Mdada amwaga chozi, imeniumiza moyo sana

Mdada amwaga chozi, imeniumiza moyo sana

Msandawe Halisi

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2010
Posts
647
Reaction score
351
Jana nilitumwa na bosi wangu kwenda kuchukuwa document katika kampuni moja hivi. Nilipofika sikumkuta secretary, niliambiwa ameenda lunch. Nikamkuta kijana mmoja ambaye ni bosi wake na ndiye aliyekuwa anawasiliana na bosi wangu.

Yule kijana akampigia simu afahamu document zilipo. Yule dada akamwambia amezifungia kwenye kabati yake na ufungua anao yeye. Inaonyesha sehemu aliyoenda kupata lunch pana umbali kidogo.


Aliporudi yule kijana alimfokea sana, yule kaka akamaliza hasira zake kwa kumwambia kwa tabia zako ndio maana wanaume wa kukuoa wanakukimbia.Yule dada alianza kulia mpaka na mimi nusu nilie. Nikimwangalia hivi, umri wake waweza kuwa kati ya miaka 34-36.

Tuchunge ulimi ndugu zangu, maneno yanauma.
 
Mdada umri huo analia hadharani kwa kuambiwa hivyo
 
Ni kweli lazma alie kauli mbaya sana hyo.....
 
Emotional abuse, ikikutana na weak personality, majanga.
Ningekuwa mie, ningempa jibu hilo hadi angeshangaa na roho yake.
 
Duh nyie mabosi nyie! Mimi ni ombi langu kwa MUNGU kuwa kwa nafasi yangu Nataka 90% if not 100% plus nitakaowahudumia watoke wakiwa na furaha hata kama lile lililowaleta sina uwezo wa kulifanikisha!!!!
 
Mdada umri huo analia hadharani kwa kuambiwa hivyo

Loh! Hiyo inaweza kukuliza kweli. Ukiangalia huyo dada ana kama miaka 35, umri tu ni sababu tosha ya kumfanya alie, sasa utamkitukana tena lazima aumie zaidi. Afu ukiangalia anayemtukana ni mwanaume.
 
kauli nyingine sio za hivi hvi tu pengine anamtaka huyo dada lakin anamkataa kwa sababu kwa harka haraka hamhusu hata akifikia umri wa uzee
 
Jana nilitumwa na bosi wangu kwenda kuchukuwa document katika kampuni moja hivi. Nilipofika sikumkuta secretary, niliambiwa ameenda lunch. Nikamkuta kijana mmoja ambaye ni bosi wake na ndiye aliyekuwa anawasiliana na bosi wangu.

Yule kijana akampigia simu afahamu document zilipo. Yule dada akamwambia amezifungia kwenye kabati yake na ufungua anao yeye. Inaonyesha sehemu aliyoenda kupata lunch pana umbali kidogo.


Aliporudi yule kijana alimfokea sana, yule kaka akamaliza hasira zake kwa kumwambia kwa tabia zako ndio maana wanaume wa kukuoa wanakukimbia.Yule dada alianza kulia mpaka na mimi nusu nilie. Nikimwangalia hivi, umri wake waweza kuwa kati ya miaka 34-36.

Tuchunge ulimi ndugu zangu, maneno yanauma.



Na wewe ukaka kimya tu? Hukusema hata neno kumkemea boss wake unaona mtu ananyanyaswa. Kwa namna moja au nyingine na wewe umeshiriki katika kumnyanyasa huyo dada. Halafu unaletea hapa, wakati umeshindwa kumsaidia huyo. Kumbe na wewe huna maana kabisa kwa kiasi fulani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom