Hii michezo ya kuigiza itakwisha lini?
Watanzania tumechoshwa na michezo ya kuigiza, vyama vya upinzani vikuwa ni vichekesho vitupu, sisemi kwamba watanzania hatuna uchungu na nchi yetu au tunafurahia vitendo vy a kifisadi vinavyofanywa na CCM bali kinachotia uchungu ni vyama vya upinzani kukosa dira ya ushindi na kujaza mamluki wa CCM ndani ya vyama. Mfano kitendo cha kuiachia CCM kupitisha wagombea zaidi 10 bila kupingwa kama si usaliti kwa watanzania ni kitu gani? CCM inatumia kila mbinu kudhoofisha upinzani ; ukweli uliopo hivi vyama havikubaliki kila sehemu je wapinzani wamekosa busara kuungaisha nguvu ili kupambana na CCM? Lingekuwa jambo rahisi pale inapokubalika Chadema wapinzani waiunge mkono Chadema, pale inapokubalika CUF waiunge mkono CUF hata uraisi ilipidi wakubaliane asimame mgombea mmoja tu, viongozi wa upinzani wanalijua jambo hili lakini kwa kuwa hawapo kwa maslahi ya watanzania hawawezi hata siku moja wakakubaliana, kimsingi hii michezo ya kuigiza itaendelea siku hadi siku jana ilikuwa Mrema, akaja Mbowe leo hii Dr. Slaa hakuna kitachofanikiwa hadi watakapo tokea viongozi wa kweli kama akina LECH WALESA alipoongoza mapinduzi ya Poland; mapinduzi si lazima damu imwagike; tukipata viongozi wa kweli CCM itaondoka madarakani kwa nderemo na vifijo. Watanzania vyama vyama vya kweli tunavyo bali hatujajua namna ya kivitumia. Vyama vya wafanyakazi na wakulima vikisimama kidedea kutetea maslahi ya watanzania ndio pekee watakaoing`oa CCM madarakani. CCM wameshajifunza kilichotokea Kenya haitakuwa rahisi kuitoa madarakani watatumia kila mbinu chafu wanayoijua kutetea maslahi yao. WATANZANIA AMKENI !!!!!!!!!!
Watanzania tumechoshwa na michezo ya kuigiza, vyama vya upinzani vikuwa ni vichekesho vitupu, sisemi kwamba watanzania hatuna uchungu na nchi yetu au tunafurahia vitendo vy a kifisadi vinavyofanywa na CCM bali kinachotia uchungu ni vyama vya upinzani kukosa dira ya ushindi na kujaza mamluki wa CCM ndani ya vyama. Mfano kitendo cha kuiachia CCM kupitisha wagombea zaidi 10 bila kupingwa kama si usaliti kwa watanzania ni kitu gani? CCM inatumia kila mbinu kudhoofisha upinzani ; ukweli uliopo hivi vyama havikubaliki kila sehemu je wapinzani wamekosa busara kuungaisha nguvu ili kupambana na CCM? Lingekuwa jambo rahisi pale inapokubalika Chadema wapinzani waiunge mkono Chadema, pale inapokubalika CUF waiunge mkono CUF hata uraisi ilipidi wakubaliane asimame mgombea mmoja tu, viongozi wa upinzani wanalijua jambo hili lakini kwa kuwa hawapo kwa maslahi ya watanzania hawawezi hata siku moja wakakubaliana, kimsingi hii michezo ya kuigiza itaendelea siku hadi siku jana ilikuwa Mrema, akaja Mbowe leo hii Dr. Slaa hakuna kitachofanikiwa hadi watakapo tokea viongozi wa kweli kama akina LECH WALESA alipoongoza mapinduzi ya Poland; mapinduzi si lazima damu imwagike; tukipata viongozi wa kweli CCM itaondoka madarakani kwa nderemo na vifijo. Watanzania vyama vyama vya kweli tunavyo bali hatujajua namna ya kivitumia. Vyama vya wafanyakazi na wakulima vikisimama kidedea kutetea maslahi ya watanzania ndio pekee watakaoing`oa CCM madarakani. CCM wameshajifunza kilichotokea Kenya haitakuwa rahisi kuitoa madarakani watatumia kila mbinu chafu wanayoijua kutetea maslahi yao. WATANZANIA AMKENI !!!!!!!!!!