Binti wa zamani
Platinum Member
- Nov 19, 2011
- 11,763
- 27,149
Kama mtanzania ambaye nimempigia kura Mheshimiwa Lissu mara mbili kwenye chaguzi zilizopita (jimboni na uraisi), naamini hajafanya kosa la uhaini na hayo ni mashtaka ni ya kutengeneza na hewa, THAT BEING SAID sikubaliani na kauli ambazo Mh. Lissu amekua anazitoa kwenye mikutano hivi karibuni, sababu si za busara.
Naona kila mtu ambaye hakubaliani na umma wa mitandaoni anashambuliwa, tunakosa ukomavu kwa kisiasa wa kuchambua hoja bila kebehi na matusi. Mitandao ina tabia ya kutengeneza echo chambers za kusikia yale tu tunayotaka kusikia na kujiaminisha kuhusu usahihi wake.
Si lazima tuchukue yote wanayofanya viongozi wetu bila kuchuja, kukosoa, kushauri au kupinga.
Vitu viwili vinaweza kuwa sahihi kwa wakati mmoja.
CCM wamefanya hizi siasa za uchawa na “ndiyo mzee” na sasa tunataka mbadala wao. Naona kuna watu wanalazimisha upande wa upinzani uelekea kule kule ambapo tumekua tunakupinga kwa chama tawala.
Unakubaliana na haya au lah, jibu kwa hoja na si mihemuko. Kama unaamini mabadiliko lazima yaambatane na machafuko au vurugu, then tueleweshe kwanini ni lazima iwe hivyo!
Soma pia: Uchambuzi wa Kisheria juu ya Hati ya Mashtaka ya Uhaini dhidi ya Tundu Lissu
Naona kila mtu ambaye hakubaliani na umma wa mitandaoni anashambuliwa, tunakosa ukomavu kwa kisiasa wa kuchambua hoja bila kebehi na matusi. Mitandao ina tabia ya kutengeneza echo chambers za kusikia yale tu tunayotaka kusikia na kujiaminisha kuhusu usahihi wake.
Si lazima tuchukue yote wanayofanya viongozi wetu bila kuchuja, kukosoa, kushauri au kupinga.
Vitu viwili vinaweza kuwa sahihi kwa wakati mmoja.
- Mh. Lissu amefunguliwa mashtaka hewa ya kuzuia harakati zake kisiasa na hili si jambo sahihi wala la kufumbia macho.
- Mh. Lissu akosolewe asiendelee kutoa kauli ambazo hazina afya kwa taifa letu, hasa kama kweli tunataka mabadiliko bila machafuko.
CCM wamefanya hizi siasa za uchawa na “ndiyo mzee” na sasa tunataka mbadala wao. Naona kuna watu wanalazimisha upande wa upinzani uelekea kule kule ambapo tumekua tunakupinga kwa chama tawala.
Unakubaliana na haya au lah, jibu kwa hoja na si mihemuko. Kama unaamini mabadiliko lazima yaambatane na machafuko au vurugu, then tueleweshe kwanini ni lazima iwe hivyo!
Soma pia: Uchambuzi wa Kisheria juu ya Hati ya Mashtaka ya Uhaini dhidi ya Tundu Lissu