Mdahalo wa amani kufanyika kesho, Oktoba 11, 2015, Blue Pearl Ubungo Plaza

Amani haipatikani kwa mdahalo,pia haipatikani kwa mikesha ya kinafiki ya maombi. Amani Tanzania itadumu haki ikitendeka Oct 25. Bila haki ni vurugu tu Zanzibar na Tangayika.
Neno haki ni pana sana kiasi kwamba kile ambacho wewe unadhani ni haki kwa watu wengine siyo haki na kile unachodhani siyo haki kwa wengine ni haki.

Kupitia midahalo, unaweza kufahamu haki ni ipi kwa wananchi wengi nchini, msingi/misingi ya upatikanani wake na namna ya kuienzi.
 
Hawa wanaenda kujadili AMANI tu na sio UKAWA sasa agenda ya ukawa imetoka wapi labda wawe na kiherehere waende nje ya mdahalo..

lakiwosha yaani wewe huoni huo mchezo hapo, ngoja nikupe darasa kidogo hapa, ili ugundue kitu.
1/Hao wote ni makada waandamizi wa CCM waliopo kwenye timu maalum ya kampeni ya CCM inayojulikana kama Jukwaa huru(Mongella(wanawake), Butiku(wazee), Polepole(Vijana)).

2/Toka lini Amani ikadumishwa kwa kufanya midahalo? Kuna sababu gani ya msingi ya kuwaweka watanzania kwenye wasiwasi wa kupoteza Amani katika kipindi hiki?

3/Kwanini waongeaji wakuu wawe ni watu wenyewe mlengo mmoja tu wa kisiasa tena katika kipindi hiki?

4/Toka lini Polepole akawa mtetezi wa Amani wakati kila mara amekuwa live kwenye Tv akiipigia kampeni CCM kwa kutumia Propaganda chafu dhidi ya UKAWA zenye kuchochea chuki na ubaguzi?
 
Last edited by a moderator:
Halafu wamepanga kiujanja sana, Hao wote ni makada wa CCM, Getrude Mongela anawakilisha wanawake, Joseph Butiku(Wazee), Humphrey Polepole(Vijana). Star Tv kikiwa ndio kitengo chao rasmi cha Propaganda, wamegundua Mkikimkiki wa Uchaguzi hauna watazamaji tena, Twaweza ilishashtukiwa, sasa wamebadili gear, lakini imegoma mapema.

Sitajishughulisha kuangalia huo mdahalo kwa maoni yangu wazungumzaji wote tunawajua ni watu wa aina gani na kituo kinachorusha huo mdahalo tunakijua na kinachokitarajiwa kuzungumzwa tunakijua...
 
safi sana simplemind
Hata viongozi wetu wa dini wamekuwa wakituhubiria juu ya kudumisha amani.hatuna ubishi juu ya hilo lkn pia ni vyema viongozi wetu wanapotuhusia juu ya kuilinda amani,wasiache pia kuwaasa viongozi wetu tuliowapa mamlaka kuhakikisha wanazingatia misingi ya utoaji haki.
Amani bila haki ni sawa na utumwa.
 
Last edited by a moderator:
lakiwosha yaani wewe huoni huo mchezo hapo, ngoja nikupe darasa kidogo hapa, ili ugundue kitu.
1/Hao wote ni makada waandamizi wa CCM waliopo kwenye timu maalum ya kampeni ya CCM inayojulikana kama Jukwaa huru(Mongella(wanawake), Butiku(wazee), Polepole(Vijana)).

2/Toka lini Amani ikadumishwa kwa kufanya midahalo? Kuna sababu gani ya msingi ya kuwaweka watanzania kwenye wasiwasi wa kupoteza Amani katika kipindi hiki?

3/Kwanini waongeaji wakuu wawe ni watu wenyewe mlengo mmoja tu wa kisiasa tena katika kipindi hiki?

4/Toka lini Polepole akawa mtetezi wa Amani wakati kila mara amekuwa live kwenye Tv akiipigia kampeni CCM kwa kutumia Propaganda chafu dhidi ya UKAWA zenye kuchochea chuki na ubaguzi?

Kaka umeongea Maneno Kuntu Sana. Hapa wanachokifanya Ccm ni Kuwajaza Hofu Wananchi Kwamba Mkichagua Upinzani Utavunja Amani, Ila Mkiichagua ccm Amani itakuwepo.

Ninyi Hamshangai Mdaalo Kurushwa na Star Tv?

Star Tv ni Adui namba Moja wa Lowassa + Butiku + Mongela + Pole Pole = Wametumwa na ccm Kuwachanganya Wapiga Kura kwa Propaganda za Uvunjifu wa Amani.
 
Last edited by a moderator:
Hakuna sababu ya kwenda kuwasikiliza. Hawana jipya na wanaipigia kampeni CCM.
 
Mimi nashangaa sana juu ya watu katika maandalizi ya midahalo. Kwa nini hufanya Midahalo ikiwa wahusika wote wana msimamo mmoja? Kwa nini wagombea Urais na hata Ubunge ndio wasipewe nafasi za Mdahalobadala yake wachukue watu wanauzungumzia siasa tu za porojo kunyoosheana vidole wakati haibadilishi kitu pasipo wao kujua kitafuata nini katika Utawala ujao? Je kweli wanayajua ya Magufuli ama wanaweka matumaini kama walokuwa nayo wakati JK akiingia madarakani!..

Wataalam wa siasa walisema kuwa mwanzo wa kuwepo vyama vingi sii ushindani wa Kulia (Marekani) na Kushoto (Urusi) bali watu kutokubaliana na sheria mama za kikatiba ambazo zilihitaji mitazamo na mwelekeo mpya. Na katika kupambanua umuhimu wa mabadiliko hayo kikatiba ndio kukaundwa vyama vya Liberal ambavyo vilipingana na sheria mama inayolinda maadili na Utaifa wa wananchi wake (Conservatives).

Sasa kama tulianza na Ujamaa na Kujitegemea na ikiwa ndio chimbuko la Utaifa wetu, ikaundwa miiko na maadili yake, changamoto za kubadilisha mambo hayo kikatiba ndipo hutokea kuundwa kwa vyama vingine kupingana na mwelekeo uliopo. Kundi jingine likiendelea kulinda misingi ile ile iloyolizaa Utaifa wao sio habari za ugonvi wa Warusi na Wamarekani juu ya mambo yao ya kutawala.

Maadam sisi hatufungamani na yeyote juu ya misimamo yao na kwa maslahi yao ni muhimu sana kupambana katika majukwaa ya kisiasa na kudadavua marekebisho ya kikatiba juu ya mwelekeo wa Taifa letu bila kupoteza Mila, desturi na Tamaduni zetu muhimu katika kujitambua.

Is this u?!!....toroka uje
 
Hii Star TV naifananisha na redio moja ya Rwanda enzi za interahamwe 1994. Sidhani kama Dialo anafikiria hatima ya star tv baada ya uchaguzi. Namfananisha Kamonte kama Kabendela Shinani. Haya, endeleeeni, tutayaona.
 
CCM wahaidi kwamba hakutakuwa na matusi…maana tumechoka na matusi yao...
 
Mdahalo utarushwa moja kwa moja (Live) na kituo cha Star TV.

12107231_752632098193632_1720672816855472836_n.jpg
hiyo lazima niwepo
 
Back
Top Bottom