Mchezo huu utaisha lini?

chama

JF-Expert Member
Aug 6, 2010
8,001
2,418
Hii michezo ya kuigiza itakwisha lini?

Watanzania tumechoshwa na michezo ya kuigiza, vyama vya upinzani vikuwa ni vichekesho vitupu, sisemi kwamba watanzania hatuna uchungu na nchi yetu au tunafurahia vitendo vy a kifisadi vinavyofanywa na CCM bali kinachotia uchungu ni vyama vya upinzani kukosa dira ya ushindi na kujaza mamluki wa CCM ndani ya vyama. Mfano kitendo cha kuiachia CCM kupitisha wagombea zaidi 10 bila kupingwa kama si usaliti kwa watanzania ni kitu gani? CCM inatumia kila mbinu kudhoofisha upinzani ; ukweli uliopo hivi vyama havikubaliki kila sehemu je wapinzani wamekosa busara kuungaisha nguvu ili kupambana na CCM? Lingekuwa jambo rahisi pale inapokubalika Chadema wapinzani waiunge mkono Chadema, pale inapokubalika CUF waiunge mkono CUF hata uraisi ilipidi wakubaliane asimame mgombea mmoja tu, viongozi wa upinzani wanalijua jambo hili lakini kwa kuwa hawapo kwa maslahi ya watanzania hawawezi hata siku moja wakakubaliana, kimsingi hii michezo ya kuigiza itaendelea siku hadi siku jana ilikuwa Mrema, akaja Mbowe leo hii Dr. Slaa hakuna kitachofanikiwa hadi watakapo tokea viongozi wa kweli kama akina LECH WALESA alipoongoza mapinduzi ya Poland; mapinduzi si lazima damu imwagike; tukipata viongozi wa kweli CCM itaondoka madarakani kwa nderemo na vifijo. Watanzania vyama vyama vya kweli tunavyo bali hatujajua namna ya kivitumia. Vyama vya wafanyakazi na wakulima vikisimama kidedea kutetea maslahi ya watanzania ndio pekee watakaoing`oa CCM madarakani. CCM wameshajifunza kilichotokea Kenya haitakuwa rahisi kuitoa madarakani watatumia kila mbinu chafu wanayoijua kutetea maslahi yao. WATANZANIA AMKENI !!!!!!!!!!
 
Unafiki wa kipimo cha kwanza.

Kwa nini wewe usianzishe hicho chama cha wakulima na wafanyakazi ili kipambane na ccm? Hata marekani kwenyewe kuna chaguzi huwa vyama vikubwa hivi havina kabisa wagombea (na hata vikiwa nao, havifanyi kabisa kampeni kwenye baadhi ya majimbo).

Katika siasa hili ni jambo la kawaida kabisa. Vyama vya upinzani vinashindana na chama chenye dola na pesa zote zilitumika kujenga ccm kwa kodi za watanzania wote kipindi kile cha chama chashika hatamu. Itachukua muda kwa vyama vya upinzani kuwa strong Tanzania nzima.

Na hata huo muda ukifika, kuna wakati chama fulani kitakuwa na nguvu sehemu fulani ya nchi (au kwenye tabaka fulani la wananchi) na sio nchi nzima ya Tanzania.
 
Karibu sana chama

Chama

Junior Member


--------------------------------------------------------------------------------

Join Date:Fri Aug 2010
Posts:8
Thanks : 0:Thanked 2 Times in 2 Posts
 
Hii michezo ya kuigiza itakwisha lini?

Watanzania tumechoshwa na michezo ya kuigiza, vyama vya upinzani vikuwa ni vichekesho vitupu, sisemi kwamba watanzania hatuna uchungu na nchi yetu au tunafurahia vitendo vy a kifisadi vinavyofanywa na CCM bali kinachotia uchungu ni vyama vya upinzani kukosa dira ya ushindi na kujaza mamluki wa CCM ndani ya vyama. Mfano kitendo cha kuiachia CCM kupitisha wagombea zaidi 10 bila kupingwa kama si usaliti kwa watanzania ni kitu gani? CCM inatumia kila mbinu kudhoofisha upinzani ; ukweli uliopo hivi vyama havikubaliki kila sehemu je wapinzani wamekosa busara kuungaisha nguvu ili kupambana na CCM? Lingekuwa jambo rahisi pale inapokubalika Chadema wapinzani waiunge mkono Chadema, pale inapokubalika CUF waiunge mkono CUF hata uraisi ilipidi wakubaliane asimame mgombea mmoja tu, viongozi wa upinzani wanalijua jambo hili lakini kwa kuwa hawapo kwa maslahi ya watanzania hawawezi hata siku moja wakakubaliana, kimsingi hii michezo ya kuigiza itaendelea siku hadi siku jana ilikuwa Mrema, akaja Mbowe leo hii Dr. Slaa hakuna kitachofanikiwa hadi watakapo tokea viongozi wa kweli kama akina LECH WALESA alipoongoza mapinduzi ya Poland; mapinduzi si lazima damu imwagike; tukipata viongozi wa kweli CCM itaondoka madarakani kwa nderemo na vifijo. Watanzania vyama vyama vya kweli tunavyo bali hatujajua namna ya kivitumia. Vyama vya wafanyakazi na wakulima vikisimama kidedea kutetea maslahi ya watanzania ndio pekee watakaoing`oa CCM madarakani. CCM wameshajifunza kilichotokea Kenya haitakuwa rahisi kuitoa madarakani watatumia kila mbinu chafu wanayoijua kutetea maslahi yao. WATANZANIA AMKENI !!!!!!!!!!

bange!
 
Hii michezo ya kuigiza itakwisha lini?

Watanzania tumechoshwa na michezo ya kuigiza, vyama vya upinzani vikuwa ni vichekesho vitupu, sisemi kwamba watanzania hatuna uchungu na nchi yetu au tunafurahia vitendo vy a kifisadi vinavyofanywa na CCM bali kinachotia uchungu ni vyama vya upinzani kukosa dira ya ushindi na kujaza mamluki wa CCM ndani ya vyama. Mfano kitendo cha kuiachia CCM kupitisha wagombea zaidi 10 bila kupingwa kama si usaliti kwa watanzania ni kitu gani? CCM inatumia kila mbinu kudhoofisha upinzani ; ukweli uliopo hivi vyama havikubaliki kila sehemu je wapinzani wamekosa busara kuungaisha nguvu ili kupambana na CCM? Lingekuwa jambo rahisi pale inapokubalika Chadema wapinzani waiunge mkono Chadema, pale inapokubalika CUF waiunge mkono CUF hata uraisi ilipidi wakubaliane asimame mgombea mmoja tu, viongozi wa upinzani wanalijua jambo hili lakini kwa kuwa hawapo kwa maslahi ya watanzania hawawezi hata siku moja wakakubaliana, kimsingi hii michezo ya kuigiza itaendelea siku hadi siku jana ilikuwa Mrema, akaja Mbowe leo hii Dr. Slaa hakuna kitachofanikiwa hadi watakapo tokea viongozi wa kweli kama akina LECH WALESA alipoongoza mapinduzi ya Poland; mapinduzi si lazima damu imwagike; tukipata viongozi wa kweli CCM itaondoka madarakani kwa nderemo na vifijo. Watanzania vyama vyama vya kweli tunavyo bali hatujajua namna ya kivitumia. Vyama vya wafanyakazi na wakulima vikisimama kidedea kutetea maslahi ya watanzania ndio pekee watakaoing`oa CCM madarakani. CCM wameshajifunza kilichotokea Kenya haitakuwa rahisi kuitoa madarakani watatumia kila mbinu chafu wanayoijua kutetea maslahi yao. WATANZANIA AMKENI !!!!!!!!!!

Ndugu yangu usiumize kichwa chako, wewe kula ugali wako kwa maharagwe malizia na kangara siku ipite..waTz ukitaka kuwaamulia mustakabali wao watakukera tu.
 
Ndugu Solomon, nadhani upeo wako wa kuelewa ni mdogo ama unaongea kama kada wa ccm, hoja yako haina msingi wowote. Unafiki hauna kipimo, si lazima tukubaliane kwenye kila hoja kinachotakiwa ni kujibu kwa hoja ya nguvu ama nguvu za hoja. Inaeleweka wazi kipindi hiki cha uchaguzi ni kipindi cha kuganga njaa bila kujali athari za baadaye na hicho ndicho kinachotuponza watanzania, suala la kuanzisha chama nadhani hukuelewa nilichokisema hapo ndipo ninapohoji upeo wako; sidhani kama unafuatilia mabadiliko ya kisiasa yanayotokea sehemu mbalimbali duniani, mapinduzi mengi yametokana na nguvu za wafanyakazi pale wanapochoshwa na dhuluma; hasa pale uwiano wa kipato na hali ya maisha vinapokuwa havioni huku watu wachache wakiwafurahia maisha hilo lipo njiani kutokea Tanzania, ukweli njaa huvuruga amani kuliko udini na ukabila, fuatilia mapinduzi yaliyomuondoa Bokasa, Marcias Nguema na Mobutu, umegusia siasa za marekani bahati huzijui. Marekani kuna vyama viwili Republican na Democrat vipo vyama vidogo kama Green party hivi vyama vidogo havina athari yoyote kwenye chaguzi za Marekani vishiriki ama visishiriki ni sawa tu. Kimsingi pale Republican inapoona haikubaliki hutumia pesa nyingi kwenye kampeni zake ili kushinda, Democrat hutumia mbinu hizo hizo kuuza sera zake, kuhusu kukishinda chama chenye dola fuatilia kilichoindoa KANU madarakani; siku nyingine usirukie mada kama ulieamkia mlango wa fisi.
 
Acid mimi sisapoti chama chochote ila nasapoti mabadiliko ya kisiasa Tanzania, vyama vya upinzani vilivyopo Tanzania vilianzishwa ili kuleta demokrasia ya kweli; bahati mbaya sana vimeingia kwenye mtego wa ccm badala ya kulenga kwenye kuleta mabadiliko vimekimbilia kwenye kupigania ruzuku.
 
vyama vya siasa vyote vina uchu wa madaraka.Havina dhamira ya kweli ya kuleta mabadiliko. CCM OYEE?
 
Hii michezo ya kuigiza itakwisha lini?

Watanzania tumechoshwa na michezo ya kuigiza, vyama vya upinzani vikuwa ni vichekesho vitupu, sisemi kwamba watanzania hatuna uchungu na nchi yetu au tunafurahia vitendo vy a kifisadi vinavyofanywa na CCM bali kinachotia uchungu ni vyama vya upinzani kukosa dira ya ushindi na kujaza mamluki wa CCM ndani ya vyama. Mfano kitendo cha kuiachia CCM kupitisha wagombea zaidi 10 bila kupingwa kama si usaliti kwa watanzania ni kitu gani? CCM inatumia kila mbinu kudhoofisha upinzani ; ukweli uliopo hivi vyama havikubaliki kila sehemu je wapinzani wamekosa busara kuungaisha nguvu ili kupambana na CCM? Lingekuwa jambo rahisi pale inapokubalika Chadema wapinzani waiunge mkono Chadema, pale inapokubalika CUF waiunge mkono CUF hata uraisi ilipidi wakubaliane asimame mgombea mmoja tu, viongozi wa upinzani wanalijua jambo hili lakini kwa kuwa hawapo kwa maslahi ya watanzania hawawezi hata siku moja wakakubaliana, kimsingi hii michezo ya kuigiza itaendelea siku hadi siku jana ilikuwa Mrema, akaja Mbowe leo hii Dr. Slaa hakuna kitachofanikiwa hadi watakapo tokea viongozi wa kweli kama akina LECH WALESA alipoongoza mapinduzi ya Poland; mapinduzi si lazima damu imwagike; tukipata viongozi wa kweli CCM itaondoka madarakani kwa nderemo na vifijo. Watanzania vyama vyama vya kweli tunavyo bali hatujajua namna ya kivitumia. Vyama vya wafanyakazi na wakulima vikisimama kidedea kutetea maslahi ya watanzania ndio pekee watakaoing`oa CCM madarakani. CCM wameshajifunza kilichotokea Kenya haitakuwa rahisi kuitoa madarakani watatumia kila mbinu chafu wanayoijua kutetea maslahi yao. WATANZANIA AMKENI !!!!!!!!!!

ni sahihi, hasa hili la vyama vya upinzani kutoshirikiana ndiyo linaleta kinyaa zaidi. haiwezekani wagombea wa upinzani 8 against 1 wa chama tawala. wangekubaliana kumwacha mmoja vs CCM hapo tungeona kuwa nia ya vyama pinzani ni kuleta mabadiliko otherwise mtazamo unabaki kwamba watu wanatafuta tu maisha (rejea Songs of Ocol & Lawino kwa wale walikisoma)
 
vyama vya siasa vyote vina uchu wa madaraka.Havina dhamira ya kweli ya kuleta mabadiliko. CCM OYEE?

Huu ndo ukweli na huenda ikawa ni kweli kuwa Lipumba na Hamad wako mfukoni mwa Rostam Aziz. Mrema yeye anajulikana ni CCM damudamu na kapelekwa huko kuwavuruga wapinzani.
 
Back
Top Bottom