TAJIRI MKUU WA MATAJIRI
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 5,719
- 10,215
JE, NI VIPI VIGEZO VYA KUSOMEA URUBANI?
Unataka kuwa rubani?
Je, umekosa ndoto nyengine ambayo haitafirisi mzazi, mlezi au mdhamini?
Usijali, huu ni utani wenye ukweli ndani yake.
Kabla ya kupata dokezo la huko tuendapo, Kwanza tuanze na matumizi matatu ya msingi ya Usafiri wa Anga:
1>Mashirika Ya Ndege
2>Matumizi Binafsi, na
3> Matumizi ya Kijeshi.
MASHIRIKA YA NDEGE:
Mashirika/Makampuni hizi ni ndege zilizosajiliwa kufanya biashara ya kutoa huduma za usafiri wa anga kama kubeba abiria au mizigo kutoka sehemu moja kwenda nyengine.
BINAFSI
Hizi ni ndege binafsi za kiraia.
Usafiri huu unaweza kutumika kwa matembezi binafsi kama kula bata, biashara, tafiti, ufundishaji n.k
Umiliki wa sehemu hii sio rafiki sana kwa raia wa kusadikika.
Kumiliki ghali, kusajili ghali, uendeshaji ghali, kuegesha ghali, vipuri ghali, ufundi ghali na pia mafuta ghali.
KIJESHI:
Huu ni usafiri wa anga wa kijeshi.
Majeshi, hasa ya anga yanaweza kutumia usafiri huu kwa kusafirisha Askari, Mizigo, Ujasusi, Uokoaji, Kumpiga adui, Kujilinda n.k
Kwa Dunia ya sasa jeshi la anga ndiyo kama uti wa mgongo.
Wanasema Adui akikuwahi angani basi kashinda nusu ya vita, kwahiyo sio bunduki wala kifaru vitakusaidia sana na ndiyo maana nchi nyingi zinajitutumua kuimalisha ulinzi wa anga.
Hapa nisiongelee sana.
VIGEZO VYA KUJIFUNZA URUBANI
1>VIPIMO/MATIBABU
Cha kwanza lazima ukapime afya katika hospitali walizotibitisha Mamlaka ili uwe na Cheti cha Afya Daraja la 1 na utaendelea kupima kupata Vyeti vya madaraja mengine kadri unavyosoma leseni kubwa zaidi.
Utapimwa vitu kama Macho, Usikivu, Shinikizo la Moyo, ulemavu wa viungo vya msingi na Akili.
Hakuna mtu anayetaka kupaishwa na Rubani saa mbovu' futi 30,000.
2> ELIMU
Vigezo vinatofautiana kati ya shule na shule.
Wengine wanachukua kidato cha Nne, wengine cha sita, na hata wengine wanaangalia kichwa chako kinauwezo kiasi gani cha kujifunza na kuwasiliana kwa lugha inayotakiwa.
Kitu kimoja ningependa ufahamu hapa.
Nchi nyingi unaweza kujifunza urubani hata kama uliishia darasa la saba, ilihali uwe na vigezo vya Mdhibiti.
Mfano, umri wa kisheria kutoka Mamlaka za nchi tofauti zinataja mtu anaweza kujifunza urubani kuanzia umri wa miaka 16, 17 na 18 na kuendelea na ukomo wa miaka 60 au zaidi.
Hii ni kwasababu sio kila anayejifunza urubani anahitaji kurusha ndege ya biashara, bali wengine hujifunza kwaajili ya kurusha ndege binafsi.
Kumbuka muigizaji maarufu wa filamu Morgan Freeman alipata leseni ya urubani akiwa na miaka 65.
Mafunzo ya Urubani yanakuwa rahisi zaidi kwa mtu aliyepitia masomo ya Kiingereza, Hesabu na Jiografia na hata Fizikia kiasi.
Lakini hii haimaanishi mtu mwenye masomo tofauti hana vigezo vya kusomea urubani.
Hata mwanafunzi wa HKL anaweza kuwa Rubani sababu tayari ana msingi wa masomo tajwa kutoka 'Ordinary Level'
Changamoto ya kwanza endapo ukiwa na elimu chini ya ile iliyopendekezwa katika kujifunza Urubani, jiandae kukutana na ugumu wa kiasi chake.
Usingependa urudi nyumbani unaongea mwenyewe "Bora ningefunguliwa duka kariakoo"
Changamoto ya pili pia kama ukifanikiwa kupata Leseni ya urubani na elimu ndogo, fahamu kwamba mashirika mengi makubwa ya Ndege sasa yanapenda kuajiri kwa kuangalia Leseni pamoja na elimu yako (Leseni +Diploma au Degree)
Kama ilivyo kwa leseni ya gari, unaweza kuwa na Class C na elimu ya darasa la saba, ila kazi inahitaji mtu mwenye class C na elimu ya kidato cha 4 au 6.
Kwa kupitia shule ya mafunzo, Leseni unayohitaji inategemea unataka kuwa rubani wa aina gani.
Ikiwa unataka kuwa rubani wa ndege binafsi basi itabidi upate
'Private Pilot License' (PPL) ambayo ni masaa 40 hadi 50 ya ujuzi wa kupaa kabla ya kufanya mtihani wa kupata leseni.
Kama urubani wa abiria/biashara, basi upate
'Commercial Pilot License (CPL) masaa kuanzia 200 au 250 na kuendelea.
Pia ngazi nyengine ni 'Airline Transport Pilot License' (ATPL) ambayo ni mchanganyiko wa masaa ya kutosha, ujuzi na taaluma
3> ADA
Hapa jiandae kisaikolojia maana huyu ndiyo mchawi wa ndoto za urubani kwa kila mtu, hii hata Ulaya na Marekani.
Kama ulikuwa hujui anza kufahamu sasa masuala ya Usafiri wa anga hakuna kitu rahisi rahisi kama sekta nyengine.
Kupaa na ndege saa moja ya mafunzo ni kati ya dola za kimarekani $200-$300.
Unahitaji saa 40-45 ili kuweza kufanya mtihani kupata leseni binafsi tu (PPL), kisha zinahitajika saa 200 za kufanya mtihani wa Leseni za biashara (CPL) hapo sijaongelea gharama za darasani (ground school) na matakwa mengine.
Ingawa baadhi watu huomba kudandia ndege za walimu baada ya kupata Leseni ya PPL ili kutafuta ujuzi kujenga masaa na kupunguza gharama kuelekea CPL.
Bahati mbaya zaidi kupata udhamini wa kusomeshwa Urubani kutoka kwa mtu baki, Taasisi au kampuni si jambo rahisi hata kidogo.
Tuelewane hapa, mzazi, mlezi, mdhamini, mtoaji mikopo anahitaji kujidhatiti na kujitoa kwelikweli ili kufanikisha malengo ya mlengwa anayehitaji kuwa rubani.
Tuliona kijana #NarcentMeena aliamua kuuza karanga za jumla na rejareja ili apate ada ya kujisomesha urubani ili kutimiza ndoto yake.
Mbali na yote, kuwa rubani inawezekana hata kwa mtu wa chini wa kawaida.
Muda mwingine 'mchawi sio kibunda' mchawi matumizi na akiba.
Kama mwanao ana miaka mi 5,10,15 mfungulie fixed akaunti ili kila ukiokota miambili unaweka, au wale wa Bia unagawanya nusu kaunta nusu akaunti.
Usingoje Kafika miaka18 ndiyo utafute pesa kwa mkupuo za mkupuo, ni ngumu sana.
Wanasema cha kesho jenga leo.
La sivyo utasikia lawama tu "mbona marubani wengi ni wale wenye ngozi ile"
Kama hatujakosea sana, hapa nchini kuna vyuo kama Vinne vinavyotoa Mafunzo ya Urubani
Fly Zanzibar
NIT-Mabibo
Tanzania Pilot Training Centre na
ZRP-Zanzibar.
Unataka kuwa rubani?
Je, umekosa ndoto nyengine ambayo haitafirisi mzazi, mlezi au mdhamini?
Usijali, huu ni utani wenye ukweli ndani yake.
Kabla ya kupata dokezo la huko tuendapo, Kwanza tuanze na matumizi matatu ya msingi ya Usafiri wa Anga:
1>Mashirika Ya Ndege
2>Matumizi Binafsi, na
3> Matumizi ya Kijeshi.
MASHIRIKA YA NDEGE:
Mashirika/Makampuni hizi ni ndege zilizosajiliwa kufanya biashara ya kutoa huduma za usafiri wa anga kama kubeba abiria au mizigo kutoka sehemu moja kwenda nyengine.
BINAFSI
Hizi ni ndege binafsi za kiraia.
Usafiri huu unaweza kutumika kwa matembezi binafsi kama kula bata, biashara, tafiti, ufundishaji n.k
Umiliki wa sehemu hii sio rafiki sana kwa raia wa kusadikika.
Kumiliki ghali, kusajili ghali, uendeshaji ghali, kuegesha ghali, vipuri ghali, ufundi ghali na pia mafuta ghali.
KIJESHI:
Huu ni usafiri wa anga wa kijeshi.
Majeshi, hasa ya anga yanaweza kutumia usafiri huu kwa kusafirisha Askari, Mizigo, Ujasusi, Uokoaji, Kumpiga adui, Kujilinda n.k
Kwa Dunia ya sasa jeshi la anga ndiyo kama uti wa mgongo.
Wanasema Adui akikuwahi angani basi kashinda nusu ya vita, kwahiyo sio bunduki wala kifaru vitakusaidia sana na ndiyo maana nchi nyingi zinajitutumua kuimalisha ulinzi wa anga.
Hapa nisiongelee sana.
VIGEZO VYA KUJIFUNZA URUBANI
1>VIPIMO/MATIBABU
Cha kwanza lazima ukapime afya katika hospitali walizotibitisha Mamlaka ili uwe na Cheti cha Afya Daraja la 1 na utaendelea kupima kupata Vyeti vya madaraja mengine kadri unavyosoma leseni kubwa zaidi.
Utapimwa vitu kama Macho, Usikivu, Shinikizo la Moyo, ulemavu wa viungo vya msingi na Akili.
Hakuna mtu anayetaka kupaishwa na Rubani saa mbovu' futi 30,000.
2> ELIMU
Vigezo vinatofautiana kati ya shule na shule.
Wengine wanachukua kidato cha Nne, wengine cha sita, na hata wengine wanaangalia kichwa chako kinauwezo kiasi gani cha kujifunza na kuwasiliana kwa lugha inayotakiwa.
Kitu kimoja ningependa ufahamu hapa.
Nchi nyingi unaweza kujifunza urubani hata kama uliishia darasa la saba, ilihali uwe na vigezo vya Mdhibiti.
Mfano, umri wa kisheria kutoka Mamlaka za nchi tofauti zinataja mtu anaweza kujifunza urubani kuanzia umri wa miaka 16, 17 na 18 na kuendelea na ukomo wa miaka 60 au zaidi.
Hii ni kwasababu sio kila anayejifunza urubani anahitaji kurusha ndege ya biashara, bali wengine hujifunza kwaajili ya kurusha ndege binafsi.
Kumbuka muigizaji maarufu wa filamu Morgan Freeman alipata leseni ya urubani akiwa na miaka 65.
Mafunzo ya Urubani yanakuwa rahisi zaidi kwa mtu aliyepitia masomo ya Kiingereza, Hesabu na Jiografia na hata Fizikia kiasi.
Lakini hii haimaanishi mtu mwenye masomo tofauti hana vigezo vya kusomea urubani.
Hata mwanafunzi wa HKL anaweza kuwa Rubani sababu tayari ana msingi wa masomo tajwa kutoka 'Ordinary Level'
Changamoto ya kwanza endapo ukiwa na elimu chini ya ile iliyopendekezwa katika kujifunza Urubani, jiandae kukutana na ugumu wa kiasi chake.
Usingependa urudi nyumbani unaongea mwenyewe "Bora ningefunguliwa duka kariakoo"
Changamoto ya pili pia kama ukifanikiwa kupata Leseni ya urubani na elimu ndogo, fahamu kwamba mashirika mengi makubwa ya Ndege sasa yanapenda kuajiri kwa kuangalia Leseni pamoja na elimu yako (Leseni +Diploma au Degree)
Kama ilivyo kwa leseni ya gari, unaweza kuwa na Class C na elimu ya darasa la saba, ila kazi inahitaji mtu mwenye class C na elimu ya kidato cha 4 au 6.
Kwa kupitia shule ya mafunzo, Leseni unayohitaji inategemea unataka kuwa rubani wa aina gani.
Ikiwa unataka kuwa rubani wa ndege binafsi basi itabidi upate
'Private Pilot License' (PPL) ambayo ni masaa 40 hadi 50 ya ujuzi wa kupaa kabla ya kufanya mtihani wa kupata leseni.
Kama urubani wa abiria/biashara, basi upate
'Commercial Pilot License (CPL) masaa kuanzia 200 au 250 na kuendelea.
Pia ngazi nyengine ni 'Airline Transport Pilot License' (ATPL) ambayo ni mchanganyiko wa masaa ya kutosha, ujuzi na taaluma
3> ADA
Hapa jiandae kisaikolojia maana huyu ndiyo mchawi wa ndoto za urubani kwa kila mtu, hii hata Ulaya na Marekani.
Kama ulikuwa hujui anza kufahamu sasa masuala ya Usafiri wa anga hakuna kitu rahisi rahisi kama sekta nyengine.
Kupaa na ndege saa moja ya mafunzo ni kati ya dola za kimarekani $200-$300.
Unahitaji saa 40-45 ili kuweza kufanya mtihani kupata leseni binafsi tu (PPL), kisha zinahitajika saa 200 za kufanya mtihani wa Leseni za biashara (CPL) hapo sijaongelea gharama za darasani (ground school) na matakwa mengine.
Ingawa baadhi watu huomba kudandia ndege za walimu baada ya kupata Leseni ya PPL ili kutafuta ujuzi kujenga masaa na kupunguza gharama kuelekea CPL.
Bahati mbaya zaidi kupata udhamini wa kusomeshwa Urubani kutoka kwa mtu baki, Taasisi au kampuni si jambo rahisi hata kidogo.
Tuelewane hapa, mzazi, mlezi, mdhamini, mtoaji mikopo anahitaji kujidhatiti na kujitoa kwelikweli ili kufanikisha malengo ya mlengwa anayehitaji kuwa rubani.
Tuliona kijana #NarcentMeena aliamua kuuza karanga za jumla na rejareja ili apate ada ya kujisomesha urubani ili kutimiza ndoto yake.
Mbali na yote, kuwa rubani inawezekana hata kwa mtu wa chini wa kawaida.
Muda mwingine 'mchawi sio kibunda' mchawi matumizi na akiba.
Kama mwanao ana miaka mi 5,10,15 mfungulie fixed akaunti ili kila ukiokota miambili unaweka, au wale wa Bia unagawanya nusu kaunta nusu akaunti.
Usingoje Kafika miaka18 ndiyo utafute pesa kwa mkupuo za mkupuo, ni ngumu sana.
Wanasema cha kesho jenga leo.
La sivyo utasikia lawama tu "mbona marubani wengi ni wale wenye ngozi ile"
Kama hatujakosea sana, hapa nchini kuna vyuo kama Vinne vinavyotoa Mafunzo ya Urubani
Fly Zanzibar
NIT-Mabibo
Tanzania Pilot Training Centre na
ZRP-Zanzibar.