AbuuMaryam
JF-Expert Member
- Dec 26, 2015
- 2,537
- 4,517
Mshaurini huyu jamani...
MCHUMBA WANGU ANANISHIRIKISHA KATIKA KILA KITU CHA MAENDELEO ANACHOFANYA!
Mimi ni binti wa miaka 28, sijaolewa ila nina mchumba ambaye yeye ana miaka 30, nampenda sana na yeye anaonyesha kunipenda kwakuwa kashanitambulisha mpaka kwao na kwetu pia nimeshamtambulisha. Tatizo ni kuwa mpenzi wangu huwa ni muwazi sana, ananishirikisha katika kila kitu chake cha maendeleo anachokifanya na mara nyingi anakuwa anataka mawazo yangu, akitaka kununua kiwanja, kujenga, akitaka kitu chochote hata kama ni mapazia anataka tufanye pamoja.
Mimi nafanya kazi na yeye pia anafanya kazi, haniombi pesa na wala hajawahi lakini tatizo ni kuwa kwakuwa ananishirikisha katika mambo yake basi nashindwa kumuomba pesa kubwa kubwa kwaajili ya kufanya mambo yangu kwani kila hela yake najua imeenda wapi? Kwa mfano labda nataka laki mbili, ninataka kununua kitu changu labda kutoka na marafiki, nikimuambia pesa ananiambia hana si tumenunulia kitu flani, ukiangalia kweli alinunua hicho kitui na alinishirikisha hivyo naona aibu hata kumkasirikia kwani kinakuwa cha maendeleo na najua pesa yake yote.
Naumia sana kwani mimi kama msichana nahitaji kudekezwa na kufanyiwa suprize za zawadi kama marafiki zangu ambao wanaweza kufanyiwa birthday na wapenzi wao, kutolewa out, kununuliwa nguo na zawadi. Mimi nikihitaji kitu inabidi nimuambie mapema kabla ya mshahara ili aniweke kwenye bajeti na sanasana atakupa elfu hamsini hata laki hakupi kwani anakuwa anafanya vitu vingi vya maendeleo ambavyo ananiomba ushauri na ukiangalia anakuwa kweli hana kwani hata yeye hafanyi hizo starehe
Kinachoniuma zaidi ni kuwa hawezi kufanya maamuzi yake mwenyewe kama mwanaume ni lazima aniambie na mara nyingi hupenda kufuata ushauri wangu na si wake. Kunipenda kweli ananipenda lakini nina wasiwasi je tukioana itakuaje kwani mara nyingi anasema tukioana itakua vizuri kama tukishirikiana kwenye mambo ya familia eti mshahara wangu nao tufanyie mambo ya maendeleo wakati yeye kama mwanaume anatakiwa kufanya kila kitu, niko njia panda nawaza je huyu ni mtu sahihi kwangu au nifanyeje?
MCHUMBA WANGU ANANISHIRIKISHA KATIKA KILA KITU CHA MAENDELEO ANACHOFANYA!
Mimi ni binti wa miaka 28, sijaolewa ila nina mchumba ambaye yeye ana miaka 30, nampenda sana na yeye anaonyesha kunipenda kwakuwa kashanitambulisha mpaka kwao na kwetu pia nimeshamtambulisha. Tatizo ni kuwa mpenzi wangu huwa ni muwazi sana, ananishirikisha katika kila kitu chake cha maendeleo anachokifanya na mara nyingi anakuwa anataka mawazo yangu, akitaka kununua kiwanja, kujenga, akitaka kitu chochote hata kama ni mapazia anataka tufanye pamoja.
Mimi nafanya kazi na yeye pia anafanya kazi, haniombi pesa na wala hajawahi lakini tatizo ni kuwa kwakuwa ananishirikisha katika mambo yake basi nashindwa kumuomba pesa kubwa kubwa kwaajili ya kufanya mambo yangu kwani kila hela yake najua imeenda wapi? Kwa mfano labda nataka laki mbili, ninataka kununua kitu changu labda kutoka na marafiki, nikimuambia pesa ananiambia hana si tumenunulia kitu flani, ukiangalia kweli alinunua hicho kitui na alinishirikisha hivyo naona aibu hata kumkasirikia kwani kinakuwa cha maendeleo na najua pesa yake yote.
Naumia sana kwani mimi kama msichana nahitaji kudekezwa na kufanyiwa suprize za zawadi kama marafiki zangu ambao wanaweza kufanyiwa birthday na wapenzi wao, kutolewa out, kununuliwa nguo na zawadi. Mimi nikihitaji kitu inabidi nimuambie mapema kabla ya mshahara ili aniweke kwenye bajeti na sanasana atakupa elfu hamsini hata laki hakupi kwani anakuwa anafanya vitu vingi vya maendeleo ambavyo ananiomba ushauri na ukiangalia anakuwa kweli hana kwani hata yeye hafanyi hizo starehe
Kinachoniuma zaidi ni kuwa hawezi kufanya maamuzi yake mwenyewe kama mwanaume ni lazima aniambie na mara nyingi hupenda kufuata ushauri wangu na si wake. Kunipenda kweli ananipenda lakini nina wasiwasi je tukioana itakuaje kwani mara nyingi anasema tukioana itakua vizuri kama tukishirikiana kwenye mambo ya familia eti mshahara wangu nao tufanyie mambo ya maendeleo wakati yeye kama mwanaume anatakiwa kufanya kila kitu, niko njia panda nawaza je huyu ni mtu sahihi kwangu au nifanyeje?