishana. Karibuni
UTANGULIZI
Melchizidek anaongelewa kwa mara ya kwanza ndani ya Biblia kwenye kitabu cha mwanzo 14:18 ambapo baada ya Abraham kutokea vitani alikutana na Mfalme wa eneo la Salem (Jerusalem ya leo) ambapo alimbariki na Adam alimpa kikumi cha kila alichokuwa nacho wakati huo.
Kwahiyo kitabu cha mwanzo kinamueleza kama MFALME WA SALEM na kuhani wa Mungu YAHWEH
View attachment 1176929
AGANO JIPYA
Upande wa agano Jipya Melchizedek anaelezwa kuwa ana uhusiano ma Yesu.
Waebrania 5
6 kama asemavyo mahali pengine,Ndiwe kuhani milele Kwa mfano wa Melkizedeki
Zaburi 110:4, Waebrania 5:10,6:20 zote zinaeleza kuwa Yesu ni kuhani kwa mfuatano na huyu melchizedek. Ikumbukwe Makuhani wengi wamepita hapo kati na Yesu ametokea kwenye uzao wa Abraham sasa iweje afananishwe na melchizedek na sio kuhani yeyote yule??
Je huyu melchizedek ni nani hasa?
UTATA ZAIDI
Utata zaidi unaibuka pale ambapo muandishi wa kitabu cha waebrania (ambaye mpaka leo hafahamiki ni nani) anaandika haya
Waebrania 7
3 hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.
Tunaambiwa huyu ''Jembe'' hakuwa na baba wala mama na anaishi milele hata sasa???
Ukisoma sura yote inamsifia mtu huyu wa ajabu (mysterious) na kusema licha ya ukuu wa Abraham kama Baba wa wayahudi ila haoni ndani kwa huyu Melchizedek!!
Book of Enoch
Muandishi wa kitabu hiki anajaribu kutupa mwanga kidogo kuhusu utata huu. Ukisoma Enoch 2 sura ya 71 inaeleza kuwa Kuhani Nir (Kaka yake Nuhu) alikuwa na mke ambaye hakulala naye toka alipoteuliwa na Mungu kuwa kuhani. Siku moja anagundua mke wake ana mimba, hivyo ukazuka ugomvi mkubwa mwishowe yule mama akapata presha akaanguka akafa, sasa cha ajabu walipotaka kuizika maiti haraka haraka ''kuua soo'' Wakashangaa mtoto ametoka tayari!!!. Yaani maiti imezaa!!!
Hivyo ikawa concluded kuwa kazaliwa bila baba wala mama.
Ikumbukwe alizaliwa kabla ya gharika, hivyo ili unabii utimie kuwa atakuwa kuhani wa makuhani wote ikabidi Malaika Gabriel amchukue na kumficha bustani ya Eden hivyo akapona gharika na akarudishwa baada ya gharika kupita.
HITIMISHO
Katika pekua pekua zangu sijakutana kabisa na maandiko yeyote kwenye biblia na pseudepigrapha (vilivyoachwa) ambacho kinagusia mwisho wake zaidi vyote vinasema anaishi milele ingawa havisemi wapi ama lini aliacha kuwa mfalme wa Salem.
Sasa wajuvi wa Historia na Dini mtusaidie je mtu huyu alikua nani hasa??
Pia kma alikuwa mkuu kuliko Abraham na amefananishwa na Yesu kwanini hajaongelewa sana kwenye Bible??
Je historia yake ni ipi??
Je mwisho wake ni upi hapa duniani? Au bado anaishi na sisi kwa sura tofauti?
Karibuni....
Mkuu hii mada ni pana kidogo na nlishaijadili huku na great thinkers walitiririka naona kama una querry basi ipitie ujue wapi tofauti ilipoanza. Humu tutahama mjadala
Je, Biblia ya ukweli/Halisi ni ipi?
UTANGULIZI Historia ya Biblia ya kikristo ni ndefu jinsi vitabu vilivyopatikana lakini ntaandika kwa kifupi sana na mengine tutaandaika tunavyozidi kuchangia kwenye uzi huu. Na pia nitoe rai mapema kuwa uzi huu sio wa kidini bali wa kielimu/historia hivyo sitegemei watu kurushiana matusi ya...www.jamiiforums.com
Okay basi naomba unisaidie Yesu anaposema ametumia mafumbo (Parables) ili "kuficha" alimaanisha nni?? Je ili uweze unlock hizo siri ufanyeje??Msingi wa hoja yangu ni kukataa kumsingizia roho mtakatifu kwamba wasioelewa jambo basi hawana huyo roho mtakatifu, huenda kuna wasioelewa kwa sababu "wanafalsafa" wamewachanganyachanganya kwa falsafa zao badala ya ukweli ulio wazi na ulio simple kabisa aliofundisha Yesu Kristo wa Nazareti