PreGE2025 Mchome amuomba Msajili kutengua maamuzi ya Baraza Kuu la CHADEMA kwa kukiuka Katiba

PreGE2025 Mchome amuomba Msajili kutengua maamuzi ya Baraza Kuu la CHADEMA kwa kukiuka Katiba

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Mwanga, Lembrus Mchome amesema amemuomba Msajili wa vyama vya siasa kutengua maamuzi ya Baraza Kuu la chama hicho yaliyofanyika kwenye kikao cha Baraza Kuu kilichofanyika Januari 22, 2025 kwa kuwa kilikuwa na kasoro.

Akizungumza na wanahabari leo April 8, Mchome amesema Baraza kuu halikuwa halali kwani akidi haikutimia lakini pia ndani yake kulikuwemo na watu ambao sio wajumbe halali wa Baraza kuu kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA.

Soma: Msajili wa Vyama vya Siasa aipa wiki moja CHADEMA ijibu barua ya Mchome

Mchome ameeleza kuwa amemuomba Msajili abatilishe vikao vyote vya kamati kuu viliyokaliwa kuanzia baada ya tarehe 22 kwani wajumbe wake akiwemo Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu Bara na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar uteuzi wao sio halali.

Aidha ameongeza kuwa amepokea barua leo kutoka kwa Msajili wa Vyama Vyama Siasa ikimjibu maombi yake kuwa Msajili amemtaka Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika kujibu malalamiko ya Mchome ndani ya siku tatu.

 
Kuna msemo niliusikia zamani kwenye tamthilia moja ya Zambia, inaitwa ka banana,
Msemo ni "if you squeeze them by the ball, the head will follow" Chadema imewashika ccm makende, sasa, hv vichwa vinawaka moto, kila mtu ananena kwa lugha!!
Shikilia hapo hapo mkuu Lisu, Malaya wa, kisiasa ni wengi, hapa nipo na vunja measure kwa kucheka, jinsi "makada" Wa, chadema wanavyoishambulia chadema! Badala, ya, ccm!
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Mwanga, Lembrus Mchome amesema amemuomba Msajili wa vyama vya siasa kutengua maamuzi ya Baraza Kuu la chama hicho yaliyofanyika kwenye kikao cha Baraza Kuu kilichofanyika Januari 22, 2025 kwa kuwa kilikuwa na kasoro.

Akizungumza na wanahabari leo April 8, Mchome amesema Baraza kuu halikuwa halali kwani akidi haikutimia lakini pia ndani yake kulikuwemo na watu ambao sio wajumbe halali wa Baraza kuu kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA.

Soma: Msajili wa Vyama vya Siasa aipa wiki moja CHADEMA ijibu barua ya Mchome

Mchome ameeleza kuwa amemuomba Msajili abatilishe vikao vyote vya kamati kuu viliyokaliwa kuanzia baada ya tarehe 22 kwani wajumbe wake akiwemo Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu Bara na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar uteuzi wao sio halali.

Aidha ameongeza kuwa amepokea barua leo kutoka kwa Msajili wa Vyama Vyama Siasa ikimjibu maombi yake kuwa Msajili amemtaka Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika kujibu malalamiko ya Mchome ndani ya siku tatu.

Ingesomeka hivi: Mchome amuomba mumewe........ . Maana sasa wanapika na kupakua huko Masaki. Mchome rasmi ni mke wa msajili.
 
Back
Top Bottom