Mchumba amepata mimba na mimi najenga

Mchumba amepata mimba na mimi najenga

emperor mo

Member
Joined
Nov 9, 2014
Posts
41
Reaction score
6
Habari zenu wadau,

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 24,ninamchumba wangu ana miaka 20 tunapendana sana lakini hivi majuzi ananiambia hajidikii vizuri na hajaona siku zake ambazo hua zinawahi lakini Leo ndio alitakiwa apate hedhi.

Anadai ana mimba yangu lakini changamoto inakuja kwamba Mimi naishi na wazazi na ndio nimeanza kuchimba msingi nijenge na nilimwambia asubiri nijenge niende kwao lakini sasa majukumu yamekua mawili nashindwa nifanyeje, nimwambie aende kwao ili nimalize ujenzi au nipange chumba nimuoe kabla mimba haijawa kubwa ujenzi usubiri.
 
nimekua nikilinfa zile Siku salama na sikutegemea hill kwa sasa,na yeye ni kama amefurahia iyo hali hata dadaake ananichangamkia kuliko awali,sikuwa napanga kujenga ndani yake
 
Nani alikwambia ukioa hauwezi kujenga? Wengi tumeoa hatuna hata viwanja lakini pamoja na wake zetu tumelea watoto, tumesomesha na tumejenga vile vile.

Nakwasababu umesema unataka ujenge inaonyesha una kipato fulani. Hivyo nakushauri upange nyumba, uoe na mlee mtoto. Mambo mengine yatakuja tu kwa juhudi na mipango yenu wote wawili.
 
Muoe bhana wangapi wamejenga baada yakuoana uclete zileeeeee zakukimbia
 
Huyo alikuwa mke na sio mchumba kwasababu katika mila na desturi zetu, hupaswi kufanya tendo la ndoa kipindi cha uchumba mpaka uoe rasmi.
 
Nani alikwambia ukioa hauwezi kujenga? Wengi tumeoa hatuna hata viwanja lakini pamoja na wake zetu tumelea watoto, tumesomesha na tumejenga vile vile.

Nakwasababu umesema unataka ujenge inaonyesha una kipato fulani. Hivyo nakushauri upange nyumba, uoe na mlee mtoto. Mambo mengine yatakuja tu kwa juhudi na mipango yenu wote wawili.

sio kwamba nashindwa kumuoa ila nikimuoa kujenga ni baadae sana mana plus mahari na kulipa kodi na garama za kuendesha maisha zitakua tofauti
 
acha bangi, acha viroba acha na uzinzi
ivo vitu vinahusikaje hapo,nani alikwambia Mimi natumia hivyo vitu,nani alikwambia waliowachumba wakifanya ngono wanazini,soma biblia yako vizuri kitabu cha mambo ya walawi kama huna ushauri ni ushauri wangu kwako refer to your post
(na uache ushamba)
 
Emperor mo,pole sana dogo,nadhani kama angekuwa binti smart angeelewa wewe bado unahitaji kukua kiakili na msingebebeshana mimba za utotoni.
 
Huyo alikuwa mke na sio mchumba kwasababu katika mila na desturi zetu, hupaswi kufanya tendo la ndoa kipindi cha uchumba mpaka uoe rasmi.

nilipokua nafanya maamuzi ya kulala nae nilikua nimwjihakikishia nitamwoa__kwetu hill sio tatiZo
 
Pole sana ! Hii huaga inatokea kwa wadada

Kipindi anasumbuliwa mitaani anatongozwa hua anakataaga ,lakini akishapata mchumba na anajua tayari kashaolewa sasa ndo anajiachia tu ,kila mtu unakuta kabla ya mwezi mmoja wafunge ndo utakuta yeye tayari anaujauzito ! Kwa kifupi huaga wanasema wanalipa deni ! Sasa ukisha muoa unakuta anakaa miezi saba iv anazaa tayari ,utajiuliza yeye mbona hata miezi tisa bado?????
 
ivo vitu vinahusikaje hapo,nani alikwambia Mimi natumia hivyo vitu,nani alikwambia waliowachumba wakifanya ngono wanazini,soma biblia yako vizuri kitabu cha mambo ya walawi kama huna ushauri ni ushauri wangu kwako refer to your post
(na uache ushamba)

acha kulialia, acha kelele na acha kuropoka.
 
Back
Top Bottom