MEDUSA: Malkia wa Damu

MEDUSA: Malkia wa Damu

Chilojnr

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2012
Posts
308
Reaction score
1,354
NYEMO CHILONGANI

0718069269

Sehemu ya 01

Ndiyo ni mzuri!
Tena hasaaa!
Kwanza ni mweupe.
Ana mwili ulionyambulika.
Macho ya goroli, ya kurembua ambapo akiamua kukuangalia, basi tuseme umepata bahati ya kuangaliwa na mwanamke mzuri, inawezekana kuliko wote waliokuwa wakikaa jijini Dar es Salaam.
Kwa jina aliitwa Nasria Abdul, msichana aliyekuwa na mchanganyiko wa rangi, baba yake alikuwa Mwarabu wa Oman aliyezaliwa na kukulia Zanzibar huku mama yake akiwa Mzigua kutoka Handeni, jijini Tanga.
Nasria alikuwa na uzuri wa asili, alivutia, alipendeza kila alipokuwa akitembea, alijua kuringa, kama watu walisema twiga walikuwa wakitembea kwa maringo, basi tuseme hao twiga walijifunza kwa binti huyu mrembo namna ya kutembea.
Naam!
Alijua kutembea.
Alirusha mikono yake kwa madaha.
Alikilegeza kiuno chake.
Kifua saa sita.
Huku lipsi zake nene na laini akipenda kuzipitishia ulimi.
Kila aliyekuwa akiziangalia, alitamani kuzinyonya, tena azinyonye hasa, azipake hata asali, halafu azinyonye tena mpaka asali iishe mdomoni, yaani huyu msichana hakuisha hamu hata kidogo, na kama ungepewa karatasi uandike sifa za uzuri wake, si ajabu ukajaza kitabu kikubwa na bado isitoshe kuzimaliza.
Nasria alikuwa akiishi Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam, mahali kulipokuwa na wanawake wengi wa Kipemba, waliojua kuvaa, kunukia na hata kuringa. Nasria alikuwa miongoni mwao, alikuwa binti mrembo kupita kawaida, halafu hakuwa yule mwepesi kwamba mwanaume huyu akienda, amvulie nguo, yule akienda basi aende nyumbani kwake.
Huyu Nasria alikuwa tofauti kabisa. Alijiheshimu, alikuwa na nidhamu na kitu kikubwa kabisa alikuwa msafi, tena msafi sana, yaani hakuwahi kunuka kwapa wala jasho, hakuwahi kunuka sehemu yoyote ile mwilini mwake, na endapo ungebahatika kuvuliwa nguo na msichana huyu, basi ungesema sasa uliingia kwenye duka la manukato, yaani alinukia kila harufu ya pafyumu.
Unadhani kuna mtu Magomeni ambaye hakuwa akimfahamu msichana huyu? Atoke wapi? Wanaume wote waroho walimtamani, kulikuwa na wanamuziki waliokuwa wakimuimbia yeye tu, kuna waandishi walikuwa wakiandika simulizi na kulitumia jina lake, wapo watu waliokuwa wakifanya kila kitu kwa ajili yake lakini huyu Nasria, hakuwa msichana wa kawaida hata kidogo.
Ulipomuita.
Alikuitikia.
Uliongea naye.
Unamuomba namba ya simu.
Bila hiyana anakupa huku akitabasamu.
Ila ukimpigia na kumwambia ushenzi, anakubloku.
Ndiyo!
Anakubloku.
Kulikuwa na wanaume wengi waliblokiwa na msichana huyo, si kwamba hakutaka kuwa na mwanaume yeyote yule, alitamani lakini alisema hakuwahi kumuona mwanaume muoaji, yaani kwake wote walikuwa wababaishaji tu.
Huyo alikuwa Nasria.
Msichana mzuri kupindukia.
Nasria hakuwa bikira, kwa miaka yake ishirini tayari kulikuwa na wanaume wawili ambao walifanikiwa kumvua nguo zake, wakambakiza mtupu kabisa, kama alivyotoka tumboni mwa mama yake, wakamwambia alale kitandani, alitii na hivyo kumfanya walivyotaka wao.
Aliyemtoa bikira aliitwa Rahim, alidumu naye kwa miezi kadhaa tu, wakaachana, kisa tu alimfumania akiwa na mwanamke mwingine, tena chumbani kwake alipokwenda kumtembelea kwa kushtukiza.
Akajiapiza kwa viapo vyote kwamba asingeweza kuwa na mwanaume yeyote yule, kama ingekuwa rahisi kwake kwenda mahakamani na kuapa, basi angekwenda ili akaape vizuri kuwa hakutaka kuwa na mwanaume yeyote yule kwani kwa jinsi Rahim alivyomfanya, mapenzi yakaingia shubiri na kumuumiza kupita kawaida.
Sasa moyo wake ukachomwa na mkuki.
Ndiyo, mkuki wa mapenzi moyoni mwake.
Moyo ukavuja damu.
Ikachuruzika mpaka kiganjani mwake.
Akalia weee, akajiapiza angekufa akiwa peke yake, kama alivyokuwa amezaliwa leba miaka kadhaa iliyopita. Alibaki na msimamo wake huo kwa miezi michache, lakini kuna siku isiyokuwa na jina, mbele ya macho yake akapita mwanaume mzuri wa sura, moyo wake ukapiga paa! Hakuamini kumuona mwanaume mzuri kama huyo akiishi Tanzania hii.
Alikuwa mrefu.
Maji ya kunde.
Kifua kipana.
Ndevu nyingi kidogo na kichwani alikuwa na upara.
Nasria alibaki akimwangalia mwanaume huyo kwa jinsi alivyokuwa akitembea, alimpenda, moyo wake ukamwambia sasa huyo ndiye alikuwa mwanaume sahihi wa kuwa naye, yaani atengeneze naye familia, wapendane kufa na kuzikana.
Akasahau kiapo chake alichojiwekea, akajiuliza kwani wakati anaapa kulikuwa na mtu aliyemsikia? Hakuna! Alikuwa mahakamani? Hapana! Alishika Msaafu? Hapana! Sasa kwa nini asiamue kujirudi tu?
Kama kulikuwa na watu waliokuwa na kesi walipelekwa mahakamani, wakapewa Biblia ama Msaafu waape na swali la kwanza kwamba walifanya hilo tukio ama la, bado walidanganya kwa kusema hawakufanya, yeye alikuwa nani sasa?
Pale alipokuwa amekaa kibarazani kwao, alitamani kusimama na kumfuata mwanaume huyo. Alikuwa mzuri sana machoni mwake, yaani alijisemea kama kweli wanawake hawakuwa huru kumfuata mwanaume na kumtongoza, basi yeye angekuwa wa kwanza.
Ndiyo!
Angeamua kumfuata tu.
Amwambie kaka nakupenda.
U mzuri sana na nimeshindwa kuvumilia.
Huku akiwa anamwangalia na moyo wake ukiwa na hamu ya kutaka kuzungumza naye, ghafla bin vuu naye akageuza macho na kugongana, tobaaaaa.
Moyo wa Nasria ukapiga paaa! Hakuamini kama angeangaliwa na mwanaume huyo ambaye pia akaamua kutoa tabasamu pana usoni mwake, tabasamu lililomwambia Nasria yeye na majeshi yake waweke silaha chini na kusalimu amri, na kweli wakafanya hivyo.
Alitamani kubaki pale kibarazani alipokaa lakini mwili wake ulitamani kusimama na kumfuata mwanaume huyo, hakuwahi kumuona, hakumjua, hakujua aliitwa nani lakini alitamani sana kumfuata na kuzungumza naye. Huku akiwa hajui nini la kufanya, Mungu akawa upande wake, mwanaume yule akaanza kumfuata yeye.
“Mambo!” alimsalimia baada ya kumfikia, Nasria akapagawa.
“Poa! Karibu!”
“Ahsante sana. Naomba kuuliza,” alimwambia.
“Uliza tu!”
“Namtafuta jamaa mmoja anaitwa Iqram Maduro, aliniambia anaishi huku Magomeni Mapipa, sijui utakuwa unamfahamu?” alimuuliza.
“Oh! I guess!” (Oh! Nadhani) akaingizia Kiingereza safi kidogo, alikwishawahi kusikia mwanamke mzuri akiongea Kiingereza, anakuwa mzuri zaidi, hivyo akafanya kama alivyosikia.
“Anaishi nyumba gani?”
“Wewe nani kwanza?”
“Naitwa Osman!”
“Unaishi wapi?”
“Hapo Kagera Oilcom!”
“Ooh! Sawa. Iqram anaishi nyumba ile pale ya bluu!” alimwambia huku akiinyooshea kidole nyumba hiyo.
“Nashukuru sana!” alisema kijana yule, akaanza kupiga hatua kuelekea mbele kuifuata nyumba ile.
Huku nyuma Nasria alibaki akimwangalia Osman, alitamani kumuita na kumwambia kuna kitu amesahau kumpatia, nacho ni namba ya simu, ampigie na kuzungumza naye.
Huyo Osman alikuwa mzuri.
Ilikuwa vigumu kumuacha tu akiondoka.
Kama kweli alimpenda, basi amwambie tu.
Ghafla akamuona mwanaume huyo akisimama, akageuka na kuanza kurudi nyuma alipokuwa amekaa, akamsogelea huku akiangalia kila upande kama mtu aliyekuwa akiogopa.
“Nimerudi lakini naogopa,” alisema kijana yule.
“Unaogopa nini?”
“Umeolewa?”
“Hapana!”
“Una mchumba?”
“Hapana! Kwani unataka nini?”
“Kitu kimoja tu! Namba yako ya simu, nadhani leo ni siku njema sana kwangu kukutana na msichana mrembo kama wewe. Nimejitahidi sana kuvumilia, niondoke zangu lakini moyo wangu umeniambia weeee, hebu rudi huko,” alisema Osman huku akitoa tabasamu kwa mbali, moyo wa Nasria ukalegea, ukaisha kabisa, yaani ukapagawa kupita kawaida.
“Sina simu!”
“Oh! Huna simu! Kila msichana mrembo hana simu, wale wasichana wabaya wote wana simu. Sawa. Haina shida. Mungu akipenda tutaonana tena,” alisema Osman, hakutaka kubaki, huyo akaanza kuondoka zake.
Nasria sasa akabaki anajuta.
Ndiyo!
Yalikuwa majuto makubwa mno.
Akajiona mjinga.
Tena mama wa wajinga duniani.
Inakuwaje mwanaume umetokea kumpenda, tena umemuona siku hiyo tu akakuomba namba ya simu halafu ukamletea pozi kwa kumwambia huna na wakati unayo? Alihisi labda Osman angembembeleza lakini haikuwa hivyo, akaamua kuondoka zake.
Kichwani mwa Nasria kulimwambia Osman aliamua kufanya hivyo kwa kuwa alikuwa mzuri wa sura, yeye hakutakiwa kumbembeleza mwanamke bali mwanamke alitakiwa kumbembeleza yeye.
Ndiyo!
Hivi mwanaume kama huyo anapata wapi nafasi ya kukubembeleza mwanamke kama wewe? Kwanza kila siku anafuatiliwa na wanawake wazuri, tena zaidi yako.
Ghafla akamuona mwanaume huyo akirudi tena.
“Basi naomba nikupe yangu,” alimwambia.
“Sawa,” akaitikia haraka haraka.
“Naweza kupata kalamu nikuandikie?”
“Usijali! Ngoja nifuate hapo dukani.”
Ilikuwa ni kama bahati, kama wahenga walisema bahati haiji mara mbili basi kwa Nasria ilikuwa tofauti, mwanaume huyo akarudi na kutaka kumwandikia namba ya simu. Hilo likafanyika, namba ikaandikwa na wawili hao kuanza kuwasiliana.
Wakapendana.
Tena sana.
Sana kabisa ila kilichotokea sasa....
Kuna wahenga wa kizazi kipya wakasema mtaachana tu.
Na kweli wakaachana baada ya miezi sita.
Siku walipoachana Nasria alilia sana, hakuamini macho yake kama kweli aliachwa, alimpenda sana Osman, mwanaume huyo alimuacha na kumwambia sasa alitaka kumuoa mchumba wake, alichoka kumsaliti. Alishangaa mno.
Ilikuwaje amwambie hayo? Inamaana yeye hakuwa mchumba wake? Kumbe alipokuwa naye alikuwa na mwanamke mwingine! Halafu hakumwambia, yaani yalikuwa ni mauamivu yake kwa mara nyingine.
Sasa akajiambia ni muda wa kuwa siriazi na viapo vyake, kama kile cha kwanza alikikana na kujiingiza tena kwenye mahusiano, sasa alitakiwa kuwa siriazi kabisa, kama kuapa, sasa aape kikwelikweli, basi akajiapiza zake huku akiugulia maumivu makali moyoni mwake.
Siku zikaenda mbele, zikakatika tu kama kawaida, hazikumsubiri mtu. Akayapiga teke mapenzi, hakutaka kuwa na mwanaume mwingine yeyote yule.
Mwaka wa kwanza ukapita, wa pili ukaingia, ulipofika wa tatu, wazazi wake wakamuita na kumwambia sasa kuna mwanaume amejitokeza, anataka kumuoa, alikuwa akiishi huko Oman.
“Mwanaume gani?” aliuliza kwa mshtuko.
“Utamuona akija,” aliambiwa.
Alichaguliwa mume, kilikuwa kitu asichokipenda kabisa, hizo zama zilikuwa za zamani bwana, si za siku hizi, siku hizi unaingia vitani mwenyewe, unamtafuta mateka wako, unamteka na kuondoka naye, ila si kama zamani.
Hilo hakulipenda lakini akaona bora aolewe, aondoke zake kwani aliamini sasa angeishi maisha ya peke yake, akiwa na mume wake, ampikie, ampakulie, amtengee chakula, akile na akimaliza, aende chumbani na yeye kuliwa.
Moyo wake ukawa na presha ya kumfahamu mwanaume huyo, alitaka kumuona, aliambiwa alitoka huko Oman, bila shaka alikuwa mzuri, labda zaidi ya Rahim na Osman, hivyo akasubiri kwa hamu kubwa mno.
Siku zikakatika, binti wa watu akazidi kujilinda, hakumwambia mtu kuhusu kuolewa huko mpaka pale ambapo angapata nafasi ya kuonana na mwanaume huyo, aolewe na kuondoka zake huku akiacha heshima nyumbani kwao.
Baada ya mwezi mmoja hatimaye ule ugeni uliokuwa ukisubiriwa ukafika, walikuwa wanaume watatu, wote walikuwa na umri kuanzia miaka hamsini, wakakaribishwa nyumbani hapo na kuanza kuzungumza na wazazi wake, walipomaliza akaitwa na kwenda sebuleni kwa heshima zote.
Aliwaangalia watu hao, alihisi labda mwanaume aliyetakiwa kumuoa aliwapeleka watu wake hapo kumuona yeye kwani wote walikuwa wakubwa kiumri, sasa na wazazi wake.
“Ni mwanamke mzuri sana,” alisema mwanaume mmoja.
Huyo ndiye ambaye alitakiwa kumuoa Nasria, alipoambiwa hivyo, alijisikia huzuni moyoni mwake, hakuamini kama mrembo yeye leo alitakiwa kuolewa na mwanaume aliyekuwa na umri kama wa baba yake.
Alimwangalia, alikuwa mwanaume mzee, ndevu nyingi na alionekana kutisha sana, alikuwa mbaya, kitambi kikubwa na alionekana kupenda sana ngono kutokana na ndevu zake zilivyokaa tu. Nasria alitamani kukataa, awakatalie lakini angeanzia wapi?
Unawezaje kuwakatalia wazazi wako?
Hilo likamuogopesha, hakuwa na jinsi, akakubali kuolewa lakini kamwe asingeuruhusu moyo wake umpende hata kidogo, yaani msichana mzuri kama yeye aolewe na mwanaume mtu mzima kama huyo! Tena aje kumpenda! Kwake lilikuwa jambo lisilowezekana hata kidogo.
“Sitoweza kumpenda, sitoweza kuwa naye miaka yote, nitaishi naye kidogo tu na kuomba talaka yangu!” alijisemea huku akimwangalia mwanaume huyo ambaye muda mwingi alikuwa akiifuta simu yake kwa kutumia kitambi chake. Kwa jina aliitwa Hussein Bin Kaifah, moja ya ukoo mkubwa sana huko Oman.

Je, nini kitaendelea?

Kitabu changu cha MZIGO USIO NA ANUANI kitakujia mwezi huu kwa shilingi 10,000 tu.
Capture.JPG


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Nipo seat ya mbele kabisa mubashara na Medusa twende kazi poti
 
NYEMO CHILONGANI

0718069269

Sehemu ya 01

Ndiyo ni mzuri!
Tena hasaaa!
Kwanza ni mweupe.
Ana mwili ulionyambulika.
Macho ya goroli, ya kurembua ambapo akiamua kukuangalia, basi tuseme umepata bahati ya kuangaliwa na mwanamke mzuri, inawezekana kuliko wote waliokuwa wakikaa jijini Dar es Salaam.
Kwa jina aliitwa Nasria Abdul, msichana aliyekuwa na mchanganyiko wa rangi, baba yake alikuwa Mwarabu wa Oman aliyezaliwa na kukulia Zanzibar huku mama yake akiwa Mzigua kutoka Handeni, jijini Tanga.
Nasria alikuwa na uzuri wa asili, alivutia, alipendeza kila alipokuwa akitembea, alijua kuringa, kama watu walisema twiga walikuwa wakitembea kwa maringo, basi tuseme hao twiga walijifunza kwa binti huyu mrembo namna ya kutembea.
Naam!
Alijua kutembea.
Alirusha mikono yake kwa madaha.
Alikilegeza kiuno chake.
Kifua saa sita.
Huku lipsi zake nene na laini akipenda kuzipitishia ulimi.
Kila aliyekuwa akiziangalia, alitamani kuzinyonya, tena azinyonye hasa, azipake hata asali, halafu azinyonye tena mpaka asali iishe mdomoni, yaani huyu msichana hakuisha hamu hata kidogo, na kama ungepewa karatasi uandike sifa za uzuri wake, si ajabu ukajaza kitabu kikubwa na bado isitoshe kuzimaliza.
Nasria alikuwa akiishi Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam, mahali kulipokuwa na wanawake wengi wa Kipemba, waliojua kuvaa, kunukia na hata kuringa. Nasria alikuwa miongoni mwao, alikuwa binti mrembo kupita kawaida, halafu hakuwa yule mwepesi kwamba mwanaume huyu akienda, amvulie nguo, yule akienda basi aende nyumbani kwake.
Huyu Nasria alikuwa tofauti kabisa. Alijiheshimu, alikuwa na nidhamu na kitu kikubwa kabisa alikuwa msafi, tena msafi sana, yaani hakuwahi kunuka kwapa wala jasho, hakuwahi kunuka sehemu yoyote ile mwilini mwake, na endapo ungebahatika kuvuliwa nguo na msichana huyu, basi ungesema sasa uliingia kwenye duka la manukato, yaani alinukia kila harufu ya pafyumu.
Unadhani kuna mtu Magomeni ambaye hakuwa akimfahamu msichana huyu? Atoke wapi? Wanaume wote waroho walimtamani, kulikuwa na wanamuziki waliokuwa wakimuimbia yeye tu, kuna waandishi walikuwa wakiandika simulizi na kulitumia jina lake, wapo watu waliokuwa wakifanya kila kitu kwa ajili yake lakini huyu Nasria, hakuwa msichana wa kawaida hata kidogo.
Ulipomuita.
Alikuitikia.
Uliongea naye.
Unamuomba namba ya simu.
Bila hiyana anakupa huku akitabasamu.
Ila ukimpigia na kumwambia ushenzi, anakubloku.
Ndiyo!
Anakubloku.
Kulikuwa na wanaume wengi waliblokiwa na msichana huyo, si kwamba hakutaka kuwa na mwanaume yeyote yule, alitamani lakini alisema hakuwahi kumuona mwanaume muoaji, yaani kwake wote walikuwa wababaishaji tu.
Huyo alikuwa Nasria.
Msichana mzuri kupindukia.
Nasria hakuwa bikira, kwa miaka yake ishirini tayari kulikuwa na wanaume wawili ambao walifanikiwa kumvua nguo zake, wakambakiza mtupu kabisa, kama alivyotoka tumboni mwa mama yake, wakamwambia alale kitandani, alitii na hivyo kumfanya walivyotaka wao.
Aliyemtoa bikira aliitwa Rahim, alidumu naye kwa miezi kadhaa tu, wakaachana, kisa tu alimfumania akiwa na mwanamke mwingine, tena chumbani kwake alipokwenda kumtembelea kwa kushtukiza.
Akajiapiza kwa viapo vyote kwamba asingeweza kuwa na mwanaume yeyote yule, kama ingekuwa rahisi kwake kwenda mahakamani na kuapa, basi angekwenda ili akaape vizuri kuwa hakutaka kuwa na mwanaume yeyote yule kwani kwa jinsi Rahim alivyomfanya, mapenzi yakaingia shubiri na kumuumiza kupita kawaida.
Sasa moyo wake ukachomwa na mkuki.
Ndiyo, mkuki wa mapenzi moyoni mwake.
Moyo ukavuja damu.
Ikachuruzika mpaka kiganjani mwake.
Akalia weee, akajiapiza angekufa akiwa peke yake, kama alivyokuwa amezaliwa leba miaka kadhaa iliyopita. Alibaki na msimamo wake huo kwa miezi michache, lakini kuna siku isiyokuwa na jina, mbele ya macho yake akapita mwanaume mzuri wa sura, moyo wake ukapiga paa! Hakuamini kumuona mwanaume mzuri kama huyo akiishi Tanzania hii.
Alikuwa mrefu.
Maji ya kunde.
Kifua kipana.
Ndevu nyingi kidogo na kichwani alikuwa na upara.
Nasria alibaki akimwangalia mwanaume huyo kwa jinsi alivyokuwa akitembea, alimpenda, moyo wake ukamwambia sasa huyo ndiye alikuwa mwanaume sahihi wa kuwa naye, yaani atengeneze naye familia, wapendane kufa na kuzikana.
Akasahau kiapo chake alichojiwekea, akajiuliza kwani wakati anaapa kulikuwa na mtu aliyemsikia? Hakuna! Alikuwa mahakamani? Hapana! Alishika Msaafu? Hapana! Sasa kwa nini asiamue kujirudi tu?
Kama kulikuwa na watu waliokuwa na kesi walipelekwa mahakamani, wakapewa Biblia ama Msaafu waape na swali la kwanza kwamba walifanya hilo tukio ama la, bado walidanganya kwa kusema hawakufanya, yeye alikuwa nani sasa?
Pale alipokuwa amekaa kibarazani kwao, alitamani kusimama na kumfuata mwanaume huyo. Alikuwa mzuri sana machoni mwake, yaani alijisemea kama kweli wanawake hawakuwa huru kumfuata mwanaume na kumtongoza, basi yeye angekuwa wa kwanza.
Ndiyo!
Angeamua kumfuata tu.
Amwambie kaka nakupenda.
U mzuri sana na nimeshindwa kuvumilia.
Huku akiwa anamwangalia na moyo wake ukiwa na hamu ya kutaka kuzungumza naye, ghafla bin vuu naye akageuza macho na kugongana, tobaaaaa.
Moyo wa Nasria ukapiga paaa! Hakuamini kama angeangaliwa na mwanaume huyo ambaye pia akaamua kutoa tabasamu pana usoni mwake, tabasamu lililomwambia Nasria yeye na majeshi yake waweke silaha chini na kusalimu amri, na kweli wakafanya hivyo.
Alitamani kubaki pale kibarazani alipokaa lakini mwili wake ulitamani kusimama na kumfuata mwanaume huyo, hakuwahi kumuona, hakumjua, hakujua aliitwa nani lakini alitamani sana kumfuata na kuzungumza naye. Huku akiwa hajui nini la kufanya, Mungu akawa upande wake, mwanaume yule akaanza kumfuata yeye.
“Mambo!” alimsalimia baada ya kumfikia, Nasria akapagawa.
“Poa! Karibu!”
“Ahsante sana. Naomba kuuliza,” alimwambia.
“Uliza tu!”
“Namtafuta jamaa mmoja anaitwa Iqram Maduro, aliniambia anaishi huku Magomeni Mapipa, sijui utakuwa unamfahamu?” alimuuliza.
“Oh! I guess!” (Oh! Nadhani) akaingizia Kiingereza safi kidogo, alikwishawahi kusikia mwanamke mzuri akiongea Kiingereza, anakuwa mzuri zaidi, hivyo akafanya kama alivyosikia.
“Anaishi nyumba gani?”
“Wewe nani kwanza?”
“Naitwa Osman!”
“Unaishi wapi?”
“Hapo Kagera Oilcom!”
“Ooh! Sawa. Iqram anaishi nyumba ile pale ya bluu!” alimwambia huku akiinyooshea kidole nyumba hiyo.
“Nashukuru sana!” alisema kijana yule, akaanza kupiga hatua kuelekea mbele kuifuata nyumba ile.
Huku nyuma Nasria alibaki akimwangalia Osman, alitamani kumuita na kumwambia kuna kitu amesahau kumpatia, nacho ni namba ya simu, ampigie na kuzungumza naye.
Huyo Osman alikuwa mzuri.
Ilikuwa vigumu kumuacha tu akiondoka.
Kama kweli alimpenda, basi amwambie tu.
Ghafla akamuona mwanaume huyo akisimama, akageuka na kuanza kurudi nyuma alipokuwa amekaa, akamsogelea huku akiangalia kila upande kama mtu aliyekuwa akiogopa.
“Nimerudi lakini naogopa,” alisema kijana yule.
“Unaogopa nini?”
“Umeolewa?”
“Hapana!”
“Una mchumba?”
“Hapana! Kwani unataka nini?”
“Kitu kimoja tu! Namba yako ya simu, nadhani leo ni siku njema sana kwangu kukutana na msichana mrembo kama wewe. Nimejitahidi sana kuvumilia, niondoke zangu lakini moyo wangu umeniambia weeee, hebu rudi huko,” alisema Osman huku akitoa tabasamu kwa mbali, moyo wa Nasria ukalegea, ukaisha kabisa, yaani ukapagawa kupita kawaida.
“Sina simu!”
“Oh! Huna simu! Kila msichana mrembo hana simu, wale wasichana wabaya wote wana simu. Sawa. Haina shida. Mungu akipenda tutaonana tena,” alisema Osman, hakutaka kubaki, huyo akaanza kuondoka zake.
Nasria sasa akabaki anajuta.
Ndiyo!
Yalikuwa majuto makubwa mno.
Akajiona mjinga.
Tena mama wa wajinga duniani.
Inakuwaje mwanaume umetokea kumpenda, tena umemuona siku hiyo tu akakuomba namba ya simu halafu ukamletea pozi kwa kumwambia huna na wakati unayo? Alihisi labda Osman angembembeleza lakini haikuwa hivyo, akaamua kuondoka zake.
Kichwani mwa Nasria kulimwambia Osman aliamua kufanya hivyo kwa kuwa alikuwa mzuri wa sura, yeye hakutakiwa kumbembeleza mwanamke bali mwanamke alitakiwa kumbembeleza yeye.
Ndiyo!
Hivi mwanaume kama huyo anapata wapi nafasi ya kukubembeleza mwanamke kama wewe? Kwanza kila siku anafuatiliwa na wanawake wazuri, tena zaidi yako.
Ghafla akamuona mwanaume huyo akirudi tena.
“Basi naomba nikupe yangu,” alimwambia.
“Sawa,” akaitikia haraka haraka.
“Naweza kupata kalamu nikuandikie?”
“Usijali! Ngoja nifuate hapo dukani.”
Ilikuwa ni kama bahati, kama wahenga walisema bahati haiji mara mbili basi kwa Nasria ilikuwa tofauti, mwanaume huyo akarudi na kutaka kumwandikia namba ya simu. Hilo likafanyika, namba ikaandikwa na wawili hao kuanza kuwasiliana.
Wakapendana.
Tena sana.
Sana kabisa ila kilichotokea sasa....
Kuna wahenga wa kizazi kipya wakasema mtaachana tu.
Na kweli wakaachana baada ya miezi sita.
Siku walipoachana Nasria alilia sana, hakuamini macho yake kama kweli aliachwa, alimpenda sana Osman, mwanaume huyo alimuacha na kumwambia sasa alitaka kumuoa mchumba wake, alichoka kumsaliti. Alishangaa mno.
Ilikuwaje amwambie hayo? Inamaana yeye hakuwa mchumba wake? Kumbe alipokuwa naye alikuwa na mwanamke mwingine! Halafu hakumwambia, yaani yalikuwa ni mauamivu yake kwa mara nyingine.
Sasa akajiambia ni muda wa kuwa siriazi na viapo vyake, kama kile cha kwanza alikikana na kujiingiza tena kwenye mahusiano, sasa alitakiwa kuwa siriazi kabisa, kama kuapa, sasa aape kikwelikweli, basi akajiapiza zake huku akiugulia maumivu makali moyoni mwake.
Siku zikaenda mbele, zikakatika tu kama kawaida, hazikumsubiri mtu. Akayapiga teke mapenzi, hakutaka kuwa na mwanaume mwingine yeyote yule.
Mwaka wa kwanza ukapita, wa pili ukaingia, ulipofika wa tatu, wazazi wake wakamuita na kumwambia sasa kuna mwanaume amejitokeza, anataka kumuoa, alikuwa akiishi huko Oman.
“Mwanaume gani?” aliuliza kwa mshtuko.
“Utamuona akija,” aliambiwa.
Alichaguliwa mume, kilikuwa kitu asichokipenda kabisa, hizo zama zilikuwa za zamani bwana, si za siku hizi, siku hizi unaingia vitani mwenyewe, unamtafuta mateka wako, unamteka na kuondoka naye, ila si kama zamani.
Hilo hakulipenda lakini akaona bora aolewe, aondoke zake kwani aliamini sasa angeishi maisha ya peke yake, akiwa na mume wake, ampikie, ampakulie, amtengee chakula, akile na akimaliza, aende chumbani na yeye kuliwa.
Moyo wake ukawa na presha ya kumfahamu mwanaume huyo, alitaka kumuona, aliambiwa alitoka huko Oman, bila shaka alikuwa mzuri, labda zaidi ya Rahim na Osman, hivyo akasubiri kwa hamu kubwa mno.
Siku zikakatika, binti wa watu akazidi kujilinda, hakumwambia mtu kuhusu kuolewa huko mpaka pale ambapo angapata nafasi ya kuonana na mwanaume huyo, aolewe na kuondoka zake huku akiacha heshima nyumbani kwao.
Baada ya mwezi mmoja hatimaye ule ugeni uliokuwa ukisubiriwa ukafika, walikuwa wanaume watatu, wote walikuwa na umri kuanzia miaka hamsini, wakakaribishwa nyumbani hapo na kuanza kuzungumza na wazazi wake, walipomaliza akaitwa na kwenda sebuleni kwa heshima zote.
Aliwaangalia watu hao, alihisi labda mwanaume aliyetakiwa kumuoa aliwapeleka watu wake hapo kumuona yeye kwani wote walikuwa wakubwa kiumri, sasa na wazazi wake.
“Ni mwanamke mzuri sana,” alisema mwanaume mmoja.
Huyo ndiye ambaye alitakiwa kumuoa Nasria, alipoambiwa hivyo, alijisikia huzuni moyoni mwake, hakuamini kama mrembo yeye leo alitakiwa kuolewa na mwanaume aliyekuwa na umri kama wa baba yake.
Alimwangalia, alikuwa mwanaume mzee, ndevu nyingi na alionekana kutisha sana, alikuwa mbaya, kitambi kikubwa na alionekana kupenda sana ngono kutokana na ndevu zake zilivyokaa tu. Nasria alitamani kukataa, awakatalie lakini angeanzia wapi?
Unawezaje kuwakatalia wazazi wako?
Hilo likamuogopesha, hakuwa na jinsi, akakubali kuolewa lakini kamwe asingeuruhusu moyo wake umpende hata kidogo, yaani msichana mzuri kama yeye aolewe na mwanaume mtu mzima kama huyo! Tena aje kumpenda! Kwake lilikuwa jambo lisilowezekana hata kidogo.
“Sitoweza kumpenda, sitoweza kuwa naye miaka yote, nitaishi naye kidogo tu na kuomba talaka yangu!” alijisemea huku akimwangalia mwanaume huyo ambaye muda mwingi alikuwa akiifuta simu yake kwa kutumia kitambi chake. Kwa jina aliitwa Hussein Bin Kaifah, moja ya ukoo mkubwa sana huko Oman.

Je, nini kitaendelea?

Kitabu changu cha MZIGO USIO NA ANUANI kitakujia mwezi huu kwa shilingi 10,000 tu.View attachment 1718533

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Napenda sana uandishi wako jinsi unavyopangilia tukio baada ya tukio na upangiliaji wa sarufi big up Bro
 
NYEMO CHILONGANI
MEDUSA: MALKIA WA DAMU
0718069269

SEHEMU YA 02

Kwa nchini Oman kulikuwa na koo mbalimbali zilizokuwa na sifa kemkem. Wapo waliokuwa maarufu kwa kuwa na wasichana warembo, wapo waliokuwa na sifa za kuwa matajiri na pia kulikuwa na koo ambazo zilitoa sana viongozi wa dini na nchi.
Kila koo nchini Oman ilikuwa na sifa yake, hasa zile koo kubwa ambazo zilikuwa kama nne, maarufu na zilijulikana kila kona, miongoni mwa koo hizo kulikuwa na ukoo uitwao Kaifah, ukoo mkubwa uliyokuwa na sifa kubwa ya kuwa na uchawi wa kutisha.
Ukoo huo uliogopeka kila kona, watu waliotoka humo waliogopwa kama ukoma, hapakuwa na mtu ambaye alibishana na watu wa ukoo huo kwani walijua kutumia uchawi, walijua kufanya kila jambo kwa njia ya kishirikina.
Nchini Oman ukoo huo ulikuwa na watu wasiopungua elfu hamsini, ilikuwa moja ya koo kubwa sana nchini humo. Pamoja na kujulikana kwa uchawi sana lakini ukoo huo ulikuwa mkongwe kuliko zote, ulianza tangu huko karne ya saba na wao walijiweka zaidi kwenye mambo ya uchawi tu.
Waliamini uchawi zaidi ya walivyokuwa wakimwamini Mungu, kwenye kila kitu walichokuwa wakikifanya, kitu cha kwanza kilikuwa ni uchawi. Watu ambao walicheza na watu hao, walipotea kwenye mazingira ya kutatanisha, wengine walikuwa mataahira na wengine kuugua magonjwa makubwa na kufariki dunia.
Viongozi waliokuwa wakipitishwa kuongoza nyadhifa mbalimbali nchini humo kitu cha kwanza kilikuwa ni kufikishwa kwenye vijiji vya ukoo huo na kuwekewa zindiko kubwa, lililokuwa likiwafanya kuwa imara na nguvu kubwa zaidi.
Japokuwa koo mbalimbali hawakuwa wakiruhusiwa kuoa watu wa koo tofauti lakini ilikuwa ni tofauti kwa hii ya Kaifah, ulikuwa ukoo wenye uhuru wa kuoa sehemu yoyote ile ila kitu ambacho hawakutaka kabisa kuona kikitokea ni kuacha mambo ya kichawi, waliamini uchawi ndiyo ulikuwa na nguvu kubwa namba mbili nyuma ya Mungu.
Ni miaka mingi tu ikapita, karne zilisonga mbele huku hofu kubwa ya watu wa Oman ikiwa kwenye ukoo huo, watu walizaliana na kuzaliana na ndipo alipokuja kuzaliwa mtu aliyeitwa kwa jina la Hussein.
Tangu alipokuwa kijana mdogo kila mmoja alimtabiria angekuja kuwa na uzuri wa sura hapo baadaye na angekuwa chachu kubwa kwa akina dada wa kipindi hicho cha ujana wake.
Kila mtu aliyemwangalia, alimsifu Mungu kwa kujua kumuumba mtoto huyo, alivutia na wasichana wengi wa umri wake waliokuwa wakimwangalia, kila mmoja akapata wivu wa kutamani kuwa naye.
Pamoja na kutoka kwenye ukoo uliokuwa na nguvu kubwa ya kichawi lakini Hussein alijitahidi sana kufanya biashara, alikuwa mtafutaji, alisafiri nchi nyingi kufanya biashara, alianzisha kampuni yake ya kutengeneza viatu nchini Uingereza, akapata pesa na kuwekeza sehemu mbalimbali.
Alikuwa na utajiri mkubwa na ulevi wake mkubwa ulikuwa mmoja tu, wanawake.
Ndiyo! Wanawake.
Alipenda wanawake kuliko chakula, aliwapenda kuliko maji, kwake kulala na wanawake ilikuwa ni kama ibada kwenye maisha yake. Hakuwa akiridhika, alikuwa mtu wa kubadilisha tu, leo alilala na huyu, kesho yule na keshokutwa na mwingine.
Wazazi wake waliongea sana, walimuweka vikao na kumwambia mambo mengi lakini wala hakubadilika, aliendelea na hali yake ileile, aliwabadilisha wanawake kama alikuwa akibadilisha nguo.
Baada ya kufikisha miaka ishirini na mbili, akaambiwa aoe, hakuwa na kipingamizi, akaamua kuwaheshimu wazazi wake kwenye hilo na hivyo kumuoa msichana mmoja mrembo aliyeitwa kwa jina la Aishar.
Aishar alikuwa mmoja wa wanawake waliokuwa wakivutia kwa mvuto, alikuwa na uzuri wa ajabu sana, wanaume wengi walimfuata, walimkosa na kufanikiwa kumpata huyo Hussein.
Kuwa na Aishar hakuwa akijiamini, alihisi inawezekana ingetokea siku moja kuondoka mikononi mwake hivyo kitu alichokifanya ni kumloga kwa uchawi wao, Aishar akatokea kumpenda, akafa na kuoza kwake, akawa haambiwi wala hasikii, na akawa na wivu mkubwa.
Wakapendana, maisha yalikuwa ya raha, wakapata watoto huku Hussein akiendelea kutembea na wanawake wengine kwa siri kubwa kwani bado pepo la ngono lilikuwa likimuendesha kupita kawaida.
Aliendelea na maisha hayo mpaka alipofikisha umri wa miaka arobaini na nane, mkewe akafa kwenye mazingira ya kutatanisha, wengi wakasema alimtoa kafara kwani baada ya kifo cha mkewe, biashara zake zilichanganya.
Japokuwa watu waliongea mengi lakini hakutaka kujali, aliendelea na maisha yake na baada ya kipindi fulani kwenda Zanzibar kutembea ndipo akaambiwa kuhusu msichana Nasria. Aliambiwa na rafiki yake jinsi alivyokuwa mzuri, alivyokuwa gumzo na watu wote kumtaka.
Alisifiwa sana na kuhitaji kumuona, hilo halikuwa tatizo, akaambiwa ajiandae kwani angepelekwa mpaka nyumbani kwao jijini Dar es Salaam na kuonana na msichana huyo mrembo.
Kwa kuwa alimwamini sana rafiki yake, alichomwambia ni mpango wa kumuoa mwanamke huyo, kama kweli alikuwa mzuri kama alivyomwambia basi ilikuwa ni lazima kumuoa, wakakubaliana na hatimaye kuwasiliana na wazazi wake ambao wala hawakuwa na shida, nao wakakubali na hivyo kilichobaki ni yeye kwenda jijini humo kwa lengo la kuonana naye.
Siku ya kwanza kumuona, hakika alichanganyikiwa, alipewa sifa nyingi kuhusu msichana huyo lakini akaamini alidanganywa kwani huyo Nasria alikuwa mzuri zaidi ya zile sifa alizoambiwa, alikuwa mithili ya malaika, yaani kwenye watu wazuri duniani, naye alikuwa nafasi za juu.
Hakuyapepesa macho yake, alibaki akimwangalia, hakika kwa uzuri ule alitakiwa kuwa mrithi sahihi wa mke wake, hakutaka kujali umri, mwanaume huwa hazeeki kwa mwanamke na hicho ndicho ambacho alikiamini siku zote katika maisha yake.
“Ni msichana mrembo sana,” alisema, alikuwa akimwambia rafiki yake.
“Umempenda?”
“Sana aisee! Ni mrembo mno!”
“Basi haina shida.”
Wazazi wa Nasria waliposikia Hussein amemkubali binti yao, wakafurahi na hatimaye ndugu kuambiwa na siku ya harusi kutajwa huku Nasria akitakiwa kuolewa na kuondoka zake kuelekea nchini Oman.
Upande wa pili msichana huyo hakuwa na furaha hata kidogo. Aliambiwa kuhusu Hussein kwamba alikuwa na pesa, tajiri mkubwa na alikuwa na heshima nchini Oman lakini kwake hakutaka kukubaliana naye, yaani hayo hayakumfanya kubadili uamuzi wake wa kutokumpenda na siku moja kuomba talaka yake.
Msichana mrembo kama yeye alitakiwa kuwa na mwanaume mzuri, kijana mwenzake, wakue, wazeeke pamoja lakini si kwa mzee kama Hussein, yaani ingekuwaje aishi naye, awe anamuita mume wangu ama baba?
Pamoja na kutokutaka kumpenda kwa dhati lakini huyo ndiye akamuoa, harusi kubwa ikafanyika Kariakoo na baada ya hapo, wakaondoka na kuelekea Zanzibar kula raha kwanza kabla ya kurudi nchini Oman.
Nasria hakuwa na furaha, alionekana kuwa na majonzi moyoni mwake, alimwangalia mume wake, hakumpenda, aliulazimisha moyo wake umpende lakini alishindwa kabisa, alitamani kumwambia hilo lakini aliogopa kufanya hivyo.
Ni kweli aliogopa.
Wazazi wake wangemfikiriaje?
Vipi kuhusu marafiki?
Na wale maadui?
Hakika alikuwa kwenye wakati mgumu.
Usiku walipokuwa wakilala, aligeukiwa na kushikwa mgongo, mkono wa Hussein ulikuwa ukipita mgongoni mwake, alicheza mgongo huo na kushuka chini mpaka kiunoni. Kwa kuwa alikuwa mtu wa wanawake, alijua ni kwa namna gani alitakiwa kumdatisha mwanamke.
Nasria hakutaka kabisa ila kuna maeneo alipokuwa akishikwa, bila ajizi mdomo wake ukaanza kutoa mguno wa mahaba huku akimtaka mwanaume huo aendelee zaidi na zaidi, mwisho wa siku akamkuta akiwa juu ya kifua chake na kuanza kufanya mapenzi.
Hakufurahia tendo, alifanya kama kumridhisha lakini hakika hakuwa na furaha hata kidogo. Mumewe aliligundua hilo na mara kibao alikuwa akimuuliza tatizo lilikuwa nini lakini hakutaka kumwambia ukweli, alimwambia anaumwa, mara anajisikia vibaya.
Walipanga kukaa Zanzibar kwa mwezi mzima, hizo siku zilikuwa ni za mateso kweli kwa Nasria, kila alipokuwa akimsogelea mume wake, alisikia harufu ya uzee wake, ilimchefua kupita kawaida, alitamani kukimbia lakini kila siku alijiambia nitakimbia kesho.
Kwa kuwa tayari alizijua akaunti za mume wake, akatamani kumuibia pesa kiasi fulani na kisha kumkimbia, hakutaka kufikia nyumbani kwao, kwa pesa ambazo angeziiba basi angeanzisha maisha yake mengine jijini Dar es Salaam.
Akatamani kuwa na kadi ile, na ili kuipata alitakiwa kuonyesha mapenzi mazito, hilo halikuwa tatizo, akaanza kuonyesha, penzi likamvuruga Hussein na hata alipoulizwa mambo mengi kuhusu kadi yake, hakuwa na jinsi, alimwambia kila kitu.
Hilo likawa kosa.
Msichana huyo akataka kuutumia mwanya huo.
Akahamisha kiasi cha dola elfu hamsini kwenda kwenye akaunti yake, pesa nyingi, zaidi ya shilingi milioni mia moja na ishirini, alipofanikiwa, akapanga mipango yake. Kichwa chake kikajifikiria ni kwa namna gani angeweza kuondoka Zanzibar na kuelekea Dar es Salaam, aliogopa kutumia boti hivyo ilikuwa ni lazima atumie njia nyingine.
Akawasiliana na rafiki yake aitwaye kwa jina la Zuhura na kumuuliza, msichana huyo ndiye aliyemwambia atumie mtumbwi, kulikuwa na vijana wengi waliokuwa wakitumia mitumbwi kutoka Zanzibar kwenda jijini Dar es Salaam kwa kupitia Bagamoyo ambapo kwake ilionekana kuwa sehemu salama zaidi kuliko Dar es Salaam ambapo alihisi angeweza kukutana hata na ndugu yake yeyote bandarini.
“Basi naomba unipeleke, mimi sijui nitapapata vipi huko kwenye mitumbwi,” alimwambia.
“Haina shida. Nitakusaidia shoga’ angu, najua umepata tabu sana kuishi na huyo babu!” alisema Zuhura huku kicheko chake kikisikika kwenye simu.
Nasria hakulala, usiku wa saa sita, akayatupia macho kwa mume wake, alikuwa akikoroma tu, alilala usingizi fofofo, akaanza kujitoa kitandani pale, akachukua begi lake na kuanza kuweka nguo zake, aliweka nguo zote ndani ya begi na kuanza kuondoka humo.
Akasahau chupi yake.
Ndiyo! Aliisahau kabatini bila kujua.
Likawa kosa kubwa.
Akakishika kitasa, akakinyonga na kuufungua mlango na kilichofuata ni kuondoka mahali hapo na kutokomea zake, baada ya dakika chache, akaonana na Zuhura, akamchukua na kwenda naye mahali kulipokuwa na mitumbwi, akaingia.
“Tutaonana shoga ‘angu, mimi siwezi kukaa na kile kibabu,” alisema Nasria, sasa alikuwa akitamba, hakumtaka mzee Hussein, alitaka kuwa na maisha yake.
Baharini ilikuwa ni usiku, upepo ulikuwa ukivuma, ndani ya mtumbwi hakuwa peke yake, kulikuwa na watu wengine kama wanne ukiachana na mmiliki wa mtumbwi huo aliyekuwa akipiga kasia na mwenzake. Alilivaa begi lake, alikuwa kiogopa kwa kuhisi angeweza kuzama na kupotea baharini.
Moyoni mwake alikuwa akimuomba Mungu, alihisi kabisa angeweza kufa na kupotea, alisali kimoyomoyo mpaka baada ya saa tano ndipo mtumbwi ukaanza kuingia katika pwani ya Bagamoyo huku tayari ikiwa ni saa kumi na mbili asubuhi.
“Allahamdulilah!” alijisemea, akateremka na wenzake na kuanza kuondoka, sasa akaanza kukitafuta kituo cha daladala, alipokipata, akapanda na kuanza safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam huku akitaka kufanya siri kubwa, ajifiche, hata kama angetafutwa vipi, hakika asionekane.
Awe na maisha yake.
Atanue atakavyo na pesa alizomuibia mume wake.

Je, nini kitaendelea?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom