Bawabu wa pili
Senior Member
- Nov 14, 2025
- 147
- 432
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo bara, Isihaka Mchinjita, ametoa wito kwa Watanzania kutokubali kukata tamaa kufuatia matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, akisisitiza kuwa silaha kubwa ya "mkandamizaji" ni kuuvunja moyo na mtazamo wa wanaokandamizwa.
Akizungumza jana, Januari 13, 2026, katika mkutano wa ndani na viongozi pamoja na wajumbe wa Jimbo la Ubungo, Mchinjita alitumia nukuu ya mpigania haki wa Marekani, Malcolm X, kuelezea umuhimu wa raia kulinda haki zao wenyewe badala ya kusubiri msaada kutoka nje au kwa viongozi pekee.
Soma pia: Mchinjita: Kilichotokea Oktoba 29 kimedhihirisha CCM imekosa ushawishi
“Wajibu wetu wa kiuongozi ni kuwaambia ukweli kwamba lazima sisi ndio tukalinde haki zetu, sio maneno ya viongozi. Tujenge hoja tukikaa mezani lakini nguvu ya umma ndio itakayoweza kuleta mabadiliko kwa sababu hoja zimeshajaa mezani", amesisitiza Makamu Mwenyekiti huyo mbele ya wafuasi wa chama hicho waliojitokeza kueleza dukuduku lao kuhusu uchaguzi uliopita.
Akizungumza jana, Januari 13, 2026, katika mkutano wa ndani na viongozi pamoja na wajumbe wa Jimbo la Ubungo, Mchinjita alitumia nukuu ya mpigania haki wa Marekani, Malcolm X, kuelezea umuhimu wa raia kulinda haki zao wenyewe badala ya kusubiri msaada kutoka nje au kwa viongozi pekee.
Soma pia: Mchinjita: Kilichotokea Oktoba 29 kimedhihirisha CCM imekosa ushawishi
“Wajibu wetu wa kiuongozi ni kuwaambia ukweli kwamba lazima sisi ndio tukalinde haki zetu, sio maneno ya viongozi. Tujenge hoja tukikaa mezani lakini nguvu ya umma ndio itakayoweza kuleta mabadiliko kwa sababu hoja zimeshajaa mezani", amesisitiza Makamu Mwenyekiti huyo mbele ya wafuasi wa chama hicho waliojitokeza kueleza dukuduku lao kuhusu uchaguzi uliopita.