Martin Maranja Masese
Member
- Apr 24, 2011
- 30
- 555
Mchengerwa, Makonda; Nyani na Ngedere
Hoja za ufisadi katika ujenzi wa miradi ya maendeleo Arusha iliyotolewa na Mrisho Gambo haitakiwi kujibiwa na Waziri wa TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa au Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda.
Mbunge wa Arusha, Mrisho Gambo aliibua tuhuma za ufisadi matumizi mabaya ya fedha kwenye miradi ya maendeleo. Akisema katika ujenzi wa jengo la utawala gharama zake jumla hazipungui Tsh. Bilioni 9.
Akaongeza, jengo la ghorofa 8 limejengwa kwa Tsh. Bilioni 9, kila ‘floo’ moja imejengwa kwa Tsh. Bilioni 1. Kwamba, waliingia mkataba wa wa Tsh. Bilioni 6.2 na vipimo katika BOQ na utekelezaji ni tofauti.
Thamani ya makadirio ya ujenzi (Bill of Quantities (BOQ)) 1,821 m², mkandarasi ametoa zabuni kwa 11,828 m², vipimo vilivyoongeza gharama ya Tsh. Bilioni 252. Katika hili TAMISEMI ni mtuhumiwa.
Kwa maelezo ya Mrisho Gambo, aliyotoa bungeni, kutokana na tofauti kati ya maandishi ya mkataba na utekelezaji halisi wa kazi, gharama za ujenzi zimeongezeka kwa zaidi ya Tsh. bilioni 8 bila maelezo.
Wameingia mkataba wa Tsh. Bilioni 6.2, gharama zilitakiwa kuwa Tsh. Bilioni 8. Kwamba Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) wanao ushahidi wa jambo hilo, lakini hatua hazichukuliwi.
Kwamba, zimetengwa Tsh. Bilioni 1.6 kubomoa eneo dogo la Stendi ambalo linaingiza Tsh. Milioni 800 kwa halmashauri kwa mwezi, linabomolewa kujengwa jengo lingine. Mrisho Gambo anasema kuna ufisadi.
Kwamba, wanajenga ukumbi wa zaidi ya Tsh. Bilioni 3 wakati kuna ukumbi wa halmashauri (ambao wanafanya biashara ya kukodisha) wakati huo, Arusha kuna ukumbi mkubwa wa mikutano wa kimataifa wa AICC.
Tuhuma za Mrisho Gambo (MB) hazijatolewa na Paul Makonda (RC). Fedha zimetoka TAMISEMI, hivyo TAMISEMI ni watuhumiwa. Bunge kutumia ushahidi wa Waziri TAMISEMI bungeni ni michezo ya kitoto.
Bunge timamu lilitakiwa kuagiza ukaguzi maalum (special audit) katika miradi ambayo Mrisho Gambo anailalamikia umefanyika ufisadi. Ukaguzi maalum ungefanywa na kamati teule ya bunge au CAG.
The Public Audit Act, kifungu 29(1)(2) kinampa mamlaka CAG kufanya ukaguzi maalum (special audit) kwa kuombwa na mtu, taasisi, mamlaka za serikali, wizara, idara, wakala, mamlaka za Serikali za Mitaa
The Public Audit Act, kifungu 36(1) kinaelekeza, wakati wowote ambao CAG atahitajika kufanya ukaguzi katika fedha au mali ya umma bila kuchelewa atafanya ukaguzi maalum na kuandaa ripoti kupeleka kwa Rais
TAMISEMI haiwezi kuchunguza na kutoa taarifa katika fedha za miradi ya maendeleo ambazo zilitolewa na WIZARA. TAMISEMI haiwezi kujichunguza yenyewe katika tuhuma ambazo imetuhumiwa bungeni.
Kwa hali ya kawaida, inawezekana, TAMISEMI kwa mamlaka ya baadhi ya watendaji wake, wakatumia miradi ya maendeleo kuchepusha fedha za umma na kufanya ufisadi. TAMISEMI hawawezi kujichunguza.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika ziara ya kikazi Kigoma, 20-22 Septemba 2023, alipata taarifa za uwepo wa fedha zilizoingizwa kwenye akaunti ya AMANA ya Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma.
Fedha hizo ikaonekana zilitoka TAMISEMI, na kisha kuondolewa baada ya muda bila maelekezo maalum au kufahamu fedha hizo zilitumika katika namna gani. Baada ya hapo ikaundwa timu maalum ya uchunguzi.
Oktoba 25, 2023 timu ya uchunguzi ikawasilisha taarifa kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa taarifa ya uchunguzi ulihusu tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika halmashauri ya Manispaa ya Kigoma - Ujiji
Taarifa ikabainisha watu 10 wanahusika na mtandao wa uhamishaji fedha kinyume cha taratibu, Tsh. Milioni 463.59 zilitumwa katika halmashauri ya Manispaa ya Kigoma na hazikuwa katika mpango/bajeti.
Fedha hizo hazikuwa katika mpango au bajeti ya Manispaa na hazijawahi kuombewa matumizi kama bajeti ya ziada. Taarifa iliwataja maafisa wa manispaa kwa kushirikiana na maafisa wa TAMISEMI na hazina.
Timu ya uchunguzi iliyoundwa na Waziri Mkuu ikabaini, kuna ubadhirifu mkubwa unafanyika kupitia kitengo cha usimamizi wa fedha katika akaunti ya jumuifu ya AMANA, kitengo kilichopo OR-TAMISEMI.
Timu ya uchunguzi ilibaini kitengo cha usimamizi wa fedha katika akaunti jumuifu ya AMANA, TAMISEMI kinahusika kutuma fedha halmashauri na kuzitoa kwa kushirikiana na watumishi wa halmashauri.
Baadhi ya halmashauri zinakuwa hazijaomba kibali cha kuvuka na fedha za bakaa (fedha zinazobaki katika bajeti) kutoka hazina lakini zinatumiwa fedha hizo. Zipo zinaombewa kibali lakini zinapewa pungufu ya fedha.
Pesa ambazo zinabaki hazijulikani zinakwenda wapi na matumizi yake ni gani. Hizo pesa nyingi zinapigwa na maafisa wa TAMISEMI, maafisa wa HAZINA, wafanyabiashara, na maafisa wa halmashauri.
Huenda tungepata ukaguzi na uchunguzi maalum, labda tungepata kuelewa kama WIZARA inahusika au haiusiki na uchepushaji wa fedha hizo. Hiyo ingetusaidia walipa kodi. Hizo ni fedha za umma. Hizo ni fedha zetu.
Katika hili, TAMISEMI ni watuhumiwa. Hawawezi kujichunguza katika tuhuma za ufisadi ambazo zimeibuliwa bungeni. Tuelewane, hatumtetei Mrisho Gambo, hoja zake za ufisadi wanazipiga nyundo.
Mrisho Gambo ameomba radhi na kuwa mpole, kwa sababu amezidiwa nguvu na kundi la wezi na mafisadi ndani ya halmashauri, TAMISEMI na chama chake, CCM. Pia, hofu ya kupoteza ubunge. Ameufyata.
MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.
Hoja za ufisadi katika ujenzi wa miradi ya maendeleo Arusha iliyotolewa na Mrisho Gambo haitakiwi kujibiwa na Waziri wa TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa au Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda.
Mbunge wa Arusha, Mrisho Gambo aliibua tuhuma za ufisadi matumizi mabaya ya fedha kwenye miradi ya maendeleo. Akisema katika ujenzi wa jengo la utawala gharama zake jumla hazipungui Tsh. Bilioni 9.
Akaongeza, jengo la ghorofa 8 limejengwa kwa Tsh. Bilioni 9, kila ‘floo’ moja imejengwa kwa Tsh. Bilioni 1. Kwamba, waliingia mkataba wa wa Tsh. Bilioni 6.2 na vipimo katika BOQ na utekelezaji ni tofauti.
Thamani ya makadirio ya ujenzi (Bill of Quantities (BOQ)) 1,821 m², mkandarasi ametoa zabuni kwa 11,828 m², vipimo vilivyoongeza gharama ya Tsh. Bilioni 252. Katika hili TAMISEMI ni mtuhumiwa.
Kwa maelezo ya Mrisho Gambo, aliyotoa bungeni, kutokana na tofauti kati ya maandishi ya mkataba na utekelezaji halisi wa kazi, gharama za ujenzi zimeongezeka kwa zaidi ya Tsh. bilioni 8 bila maelezo.
Wameingia mkataba wa Tsh. Bilioni 6.2, gharama zilitakiwa kuwa Tsh. Bilioni 8. Kwamba Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) wanao ushahidi wa jambo hilo, lakini hatua hazichukuliwi.
Kwamba, zimetengwa Tsh. Bilioni 1.6 kubomoa eneo dogo la Stendi ambalo linaingiza Tsh. Milioni 800 kwa halmashauri kwa mwezi, linabomolewa kujengwa jengo lingine. Mrisho Gambo anasema kuna ufisadi.
Kwamba, wanajenga ukumbi wa zaidi ya Tsh. Bilioni 3 wakati kuna ukumbi wa halmashauri (ambao wanafanya biashara ya kukodisha) wakati huo, Arusha kuna ukumbi mkubwa wa mikutano wa kimataifa wa AICC.
Tuhuma za Mrisho Gambo (MB) hazijatolewa na Paul Makonda (RC). Fedha zimetoka TAMISEMI, hivyo TAMISEMI ni watuhumiwa. Bunge kutumia ushahidi wa Waziri TAMISEMI bungeni ni michezo ya kitoto.
Bunge timamu lilitakiwa kuagiza ukaguzi maalum (special audit) katika miradi ambayo Mrisho Gambo anailalamikia umefanyika ufisadi. Ukaguzi maalum ungefanywa na kamati teule ya bunge au CAG.
The Public Audit Act, kifungu 29(1)(2) kinampa mamlaka CAG kufanya ukaguzi maalum (special audit) kwa kuombwa na mtu, taasisi, mamlaka za serikali, wizara, idara, wakala, mamlaka za Serikali za Mitaa
The Public Audit Act, kifungu 36(1) kinaelekeza, wakati wowote ambao CAG atahitajika kufanya ukaguzi katika fedha au mali ya umma bila kuchelewa atafanya ukaguzi maalum na kuandaa ripoti kupeleka kwa Rais
TAMISEMI haiwezi kuchunguza na kutoa taarifa katika fedha za miradi ya maendeleo ambazo zilitolewa na WIZARA. TAMISEMI haiwezi kujichunguza yenyewe katika tuhuma ambazo imetuhumiwa bungeni.
Kwa hali ya kawaida, inawezekana, TAMISEMI kwa mamlaka ya baadhi ya watendaji wake, wakatumia miradi ya maendeleo kuchepusha fedha za umma na kufanya ufisadi. TAMISEMI hawawezi kujichunguza.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika ziara ya kikazi Kigoma, 20-22 Septemba 2023, alipata taarifa za uwepo wa fedha zilizoingizwa kwenye akaunti ya AMANA ya Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma.
Fedha hizo ikaonekana zilitoka TAMISEMI, na kisha kuondolewa baada ya muda bila maelekezo maalum au kufahamu fedha hizo zilitumika katika namna gani. Baada ya hapo ikaundwa timu maalum ya uchunguzi.
Oktoba 25, 2023 timu ya uchunguzi ikawasilisha taarifa kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa taarifa ya uchunguzi ulihusu tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika halmashauri ya Manispaa ya Kigoma - Ujiji
Taarifa ikabainisha watu 10 wanahusika na mtandao wa uhamishaji fedha kinyume cha taratibu, Tsh. Milioni 463.59 zilitumwa katika halmashauri ya Manispaa ya Kigoma na hazikuwa katika mpango/bajeti.
Fedha hizo hazikuwa katika mpango au bajeti ya Manispaa na hazijawahi kuombewa matumizi kama bajeti ya ziada. Taarifa iliwataja maafisa wa manispaa kwa kushirikiana na maafisa wa TAMISEMI na hazina.
Timu ya uchunguzi iliyoundwa na Waziri Mkuu ikabaini, kuna ubadhirifu mkubwa unafanyika kupitia kitengo cha usimamizi wa fedha katika akaunti ya jumuifu ya AMANA, kitengo kilichopo OR-TAMISEMI.
Timu ya uchunguzi ilibaini kitengo cha usimamizi wa fedha katika akaunti jumuifu ya AMANA, TAMISEMI kinahusika kutuma fedha halmashauri na kuzitoa kwa kushirikiana na watumishi wa halmashauri.
Baadhi ya halmashauri zinakuwa hazijaomba kibali cha kuvuka na fedha za bakaa (fedha zinazobaki katika bajeti) kutoka hazina lakini zinatumiwa fedha hizo. Zipo zinaombewa kibali lakini zinapewa pungufu ya fedha.
Pesa ambazo zinabaki hazijulikani zinakwenda wapi na matumizi yake ni gani. Hizo pesa nyingi zinapigwa na maafisa wa TAMISEMI, maafisa wa HAZINA, wafanyabiashara, na maafisa wa halmashauri.
Huenda tungepata ukaguzi na uchunguzi maalum, labda tungepata kuelewa kama WIZARA inahusika au haiusiki na uchepushaji wa fedha hizo. Hiyo ingetusaidia walipa kodi. Hizo ni fedha za umma. Hizo ni fedha zetu.
Katika hili, TAMISEMI ni watuhumiwa. Hawawezi kujichunguza katika tuhuma za ufisadi ambazo zimeibuliwa bungeni. Tuelewane, hatumtetei Mrisho Gambo, hoja zake za ufisadi wanazipiga nyundo.
Mrisho Gambo ameomba radhi na kuwa mpole, kwa sababu amezidiwa nguvu na kundi la wezi na mafisadi ndani ya halmashauri, TAMISEMI na chama chake, CCM. Pia, hofu ya kupoteza ubunge. Ameufyata.
MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.