Mechanical engineers wa Tanzania wana msaada gani kwa nchi?

Mechanical engineers wa Tanzania wana msaada gani kwa nchi?

RAYAN THE DON

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2019
Posts
679
Reaction score
1,220
Habari wanaJF?

Hivi hawa MECHANICAL ENGINEERS wana kazi gani hapa nchini Tanzani?

Nashindwa kuwaelewa kabisa kwa sababu wana ujuzi na hicho walichokisomea lakini wanshindwa kutumia huo ujuzi wao kusaidia jamii. Au elimu yenu ipo kwenye makaratasi? mfano kwa sasa tumekumbwa na janga la COVID19 ambapo tunatakiwa tuwe na vifaa vya kutosha kama VENTILATORS. Cha kushangaza hawa wenye ujuzi wao wamekaa tu na vyeti vyao badala ya kuingia maabara kutengeneza hivi vifaa ili kusaidia watu wenye maambukizi ya ugonjwa wa COrona.

Nyie ni watu wa aina gani? kwanini mnataka tuagize hivi vifaa huko nchi za nje wakati tuna wataalamu wanakula mishahara ya bure? changamkeni acheni uzwazwa wa kulalalia mavyeti yenu.
kwanini mnapenda kuwa nyuma na kujifananisha na watu waliosoma Political Science?

Hakika aliyesoma Political Science au Sociology nchini Tanzania ana msaada mkubwa sana kuliko engineers na doctors.

Kweli elimu siyo vyeti, elimu ni kile ulichonacho kichwani mwako.


Karibuni kwa michango wakuu,

Ahsanteni.
 
Kwanza ungejiuliza yafatayo
Investment yoyote inahitaji:-

1. Mtaji/ capital ..... je upo?

2. Availability ya resources .... je vipo?

3. Utayari wa serikali .... imewaandaaje wasomi wetu.

Mtaji
Unahita fedha na eneo, hakuna fedha kwa maana yoyote.... wanatengeneza kivipi?

a) conceptual phase inagharama zake

b) design phase inagharama zake

c) Implementation/manufacturing inagharama zake

d) Testing/quality assurance inagharama zake

Lawama zote ipewe serikali ya ccm kushindwa kuwekeza kwa vijana kivitendo. Wamewekeza katika kuimba ccm, ccm, ccm ushenzi mtupu

HAKUNA Karakana zilizoboreshwa kitaalamu....manufacturing centre zikiwa na: -

I) Raslimali watu
II) Malighafi
III) mitambo .... vitendea kazi mbalimbali
IV) vijana walioandaliwa vema

Cha ajabu siku hizi hata sehemu za kufanya Elimu kwa vitendo nikama hazipo.

Serikali isipokuwa na sera wala mikakati bora katika uwekezaji kwa wasomi wetu tutarajie kuwa na taifa la wajinga katika secta zote. Biashara, uzalishaji nk

Ndio maana nadharia ya kujiajiri inabakia midomoni kwa wanasiasa na Vilaza wengine wasioweza kuchanganua mahitajio sahihi ya kiuwezo ilikujiajiri.

Vijana wasomi wa discipline mbalimbali wapo wanazubaa tu sababu sera na mikakati yetu haiwajengi wala kuwawezesha kujiajili.

CCM NDIO TATIZO
 
Watu waliofeli hesabu wanahasira sana na maengineer...hao Engineers Watoe Wapi capital ya kutengeneza hizo mashine kama sio hao politiko sayansi wako na wanasiasa kutengeneza sera nzuri za kuwawezesha


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kitu kidogo sana hicho kuki design aisee, dont blame on us, you better start with your government bro. Niliwahi kuandaa proposal ya project plus drawings na kila detail lakini nahisi jamaa washavutia ganja hayo makaratasi.
 
Tusiangalie sana tulipoangukia,japo kuna juhudi za kujikinga na covid -19 bali tujitahidi kufanya reseach kupata dawa ya kuutibu ugonjwa huo hasa kwa waliosomea mambo ya medicine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahahahaha nacheka kama mazuri vile..watu huwa wanajiuliza Africa ina maprofesa, madr, maengineer na wasomi kila mahala lakini mbona wanashindwa kuvitoa walivyosoma kwenda kwenye uhalisia? Inawezekana wakoloni walituletea elimu fake na tunahitaji ukombozi mwingine ili tupate elimu halisi.
 
Hawa mainjinia unawaonea bure, hawana nyenzo zozote za kuwasaidia. kuna njemba moja huwa inabwata sana kwenye vyombo vya habari kuhusu korona, inavyoelekea inaijua korona zaidi ya dr Fauci, yule top expert wa magonjwa ya kuambukiza kule marekani, tuendelee kumsikiliza huyu top expert wetu...
 
Mkuu, naona leo umenigusa kwenye kilindi cha moyo wangu. Lakini bahatimbaya sana sijaelewa ama nahisi umechanganya mambo mbili zinazo shabihiana.
Kwani ulitaka kumaanisha Ventilations ama Oxygen..??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unawalaumu M.engineer badala uilaumu serikali yako iliyoshindwa kuwekeza kwenye sekta ya Science na Technology

Kwataarifa yako serikali yako sasa iko bize na kupokea misaada ya fedha baada ya hapo hizo fedha zitatumika Kununulia Wapinzani,na kuendesha uchakuzi feki.
 
Umesikia ventileta zikihitajika tanzania? au hata serikali umeisikia ikihitaji ventileta?
 
kusoma miaka mitano hakukupi guarantee ya kutengeneza ivo vifaa bila ya kuwa na pesa ya kutosha + imagination nzur ya scientists wetu. sio elimu yetu ya kumezeshana mambo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza, ulichokisema hakinishawishi hata kidogo mkuu. Uwezo na ujuzi wako ni mtaji tosha kabisa. Show your ability/skills the world will support you. Sasa jitu linakaa ndani na kulalia mavyeti yake. haliwezi hata kuweka ujuzi wake into practice ila anapambna na theories tu ambazo hazina manufaa yoyote.

Pili, unaposema utayari wa serikali unamaanisha nini? kama wewe haupo tayari kuonesha ujuzi na uwezo wako kivipi serikali itakuwa tayari na wewe?

Tatu, Umesoma taaluma ya Uhandisi, Udaktari/Phamsia bado unataka uajiriwe? huo ni uoga wa maisha na uzwazwa na kutokuamini uwezo na ujuzi wako ulioupata huko mshuleni. Smart and intelligent people cannot be employed kwa sababu hawatakuwa huru kuonesha uwezo na ujuzi wao na ndiyo maana huwa wanataka wawe huru na siyo kutumikishwa.

Nne, sitaki uje na lame excuse kwamba mfumo wa elimu yetu mbaya. Kama mfumo mbaya ulienda shule ili iweje? ulienda kupoteza muda wako au? Maana ya mtu msomi ni kwamba ukishapata maarifa yatumie vyema kuisaidia jamii, rekebisha na kuyaweka sawa yale mambo ambayo hayko sawa.

Tano, ukiona msomi mwenye shahada ya uhandisi, Udaktari n.k analalamika kuhusu mfumo wa elimu tambua kwamba wewe bado ni mjinga wa kutupwa na ulienda shule kupoteza muda wako huko shuleni kusoma kitu ambacho hakikusaidii.


Kwanza ungejiuliza yafatayo
Investment yoyote inahitaji:-

1. Mtaji/ capital ..... je upo?

2. Availability ya resources .... je vipo?

3. Utayari wa serikali .... imewaandaaje wasomi wetu.

Mtaji
Unahita fedha na eneo, hakuna fedha kwa maana yoyote.... wanatengeneza kivipi?

a) conceptual phase inagharama zake

b) design phase inagharama zake

c) Implementation/manufacturing inagharama zake

d) Testing/quality assurance inagharama zake

Lawama zote ipewe serikali ya ccm kushindwa kuwekeza kwa vijana kivitendo. Wamewekeza katika kuimba ccm, ccm, ccm ushenzi mtupu

HAKUNA Karakana zilizoboreshwa kitaalamu....manufacturing centre zikiwa na: -
I) Raslimali watu
II) Malighafi
III) mitambo .... vitendea kazi mbalimbali
IV) vijana walioandaliwa vema

Cha ajabu siku hizi hata sehemu za kufanya Elimu kwa vitendo nikama hazipo.

Serikali isipokuwa na sera wala mikakati bora katika uwekezaji kwa wasomi wetu tutarajie kuwa na taifa la wajinga katika secta zote. Biashara, uzalishaji nk

Ndio maana nadharia ya kujiajiri inabakia midomoni kwa wanasiasa na Vilaza wengine wasioweza kuchanganua mahitajio sahihi ya kiuwezo ilikujiajiri.

Vijana wasomi wa discipline mbalimbali wapo wanazubaa tu sababu sera na mikakati yetu haiwajengi wala kuwawezesha kujiajili.

CCM NDIO TATIZO
 
kusoma miaka mitano hakukupi guarantee ya kutengeneza ivo vifaa bila ya kuwa na pesa ya kutosha + imagination nzur ya scientists wetu. sio elimu yetu ya kumezeshana mambo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ndiyo hivyo kwanini nini sasa upoteze muda wote huo mkuu kusoma nadharia ambayo haina manufaa? unajiita mhandisi/daktari/phamasia wakati hujui hata kutengeneza penseli, huna uwezo wa kugundua hata chanjo ya COVID19, hujui hata kutengeneza dawa ya kutibu COVID19.
 
Back
Top Bottom