Mega Thread: Safari za Rais Magufuli nje ya Nchi

Mega Thread: Safari za Rais Magufuli nje ya Nchi

Sina takwimu vizuri ila nilikuta mahali wana calculate inaonyesha Mkwere miaka minne na nusu ama mitano (hesabu siku) katumia kwa safari za nje na miaka nitano mingine ndio aliyoishi nchini. Siku ambapo safari zake zilinikera na kutoa machozi ni pale madktari walipogoma na vifo vya watanzania kuzidi kila kukicha halafu yy anapepea tu wala kusema lolote hana ila alipokufa nguli wetu wa filamu Kanumba eti kaahirisha safari cjui ilikuwa ya china ama india kaenda mcbani. This man bwana.............. (every one has his/her own identity it depend with.....)

Ndugu yangu wacha, kuna mama na jamaa fulani hapa jukwaani akisikia unamsema hivyo jamaa atakuja hapa mbio, wakifika tu watasema mnamsema hivyo kwakuwa alikuwa muislam.

CC: Ritz, Faizafox
 
Tumuombee asafiri mara chache kwa manufaa.Nyerere alistahili aende nje mara nyingi kwa kuwa alikuwa anaandaa msingi wa ustawi wa taifa letu.
Lakini walomzidi yeye kwa wingi wa safari,wanatia shaka.
 
hivi magufuli anaweza kuanza kutembea nchi jirani wakati hajaunda hata serikali?
mtu mwenyewe ana weeks to madarakani mnataka kumlinganisha na watu waliokaa miaka. hebu tuambieni zaidi ya dodoma kuna mkoa gani tena magufuli ameendea? au moro wakati akienda kwa gari dodoma?
Mleta mada utakuwa mpuuzi.

Rais wa Tanzania wa awamu ya Tano mpaka sasa hivi hajasafiri nje ya nchi hata mara moja.

Hapa tutaendelea kupeana updates na kulinganisha safari zake na za Nyerere.

mkuu Saint Ivuga, rais JK amevunja rekodi ya marais wote 3 ukiwajumlisha pamoja. jk ni noumer!

Kiongozi ni kweli kabisa,
Na huyu jamaa anaweza asivunje hata record ya mwalimu Nyerere.

Hadi tarehe kama hii alietoka alishasafiri Mara ngapi?

Hivi JK hakuvunja rekodi ya Marais wa Afrika?

Rekodi ya Nyerere unaijua lakini?
China peke yake Nyerere alienda mara 13...
na alitembea nchi nyingi pia
Nyerere alitembea nchi nyingi kuliko Mwinyi na Mkapa....

kumbuka alitawala miaka 25

Sidhani kama alimfikia Obasanjo

Katika miaka yake kumi kama Rais wa Tanzania, JK alienda mara ngapi Marekani peke yake?

mzee wa msoga hivi bado anasafirii

Punde huyo Marekani na china.kumbuka kunamikataba 17 ya Siri.gess

swissme

Kikwete hajaacha Legacy yoyote ningekuwa mwanae ningeona aibu kwa niaba yake. Magufuli hana shobo za kuzurura duniani anapiga kazi.

Anaogopa kupanda ndege sasa Marekani atafika kwa barabara ipi?

Si kweli. Anachoogopa ni kupanda chopa.

Majuzi tu alikuwa pale Addis Ababa Ethiopia, sina uhakika kama kesharejea hapa nchini, kwa kuwa hivi sasa habari zake hazina tena mvuto wa kuandikwa na vyombo vya habari.

Hivi sasa talk of the town ambayo wakati wote habari zao ndiyo zinazohit headlines ni 'M-Squire' ambao ni double M ya Magufuli + Majaliwa.

Unakumbuka the so called Boys II Men? mara baada ya utawala wa awamu ya nne? Haya ni majina walipachikwa JK na EL baada ya kuingia madarakani.
Ki maono kasi ya wakuu hawa M-square kama ulivyowaita ni nzuri na inatia moyo. Tuwape muda ili tuje kuwapima na kasi yao hii baada ya miaka mitano.

Mtamhesabia miaka mitano?

Hili ni jukwaa la intellectuals usidhani kuwa na facts tu basi.for your information Kikwete kawazidi marais wote kwa kuzurura duniani. amemzidi hata Mgabe aliyekaa madarakani miaka 28.

inasemekana ktk miaka yake yote ya urais mwalm nyerere aliwahi safiri nje ya nchi takribani mara 60 tu

Una chuki binafsi na jk wewe siyo bure
 
Magufuli toka awe Waziri kwa miaka 20 ameenda nje mara 4 tu na haringi.
 
hivi magufuli anaweza kuanza kutembea nchi jirani wakati hajaunda hata serikali?
mtu mwenyewe ana weeks to madarakani mnataka kumlinganisha na watu waliokaa miaka. hebu tuambieni zaidi ya dodoma kuna mkoa gani tena magufuli ameendea? au moro wakati akienda kwa gari dodoma?
Mleta mada utakuwa mpuuzi.
JK alizidi yaan kiguu na njia utadhan sijui nini............
JK alikuwa rais dhaifu na asiyekuwa na dira
 
If UDOM is not a legacy then you have to find the new meaning of the word.
Tatizo humu wamejaa watoto wa Shule. Kama unataka kuanzisha mada ya JK anzisha!
Kuna watoto wengine wanasema JK ashitakiwe wanasahau aliyeua Rais wake!
 
JK kafanya mengi mnoo mnyonge mnyongeni haki yake mpeni...
 
ni uelewa wako tu mdogo unakusumbua. JK anamadhaifu yake hasa kwenye kupambana na rushwa lakini maeneo mengi kafanya vizuri tena sana. nani asiyejua mabarabara aliyojenga JK, nani asiyejua mavyuo kama Udom yamejengwa na JK, nani asyejua usambazaji wa umeme, maji, ujenzi wa mahosipitali, mashule na kadhalika yamefanywa na JK. achilia mbali madaraja kama malagarasi, kigamboni, nk. kwa uelewa wenu mdogo mnaaminishana hata ujiga.
nawashangaa hata kama kusoma hamjui basi hata picha ukutani hamuoni?


JK alizidi yaan kiguu na njia utadhan sijui nini............
JK alikuwa rais dhaifu na asiyekuwa na dira
 
Kikwete hakuwa kiongozi bali jambazi ambalo liliwekwa pale na mafioso kuhakikisha rasilimali za nchi zinamalizwa, hivi ni kiongozi gani ambaye ndani ya mwezi mmoja tangu aondoke madarakani uozo wote alioufanya unawekwa hadharani tena pasipo shaka yoyote kuwa alikuwa mhusika wa moja kwa moja? Ndani ya mwezi mmoja aina ya utawala wake na mrithi wake unatofautiana kama mbingu na nchi na ikizingatiwa hawa wote wanatoka chama kimoja na sera zao ni moja? Hakika nchi hii haikuwa na kiongozi kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita.

Viongozi wako wa dini wanaokupaka mafuta wanamwita 'chaguo la Mungu' wewe kapuku fedhuli unapata wapi ujasiri wa kuamini Chaguo la Mungu ni jambazi?
 
Rekodi ya Nyerere unaijua lakini?
China peke yake Nyerere alienda mara 13...
na alitembea nchi nyingi pia
Nyerere alitembea nchi nyingi kuliko Mwinyi na Mkapa....

kumbuka alitawala miaka 25
huyu jamaa aliturudisha sana nyuma baasi tu watanzania hatujui
 
mimi ninachojua kwa muda wa miaka kumi iliyopita watanzania hatukuwa na rais
 
mimi ninachojua kwa muda wa miaka kumi iliyopita watanzania hatukuwa na rais

Shibe imesha kulevya kijana.

Punda ukimpa uhuru sana mwisho lzm akupige teke.
Hii ndio shukrani ya punda.
 
Back
Top Bottom