...Mchezo Wa Vita Una Umri Wake…!

...Mchezo Wa Vita Una Umri Wake…!

maggid

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2006
Posts
1,084
Reaction score
1,250
Ndugu zangu,

Utotoni mbali ya michezo mingine kuna tuliopenda kucheza ‘ Mchezo wa vita’. Kadri miaka ilivyoenda na umri kuongezeka kuna tulioelewa maana ya vita.

Binafsi nimeishi kumsikia kwa masikio yangu Amiri Jeshi Mkuu , Rais wa nchi akitangaza vita. Ni mwaka 1978. Ni kwenye Vita ya Kagera. Jioni ile nikiwa na miaka kumi na mbili tu niliiona tofauti ya siku hiyo na nyingine zote.

Nakumbuka usiku ule taa zilizimwa . Niliyaona magari ya kijeshi yalipita barabara ile ya Morocco, Kinondoni tulikokuwa tukiishi. Yalitokea kambi ya Lugalo.

Nakumbuka kumsikia Rais wa nchi, Julius Nyerere akitamka; “ Vita si lelemama!” Katika umri wangu ule mdogo sikumwelewa Mwalimu Nyerere alimaanisha nini.

Naam, vita vya Kagera vilipomalizika nakumbuka kumsikia Julius Nyerere akitamka;

“ Ndugu Wananchi, tuna miezi 18 ya kufunga mikanda”. Julius Nyerere alimaanisha hali ngumu ya kiuchumi iliyokuwa ikija mbele yetu kama taifa.

Huenda Julius Nyerere alijua, kuwa ni zaidi ya miaka 18 migumu kiuchumi iliyo mbele yetu. Lakini, kama baba kwenye nyumba, ni vigumu kuiambia familia yako inayokutegemea, kuwa kuna miaka 18 mbele ya kuhemea chakula.

Leo naweza kabisa kuandika, kuwa sehemu ya matatizo yetu ya kiuchumi tuliyonayo sasa, yanatokana na makovu ya Vita Vya Kagera. Ni miaka 35 iliyopita.

Nahofia, kuwa hata sasa kuna miongoni mwetu wenye kutamani nchi iingie kwenye vurugu na hata vita vya wenyewe kwa wenyewe. Kwamba wamechoka na amani tuliyo nayo.

Na wakati mwingine unafikiri, kuwa huenda kuna wenye kuaangalia sana filamu za kivita, sasa wanataka waone uhalisia wake.

Naamini, bado tuna nafasi ya kutatua matatizo mengi tuliyo nayo sasa, kwa njia za mazungumzo. Kwa njia za amani.

Naam, Vita si sawa na kucheza kombolela. Vita Si Lemama!

Ni Neno Fupi La Usiku.

Maggid,
Dar es Salaam.
 
Kwa watawala ambao wanataka kuendelea kutawala hata bila ya ridhaa ya wanachi,hao kumwaga damu kwao si tatizo.

Wako tayari kuangamiza hata Mtwara au Arusha yote ili kutimiza tama zao. Kwao hawa, amani ya jamii si kitu na wanaona mali zao walizowafasidi raia wao zitakuwa kinga kwao siku zote. Hata hivyo, historia inatukumbusha mengi kama tunataka kuikubali kweli.

Kwa wanaokandamizwa na kuuawa, wanaweza kuwa na utulivu bila ya amani hadi pale watakapoacha kukubali kuumizwa na kupambana na uonevu (si waonevu)wote kama vile Nyerere,Mandela, Ghandhi na Martin Luther King (Jr).

Kwa watawala waonevu, hakuna dola iliyodumu milele isipokuwa ya mwenyezi Mungu tu; wanapaswa kujirekebisha kabla hawaufikia mwisho wa Hitla, Saddam na Gaddafi. Amani inayohubiriwa na watawala kandamizi si amani ya kweli kwani madhara yanayoipata jamii kwa mfumo kandamizi hayaelezeki na wahanga wake hawahesabiki na wanakufa kifo cha kinyonge chenye kumtoa chozi kila mpenda amani.

Hebu fikiri katika amani yetu hii tunayojivunia kinafiki mabomu yanapigwa hadi nyumba za ibada na mikutano ya siasa, mwandishi akiwa na laptop tu anazingilwa na polisi lukuki ambao wanaishishia kuutoa uhai wake kwa bomu, raia wanateswa na kubakwa, wengi wanapata madhara kwa kutumia maji yaliyochafuliwa na 'wawekezaji' wa madini wanaolindwa na watawala na polisi wetu wapendwa. Hapo sitaki kukukumbuka mama wajawazito,watoto na wagonjwa wanaokufa kila sekunde ama kwa kukosa huduma stahiki, au kupata huduma duni ikiwa na kupewa dawa feki kutokana na ama rushwa au ufusadi unaolelewa na kustawishwa na dola.

Huwezi amini au kukubali kwa hata Chalinze, kilometa kumi (10) toka Msoga, nyumbani kwa raisi, watoto hawapati chanjo muhimu kwa watoto nahivyo maisha yao yamo hatarini huku watawala wetu wakiendelea kuhubiri amani kwa waakazi wanaosubiri vifo vyao na kizazi chao.

Ni kweli wamechoka kama waziri mkuu alivyokiri bungeni hivi karibuni. Sijui na raia hawa wasio na matumaini wakichoka na kuwa kufa kama kuku wa kuchinjwa itakuwaje kwetu sote kwani vita si lelemama na wala haina macho.

Mungu na aturehemu.
 
Maggid amekua kama Joyce wowowo... anakata viuno tu huku swahiba Ludovick keshamtelekeza
 
Ni ushauri usio na ufumbuzi wa matatizo. Hutaki kuzungumzia kiini cha tatizo ila propaganda.
 
maggid,

..YES,vita ya kagera vilituathiri kiuchumi.

..but it is more than 30 yrs since the war ended.

..Now, dont u think it is IRRESPONSIBLE kudai kwamba matatizo yetu ya sasa ya uchumi yamesababishwa na, au chanzo chake ni, vita vya Kagera?

..kwanza vita ile ilipiganwa ktk eneo dogo sana la nchi yetu.

..hiyo ni tofauti na nchi kama Msumbiji ambao walipigana nchi nzima, tena kwa miaka mingi zaidi yetu sisi.

..leo hii Msumbiji wako sawa na sisi, kama siyo kutuzidi, ktk juhudi za kujikwamua kiuchumi.

..TATIZO LETU NI UONGOZI MBOVU CHINI YA SERIKALI ZA CCM.

cc: Mchambuzi, Nguruvi3, Nyani Ngabu
 
Last edited by a moderator:
Vita ni vita, na pale diplomasia inaposhindwa vita ni lazima ipiganwe ikiwa TU ina lengo la kutetea maslahi ya nchi! Vita kati ya nchi na nchi hususani linapokuja suala la kutetea maslahi ya nchi kama vile mipaka na watu wake; ni lazima vipiganwe ikiwa diplomasia imeshindwa! Nchi inayoshindwa kutetea mipaka na watu wake si nchi ya kujivunia hata kidogo! Vita vya Uganda sikubaliano nayo na chanzo chake(tusilijadili hili tusije tukavuruga mada) lakini pale ambapo tulifikia, kwa Amin kuingia Tanzania, hakika hatukuwa na namna bali ni kupigana nae bila kujali kwamba tutashindwa au hapana!

Lakini linapokuja suala la vita vya wenyewe kwa wenyewe, kwangu haina justification hususani kwa mazingira ya viongozi wa Afrika! Sina mfano wa kuutolea wa kuonesha watu fulani walipigana vita na kuundoa madarakani uongozi uliokuwapo na baadae hawa walioingia wakaleta tofauti....inashangaza, ni kama tumerogwa....kokote utakoenda viongozi wa Africa ni the same!! Hivyo basi, vita vya wenyewe kwa wenyewe ni vya kimaslahi binafsi zaidi kuliko kwa maslahi ya taifa!
 
Sasa majid, naona umeshikilia hiyo mabo ya red brigade. Wewe upo huko ccm ambako ndiko mambo haya yameanzia. Sijakusikia hata siku moja ukikikanya chama chako na kikundi chake cha green guard. Mlijivika upofu,leo ndio mnaona!

Ama kweli kunyata anyate kinyonga, akinyata kicheche anavizia kuku.
 
Damu ya Kibanda (japo kuwa hakufa), inakulalamikia kutoka ardhini...
 
Ni upuuzi na uwenda wazimu kuhusisha umaskini wetu na vita ya kagera miaka 35 iliyopita!. Hivi wajerumani waliopigana vita vya dunia mara 2 uchumi wao upoje?. Hivi kupigna vita ndo kunatunyima akili kiasi cha kuingia mikataba ya aibu?. Taifa linaongozwa na wapuuzi, wananchi nao ni wapuuzi kama mleta mada alivo jipambanua! hataki kugusa kiini cha matatizo bali kueleza matokeo ya matatizo kana kwamba vita hutokea tutokea bila sababu.
 
Hawa ndiyo wanamshauri JK kuweka mikanda ya vita vya Wanyarwanda wakati wa chaguzi hapa nchini.
Vita umeisikia wapi Tanzania?
Ni hiyo RB ndiyo inawafanya muongee kila lugha?
 
Mjengwa nimekuelewa sana.Nchi nyingi Afrika zenye mali asili kubwa huwa zinakuwa na vita mfano Kongo wao wana dhahabu,shaba,almasi,uranium etc, Angola Mafuta, sudan mafuta, Libya mafuta.Mabwana wakubwa wa dunia kama Marekani na nchi zingine za ulaya ndiyo wachochezi wakubwa wa mifarakano Afrika kwa sababu wanajua ni rahisi kuchota rasilimali kwenye nchi zenye vita hasa ya wenyewe kwa wenyewe.Baada ya utangulizi huo mdogo, Nchi yetu ni miongoni mwa nchi zenye rasilimali nyingi katika afrika kwahiyo tupo kwenye hatari kubwa ya kuchochewa na mataifa ambayo yataona hayawezi kufaidika na rasilimali zetu kwa utawala huu uliopo madarakani. Kama ni wafatiliaji wazuri wa hotuba za rais kuna siku alisema kuna nchi zinaumia kuona nchi yetu ina amani.Kwa sababu za kidiplomasia rais hakutaja nchi hizo.Ila kwa sasa ushaidi wa kimazingira unaonyesha kuna chama kinapewa misaada na nchi za ulaya.Na chama hicho kimekuwa na kauli za vita na kutaka machafuko katika nchi,Mfano:1. kiliwahi kusema nchi haitatawalika, 2. kiliwahi kusema wanataka kuunda Jamuhuri ya kaskazini yaani Kilimanjaro,Arusha na manyara iwe nchi inayojitegemea,(ndiyo maana wanashabikia sera ya majimbo kwa sababu itarahisisha hili jambo) 3. Wanataka kuanzisha jeshi la chama. Kwa hiyo ndugu zangu tusipokuwa makini na hivi vyama vya siasa tutaingia matatizoni wakati wao na watoto wao watakuwa ulaya wakipanga uongozi wa kuishika nchi baada ya vita walivyovianzisha kuisha.Sisi pangu pakavu tutakuwa kwenye matatizo makubwa. Mimi nawashauri watanzania wenzangu tuna nafasi nzuri ya kuweka mazingira bora kwa maendeleo ya kila mmoja wetu kupitia katiba mpya.Tuongeze nguvu kuiboresha kwa maoni katiba yetu.
 
Ni upuuzi na uwenda wazimu kuhusisha umaskini wetu na vita ya kagera miaka 35 iliyopita!. Hivi wajerumani waliopigana vita vya dunia mara 2 uchumi wao upoje?. Hivi kupigna vita ndo kunatunyima akili kiasi cha kuingia mikataba ya aibu?. Taifa linaongozwa na wapuuzi, wananchi nao ni wapuuzi kama mleta mada alivo jipambanua! hataki kugusa kiini cha matatizo bali kueleza matokeo ya matatizo kana kwamba vita hutokea tutokea bila sababu.
huyu majjid ni mpuuzi wa kutupwa,ndo maana hata blog yake imepungua wasomaji baada ya kugundua kua ana akili mbovu.mimi na marafiki wengi hatupiti kabisa kwake.
 
Asante Majid kwangu mimi neno "vita" ni neno chungu sana. Wasalaam
 
Mimi sio mwanasiasa ila mwananchi wa kawaida tu. Mtoa mada amepotosha kidogo kwenye hoja ya kutofanya vizuri kiuchumi kwa taifa letu. Simlaumu sana kwani bado alikuwa mdogo wakati huo. Baada ya vita vya kumng'oa nduli Amin katika miaka ya 80 hivi tuliwekewa vikwazo vigumu sana na serikali ya Reagan wakati huo. Hapo maisha yalikuwa magumu sana kwani hatukuweza kuimport chochote madukani kulikuwa hakuna kitu, mashelf yalikuwa yamepambwa na majani ya chai peke yake. Kipindi hicho hata kuoga tulikuwa tunatumia foma kama mnakumbuka. Ni dhahiri kuwa ukuaji wa uchumi wetu ulikuwa duni sana hata tulilazimika kudevalue shilingi kwa kiasi kikubwa sana. Hapo ndio ulikuwa mwanzo wa vifisadi uchwara waliobahatika kuwa RTC na NDL na wahindi wachache waliohoard mali katika majumba yao. Hali ilizidi kuwa mbaya hadi wakati ule Sokoine akiwa waziri mkuu aliwatolea uvivu wahujumu uchumi wa wakati huo. Kwa bahati mbaya Sokoine aliaga dunia baada ya ajali akitokea Dodoma kuja Dar. Katika kipindi hiki mbegu ya ufisadi ilishapandwa na ikaanza kuota miongoni mwa Watanzania na haswa katika chama tawala. Serikali ya awamu ya pili iliingia na haikufanya lolote kurekebisha ufisadi huu. Matokeo yake ni kuwepo kwa wimbi kubwa la matajiri wakiingia kwenye siasa na kugombea ubunge kupitia ticket ya chama tawala. Kwa sababu ya kulewa madaraka na kukosa dira ya uongozi serikali ilishindwa kurekebisha au ku-address changamoto ilizokuwa nazo kama tatizo la uhaba wa umeme. Badala yake serikali ilianza kuingia kwenye mikataba mibovu ambayo ndiyo imetufikisha hapa tulipo leo.
 
Mimi sio mwanasiasa ila mwananchi wa kawaida tu. Mtoa mada amepotosha kidogo kwenye hoja ya kutofanya vizuri kiuchumi kwa taifa letu. Simlaumu sana kwani bado alikuwa mdogo wakati huo. Baada ya vita vya kumng'oa nduli Amin katika miaka ya 80 hivi tuliwekewa vikwazo vigumu sana na serikali ya Reagan wakati huo. Hapo maisha yalikuwa magumu sana kwani hatukuweza kuimport chochote madukani kulikuwa hakuna kitu, mashelf yalikuwa yamepambwa na majani ya chai peke yake. Kipindi hicho hata kuoga tulikuwa tunatumia foma kama mnakumbuka. Ni dhahiri kuwa ukuaji wa uchumi wetu ulikuwa duni sana hata tulilazimika kudevalue shilingi kwa kiasi kikubwa sana. Hapo ndio ulikuwa mwanzo wa vifisadi uchwara waliobahatika kuwa RTC na NDL na wahindi wachache waliohoard mali katika majumba yao. Hali ilizidi kuwa mbaya hadi wakati ule Sokoine akiwa waziri mkuu aliwatolea uvivu wahujumu uchumi wa wakati huo. Kwa bahati mbaya Sokoine aliaga dunia baada ya ajali akitokea Dodoma kuja Dar. Katika kipindi hiki mbegu ya ufisadi ilishapandwa na ikaanza kuota miongoni mwa Watanzania na haswa katika chama tawala. Serikali ya awamu ya pili iliingia na haikufanya lolote kurekebisha ufisadi huu. Matokeo yake ni kuwepo kwa wimbi kubwa la matajiri wakiingia kwenye siasa na kugombea ubunge kupitia ticket ya chama tawala. Kwa sababu ya kulewa madaraka na kukosa dira ya uongozi serikali ilishindwa kurekebisha au ku-address changamoto ilizokuwa nazo kama tatizo la uhaba wa umeme. Badala yake serikali ilianza kuingia kwenye mikataba mibovu ambayo ndiyo imetufikisha hapa tulipo leo.

Umefafanua vizuri mkuu nahisi maggid anaikumbuka vizuri adha ya kula unga wa yanga(njano) uliotolewa na national milling wakati ule tena kwao iringa hali ndo ilikua mbaya kutokana na wahindi wa pale uhindini kucheza dili na RTC Kuhujumu uchumi......amani yetu itakua amani pale tutakapo nufaika na matunda ya uchumi wetu na wala si matunda ya ufisadi au matunda ya siasa chafu....Nawasilisha.
 
maggid,

..YES,vita ya kagera vilituathiri kiuchumi.

..but it is more than 30 yrs since the war ended.

..Now, dont u think it is IRRESPONSIBLE kudai kwamba matatizo yetu ya sasa ya uchumi yamesababishwa na, au chanzo chake ni, vita vya Kagera?

..kwanza vita ile ilipiganwa ktk eneo dogo sana la nchi yetu.

..hiyo ni tofauti na nchi kama Msumbiji ambao walipigana nchi nzima, tena kwa miaka mingi zaidi yetu sisi.

..leo hii Msumbiji wako sawa na sisi, kama siyo kutuzidi, ktk juhudi za kujikwamua kiuchumi.

..TATIZO LETU NI UONGOZI MBOVU CHINI YA SERIKALI ZA CCM.

cc: Mchambuzi, Nguruvi3, Nyani Ngabu

Kwa kuongezea tu, Vita Vya Kagera viligharimu taifa dola za kimarekani milioni mia tano ($500,000,000); Nje ya vita hivi, taifa lilikuwa katika hali ya amani na utulivu kutokana na wananchi kuwa na imani na serikali pamoja na viongozi wao lakini muhimu zaidi, matumaini makubwa juu ya hatima za maisha yao; Tanzania ya leo, amani na utulivu vimetoweka kutokana na wananchi walio wengi kuzizi kupoteza imani na serikali na viongozi wao (CCM) na pia kukata tamaa kimaisha; Katika muktadha huo, ni dhahiri kwamba kila mwaka taifa linapoteza zaidi ya fedha tulizopoteza kwenye vita vya kagera kutokana na ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma; Madhara yake ni mwananchi kuzidi kuumia, wengi wao wakiwa ni vijana; Katika mzingira kama haya, unashawishije vijana kwamba matatizo yanayowakabili yanaweza kutatuliwa kwa njia ya mazungumzo na kwa njia ya amani, vijana ambao wengi wao have nothing to lose hata vita vikija kesho? Maandamano ya amani na utulivu ni moja ya njia halali na effective katika demokrasia yoyote ile kwa watu kuonyesha kutoridhishwa na hali zao za maisha; je kwetu Tanzania, ni nani anayegeuza njia hii ya amani na utulivu (maandamano) kuwa ni njia ya kivita, wananchi au serikali waliyoiweka madarakani?
 
Kwa kuongezea tu, Vita Vya Kagera viligharimu taifa dola za kimarekani milioni mia tano ($500,000,000); Nje ya vita hivi, taifa lilikuwa katika hali ya amani na utulivu kutokana na wananchi kuwa na imani na serikali pamoja na viongozi wao lakini muhimu zaidi, matumaini makubwa juu ya hatima za maisha yao; Tanzania ya leo, amani na utulivu vimetoweka kutokana na wananchi walio wengi kuzizi kupoteza imani na serikali na viongozi wao (CCM) na pia kukata tamaa kimaisha; Katika muktadha huo, ni dhahiri kwamba kila mwaka taifa linapoteza zaidi ya fedha tulizopoteza kwenye vita vya kagera kutokana na ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma; Madhara yake ni mwananchi kuzidi kuumia, wengi wao wakiwa ni vijana; Katika mzingira kama haya, unashawishije vijana kwamba matatizo yanayowakabili yanaweza kutatuliwa kwa njia ya mazungumzo na kwa njia ya amani, vijana ambao wengi wao have nothing to lose hata vita vikija kesho? Maandamano ya amani na utulivu ni moja ya njia halali na effective katika demokrasia yoyote ile kwa watu kuonyesha kutoridhishwa na hali zao za maisha; je kwetu Tanzania, ni nani anayegeuza njia hii ya amani na utulivu (maandamano) kuwa ni njia ya kivita, wananchi au serikali waliyoiweka madarakani?
Mchambuzi,

..thanks.

..umesema vita ilitugharimu USD 500 million.

..kuna mahali nimesoma kwamba in the last 2 yrs Tanzania tume-export dhahabu yenye thamani ya USD 1.9 billion na USD 1.4 billion.

..hivi thamani ya dhahabu iliyochimbwa nchi hii over the years haiwezi ku-offset hasara tuliyoingia kutokana na vita vya Kagera??

..hivi kuna uhalali wa kuunganisha matatizo yetu ya uchumi ya leo hii na vita vya Kagera??

..naomba nikiri kwamba I am not an economist kwa hiyo naweza kuwa nimekosea.

cc😡NasDaz, chama, Mzee Mwanakijiji, EMT, Gaijin, Kobello, Kiranga, Zitto
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi,

Kwanza nianze kwa kukushukuru kwa kutupatia figure za hizo deni lililotajwa hapo juu. Mtu yeyote atakayesema ya kuwa umasikini wetu leo hii unatokana na deni la vita vya Kagera hatakuwa amechoka kufikiri. Umasikini wetu ni matokeo ya ubinafsi na ufisadi wa viongozi wetu. Deni la dola milioni 500 sio kubwa sana kwa taifa kama letu lenye vyanzo vingi vya mapato. Hebu fikiria, ndege ya Rais, Gulf Stream jet ililigharimu taifa dola milioni 40, Radar ile ya BAE nayo iligharimu kama dola milioni 40. Kali ya yote, juzi hapa Chief auditor general amesema ya kuwa zaidi dola milioni 383 zilizoko kwenye deni letu la taifa are unaccounted. ( Source: Cloud hangs over missing Sh169bn in national debt, CAG to do special audit). Kwa hiyo, hivyo vitu vitatu tuu vingetosha kabisa kulifuta hilo deni. Sasa mtu anaposema ya kuwa umasikini wetu ni kwa sababu ya vita vya Kagera bila ya kuleta data zitakazohalalisha kauli yake anataka tusemeje?

Mimi bado sijaelewa Mwandishi wa hii mada anamanisha nini anaposema " kuna watu wanatamani tuingie katika vita vya wenyewe kwa wenyewe." Je ni vigezo gani au vitu gani alivyoviona vilivyopelekea yeye kuwatuhumu wazalendo wengine shutuma nzito kama hizo?
 
Back
Top Bottom