Mchina ajinyonga, ni baada ya kuboronga katika kazi Morogoro

Mchina ajinyonga, ni baada ya kuboronga katika kazi Morogoro

pale kariakoo palifanyika ukarabatii wa mitaro ya maji taka ya chini ya ardhi, katika ukarabati ule yalitumika mabilioni ya shilingi nandio ukarabati mmbovu kuliko yote iliyowahi kutokea, hapa nchini lakini hadi leo wasimamizi wa huo mradi wanaendelea kula vijisenti vyao.

Nashauri waige ndugu mchina
 
babo Niliwahi kumzuia project manager wa kichina kuniletea wachina wasiokuwa na vyeti akiwemo yeye mwenyewe. Unamweleza akuletee vyeti vya kuonesha qualification za wafanyakazi wake ili uwaruhusu kufanya kazi kama mkataba unavyosema yeye anakuletea barua za kampuni kuwa hao ni watu wao wenye ujuzi na wamethibitishwa na kampuni zao.


Safi sana, wewe na mimi yaelekea tu katika industry moja.
Hawa jamaa hasa kwenye miradi mingi ya barabara wanaleta vijamaa havijui lolote,vipo tu. Kazi vinajifunzia huku.
Watanzania wenye viwango vikubwa zaidi yao hawana kazi wala hawathaminiwi!
Halafu linakuja jitu linasema '..serikali-sikivu-ya-ccm..' unalitizamaaa..!
Na sio kwamba wizara haijui,inajua kabisa, swali linabaki kwanini hawachukui hatua?
 
Last edited by a moderator:
Alisema kwa sasa mwili wa marehemu huyo umehifadhiwa katika Hospitali ya St Francis iliyopo Kilakala, Morogoro.

Hiyo Hospitali ipo mtaa upi Kilakala?! Kilakala niijuayo haina hospitali sanasana Dispensary ya Tuwaenzi wazee na wala haina mochuari, Huu ni upotoshaji, hivi inawagharimu kiasi gani kuhakiki habari kabla hamjaandika gazetini?

Mimi niko ifakara mwili wa marehemu uko katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hosipitali ya St. Francis iko hapahapa Ifakara sio kilakala kama mtoa maada alivyosema, aidha mkalimani aliye toa tafsiri ya awali ya ujumbe alio andika marehemu anasema alijinyonga sababu ya ugumu wa maisha na siamini kuwa sababu ni kuboronga kazi kwani hakuna daraja ambalo lilishajengwa bali ni makaravati tu ambayo bado ujenzi unaendelea na marehemu alikuwa ni mfanyakazi wa ngazi ya chini na hawajibiki na kuborongwa kwa kazi.
 
Hakuwa na option maana hata angerudi kwao angenyongwa tu kama wale waliojenga uwanja wa taifa.
 
Hospitali ya st francis haipo kilakala mbona!
 
babo ni vizuri kusema ukweli. Taarifa iliyotolewa jana na kamanda wa polisi ni kuwa mchina huyo alijinyonga. Ujumbe alioacha ambao umeandikwa kwa kichina na tafsiri ya haraka isiyo rasmi kama alivosema kamanda ni kuwa "mchina" alijinyonga kwasababu ya ugumu wa maisha. Sasa suala la kuburunda kazi umelitoa wapi? Si vizuri kufanya upotoshaji maana wapo wengine ambao hawakuona na wanaweza kukuamini wewe kumbe sivyo.

Rai yangu, kumekuwa na mfumo wa kuleta wachina kufanya kazi huku kwetu na wakati huo pesa malipo yao wanalipwa kwenye benki zao huko huko kwao. Hili linawafanya wakati mwingine waishi maisha magumu ambayo yanawafanya wawe na stress. Huku wanapewa pesa kidogo ya kujikimu na kuhifadhiwa kwenye makambi (Sites). Ingawa kwa sera ya kitaifa ni nzuri maana wanahakikisha mzunguko wa hela unabaki china. Lakini kwa upande wa nchi yetu, hili linakosesha ajira nyingi kwa wazawa ambao wangeweza kufanya kazi zinazofanywa na hao wachina au wangefungua biashara maana mzunguko wa hela ungeongezeka. Wizara ya kazi iwemakini hasa vibali wanavyotoa kwa wafanyakazi wa kigeni. Wengi wao hawana ujuzi bali inakuwa kama sehemu ya kutafutiana ajira kwa wachina wenzao. Ukiangalia reports za EIA za miradi hiyo wanasema positive effects ni ajira kwa wazawa ama wa maeneo inakofanyika miradi au watanzania wengine. Lakini wakati wa utekelezaji hata ile kazi amabayo ingefanywa na mzawa anawekwa mchina 'SHAME TO MY POOR COUNTRY" Mamlaka husika haziwezi kusimamia hilo! Wahusika wamekazana kupokea rushwa toka kwao ili kuwapatia permits. Niliwahi kumzuia project manager wa kichina kuniletea wachina wasiokuwa na vyeti akiwemo yeye mwenyewe. Unamweleza akuletee vyeti vya kuonesha qualification za wafanyakazi wake ili uwaruhusu kufanya kazi kama mkataba unavyosema yeye anakuletea barua za kampuni kuwa hao ni watu wao wenye ujuzi na wamethibitishwa na kampuni zao.

Acha uongo wewe, weka hiyo tafsiri ya haraka, ikiwezekana barua yenyewe, acha uongo, unaonekana wewe ni mfupi na mnafiki


Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
nothing to comment sababu mhusika kafa.............. alazwe alipopaandaa
 
Alisema kwa sasa mwili wa marehemu huyo umehifadhiwa katika Hospitali ya St Francis iliyopo Kilakala, Morogoro.

Hiyo Hospitali ipo mtaa upi Kilakala?! Kilakala niijuayo haina hospitali sanasana Dispensary ya Tuwaenzi wazee na wala haina mochuari, Huu ni upotoshaji, hivi inawagharimu kiasi gani kuhakiki habari kabla hamjaandika gazetini?
Mkuu nadhani alitaka kusema St Francis Ifakara
 
Huu uwe mfano kwa wabunge wetu nao wajifunze kitu hapa ili pale wanapofeli katika ahadi zao waoneshe uzalendo kama hivi pia itapendeza sana
 
Acha uongo wewe, weka hiyo tafsiri ya haraka, ikiwezekana barua yenyewe, acha uongo, unaonekana wewe ni mfupi na mnafiki


Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Kama ungesoma kwa makini maelezo yangu niliyo highlight usingetumia lugha uliyotumia. Siwezi kukulaumu maana mfumo wa elimu nao umebadilika hivyo pengine wewe ni miongoni mwa waathirika. Ndo maana nimeamua ku-highlight na ku-underline ili pengine uweze kuelewa.
Sihitaji kuweka ushahidi wa barua maana nimekupa source ya taarifa. (Nime-report kama muhusika alivyosema) na ndo kitu nilitaka mtoa habari aseme kama kamanda alivyosema na si kupindisha kwasababu haitusisaidii. Zaidi unawapoteza wale ambao hawakusikia maelezo ya kamanda wa polisi na hivyo inaweza kupelekea kuwa na hisia tofauti. Hutaki kuamini unaacha wala hulazimishwi.
Kweli waalimu wanakazi.

babo ni vizuri kusema ukweli. Taarifa iliyotolewa jana na kamanda wa polisi ni kuwa mchina huyo alijinyonga. Ujumbe alioacha ambao umeandikwa kwa kichina na tafsiri ya haraka isiyo rasmi kama alivosema kamanda ni kuwa "mchina" alijinyonga kwasababu ya ugumu wa maisha.
Sasa suala la kuburunda kazi umelitoa wapi? Si vizuri kufanya upotoshaji maana wapo wengine ambao hawakuona na wanaweza kukuamini wewe kumbe sivyo.

Rai yangu, kumekuwa na mfumo wa kuleta wachina kufanya kazi huku kwetu na wakati huo pesa malipo yao wanalipwa kwenye benki zao huko huko kwao. Hili linawafanya wakati mwingine waishi maisha magumu ambayo yanawafanya wawe na stress. Huku wanapewa pesa kidogo ya kujikimu na kuhifadhiwa kwenye makambi (Sites). Ingawa kwa sera ya kitaifa ni nzuri maana wanahakikisha mzunguko wa hela unabaki china. Lakini kwa upande wa nchi yetu, hili linakosesha ajira nyingi kwa wazawa ambao wangeweza kufanya kazi zinazofanywa na hao wachina au wangefungua biashara maana mzunguko wa hela ungeongezeka. Wizara ya kazi iwemakini hasa vibali wanavyotoa kwa wafanyakazi wa kigeni. Wengi wao hawana ujuzi bali inakuwa kama sehemu ya kutafutiana ajira kwa wachina wenzao. Ukiangalia reports za EIA za miradi hiyo wanasema positive effects ni ajira kwa wazawa ama wa maeneo inakofanyika miradi au watanzania wengine. Lakini wakati wa utekelezaji hata ile kazi amabayo ingefanywa na mzawa anawekwa mchina 'SHAME TO MY POOR COUNTRY" Mamlaka husika haziwezi kusimamia hilo! Wahusika wamekazana kupokea rushwa toka kwao ili kuwapatia permits. Niliwahi kumzuia project manager wa kichina kuniletea wachina wasiokuwa na vyeti akiwemo yeye mwenyewe. Unamweleza akuletee vyeti vya kuonesha qualification za wafanyakazi wake ili uwaruhusu kufanya kazi kama mkataba unavyosema yeye anakuletea barua za kampuni kuwa hao ni watu wao wenye ujuzi na wamethibitishwa na kampuni zao.
 
Walete hicho kikaratasi niwatafsirie..

Cha ajabu zaidi jeshi linatafuta mtu wa kutafsiri kichina hii ni aibu sana kwa jeshi la polisi.kitengo cha inteligensia kina fanyaje kazi bila kujua lugha ya kichina? Hii imenisononesha sana. R.I.P MCHINA
 
hawa viongozi wetu wangeiga wanapokosea waji2ndike. Tanzania ingekuwa kama hongkong china.

Wewe mawazo yako haupimi, hujui kama saivi tungekua na viongozi wachache sana
 
Acha uongo wewe, weka hiyo tafsiri ya haraka, ikiwezekana barua yenyewe, acha uongo, unaonekana wewe ni mfupi na mnafiki


Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums


it seems wewe ni mmoja ya watoto wa kichina wasiojua baba zao waliotokana na miradi ka ule wa uwanja wa taifa,,,mlaumu mama yako kwa njaa zake na ulimbukeni wa kujirahisisha kwa forgeiners
 
Huyo kufa ilikuwa lazima alichofanya ni kuwahi tu. Ila wachina ukiboronga lazima kisu kipite shingoni
 
Back
Top Bottom