NYEMO CHILONGANI
MEDUSA: MALKIA WA DAMU
0718069269
SEHEMU YA 04.
Zuhura ambaye alikuwa ni rafiki yake Nasria alikuwa akiendelea na maisha yake huko Zanzibar, moyo wake ulikuwa na furaha tele baada ya rafiki yake kuachana na mumewe na kurudi jijini Dar es Salaam.
Alitumiwa kiasi cha shilingi milioni tano kwa ajili ya maisha yake, alimuona Nasria kuwa rafiki wa kweli kwani pesa aliyopewa iliyafanya maisha yake kuwa mepesi kwa sehemu fulani.
Alipokuwa ndani ya chumba chake alikuwa na furaha tele, alimshukuru sana Nasria na mara kwa mara alikuwa akimpigia simu kwa namba mpya aliyokuwa ameisajili kwa matumizi yake mapya kwani hakutaka hata kuwasiliana na wazazi wake.
Zuhura akawa mwanamke wa starehe, kila kitu alichokuwa akikifanya kwa pesa hizo zilikuwa ni starehe tu, alinunua mavazi ya bei kubwa, simu ya gharama na vitu vingine vya anasa, yote ni kwa sababu alikuwa na pesa nyingi ambayo hakuwa ameihangaikia hata kidogo.
Kila siku alikuwa akinunua pombe na kuwaita marafiki zake na kuanza kunywa pamoja kwake, ilikuwa ni sherehe kila siku, hakutaka kujali hata kidogo, kwake aliona ni bora kuula ujana kabla ya ujana kuanza kumla yeye.
Baada ya siku mbili, akampigia simu rafiki yake mwingine aliyeitwa kwa jina la Ashura na kumwambia alitaka amfuate nyumbani kwake kwani kulikuwa na mambo mengi alitaka kuzungumza naye.
Ashura akaenda mpaka nyumbani kwa rafiki yake na kuanza kuongea mambo mengi kuhusu mabuzi na hata maisha yao ya udangaji. Alimsimulia Ashura kila kitu kilichotokea kwa Nasria, Ashura alimuona Nasria kuwa mjinga kwani kwenye kitu alichokitamani maisha yake yote ni kuolewa na mwanaume aliyekuwa na pesa.
Alifuatwa na wanaume wengi lakini hapakuwa na muoaji, wengi waliomfuata walimuahidi kumuoa lakini mwisho wa siku baada ya kumvua nguo zake na kumuacha utupu kitandani, wakaachana naye na kuendelea na maisha yao.
Alikuwa na hamu ya ndoa, alitamani mno kuolewa, hakuipata bahati hiyo iliyokwenda kwa Nasria ambaye mbali na kuolewa, aliolewa na mwanaume mwenye pesa zake, aliyetaka kujenga maisha pamoja naye.
“Sasa kwa nini akamuacha?” aliuliza Ashura.
“Basi tu! Hakupenda kuishi na kibabu!” alijibu Zuhura.
“Lakini si alikuwa ana pesa?”
“Ndiyo! Nasria alisema yule mwanaume ana pesa mpaka anaumwa.”
“Na akamuacha?”
“Ndiyo! Akamuibia pesa na kutimka zake jijini,” alisema Zuhura.
Kila alichokuwa akikiongea na rafiki yake huyo, moyo wa Ashura ulikuwa na maumivu makali, hakuamini kama rafiki yake huyo angekuwa na maisha ya kijinga ya kukataa kuishi na mwanaume aliyekuwa na pesa kama ilivyotokea.
Waliongea mengi na ilipofika majira ya saa mbili usiku, akamwambia Zuhura alitaka kuondoka. Hilo halikuwa tatizo, akakubaliwa kuondoka lakini kitu alichotaka ni kutembea kwa miguu kwani haikuwa mbali na mahali alipokuwa akiishi.
“Jamani shoga’angu, si uchukue hata Uber,” alisema Zuhura, pesa zilikuwa zikimuwasha na muda wote alitaka kuombwa.
“Acha nitembee tu, wala usijali!”
“Basi acha nikusindikize,” alisema Zuhura, akasimama na kuanza kumsindikiza rafiki yake huyo.
Walitembea pembezoni mwa barabara huku wakipiga stori mbalimbali, Ashura alikuwa akilaumu uamuzi wa Nasria wa kumuacha mumewe na kutoroka na wakati alijua alikuwa na pesa lakini kwa Zuhura alimsifia kwa kuwa aliufuata moyo wake.
Huku wakiwa hapo, mara ghafla sauti za honi ya gari ikaanza kusikika kutoka nyuma, haraka sana wakageuka na kuangalia hilo gari lililokuwa likipiga honi. Waliziona taa tu tena likiwa linakuja kwa kasi. Hata kabla ya kufanya jambo lolote lile, gari likawagonga, mzinga ukasikika mahali hapo, Ashura akaangukia kama hatua tano kutoka pale walipokuwa lakini Zuhura aliangukia kama hatua ishirini kutoka hapo.
“Mamaaaaaaaaaaa.....” ilisikika sauti hiyo tu.
Ashura akashangaa pale alipoanguka hapakuwa mbali na walipokuwa wakitembea. Kwake ilishangaza kidogo kwani kwa jinsi gari lile lilivyokuwa limekuja kwa kasi na kuwagonga, hakika alitakiwa kutupwa mbali kabisa na hapo.
Lililomshangza halikuwa hilo tu bali hata mwilini mwake, hakuwa na maumivu yoyote yale zaidi ya yale aliyoyapata zaidi ya kuanguka chini. Hilo nalo lilimshangaza. Haikuwa kawaida kwa yeyote yule kugongwa na gari lililokuwa likija kwa kasi na mwili kutokuwa na maumivu yoyote yale.
Ukiachana na hayo yote, kitu cha tatu kilichomshangaza mno ni gari hilo. Walilisikia likiwa nyuma yao likipiga honi, kila mmoja alichanganyikiwa, wakajitahidi kulikwepa lakini walishindwa, yaani ilionyesha gari lilimshinda dereva hivyo kwenda pembeni na kuwagonga.
Sasa utata ulikuwa hapa.
Ni kweli waligongwa lakini kitu cha ajabu ni kwamba gari halikuwa likionekana. Baada ya kuhisi gari lilipotea njia na kuwagonga inamaana lingekuwa hata mbele limesimama, ama watu kuteremka na kuanza kuwajulia hali, la ajabu kabisa, kila kona halikuwepo gari hilo.
“Ama halikuwa gari?” alijiuliza.
Akaanza kusikika kelele za Zuhura aliyekuwa mbali na mahali hapo alipokuwa na kuanza kumsogelea, watu waliokuwa pembeni ambao nao walionekana kushangazwa na tukio hilo wakaanza kumfuata msichana huyo.
Walipomfikia, kila mmoja alishtuka, huyo Zuhura akawa kama mfu aliyekuwa akipiga kelele tu za mwisho. Alivunjika miguu yote, kichwa chake kilibonyea, mabega yalivunjika na alikuwa akitokwa na damu nyingi, yaani kwa kila walivyokuwa wakimwangalia mahali pale walijua tu hata dakika tatu hatochukua atakuwa amekufa.
Haraka sana wakambeba, ikaitwa bajaji, akapandishwa na kuanza kukimbizwa hospitalini huku wengine wakiwa kwenye pikipiki. Njiani, Ashura alikuwa akijiuliza zaidi kuhusu ajali ile, kilikuwa ni kitu kisichowezekana kwa kitu hicho kutokea.
Swali lake kubwa lilikuwa ni lile gari lililokuwa limewagonga, kwa nini dereva alikimbia bila kuwapa msaada? Na kama kweli alikimbia basi alikuwa kwa mwendo wa kasi sana kwani baada ya yeye kuanguka tu, gari hakuliona tena.
Hawakuchukua muda mrefu wakafika hospitalini, Zuhura akateremshwa, akapakizwa juu ya machela na kuanza kusukumwa kuelekea ndani. Kila mtu aliyekuwa akimuona, alijiuliza kama alikuwa mzima kwani muonekano wake haukuonyesha uzima hata mara moja.
Akaingizwa kwenye chumba cha upasuaji huku Ashura akibaki na watu wengine aliokuja nao kutoka kule barabarani. Kichwa chake kilikuwa kimechanganyikiwa, yaani hakufikiria kuhusu rafiki yake kitu kilichomuumiza kichwa ni namna ile ajali ilivyotokea.
“Kwani ilikuwaje?” aliuliza mwanaume mmoja huku akimwangalia, naye alikuwa kule barabarani, alikuwa mmoja wa vijana walimpeleka Zuhura pale hospitalini.
“Ni ajali! Tuligongwa na gari,” alijibu.
“Mligongwa na gari? Yaani ilikuwajekuwaje?” aliuliza.
“Gari ilikuja na kupiga honi, hata kabla ya kufanya kitu, tukagongwa,” alijibu.
“Gari gani?” aliuliza mwanaume huyo, alionyesha mshangao.
“Sijajua! Dereva alikimbia.”
“Kwani pale mliokuwa mmeanguka, gari liliwagonga dakika ngapi nyuma?”
“Kama nusu dakika, yaani ghafla!”
“Gari?”
“Ndiyo!”
“Unasema lilikuja na kupiga honi?”
“Ndiyo!”
“Mbona sisi hatukuona gari?” aliuliza.
“Hamkuona gari?”
“Ndiyo! Si muda ule uliokuwa mmeanguka! Kwani pale mligongwa na gari?”
“Ndiyo!”
“Hapana! Hapakuwa na gari!”
Ashura akanyamaza, alichokisema mwanaume huyo na mwezake kushadadia kwamba hapakuwa na gari kiliingia moyoni mwake na kumkumbusha kile alichokifikiria. Maneno yao yaliendana na kile kilichosumbua kichwa chake.
Walipoanguka na kuangalia huku na kule, hapakuwa na gari lolote lile lakini jambo jingine ni jinsi mwili wake ulivyokuwa. Kama kweli waligongwa na gari basi angekuwa na maumivu makali sana, cha ajabu kabisa, hakuwa na maumivu yoyote yale.
“Kama si gari lilikuwa nini?”
“Sisi ndiyo tukuulize wewe.”
“Ila lilikuwa linapiga honi sana!”
“Hatukusikia honi yoyote ile.”
Ashura akakaa kimya kwa sekunde chache, kwa kile alichoambiwa hakika kilimshangaza sana, hapo akaamini kweli uchawi ulikuwepo. Huku akiwa anafikiria hivyo ndipo akapata wazo kwamba inawezekana hayo yote yalisababishwa na mume wa Nasria kwani kwa jinsi hali ilivyokuwa haikuwa ya kawaida hata kidogo.
Huku akiwa amekaa hapo, mara mlango wa wagonjwa mahututi ukafunguliwa na daktari mmoja aliyekuwa na koti kubwa jeupe na mashine ya kupimia mapigo ya moyo, stethoscope ikiwa shingoni mwake.
“Ndugu yake nani huyu?” aliuliza daktari huku akiwaangalia.
Haraka sana Ashura akasimama.
“Nifuate ofisini!” alisema.
Hakutaka kubisha, akaanza kumfuata ofisini kwake huku akiwa na hofu tele. Wale wanaume wengine nao hawakutaka kusubiri, wakaungana na Ashura na kuanza kuelekea huko. Walitaka kujua kilichotokea kwani nao walimsaidia mpaka kumfikisha hospitalini hapo.
Walipofika nje ya ofisi hiyo, wakaingia ndani na kukaa kwenye viti huku dokta akiwa kwenye kiti kingine. Kwa kumwangalia tu tayari walihisi kulikuwa na kitu kilichotokea, sura yake haikuwa kwenye muonekano mzuri, alikuwa na majonzi.
“Poleni sana,” alisema huku akiwaangalia.
“Tunashukuru! Anaendeleaje?”
“Kwanza ni nani kwako?”
“Rafiki yangu kipenzi, kama ndugu yangu!”
“Pole sana. Tumejitahidi sana kuokoa maisha yake lakini imeshindikana kabisa,” alisema daktari huku akiwaangalia.
Hilo walilitegemea, kwa jinsi Zuhura alivyokuwa, ilionyesha kabisa hapakuwa na mategemeo yoyote ya kupona na tena walihisi kabisa alifariki akiwa njiani kuelekea hospitalini hapo.
Ashura akaanza kulia, hakuamini alichokisikia, kwake, alimpenda sana msichana huyo, alikuwa rafiki yake wa karibu, walidanga pamoja na kufanya mambo mengi tu. Leo, Zuhura hakuwepo duniani, alifariki baada ya kuhisi alipata ajali mbaya ya gari.
Yeye ndiye akaanza kuwapigia simu marafiki zake wengine, ndugu na majamaa wa karibu na kuwapa taarifa ya msiba. Kwao, ilikuwa ni maumivu makali, hawakuamini kama Zuhura angefariki kipindi cha hivi karibuni.
Siku iliyofuata haraka sana ndugu zake wakafika Zanzibar ambapo huko waliamua kuuzika mwili wake kwani hawakuwa na pesa za kutosha kuusafirisha na kwenda kuuzika jijini Dar es Salaam.
Ashura akabaki peke yake, hakuwa na rafiki yake huyo na kitu pekee kilichokuwa kikimuumiza ni namna rafiki yake huyo alivyokufa. Hakutaka kukaa tu, ilikuwa ni lazima kuujua ukweli wa kile kilichotokea, baada ya siku mbili tu, akaamua kwenda kwa mganga.
Huko ndipo alipoambiwa kilichotokea, kwa mara ya kwanza akamjua mtu aliyeitwa kwa jina la Hussein Kaifah, mwanaume aliyetoka kwenye ukoo uliokuwa na ushirikina mkubwa nchini Oman.
Alipoambiwa kuhusu mwanaume huyo, jinsi alivyokuwa na nguvu za kumuua mtu yeyote yule ndipo akapata wazo la kuwasiliana na Nasria na kumwambia kilichokuwa kikiendelea. Kama mwanaume huyo aliamua kumuua Zuhura kwa kuwa alishirikiana na Nasria, basi aliamini kama msichana huyo hakuwa amefariki, basi zamu yake ilikuwa ikifuata.
Akajaribu kumpigia simu, haikuwa ikipatikana, hakutaka kubaki Zanzibar, alichokifikiria ni kesho kuondoka huko na kuelekea jijini Dar es Salaam, aende nyumbani kwao, azungumze naye na kumwambia sasa alitakiwa kujilinda kwani yule mwanaume aliyemkimbia alikuwa mtu hatari sana kwenye masuala ya uchawi.
“Ngoja nikamuokoe, akajilinde anavyoweza,” alisema Ashura huku hata naye akionekana kuogopa, kwa kilichotokea, aliamini kweli uchawi ulikuwepo.
Je, nini kitaendelea?
Je, Ashura atamuwahi Nasria?
Je, Nasria atakufa?
Nini kitatokea endapo atakufa?
Zuhura ambaye alikuwa ni rafiki yake Nasria alikuwa akiendelea na maisha yake huko Zanzibar, moyo wake ulikuwa na furaha tele baada ya rafiki yake kuachana na mumewe na kurudi jijini Dar es Salaam.
Alitumiwa kiasi cha shilingi milioni tano kwa ajili ya maisha yake, alimuona Nasria kuwa rafiki wa kweli kwani pesa aliyopewa iliyafanya maisha yake kuwa mepesi kwa sehemu fulani.
Alipokuwa ndani ya chumba chake alikuwa na furaha tele, alimshukuru sana Nasria na mara kwa mara alikuwa akimpigia simu kwa namba mpya aliyokuwa ameisajili kwa matumizi yake mapya kwani hakutaka hata kuwasiliana na wazazi wake.
Zuhura akawa mwanamke wa starehe, kila kitu alichokuwa akikifanya kwa pesa hizo zilikuwa ni starehe tu, alinunua mavazi ya bei kubwa, simu ya gharama na vitu vingine vya anasa, yote ni kwa sababu alikuwa na pesa nyingi ambayo hakuwa ameihangaikia hata kidogo.
Kila siku alikuwa akinunua pombe na kuwaita marafiki zake na kuanza kunywa pamoja kwake, ilikuwa ni sherehe kila siku, hakutaka kujali hata kidogo, kwake aliona ni bora kuula ujana kabla ya ujana kuanza kumla yeye.
Baada ya siku mbili, akampigia simu rafiki yake mwingine aliyeitwa kwa jina la Ashura na kumwambia alitaka amfuate nyumbani kwake kwani kulikuwa na mambo mengi alitaka kuzungumza naye.
Ashura akaenda mpaka nyumbani kwa rafiki yake na kuanza kuongea mambo mengi kuhusu mabuzi na hata maisha yao ya udangaji. Alimsimulia Ashura kila kitu kilichotokea kwa Nasria, Ashura alimuona Nasria kuwa mjinga kwani kwenye kitu alichokitamani maisha yake yote ni kuolewa na mwanaume aliyekuwa na pesa.
Alifuatwa na wanaume wengi lakini hapakuwa na muoaji, wengi waliomfuata walimuahidi kumuoa lakini mwisho wa siku baada ya kumvua nguo zake na kumuacha utupu kitandani, wakaachana naye na kuendelea na maisha yao.
Alikuwa na hamu ya ndoa, alitamani mno kuolewa, hakuipata bahati hiyo iliyokwenda kwa Nasria ambaye mbali na kuolewa, aliolewa na mwanaume mwenye pesa zake, aliyetaka kujenga maisha pamoja naye.
“Sasa kwa nini akamuacha?” aliuliza Ashura.
“Basi tu! Hakupenda kuishi na kibabu!” alijibu Zuhura.
“Lakini si alikuwa ana pesa?”
“Ndiyo! Nasria alisema yule mwanaume ana pesa mpaka anaumwa.”
“Na akamuacha?”
“Ndiyo! Akamuibia pesa na kutimka zake jijini,” alisema Zuhura.
Kila alichokuwa akikiongea na rafiki yake huyo, moyo wa Ashura ulikuwa na maumivu makali, hakuamini kama rafiki yake huyo angekuwa na maisha ya kijinga ya kukataa kuishi na mwanaume aliyekuwa na pesa kama ilivyotokea.
Waliongea mengi na ilipofika majira ya saa mbili usiku, akamwambia Zuhura alitaka kuondoka. Hilo halikuwa tatizo, akakubaliwa kuondoka lakini kitu alichotaka ni kutembea kwa miguu kwani haikuwa mbali na mahali alipokuwa akiishi.
“Jamani shoga’angu, si uchukue hata Uber,” alisema Zuhura, pesa zilikuwa zikimuwasha na muda wote alitaka kuombwa.
“Acha nitembee tu, wala usijali!”
“Basi acha nikusindikize,” alisema Zuhura, akasimama na kuanza kumsindikiza rafiki yake huyo.
Walitembea pembezoni mwa barabara huku wakipiga stori mbalimbali, Ashura alikuwa akilaumu uamuzi wa Nasria wa kumuacha mumewe na kutoroka na wakati alijua alikuwa na pesa lakini kwa Zuhura alimsifia kwa kuwa aliufuata moyo wake.
Huku wakiwa hapo, mara ghafla sauti za honi ya gari ikaanza kusikika kutoka nyuma, haraka sana wakageuka na kuangalia hilo gari lililokuwa likipiga honi. Waliziona taa tu tena likiwa linakuja kwa kasi. Hata kabla ya kufanya jambo lolote lile, gari likawagonga, mzinga ukasikika mahali hapo, Ashura akaangukia kama hatua tano kutoka pale walipokuwa lakini Zuhura aliangukia kama hatua ishirini kutoka hapo.
“Mamaaaaaaaaaaa.....” ilisikika sauti hiyo tu.
Ashura akashangaa pale alipoanguka hapakuwa mbali na walipokuwa wakitembea. Kwake ilishangaza kidogo kwani kwa jinsi gari lile lilivyokuwa limekuja kwa kasi na kuwagonga, hakika alitakiwa kutupwa mbali kabisa na hapo.
Lililomshangza halikuwa hilo tu bali hata mwilini mwake, hakuwa na maumivu yoyote yale zaidi ya yale aliyoyapata zaidi ya kuanguka chini. Hilo nalo lilimshangaza. Haikuwa kawaida kwa yeyote yule kugongwa na gari lililokuwa likija kwa kasi na mwili kutokuwa na maumivu yoyote yale.
Ukiachana na hayo yote, kitu cha tatu kilichomshangaza mno ni gari hilo. Walilisikia likiwa nyuma yao likipiga honi, kila mmoja alichanganyikiwa, wakajitahidi kulikwepa lakini walishindwa, yaani ilionyesha gari lilimshinda dereva hivyo kwenda pembeni na kuwagonga.
Sasa utata ulikuwa hapa.
Ni kweli waligongwa lakini kitu cha ajabu ni kwamba gari halikuwa likionekana. Baada ya kuhisi gari lilipotea njia na kuwagonga inamaana lingekuwa hata mbele limesimama, ama watu kuteremka na kuanza kuwajulia hali, la ajabu kabisa, kila kona halikuwepo gari hilo.
“Ama halikuwa gari?” alijiuliza.
Akaanza kusikika kelele za Zuhura aliyekuwa mbali na mahali hapo alipokuwa na kuanza kumsogelea, watu waliokuwa pembeni ambao nao walionekana kushangazwa na tukio hilo wakaanza kumfuata msichana huyo.
Walipomfikia, kila mmoja alishtuka, huyo Zuhura akawa kama mfu aliyekuwa akipiga kelele tu za mwisho. Alivunjika miguu yote, kichwa chake kilibonyea, mabega yalivunjika na alikuwa akitokwa na damu nyingi, yaani kwa kila walivyokuwa wakimwangalia mahali pale walijua tu hata dakika tatu hatochukua atakuwa amekufa.
Haraka sana wakambeba, ikaitwa bajaji, akapandishwa na kuanza kukimbizwa hospitalini huku wengine wakiwa kwenye pikipiki. Njiani, Ashura alikuwa akijiuliza zaidi kuhusu ajali ile, kilikuwa ni kitu kisichowezekana kwa kitu hicho kutokea.
Swali lake kubwa lilikuwa ni lile gari lililokuwa limewagonga, kwa nini dereva alikimbia bila kuwapa msaada? Na kama kweli alikimbia basi alikuwa kwa mwendo wa kasi sana kwani baada ya yeye kuanguka tu, gari hakuliona tena.
Hawakuchukua muda mrefu wakafika hospitalini, Zuhura akateremshwa, akapakizwa juu ya machela na kuanza kusukumwa kuelekea ndani. Kila mtu aliyekuwa akimuona, alijiuliza kama alikuwa mzima kwani muonekano wake haukuonyesha uzima hata mara moja.
Akaingizwa kwenye chumba cha upasuaji huku Ashura akibaki na watu wengine aliokuja nao kutoka kule barabarani. Kichwa chake kilikuwa kimechanganyikiwa, yaani hakufikiria kuhusu rafiki yake kitu kilichomuumiza kichwa ni namna ile ajali ilivyotokea.
“Kwani ilikuwaje?” aliuliza mwanaume mmoja huku akimwangalia, naye alikuwa kule barabarani, alikuwa mmoja wa vijana walimpeleka Zuhura pale hospitalini.
“Ni ajali! Tuligongwa na gari,” alijibu.
“Mligongwa na gari? Yaani ilikuwajekuwaje?” aliuliza.
“Gari ilikuja na kupiga honi, hata kabla ya kufanya kitu, tukagongwa,” alijibu.
“Gari gani?” aliuliza mwanaume huyo, alionyesha mshangao.
“Sijajua! Dereva alikimbia.”
“Kwani pale mliokuwa mmeanguka, gari liliwagonga dakika ngapi nyuma?”
“Kama nusu dakika, yaani ghafla!”
“Gari?”
“Ndiyo!”
“Unasema lilikuja na kupiga honi?”
“Ndiyo!”
“Mbona sisi hatukuona gari?” aliuliza.
“Hamkuona gari?”
“Ndiyo! Si muda ule uliokuwa mmeanguka! Kwani pale mligongwa na gari?”
“Ndiyo!”
“Hapana! Hapakuwa na gari!”
Ashura akanyamaza, alichokisema mwanaume huyo na mwezake kushadadia kwamba hapakuwa na gari kiliingia moyoni mwake na kumkumbusha kile alichokifikiria. Maneno yao yaliendana na kile kilichosumbua kichwa chake.
Walipoanguka na kuangalia huku na kule, hapakuwa na gari lolote lile lakini jambo jingine ni jinsi mwili wake ulivyokuwa. Kama kweli waligongwa na gari basi angekuwa na maumivu makali sana, cha ajabu kabisa, hakuwa na maumivu yoyote yale.
“Kama si gari lilikuwa nini?”
“Sisi ndiyo tukuulize wewe.”
“Ila lilikuwa linapiga honi sana!”
“Hatukusikia honi yoyote ile.”
Ashura akakaa kimya kwa sekunde chache, kwa kile alichoambiwa hakika kilimshangaza sana, hapo akaamini kweli uchawi ulikuwepo. Huku akiwa anafikiria hivyo ndipo akapata wazo kwamba inawezekana hayo yote yalisababishwa na mume wa Nasria kwani kwa jinsi hali ilivyokuwa haikuwa ya kawaida hata kidogo.
Huku akiwa amekaa hapo, mara mlango wa wagonjwa mahututi ukafunguliwa na daktari mmoja aliyekuwa na koti kubwa jeupe na mashine ya kupimia mapigo ya moyo, stethoscope ikiwa shingoni mwake.
“Ndugu yake nani huyu?” aliuliza daktari huku akiwaangalia.
Haraka sana Ashura akasimama.
“Nifuate ofisini!” alisema.
Hakutaka kubisha, akaanza kumfuata ofisini kwake huku akiwa na hofu tele. Wale wanaume wengine nao hawakutaka kusubiri, wakaungana na Ashura na kuanza kuelekea huko. Walitaka kujua kilichotokea kwani nao walimsaidia mpaka kumfikisha hospitalini hapo.
Walipofika nje ya ofisi hiyo, wakaingia ndani na kukaa kwenye viti huku dokta akiwa kwenye kiti kingine. Kwa kumwangalia tu tayari walihisi kulikuwa na kitu kilichotokea, sura yake haikuwa kwenye muonekano mzuri, alikuwa na majonzi.
“Poleni sana,” alisema huku akiwaangalia.
“Tunashukuru! Anaendeleaje?”
“Kwanza ni nani kwako?”
“Rafiki yangu kipenzi, kama ndugu yangu!”
“Pole sana. Tumejitahidi sana kuokoa maisha yake lakini imeshindikana kabisa,” alisema daktari huku akiwaangalia.
Hilo walilitegemea, kwa jinsi Zuhura alivyokuwa, ilionyesha kabisa hapakuwa na mategemeo yoyote ya kupona na tena walihisi kabisa alifariki akiwa njiani kuelekea hospitalini hapo.
Ashura akaanza kulia, hakuamini alichokisikia, kwake, alimpenda sana msichana huyo, alikuwa rafiki yake wa karibu, walidanga pamoja na kufanya mambo mengi tu. Leo, Zuhura hakuwepo duniani, alifariki baada ya kuhisi alipata ajali mbaya ya gari.
Yeye ndiye akaanza kuwapigia simu marafiki zake wengine, ndugu na majamaa wa karibu na kuwapa taarifa ya msiba. Kwao, ilikuwa ni maumivu makali, hawakuamini kama Zuhura angefariki kipindi cha hivi karibuni.
Siku iliyofuata haraka sana ndugu zake wakafika Zanzibar ambapo huko waliamua kuuzika mwili wake kwani hawakuwa na pesa za kutosha kuusafirisha na kwenda kuuzika jijini Dar es Salaam.
Ashura akabaki peke yake, hakuwa na rafiki yake huyo na kitu pekee kilichokuwa kikimuumiza ni namna rafiki yake huyo alivyokufa. Hakutaka kukaa tu, ilikuwa ni lazima kuujua ukweli wa kile kilichotokea, baada ya siku mbili tu, akaamua kwenda kwa mganga.
Huko ndipo alipoambiwa kilichotokea, kwa mara ya kwanza akamjua mtu aliyeitwa kwa jina la Hussein Kaifah, mwanaume aliyetoka kwenye ukoo uliokuwa na ushirikina mkubwa nchini Oman.
Alipoambiwa kuhusu mwanaume huyo, jinsi alivyokuwa na nguvu za kumuua mtu yeyote yule ndipo akapata wazo la kuwasiliana na Nasria na kumwambia kilichokuwa kikiendelea. Kama mwanaume huyo aliamua kumuua Zuhura kwa kuwa alishirikiana na Nasria, basi aliamini kama msichana huyo hakuwa amefariki, basi zamu yake ilikuwa ikifuata.
Akajaribu kumpigia simu, haikuwa ikipatikana, hakutaka kubaki Zanzibar, alichokifikiria ni kesho kuondoka huko na kuelekea jijini Dar es Salaam, aende nyumbani kwao, azungumze naye na kumwambia sasa alitakiwa kujilinda kwani yule mwanaume aliyemkimbia alikuwa mtu hatari sana kwenye masuala ya uchawi.
“Ngoja nikamuokoe, akajilinde anavyoweza,” alisema Ashura huku hata naye akionekana kuogopa, kwa kilichotokea, aliamini kweli uchawi ulikuwepo.
Je, nini kitaendelea?
Je, Ashura atamuwahi Nasria?
Je, Nasria atakufa?
Nini kitatokea endapo atakufa?
Sent from my SM-A107F using
JamiiForums mobile app