Huyo your wife to be ameshakuambukiza gono na bado unajiuliza kumwacha du, ndo hapo atakapokuambiza ngoma sijui utasemaje pole mshikaji.Jamani wadau nisaidieni ushauri mpenzi wangu(wife to be) ameniambukiza gonorrhea(kisonono). nifanyeje na dalili zake zimeshaonekana kabisa.
Naomba ushauri wa tiba na kama ni sahihi kama nikimwacha.
Nenda kapime na HIV status yako, magonjwa ya zinaa huenda sana na maambukizo ya UKIMWI. Pata ushauri wa Dr ila strong antibiotics hutibu vizuri tu Gono mfano Ofloxacin, Cefixine, ama Ceftriaxine
Jamani wadau nisaidieni ushauri mpenzi wangu(wife to be) ameniambukiza gonorrhea(kisonono). nifanyeje na dalili zake zimeshaonekana kabisa.
Naomba ushauri wa tiba na kama ni sahihi kama nikimwacha.
...nendeni pamoja mkapatiwe tiba na ushauri nasaha. Ajali kazini tu hiyo mjomba, msamehe.
Mkuu Mbu, Mapenzi yasiyokuwa na uaminifu kati ya wapendanao siku zote hayadumu. Badala ya huyu kijana kupoteza muda wake na huyu binti ambaye si mwaminifu na anaweza tena kurudia alichokifanya ni bora tu aingie mitini na kuanza kutatafuta upya.
Naomba kutofautiana na wachangiaji wengine waliotangulia. Kwa vile huyu jamaa kaja kuomba ushauri, ina maana bado anampenda mpenzi wake. Ingawa hajasema mengi, lakini inawezekana huyo dada aliambukizwa kabla hawajawa marafiki. Kwa maana hiyo siyo sahihi kusema kuwa huyo msichana ni mhuni. Labda alikutana na ex-wake mara moja akaambukizwa. Let's give her a benefit of doubt.
Nashauri jamaa ampeleke mpenzi wake kwa dokta wapime vizuri, wapate maibabu sahihi ili waendelee kufaidi penzi lao. Kumpiga chini siyo suluhu. Anaweza kukumbia miiba akaangukia kwenye upupu. Ila kama atauchukua ushauri wangu basi ajipe muda zaidi kabla ya kwenda kwa pilato kujitia kitanzi, kwani inawezekana mbia wake kweli hajatulia! Ukiwa mtumba na ukanunua mtumba basi ukubali harufu yake hata kama haipendezi!!!
Jamani wadau nisaidieni ushauri mpenzi wangu(wife to be) ameniambukiza gonorrhea(kisonono). nifanyeje na dalili zake zimeshaonekana kabisa.
Naomba ushauri wa tiba na kama ni sahihi kama nikimwacha.
Cha kufanya mchukue mwende naye kama upo Dar mpeleke pale Makao makuu ya Polisi Central kwa pembeni kuna dispensary pale wanatibu magonjwa ya zinaa.
Mkisha jitibia muulize kalitoa wapi hili gonjwa?