assadsyria3
JF-Expert Member
- Apr 9, 2013
- 6,909
- 4,057
Mchungaji anayetuhumiwa kuwa naye alihusika katika mpango wa kumuua Dk Slaa amesema walichati na kujuana na Josephine Mushumbusi Facebook
Mytake:
Hii Facebook ni hatari wanawake muwe waangalifu. mtavunja ndoa zenu
CHANZO: Mtanzania
Mytake:
Hii Facebook ni hatari wanawake muwe waangalifu. mtavunja ndoa zenu
Si mwingine bali yule Mchungaji anayetuhumiwa kula njama za kumuua Dr. Slaa. Mchungaji ISACK LOYD aliyasema hayo mwenyewe wakati akihojiwa na gazeti MTANZANIA kuhusiana na tuhuma zinazoelekezwa kwake za kula njama za kutaka kumuua Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dr. Wilbroad SLAA.
Mchungaji Loyd alifikia uamuzi wa kufichua siri hiyo baada ya kuulizwa ana maana gani anaposema "MAPITO MAGUMU KATIKA MAISHA YAKE", ndipo alipofunguka na kusema Kabla hajaokoka na kuwa Mchungaji, ALIKUWA KIONGOZI WA GENGE LA MAJAMBAZI HUKO RUVUMA.
Mchungaji aliendelea kufunguka na kusema: "Nimewahi kuuza Madawa ya Kulevya na nilikuwa natumia. NIMESHIRIKI VITENDO VYA UJAMBAZI KWA KUONGOZA KUNDI LA WAHALIFU HUKO SONGEA NA NIMENUSURIKA KUUAWA MARA KADHAA KABLA NA BAADA YA KUOKOKA, NIMEWAHI KUJERUHIWA KWA RISASI MGUU WANGU MMOJA NA NIMEWAHI KUCHOMWA BISIBISI PUANI IKATOKEA MDOMONI.
ALIVYOJUANA NA JOSEPHINE MSHUMBUSI: anasema na hapa nanukuu: "Josephine kama ilivyo kwa watu wengine ALINIOMBA URAFIKI, NAMI NIKAMKUBALIA , AKANIPONGEZA KWA KAZI NZURI NINAYOIFANYA NA TUKAANZA KUWASILIANA MARA KWA MARA" mwisho wa kunukuu.
source: Gazeti la Mtanzania la leo 05/04/2015 , siku ya PASAKA.
Mytake: Sitaki kujiuliza maswali kama Dr. SLAA alikuwa anajua mawasiliano ya mara kwa mara ya hawa wapendwa wawili kabla Mchungaji hajakaribishwa Nyumbani kutoa huduma ya kiroho. Swali kubwa ninalobaki baki nalo leo baada ya kusoma taarifa hii ni :
1. JE Mchungaji ISACK LOYD ameacha kazi yake ya zamani ya ujambazi na kuuza na kutumia dawa za kulevya?
2. Kama alivyosema kuwa alikuwa kiongozi wa GENGE LA MAJAMBAZI, baada ya kuachana na uhalifu huo(kama ameacha kweli) ametoa ushirikiano kwa Serikali ili kuhakikisha mtandao wake wa ujambazi na dawa za kulevya unajulikana ili kusambaratishwa?
LA MSINGI KABISA: SOTE tunajua DR. SLAA si tu kwamba ni Muumini wa Dhehebu la KATHOLIKI bali aliwahi kuwa kiongozi wa juu kabisa wa Kanisa Katholiki. Huu utitiri wa Wachungaji wa ajabu ajabu kwenda kwake, wachungaji wenye tuhuma za ajabujabu tu siyo kwamba huyu MAMA MSHUMBUSI NI SHIIIIIIIIIIDA?
View attachment 240636
CHANZO: Mtanzania